قُلِ ٱللَّهُمَّ مَـٰلِكَ ٱلۡمُلۡكِ تُؤۡتِى ٱلۡمُلۡكَ مَن تَشَآءُ وَتَنزِعُ ٱلۡمُلۡكَ مِمَّن تَشَآءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَآءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَآءُۖ بِيَدِكَ ٱلۡخَيۡرُۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَىۡءٍ۬ قَدِيرٌ۬
Hiyo ni aya ya (26)iliyomo kwenye sura ya (Al-Imran) inatafsirika hivi:"Sema Ewe Mollah wangu uliyemiliki Ufalme wote, Humpa Ufalme umtakaye,na humuondolea(Ufalme)umtakaye, Na humtukuza umtakaye, Na humdhalilisha umtakaye,Kheri imo mikononi mwako, bila shaka Wewe ni Mwenye uweza juu ya kila kitu".
Aya imeanza kwa kuambiwa "Sema",Kwanini ikawa sema ?Kwa sababu ukiambiwa sema ina maana unaujua ukweli, umeshaushuhudia ukweli, unaishi ndani ya ukweli, huna khofu tena kufa katika ukweli. kwa kuwa ushaujua ukweli siku zote upo na kwenye Ufalme wa Mwenye enzi Mungu hakuna lugha ila kuna shuhuda, Sasa kwa yule Mwenye kujua au kushuhudia ukweli anaambiwa wafikishie ujumbe huu wale wasojua au wasofahamu, ufanye nini?, Uwajulishe haya"Sema hivi" Ewe Mollah Wangu uliyemiliki Ufalme wote, ikitajwa kumiliki wenye Ufahamu mdogo wanadhani na yeye pia Mfalme kwa hiyo wanaanza kuuhusisha Ufalme huo Miliki na (Imagination)zao labda yuko hivi au vile, kumbuka hapo imetumika lugha ili kuwasiliana na wewe na hizo fahamu zako juu ya tendo hilo la Ufalme.
Ewe Mollah Mwenye kumiliki huo Ufalme wa kila kitu, Uwe Ufalme wenyewe wa Vinyama au Wanaadamu au kundi la majini, basi Wewe ni Mwenye kumpa huo "Uongozi"(Ufalme)umtakaye, Uwe Ufalme au Uongozi huo kwenye (Family)au kwenye Kabila, au Ufalme wa Nchi wa kuwaongoza watu, basi Wewe Unamchagua umtakaye awe Kiongozi kwa njia unazozijua wewe katika sehemu au pahala hapo, Na humuondoshea Ufalme huo Umtakaye na haya yote yamo kwenye uwezo wako.
Sasa nini Kitatokezea iwapo kuna baadhi ya Watu Wenyewe watapinga au kukataa au kumuondosha kwa nguvu yule ulomridhia wewe? Nini Dalili zake?, Tunafahamu Wewe ni Mwenye Uweza wa kila kitu, na si mwenye kushindwa katika jambo lolote, lakini pia tunatambua umetupa Wanaadamu Uhuru au uwezo wa kujiamulia tunavyotaka wenyewe(Hiyo ndio Democracy), ila umetuwekea Shuruti ikiwa uamuzi huo ni wa makosa utatuadhibu, na ukiwa katika Matakwa na maridhio kama ulivyopanga wewe basi umetwambia katika hiyo aya hapo juu(Kheri imo mikononi mwako).
Ilipotaja aya kuwa Kheri imo mikononi mwake ndipo ilipoachia huo Uhuru yakwamba kama kikundi au kundi au Mtu pekee kakubali kuridhia anavyopanga na kutaka yule ambaye kamiliki kila jambo, na kwa njia ya (Huria kabisa)ambayo ni ridhaa ya kila mmoja wenu kukubali, anakutieni mapenzi na nyinyi waja wake kulikubali lile ambalo kakuchagulieni ili akupeni hiyo kheri, mkitokezea kuupinga Ufalme wa Mwenye enzi Mungu nini kinatokezea?
Endelea part 2
No comments:
Post a Comment