Sunday, September 20, 2015

JUU MIUJIZA CHINI MIUJIZA PART 2

Asalaam Aleiykum


يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّاسُ ٱتَّقُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِى خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٍ۬ وَٲحِدَةٍ۬ وَخَلَقَ مِنۡہَا زَوۡجَهَا وَبَثَّ مِنۡہُمَا رِجَالاً۬ كَثِيرً۬ا وَنِسَآءً۬‌ۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِى تَسَآءَلُونَ بِهِۦ وَٱلۡأَرۡحَامَ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَيۡكُمۡ رَقِيبً۬
"Enyi Wanaadamu Mcheni Mollah wenu ambaye amekuumbeni katika nafsi moja, Na akamuumba Mkewe katika nafsi ile ile, Na akaeneza Wanaume wengi na Wanawake kutoka katika wawili hao, Na Mcheni Mwenye enzi Mungu ambaye kwake mnamuomba(na kuwafanyia)haki jamaa, na kile (Kilichokuhifadhi)hakika Mwenye enzi Mungu ni Mlinzi juu yenu."
Yameshuka Maneno ya Miujiza katika aya hii lakini inatakiwa Mwanaadamu ende (Deep) kuyatizama na kuyagundua kiini na chanzo cha maneno haya ili apate ufumbuzi, kwa njia ya kawaida kama Akili imekutulia unaona kila siku uchambuzi wa aya hiyo kwa juu juu, unaona wewe sote tulivo fanana kuanzia Pua, masikio, Macho, mikono, miguu, vidole na takriban kila kitu mimi na Mwengine yoyote hatuna tafauti, awe Mtu Mfalme au Rais awe na ukubwa wowote tumefanana kuanzia ndani mpaka nje hatuna tafauti, na hicho ndio hicho cha kutizamwa mwanzo ili upate uhakika wa mwanzo.
Hiyo ndio Ardhi aliyoumbiwa kila mmoja wetu na hilo ndilo la miujiza wa chini. Kuna jengine ambalo hili hulifahamu mpaka uende (Deep) kwenye ufalme wako wa Fahamu huko ndiko utakapo kutana na hilo la Muujiza wa Juu na hapo ndipo utakapo tambua hiyo maana ya (Nafsi moja) kwani Katika Ufalme huo ndiko iliko hiyo (Singularity)huko ndiko unakutana na ukweli ya kwamba kilichomo katika nafsi yangu na kwako ndio hicho hicho hatuna tafauti, kama tulivofanana nje na ndani tumefanana(Kutokana na yeye Adam tukamuumbia Hawa) tafauti yetu ni katika (Level) ni ya Nje, huyu Mwanamke yule Mwanamme lakini sote ni sawa kama ilivyo (Ardhi) mipaka iko Juu lakini chini (Ardhi) ni Moja, Bahari ikikauka tunakwenda kote kwa miguu, basi baada ya aya hiyo ndio ikafatia hii ya pili sura ya (Al hujraat 13)



يَـٰٓأَيُّہَا ٱلنَّاسُ إِنَّا خَلَقۡنَـٰكُم مِّن ذَكَرٍ۬ وَأُنثَىٰ وَجَعَلۡنَـٰكُمۡ شُعُوبً۬ا وَقَبَآٮِٕلَ لِتَعَارَفُوٓاْ‌ۚ إِنَّ أَڪۡرَمَكُمۡ عِندَ ٱللَّهِ أَتۡقَٮٰكُمۡ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ۬ 


No comments:

Post a Comment