Sunday, May 17, 2015

UGANGA NA MAOMBEZI (RUQYA) PART 2

Asalaam Aleiykum

Hapo ndipo wanapofanya kazi Wachawi na Waombezi katika hiyo (Energy). Ama kwenye jambo la Roho(Soul)Yako, kule hana mtu yoyote (Access)Ruhusa iwe Jinn au Mwanaadamu wala Malaika kugusa isipokua kwa Idhini ya Mwenye enzi Mungu.
Darsa yetu ya leo imekita kwenye Fani ya Maombezi, Tumeona yakua Waganga ni (Bussiness)tupu, lakini tuna hamu ya kuwajua hawa Waombezi wana jambo gani muhimu, Lakini kabla ya kuendelea nasikitika kuwa mpaka kwenye Fani hii ya uombezi wameingia watu wanafanya biashara.
Sasa tuingie katika Fani hii ya Maombezi tupate kujibu lile swali la (Ruqya), Kulijibu swali hili itatubidi twende (Deep) tukatizame kwanini ikawa kuombewa?, Na ndani ya kuombewa kuna kitu gani?, Kwanza kabisa napenda ufahamu Wachawi wako wengi sana, kwa sababu ni elimu ya uharibifu, na kila kwenye uharibifu watu wanakua wengi, tizama mfano wa kwenye ngoma na msikitini utalijua hilo, wapi utapata watu wengi?.
Kwa hiyo utajua Wachawi ni wengi sana na Waombezi ni wachache sana, Kwa sababu Uombezi ni Uteule(Selected)wa Mwenyewe Mwenye enzi Mungu, Kwa (Hijaza) Maalum anayopewa (Mja) kutokana na kujikurubisha kwa Mollah wake kwa mapenzi na huruma na unyenyekevu, vikifatiwa na Ibada na Imani ya hali ya juu, akifikia kiwango(Daraja) hiyo kwa Idhini ya Mollah wake anapewa (Energy)Maalum au ita hiyo (Hijaza) ya kuponesha hayo Maradhi ya Siri yanotokezea kwenye hiyo (Etheric Body) inayo milikiwa na (Mind) wasomi wanajua baadhi ya mambo wanaoneshwa, lakini wao husema (Brain) imepeleka (Signal) na hivi na vile, tuwaachie wenyewe wanasayansi.
Sisi tunasafiri na Muombezi huyu Mwenye kutibu maradhi hayo ya Siri na kufukuza viumbe kama majini wanokaa kwenye hiyo (Etheric Body), Unaweza kuniuliza hii (Etheric Body) ni kitu gani?, wacha nikupe mifano labda unaweza kuijua na ukaelewa ni nini kitu hicho, na vipi maombezi yafanyavo kazi yake.
Maombezi yenyewe yanategemea na uwezo wa kinguvu wa Muombaji na hiyo (Energy) yake alonayo, Napenda Uelewe kila kitu ni (Exchange of Energy)basi ikiwa Muombezi huyo ana nguvu za ziada, basi inatosha kukaa karibu au kwenda nyumbani kwake tu unapona maradhi yako ya (Etheric Body) ambayo ndio mengi tulonayo, Na kama nguvu zake za Maombi ni dhaifu itabidi asome na kukutolea sadaka ili upate shufaa itokayo kwa Mollah wako, kumbuka wote hawa wawili wana (Hijaza) lakini mmoja wao ni dhaifu.
Na Mifano ya zifanyavyo kazi zake (Energy) hizi ni kama hivi, kwani haijawahi kutokea kwako wewe ukawa pengine Umekasirika akatokea (Kipenzi) chako ukafurahi hapo hapo?, Hujiulizi wewe kwanini mtu ana nyanyua simu anakwambia maneno tu hulali usiku mzima,maneno yamepita kwenye waya za simu (Physical Body)inataka kulala lakini wapi huwezi kulala, na kitu chenyewe ni maneno tu, hukumbuki kuambiwa kitu ukacheka, na ukaambiwa chengine ukaangua kilio, Jitizame wewe ukenda kwenye mikutano ya siasa unakuaje kwenye ushabiki wako pale unapoambiwa kidumu chama chako, vipi unavoshangiria huwezi kujizuia hata ukiambiwa ndugu yako atauliwa unasema na afe, ushawahi kujitizama ukiingia hospital kwenye wagonjwa mahtuti wewe mwenyewe unakuaje hali yako, hiyo ndio (energy) inayozungumziwa ambayo matatizo mengi yanatokea hapo, na iko ya aina mbili ikichafuka ni (Negetive) na ikitulia (Positive) kwa hiyo maombezi yanofanyika ni katika hiyo (Etheric Body) ambayo inaleta matatizo mpaka kwenye (Physical Body) ndio inabidi Mtu upate Maombi ya (Ruqya).

No comments:

Post a Comment