Asalaam Aleiykum
Katika maswali nisiyofurahi kuulizwa hakuna kama haya ya (Kiuganga) Watu wananifata na kuniuliza habari za Uganga na Ruqya vipi (Uhalali wake na Uharamu)wake, wanasema nini Maoni yako kuhusu jambo hili, vipi ntakua na maoni katika jambo hilo, mimi nilicho nacho ni kueleza jambo hili, ikisha wewe una hiyari kuchukua au kuniachia mwenyewe maelezo yangu.
Kwanza kabisa unapozungumzia jambo hili la Uganga ujue una kusudio la kitu gani, ukisema neno uganga umekusudia yule anayekupa matibabu, na kwa tafsiri yangu mimi watu hawa wapo wawili lakini wana kazi moja, huyu wa kwanza unamuamini na huyo wa pili unamuogopa. Mganga wa kwanza unaye muamini ni yule unayesikia au kujua kasoma miaka (7) kahitimu mafunzo yake na kuonesha (Certificate)zake ukutani, huyu ukimuona tu unaanza kupona, nafuu inakujia, unajisikia hujambo, Na akiwa mzoefu wa miaka mingi akikupa maji tu inatosha.
Halafu kuna huyu wa pili wa (Kienyeji)yeye hakusoma hana (certificate)lakini anajua dawa za kutibu baadhi ya maradhi ya mwili, na huyu yeye anatumia mbinu za kukufanya (Umuogope) kwa ukweli wawili hawa wote ni (Bussiness)tu. Wafanyabiashara hawa wanajua kuna mambo mawili ukiyaingia yana faida kubwa moja ni chakula na la pili ni maradhi, hupati hasara kabisa katika biashara hii ya chakula na matibabu ya wanaadamu, kwa sababu ni vitu muhimu na wanaadamu wanavihitaji, ndio maana utaona Waganga(Doctors) ni wenye kuweka maslahi yao mwanzo, wewe kufa papatika na maradhi lakini kama huna pesa hupati matibabu, hupewi dawa ya kupunguza maumivu.
Kwa kuwa maradhi yapo ya aina mbili wacha sasa tumtaje Bingwa wa maradhi yasio onekana na yanayo onekana nayo ni haya ya (Sipiritual)mambo ya Kiroho, kwa sababu Mwanaadamu una (body)Mbili, moja ni (Physical body) na ya pili ni (Sipiritual body).
Ili upate kufahamu kwa urahisi wacha nikufafanulie kwa njia ya rahisi, sina shaka ushapata kusikia kitu kama hichi (Body, Mind, and Soul),(Body)yaani Mwili ndio huu (Physical)unayoiona inashambuliwa na maradhi ya (Bacteria) na (Virus) na hivi na vile, halafu kuna hii (Etheric Body) hii inahusiana zaidi na (Mind) hii ndio inashambuliwa na hiyo (Energy) maalum inayotokea kwa Wanaadamu pamoja na Majini.
Endelea part 2
No comments:
Post a Comment