Sunday, May 24, 2015

DUA YA KUANZIA SALA PART 3

Asalaam Aleiykum

"Allahumma Rabba Jibril -WaMikail-Wisraafil-Fatira-Sammawati-Wal-ardhi,Aalima-Ghayib washahadah, Anta tahkum bayna Aabadika fiimaa kanoo fiih Yakhtalifuna, Ihdinii limakh-tulifa-fiih minal haqq biidhinika, Innaka tahdii man-tashaau ila siraatin Mustaqqim".
"Ewe Mollah wa Jibril na Mikail na Israfil(Malaika wakubwa) Muumba wa Mbingu na Ardhi, Mjuzi wa vyenye kuonekana na visivyo onekana, Wewe ni Mwenye kuhukumu Baina ya waja wako katika yale walo khitafiliana, Niongoze mimi katika haki ya ile khitilafu kwa uwezo wako, kwa hakika wewe unamuongoza umtakaye katika njia ilonyooka".
"Allahu Akbar Kabeera, Allahu Akbar Kabeera, Allahu Akbar Kabeera, Walhamdu lillahi katheera, Wa Subhaanallahi Bukratan waseela,Audhubillahi Mina-Shaytan, Min Nafkhihi, Wa Naftihi, Wa khamzihi".
"Mollah Mkubwa, Aliye Mkubwa,Mwenye Ukubwa, Shukran zote anasthiki yeye, Utukufu ni wake (Mollah wangu)kuchomoza kwa siku mpaka mwisho wake, Najikinga na shaytan na kuhema kwake, na sauti yake, na mnongonezo wake".
"Allahumma Lakal-Hamdu Anta noor Sammawati wal Ardhi waman fiihina, Walak hamdu anta qayyimu sammawati wal Ardhi waman fii hinna, Walakal Hamdu laka Mulku sammawati wal ardhi waman fii hinna, Walakal Hamdu anta Maliku sammawati wal ardhi walakal hamdu antal Haqq, Wawa'dukal haqq, Wakaulukal haqq, walikaukal haqq, waljannatul haqq, wannarul haqq,Wannabiyyuna haqq, wa Muhammad haqq, walisaa'atu haqq, Allahumma laka a'slamtu, wa'alaika tawakaltu, wabika amantu, wailaika anabtu, wabika khasamtu, wailaika hakamtu, Fakhfirliy maakadamtu, wamaa akhartu, wamasrartu, wamaa a'alantu antal Muqqadimu, waanta Muakhiru, laa illah ilah anta lahiy lailah anta".
"Ewe Mollah wangu  shukuran ni zako wewe, wewe Ni Nuru ya Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo, shukrani ni kwako wewe mwenye kukimiliki kila kitu kwenye Ulimwengu huu, Wewe ni Mwenye Kuimiliki (Kwa uwepo wake)Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo ndani yake, Shukurani zako wewe, Wewe ni (Mfalme)Mollah wa Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo, Wewe ni Mwenye kuitawala Mbingu na Ardhi na vyote vilivyo baina yake, Shukurani zote zinastahiki kwako, Wewe ni Ukweli(Mtupu), Ahadi yako ni ya Ukweli, Maneno yako ni ya Ukweli, uwepo wako ni wa Ukweli, Pepo yako ni ya Ukweli, Moto nao ni wa Ukweli, Mitume ni wa Ukweli, Na (Muhammad)(s.a.w) ni wa Ukweli, Na siku ya Kiyama ni ya Ukweli.
Ewe Allah kwako wewe najitupa(Nimejileta)Na kwako wewe nakutegemea, Nakuamini wewe na kwako narejea kutaka msamaha, Kwa ajili yako (Napigania) Na kwa ajili ya (Utaratibu)wako ndio na hukumu, Nisamahe kwa yale nilofanyia(Nafsi yangu)kuyatanguliza mbele yangu, na yale niloyawacha nyuma yangu, Na yale niliyoyaficha na yale niloyaweka wazi, Wewe ni yule ambaye mwenye kuyatanguliza na wewe ni ambaye Mwenye kuyachelewesha, Wala hakuna Mwenye kupaswa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Wewe Mollah wangu, Wewe ni Mollah wangu, Na hakuna Mwenye kustahiki Kuabudiwa isipokua wewe.
Halafu maliza kusali utuambie Sala yako fupi, na hivi na vile, vipi Sala yako itakua fupi ikiwa kila wakati unaanza na dua hii.Sala yako inakua fupi kwa sababu unakata kona, husomi dua, husomi chochote ukifika unaanza na sura ya (fatiha) ikisha huyo umeporomoka, ukimaliza unasema nisha simamisha Sala, ianze kwa dua na utulivu, fanya marekebisho iwe kila ukiingia kwenye sala unaanza kwa dua, na ukimaliza unamaliza kwa dua, halafu itizame jee sala yako itakua fupi?.

No comments:

Post a Comment