Sunday, October 13, 2013

MUALIKO WA IMANI PART 2

Asalaam Aleiykum,

 ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَطۡمَٮِٕنُّ قُلُوبُهُم بِذِكۡرِ ٱللَّهِ‌ۗ أَلَا بِذِڪۡرِ ٱللَّهِ تَطۡمَٮِٕنُّ ٱلۡقُلُوبُ 
(Wao)Ni wale waloamini na zikatulia Nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenye enzi Mungu, Kwa kumkumbuka Mwenye enzi Mungu nyoyo hutulia.
Maneno yaliyotajwa hapo juu ni makubwa ikiwa unayajua maana yake kwa undani, lakini kama utapita juu juu hupati kitu, maana imefichika mpaka uwe katika wale wanotaka kujishughulisha kuitafuta.
Kwa wale wanotaka kujua maana basi nitafafanua kidogo ili nikujuze japo kwa uchache maana hiyo, Pata faida mbili hizi uzitumie kuipata hiyo Imani katika moyo wako ugeuke kuwa mtu mwengine kabisa.
Aya Imeanza kwa wale waloamini. Nini Kuamini? Kuamini ni kukubali bila ya pingamizi yoyote kwa lile uliloambiwa, Lakini hiyo haitoshelezi haja, ukikubali bila ya ushahidi (Shaka inabakia) Kwa sababu umeambiwa tu, inaweza kuwa kweli au uongo, unakua na mashaka huna utulivu, mara unafanya makosa, mara unatubu, mara unajiuliza pepo ipo, mara unajipa tamaa moto hakuna, hali hiyo inatokea moyoni mwako kila siku, Ndio maana mtu akikwambia katokea mjini unakubali, unamuamini, lakini ikiwa umemuagizia kitu hajakuletea unabaki na wasiwasi sijui kenda kweli au ananidanganya, lakini wakati huo ushaamini, inakua nusu umeamini nusu una shaka, kutokana na hali hiyo moyo wako unakua (Split)umegawika hauko kwenye Imani wala kwenye kukanusha.
Na unajiona hivi sasa Unakubali Mwenye enzi Mungu yupo, unaogopa adhabu zake, lakini bado unachungulia dirishani huku shaka imekushika, inaweza kuwa kweli inaweza kuwa uongo, Na kama kweli wacha Nisali, Na ikiwa uongo sijapata hasara yoyote, hivi ndio fikra zetu zilivo, zimejaa kila shaka, zimejaa mambo chungu nzima, Unapeleka dua bila ya tamaa, Sala yako inakua kama ya kulazimishwa.
Sasa kwenye aya hii unakumbushwa kitu muhimu sana na kama utakifanyia kazi unaweza kupata manufaa makubwa ya kuipata hiyo Imani. Wale wenye kuamini wanapata utulivu kwa kumkumbuka Mollah wao, Kukumbuka kuko kwa aina mbili, aina ya kwanza hii ni ngumu sana, wachache sana wanoweza kuipata hiyo Imani kupitia njia hii, na hiyo njia ya pili ni rahisi wengi wanaweza kuipata hiyo Imani kama watafata maelekezo yake.
Ama hii ya ugumu unatakiwa Uweke uwepo wa Mwenye enzi Mungu wakati wote (Presence) kila unapokuwepo fikra zako, na wewe mwenyewe uwe kwa Mollah wako, Ukiona Mti, Ukiona Ndege, Ukiona Mbingu, Ukiona Jua, Ukiona mwezi iwe unaviona vyote hivyo na huku unamkumbuka Mollah wako ndie aliyeviumba, ni Vigumu sana huwezi kumkumbuka Mollah kwenye Sala yako, utamkumbuka ukiona Mti, ndio maana nikasema hii ni ngumu wacha sasa tuitizame hiyo ilo rahisi ili tupate kuona kama tutaipata hiyo Imani.
Endelea Part 3

No comments:

Post a Comment