Wednesday, June 1, 2016

RAMADHAN NI VAZI LA UCHA MUNGU PART 2

Asalaam Aleiykum

Tuanze na aya iliyomo kwenye sura ya (Aaraf)aya ya 26, tunalitafuta guo la Ucha Mungu aya hii itatufunganisha na darsa yetu ya leo ili tupate kuanza safari yetu ya uchambuzi, aya inasema nini kuhusu kadhia hii.

يَـٰبَنِىٓ ءَادَمَ قَدۡ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمۡ لِبَاسً۬ا يُوَٲرِى سَوۡءَٲتِكُمۡ وَرِيشً۬ا‌ۖ وَلِبَاسُ ٱلتَّقۡوَىٰ ذَٲلِكَ خَيۡرٌ۬‌ۚ ذَٲلِكَ مِنۡ ءَايَـٰتِ ٱللَّهِ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ
Enyi Wanaadamu hakika tumekuteremshieni nguo zifichazo tupu zenu na nguo za pambo, Na nguo za utawa(Ucha Mungu)ndizo bora, hayo ni katika ishara za Mwenye enzi Mungu ili wapate kukumbuka.
Nataka uyatizame maneno mawili yaliyomo katika aya hiyo yanosema (Ishara na Kukumbuka)hayo yatakua na faida kubwa na wewe katika kuifahamu darsa hii.
Naam:tumepewa aina mbili za nguo, ama ile ya kwanza sote tunaijua ni kwa ajili ya kuhifadhi tupu zetu na kadhalika kujipamba, unalikumbuka neno (Ishara) basi inaanzia hapa, kwanini ikatajwa tupu?, kwa sababu jambo la mwanzo Mwanaadamu au tumtaje Baba yetu Nabii Adam na Mama yetu Hawa, walolipata  (Awareness)Fahamu Waligundua tupu zao. Vipi hilo linahusiana na (Saum) ya Mwezi wa Ramadhan?, endelea kusoma kwa uangalifu  ili uzipate (ishara), maana ya Ishara ni kuashiria jambo.
"Ewe Adam Msiukaribie mti huu mkala tunda lake" Pasipo na uwerevu, na ushawishi wa (Shetani)wakapinga Amri ya Mwenye enzi Mungu wakala tunda kutoka kwenye ule mti na kutolewa Peponi, Yote haya yamehusiana na hiyo (Awareness)Fahamu waloipata, ndio sasa ikaonekana itakua shida kuishi katika Ulimwengu huu, vipi tutatizamana na vizazi vyetu, vipi tutawaangalia wazee wetu ndipo Mollah akatuteremshia vazi la kujistiri, Na hii imekwenda (Deep)hata yale Makabila (Primitive)yanafunika tupu zao, kwa sababu ingekua hatari ee tunafunika hali hii(sex)imo mawazoni nyakati zote, ukiona mtu kajipamba unawacha mpaka(tasbih).
Kilichokusudiwa kuhifadhiwa Rasmi sio hiyo tupu kumbuka kuna neno ishara ambalo linaashiria kuhifadhiwa na kutulizwa ni hiyo (Mind)yako(Akili), au ita (awareness), hilo ndilo kusudio ya guo la kwanza lilotajwa kwenye hiyo aya. Kumbuka umo katika Safari ya kulijua Vazi la Ucha Mungu katika Mwezi huu wa Ramadhan, Vipi tuifunge na vipi tuipate Taqwa inokuja na hayo mambo matatu yalotajwa mwanzoni mwa Darsa hii.
Sasa Wacha tulifungue Guo la pili ambalo ndio hilo vazi la Ucha Mungu.
Endelea Part 3





No comments:

Post a Comment