Sunday, October 4, 2015

MATIBABU YA ROHO PART 3

Asalaam Aleiykum

Sasa ukitaka hiyo Dawa lazima ukijue hichi cha Nne ambacho si (Madoctor)wala(Waganga)wenye kukijua, hukipati kitu hicho ambacho ndio dawa yenyewe kwa kutoa Rushwa wala kujidai kwa cheo chako ulo nacho, Dawa hii au kitu hicho anatoa Mwenyewe alokupa hiyo (Roho), Akikupa dawa hii wewe unakua Furahani, sasa dawa gani hii yenye kutakiwa na kila mtu.
Dawa hii hapewi ila Mtu ila wachache wenye kutimiza masharti yake, ita Dawa hii au kitu hichi upendavyo, Kiite (Taqwa) au Mapenzi, kiite Utiifu au Ucha Mungu lakini Muhimu ukipate kama alivosema Mwenye enzi Mungu wakati anazungumza au kumpelekea (Wahyi) Nabii Musa a.s kwa kumwambia(Mwisho wa aya ya 39)" ۥ‌ۚ وَأَلۡقَيۡتُ عَلَيۡكَ مَحَبَّةً۬ مِّنِّى وَلِتُصۡنَعَ عَلَىٰ عَيۡنِىٓ (٣"
Na Nimekutia Mapenzi yanotokana na Mimi, Na ili ulelewe machoni mwangu(Katika uangalizi wangu )
Hapo kumetajwa mambo makubwa yanataka siku nzima kuchambuliwa ila kwa haraka nakufahamisha hivi, huna furaha katika Dunia hii isipokua uteremkiwe na mapenzi ya Mwenye enzi Mungu, na yakisha teremka ndio unaweza (Kushare)na wenzio kama alivofanya Nabii Musa a.s baada ya kuwaona watu wake wanateseka ndio yakamunigia mapenzi ya kuwavua kutoka kwenye mateso hayo.
Tunaendelea na sisi kutafuta hali kama hiyo ya mapenzi na Furaha, kukitafuta hicho cha nne, huwezi kukipata lazima urejee au niite (repentance)uondokane na tabia ya uasi wowote ule ulo nao, pengine umeacha tu lakini (Inward)kwenye nafsi yako hujabadilika, kwa hiyo kama unaendelea na jeuri na (punishment)adhabu inaendelea unafanywa uwe huna furaha kwa kila ambacho hujakitakia msamaha au kutubu kama mnavyoita, au kusamehe na kusamehewa.
Sasa ufanye nini kuyapata hayo Mapenzi? kuna Masharti yake lazima yatimizwe ndio uwe unaishi kwenye Furaha, kumbuka mapenzi ndio yalobeba hiyo Furaha, kwa hiyo lazima uyapate mapezi ndio uwe furahani kama dunia hii ilivozungukwa na mapenzi matupu ikiwa utafungua macho yako na kuona hilo. Sasa ikiwa hivyo lazima ujiulize mbona wewe unaishi na maradhi? ya Chuki,Hamaki,Hasira,Wivu,na Choyo na mengineyo, daima huko Furahani.
Inatakiwa jambo la mwanzo ulitizame kwenye Ulimwengu huu kila kitu kwenye Ulimwengu huu kimeumbwa kwa Mapenzi ya Mwenye enzi Mungu kuanzia kuumbwa kwako na kila kilichomo, sasa nini kosa lako, Kosa lako wewe umetoka kwenye njia ilonyooka kutokana na mambo mengi sio ya haki na sheria uliyoyafanya ili kuipata hiyo Furaha na mapenzi ndio unatakiwa urejee au urudi ujisafishe. Na hapo ndio unakutana na tafsiri yangu ya neno (Love), maana yake kutokana na mimi ni hii.
(Look Over and View your Emptiness).
Na hiyo pia ndio maana ya yale maneno (Yafanyie wepesi Mizigo yako).
Endelea part 4


No comments:

Post a Comment