Sunday, October 6, 2013

SIRI NDANI YA SIRI PART 3

Asalaam Aleiykum,

Kwanza kabisa napenda nifahamishe harufu yenyewe ilokusudiwa kushindaniwa ni hiyo ilotajwa katika aya ya 21 mpaka ya 28 ya sura ya Al Mutaffifyn, Harufu yenyewe ya kushindaniwa ni hiyo Ibada, harufu yenyewe ya mambo mema, na harufu ya Ucha Mungu ili uyapate hayo yalotajwa nyuma katika hiyo sura.
Kavunja ukuta wa watu kwa harufu ya (Chakula kitamu)Kajuaje kama hiyo alonusa ni ya chakula kitamu, lazima mwanzo iwe kakaribishwa, lazima alialikwa na kukila chakula hicho, ndipo aliposikia harufu akakumbuka ni ya chakula kitamu, hakusema chakula pekee bali kaongeza na utamu.
Nini Utamu? Utamu ni wenye kukaa kwenye ulimi, nikisema kukaa sina maana uko hapo, ila unapitia hapo kama harufu inavopitia puani, na unafanya kazi zake kwa mashirikiano ya pamoja na harufu, ndio maana mvunjaji akavunja ukuta kwa harufu ya chakula kitamu. Na inavoelekea sote tushaonja chakula hichi na bado tuna hamu ya chakula kitamu, ila upo wetu umetufikisha katika kukijua tu na bado hatujakifahamu, Na tafauti ya kufahamu na kujua ni kubwa sana, kwani kufahamu kunatokana na (Roho) na kujua kunapatikana kwenye (Akili), Kwa hiyo aliponusa harufu akafahamu ni ya Biriani, alipokiona chakula akajua ni kitamu,( au mfano mwengine wa maneno unaambiwa Mgonjwa anafahamu zake anamjua anoingia na kutoka)ukizama kwenye maneno hayo utajua nimekusudia nini.
Usije ukakurupuka ukanusa vitunguu ukadhani Biriani, kumbe ni wali wa Ki Iran, Naam kwanini chakula , katika mambo yote mwanaadamu anaweza kuyakana isipokua chakula.Anao uwezo mwanaadamu wa siku 90 tu, baada ya hapo bila ya chakula anakufa, watu wanapigana vita kwa ajili ya chakula, Binaadamu anaweza kukamilisha kila kitu lakini akifika kwenye chakula anashangaa, anatoa macho, anajiuliza kama kikikosekana au ikawa Mollah kazuia kisiote chochote nini utakua mwisho wetu.
Ndio tunaambiwa msitoe macho kwenye hicho chakula kuna ushahidi wa kutosha kuonesha kuwapo kwa Mwenye enzi Mungu na mambo ya Akhera, Inatosha kukufahamisha kama Muumbaji yupo na kama unavo kitizama chakula chake na yeye anakutizama wewe, Na huyo Mollah wako alokuumba sasa anakwambia huna haja ya kuvunja ukuta, kwanza kitizame chakula chenyewe upate kukifahamu, فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَـٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦۤ,(Abbasa 24)
"Na Atazame mwanaadamu chakula chake"
Siri ndani ya Siri, Sisi ndio yulomuoteshea, tukaifungua ardhi na kuotesha vyote vilivyomo na kutajwa katika sura hiyo na venginevyo visivotajwa.
 مَّتَـٰعً۬ا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَـٰمِكُمۡ
Kwa ajili ya kukustarehesheni nyinyi na wanyama wenu(Abbasa 32) Itizame siri ilofichikana kwa upande wa nje kukustarehesheni(Kavunja ukuta wa watu kwa harufu ya chakula kitamu) lakini kwa upande wa ndani chakula hicho hicho ni dawa kinatibu maradhi haya na yale, ndani ya chakula inapatikana Vitamin, ndani ya chakula inapatikana hizo nguvu unazoringia, Kitizame chakula chako ikisha jiulize nani alotia maji kwenye Dafu, Nani aloufanya mua kutoa sukari ukakutia nguvu, Nani aloweka sukari kwenye Tende, Ndizi, na Zabibu, Jee ushawahi kuzijua ladha yake kwa undani, au unakula zikujaze tumbo, Ushawahi kula chakula bila ya mazungumzo wala tafsiri yoyote ikawa wewe na chakula mnatafutana maana laa bado, basi hebu fanya japo siku moja amua kula chako mwanzo mpaka mwisho bila ya kuzungumza au kutizama TV na kadhalika, iwe wewe na chakula tu uone ladha yake itakuaje, kitafute chakula siri yake na ukiijua hutotaka tena kula huku unazungumza, utakua mwenye hamu ya kujua ikiwa Duniani nahisi ladha hii huko Akhera itakuaje nikipewa(Fresh)Zama kwenye vyakula utapata siri hizo ndogo ndogo zitakuchukua kwenye hiyo siri kubwa, na ukiweza kufika kwenye siri hiyo ndio unakua huna haja ya kuvunja ukuta wa watu, Unaingia kwenye Siri ndani ya Siri, Na utakayo yakuta huko ni Siri yako huna haja ya kuhadithia kama nilivofanya mimi.
Nakutakieni siku kumi njema za Dhul-Hijja.




No comments:

Post a Comment