Sunday, October 20, 2013

LIJUE KUNDI LAKO PART 3

Asalaam Aleiykum,

Litaje jina la Mollah wako, nini kimo ndani ya hilo jina, Elewa ndani ya hilo jina yamefichwa mambo, Ndani ya hilo jina utapata kumjua Mollah wako, Sio Kumuona, Na siri ya kujua haina mwisho, daima utaendelea kufunguliwa maajabu yaliyomo kwenye Ulimwengu huu kama wanasayansi wanavoendelea kuvumbua kila siku mambo mepya mepya, Basi na wewe kama umo katika kundi la Mwenye enzi Mungu unayo nafasi hiyo ikiwa utadumisha kulitaja na kulikumbuka jina la Mollah wako.
Kwani ikiwa utakua unalitaja pekee utaingia katika kusahau, utakua kama kasuku, inatakiwa lazima ulikumbuke kwa hamu kubwa na Shauku, kama unavokumbuka mbona sijasali, ni kitu kimoja ila umebadilisha jina, Sababu unakwenda kutaja hilo hilo jina la Mwenye Enzi Mungu. Jitupe kikamilifu, vipi kujitupa kikamilifu(Devotion) Unakumbuka wakati unashida au jambo baya litakutokea unavomuomba Mollah wako akuvue, hivyo ndio kujitupa, Na huko kujitupa isiwe kwa ajili ya kuonesha watu iwe siri baina ya wewe na Mollah wako, Na Mollah wako ni mwenye kukujua vipi ukweli wa mapenzi yako juu yake, usijali wengine kama wanajua wewe Mcha mungu au sio usiwajali kabisa hawapunguzi wala kuongeza chochote katika dini yako, Kujitupa kwenyewe lazima kuwe kwa Roho yako, Akili yako, na kila tendo lako kwa ajili ya kumkumbuka Mollah wako.Na hiyo ndio maana halisi ya( وَتَبَتَّلۡ إِلَيۡهِ تَبۡتِيلاً۬).
Na hayo ndio makundi mawili ama utakua kushoto au kuliani, lipo la tatu lakini nimeamua nisilizungumze kwa sababu watu wachache sana wanofanikiwa kubakia katika hilo kundi la katikati la (Ashab-Aaraf)ambalo hili kwa viumbe haliko na kwa Mollah wao halitaki.
Inshaa Allah tutalizungumza siku za mbele penye majaaliwa tukipata nafasi. Na mpaka sasa ushapata nafasi ya kujijua wewe mtu wa kundi gani, Basi ikiwa la hasara fanya haraka utoke kwani muda ushamalizika, umekaa siku nyingi katika kundi hilo la hasara, huna faida unayopata ila kuzidi kumsahau Mollah wako.
Na kama umo katika kundi la kheri basi zidisha mapenzi yako kwa Mollah wako na yeye atafungua pazia lake uone mambo hujapata kuyaona ya furaha katika Ulimwengu huu, Hapo utajua Mollah wako kakuridhia na wewe umemridhia, Na kuwemo katika kundi la Mwenye enzi Mungu ni mafanikio yasioelezeka.
Namuomba Mollah atujaalie sote tuwemo katika kundi la kheri aliloliridhia kwa uwezo wake Rahman. Amin.



No comments:

Post a Comment