Asalaam Aleiykum
Kitu cha Mwanzo safari hii upatacho ni (awareness of Love) vipi inakua, pengine Mja siku zote mambo haya yanakutokezea huyajui, basi anza kuyajua mambo haya kwenye Ramadhan yako ya mwanzo ili usikose makusudio na faida ya Ramadhan. Kitu cha mwanzo kama utachunguza wakati unavaa guo hili la (Taqwa) ni njaa, wewe umezoea wakati wote unakula asubuhi, mchana na usiku, leo umefika ule wakati hujatia chakula, hapo mazoea yanaondoka inakuja(1) (Awareness of Body)Fahamu ya mwili wako, unahitaji chakula wakati wake ushafika na wewe huupi chakula, Na vyakula vyote vimo kwenye nyumba na Mahotelini na madukani vinauzwa, lakini wewe kwa Mapenzi tu ya kufata amri ya Mollah wako leo Umefunga hugusi chakula.
(2)(Mind)Akili inataka mambo yake ya kusema watu, kuzini, kudhulumu,wizi,rushwa,mazungumzo yasofaa, kutizama mambo machafu, wewe umekazana hutekelezi amri za akili, ukiweza kwenda (Beyond) vitu viwili hivyo ndipo unapojikuta wewe ni (Pure Soul)Roho safi, hapo ndipo yanapokaa ita(Mapenzi)(Dhikr)(Watch)(Witness)(Remember)(Kukumbuka)(Mindful)ita jina lolote lakini hapo ndipo kwenye kusudio la (Saumu)hapo ndipo kwenye hiyo(Itikaf)unakua huna fikra chafu ila kumkumbuka Mollah wako, una (Watch)kila kitu lakini hushiriki, njaa inakuja,watu wanaendelea na upuuzi wao wewe unabaki kuwa shahidi tu, unaishi katika hali ya kusikia na kuona mambo yote yanatokea lakini wewe hayakugusi, Unaishi kwenye (Roho)uko (Alert)wakati wote unakumbuka unamtaja Mollah wako ukiwa katika hali ya (Full Aware).
Napenda nikumbushe tena wakati ule wa mwanzo Mzee wetu Adam alivopata (Awareness) kapata katika hali ya kuasi kutokana na (kutokujua). Lakini safari hii wewe umo kwenye werevu(Awareness)Fahamu yenye kutii, umejaa mapenzi ya Mollah wako, umejifunga kutekeleza amri yake, umevijua kua Mwili una njaa, na Akili ina mshipa wa Maasi vyote hivyo umeweza kuvimudu na kuvishinda, sasa umefika wakati wa kusema Mollah wangu nimeyefanya haya kwa ajili yako Mollah wangu.(Quraan Al-Anaam-162)
"قُلۡ إِنَّ صَلَاتِى وَنُسُكِى وَمَحۡيَاىَ وَمَمَاتِى لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَـٰلَمِينَ "
Sema,Hakika Sala yangu, Na Ibada zangu, na Uzima wangu, Na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenye enzi Mungu Muumba wa walimwengu wote.
Kutokana na Uwezo huo mimi nasimama kutekeleza vitendo vya mapenzi Mollah wangu, kama vipi?
Endelea part 5
No comments:
Post a Comment