Sunday, October 4, 2015

MATIBABU YA ROHO PART 1

Asalaam Aleiykum

Naanza Darsa yangu ya leo kwa maneno yalotamkwa na (Professor)mmoja kwenye (University)nilohudhuria sherehe za kuhitimu (Graduation)Mahafali ya Mwanangu hivi karibuni,"Professor" huyo alisema hivi "Na nukuu""Tumefanya uchunguzi na sasa tumegundua kuwa Ukisoma au Ukipata Elimu kuna mambo kadhaa unaepukana nayo, akayataja baadhi ya mambo hayo na kusema, "Unaepukana na mambo ya ukhalifu(Criminal activity)akataja jengine na kusema unaepusha mzigo kwa serekali ya kukutibu, akimaanisha unajiepusha na maradhi,(Unaishi vizuri)katika kuchunga Afya yako, kutokana na hilo jambo la elimu pia unakua na Maisha bora katika uhai wako.
Mimi Nakubaliana na (Professor) huyo katika suala la Mtu kukusanya (Information), unakua unajua na unafahamu kuwa ukivuta sigara utakufa na Cancer, kwa hiyo unaacha kuvuta, lakini tukumbuke maneno haya ya (Elimu)au kujua yalitamkwa ndani ya (Quraan)miaka kama 1400 ilopita kwenye sura ya (Az-Zumar-39.9)
قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الَّذِينَ يَعْلَمُونَ وَالَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ
Sasa cha kushangaza zaidi kwanini wenye kujua ndio wanateseka?,Nini kinawaponza?,Mbona imekua tafauti inaonekana wasojua ndio wanastarehe, wasojua hawana wasiwasi wanafurahia maisha haya kama vinyama vinavyofurahi. Sasa kwetu sisi kimezidi nini mpaka hatuna furaha, Majumbani hakuna mapenzi, kila mtu kachoka anaona bora aende barazani, au aende (disco)kuliko kukaa ndani, ana khofu mara mwenzie atamparura, basi ikiwa imefikia hali hiyo lazima kuna mambo ambayo yanasababisha hali hiyo.
Sasa Ingia kwenye Darsa hii ya (matibabu ya Roho)ili upate kumeza kidonge chako na kupata nafuu ya maradhi hayo, Kumbuka vizuri hakuna chenye kuigusa Roho yako, lakini hiyo Roho imeponzwa na jambo moja tu nalo hiyo uwezo wa kujua, nikiwa na maana wewe Mwenye kusoma sasa hivi, ndio Mwenye na hiyo Asili ya kujua ambayo hatimaye unaweka hizo (Information)katika kumbukumbu ya Akili yako. Japokua yenye kushikwa na maradhi ni Mwili(Body)na Akili(Mind)Lakini huwezi kuvitibu viwili hivyo mpaka kwanza uifanyie marekebisho ya matibabu Roho yako, ndio Maana Mwenye enzi Mungu akasema kutumia (Jumla)katika sura ya (Anfal aya ya 53)
ذَٲلِكَ بِأَنَّ ٱللَّهَ لَمۡ يَكُ مُغَيِّرً۬ا نِّعۡمَةً أَنۡعَمَهَا عَلَىٰ قَوۡمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُواْ مَا بِأَنفُسِہِمۡ‌ۙ وَأَنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ۬ 
Hayo (yakuawafikia hizo Balaa za kukosa Raha) ni kwa sababu Mwenye enzi Mungu habadilishi kabisa neema alizo waneemesha watu, hata(mpaka)wabadilishe wao yaliyomo nyoni mwao, hakika Mwenye enzi Mungu ni Mwenye kusikia na Mwenye Kulijua kila jambo.
Kwa hiyo Nyoyoni kwenye hiyo Roho kuna Maradhi na hiyo ndio kazi ninayo ifanya ili na wewe urejeshe na kurejeshewa Furaha yako. Lakini kwanza lazima ujijue unaumwa Nini?
Endelea Part 2


No comments:

Post a Comment