Sunday, October 27, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(ALLAH)PART 2

Asalaam Aleiykum,

Sababu hana mshirika ndio ikatajwa Umoja kutokana na Allah ina mahusiano na Lugha, na neno la (Ahad)moja lina mashiko yale yale ya kwenye lugha, sasa usije kubabaika ukaona mbona kuna Allah na Ahad, kwanini ikawa viwili hivyo vipo pamoja, kwa sababu vyote vimo ndani ya hilo moja lisilo na lugha, lisoweza kutamkwa, kama Allah ilivokusanya hayo majina 99 hilo moja limekusanya vitu vyote katika Ulimwengu huu, ukiondosha hayo 99 hilo moja linabakia, Moja hili ndilo lenye(Wahid)lenye Ufalme huu wa Ulimwengu, Katika hilo moja sote ndipo tulipotokea na huko dipo tutakaporejea.
Basi kutokana na sababu hiyo, ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ.
"Mwenye enzi Mungu ndiye anastahiki kukusudiwa" 
Na ndio liwe kusudio lako kuyapita kwa maombi hayo yote 99 kufika kwenye hilo lenye dhati yenye yakini, Kila kusudio lako liwe kwa ajili yake, Nani Allahu Ahad? Allah Jina hili kusudio lake ni ule Utukufu Ulotawala Ulimwengu, Utukufu ulokizunguka kila kitu Mbingu na Ardhi(Allahu Akbar) kwa (Zahiri na Batini)Umefichika Utukufu huo na pia uko Wazi kwa Mwenye Akili kuona. Ahad ni Mmoja kwanini isiwe hivyo wakati unajua kila kilichomo katika Ulimwengu huu kimehusiana, wewe na Mti, wewe na Nyota na vyote vilivyomo kwenye Ulimwengu huu vina jinsi moja hakuna tafauti, Mpaka jani liloanguka kutoka kwenye mti au Ua lilochanua lina (Formula ya Dna)kama ulivo wewe, hiyo ndio Ahad, Muumbaji wake nini yeye pekee anokusudiwa na kila kilichomo kati Ulimwengu huu. Hiyo ndio Ahad au (Wahid) ilojificha, vipi sisi leo tutakijua au kulijua jambo linalo onekana na kufichikana kwa wakati mmoja, hatuwezi hata kufikiria upeo wa Allah ukoje, seuze kumfananisha na chochote.
لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ
"Hakuzaa wala kuzaliwa"
Ili kuondosha zana za labda kwamba pengine ni kiumbe ama ana hivi au vile au vyenginevo ndio akatwambia (Hakuzaa wala kuzaliwa) Kilo zaa ama kuzaliwa kinategemea mambo manne, Ardhi,Hewa,Maji,Moto, na vyote hivyo kaviumba yeye Allah vipi leo atakua katika hali ya kuvitegemea vitu hivyo.
وَلَمۡ يَكُن لَّهُ ۥ ڪُفُوًا أَحَدٌ 
"Na wala hana anayefanana naye hata Mmoja" Inaweza mtu kusema ndio hakuzaa wala hakuzaliwa lakini kafanana na (Mtume Fulani) Yeye ni (Formless)hana mfano na yoyote, ikiwa hakuzaa wala kuzaliwa vipi atakua na mfano na yoyote, Anaondosha dhana zenu za kumdhania dhania, Yeye ndiye Allah ambaye mnatakiwa kumuabudu na kumuomba kwa kutumia hayo majina mazuri mazuri, usije ukataka pesa (Ukasoma Tabaytayada-Surat-Massad)utapata moto baada ya pesa, omba kwa majina mazuri upate vilivyo vizuri, na munasaba wake usije ukaishia kwenye hayo majina mkaanza kuleta (Kushubihisha)na hayo majina ukawa unafanya (Image za kila aina) unatakiwa uende (Beyond) ya hizo dhana. Tunamuomba Mollah atufikishe katika hiyo(Tawhid)ya kumjua yeye kwa uwezo  alotupangia wa kumfahamu Mollah wetu Mpenzi.Amin

No comments:

Post a Comment