Asalaam Aleiykum
Ugonjwa ulo nao ni hatari, na kama haujatibiwa basi mpaka utaondoka kwenye Dunia hii utakua unaumwa na Ugonjwa wa (usununu)hali yakua huna Furaha, Sasa Magonjwa gani ya Roho yanotusumbua? huwa nashangaa sana nikipata mashtaka au malalamiko ya Watu wengi husikii kabisa kutajwa Maradhi yanomsumbua Mtu bali hutajwa sababu nyengine, kama Mume wangu hanisaidii chochote, au Mke wangu kawa kisirani hatizami watoto ipasavyo, au Watoto wamekua (Manunda)wajeuri ndani ya nyumba, sina masikilizano na Mke wangu, au siku hizi sina furaha kabisa kwa kila nitendacho, au bure namchukia fulani, nasikia kero tu kwenye maisha yangu na ndani ya nafsi yangu, au jambo dogo tu nahamaki,Nikisikia Asalaam Aleiykum Bwana nasikia nimeitwa Mtwana naanzisha ugonvi.
Kwa Muono wangu takriban Maisha yako yote yamekua ya Chuki,Visasi, Ghadhabu, Pengine unakerwa kazini ukirudi nyumbani mtoto kamwaga maji unampiga kama vile unaua nyoka, nini kimetokezea Majumbani kwa ujumla na hata kwa kila mmoja wetu.Jee tuseme hiyo Rehma na Baraka imeondoka kile kipindi cha (Honey Moon)ilipokwisha?halafu cha ubaya zaidi Mtu akisha choka huku nje anakusanya mambo yake yote halafu anaigeukia Dini, hapo inapatikana hatari kubwa, bora ageukie mambo mengine kuliko kuvaa joho la dini, hupati isipokua chuki tupu, unamuona hana furaha kwa sababu kachanganya (Madawa).Utaona anaanza kufukuza mpaka wale wanaotaka kujisalimisha kwa Mollah wako. kwanini ikawa hivyo? kwa sababu Dini yake, Matendo yake yanakua ya Maradhi matupu tuko nao na tunawaona wanavyoteseka ,kwa kuwa hawajapata dawa ya kuitibu Roho yake.
Sasa ukitaka matibabu ufanye nini?, hapa kuna uchaguzi wa aina mbili, Ima uendelee na Maradhi ya Roho, au utafute Dawa, ambayo wengi wanakwenda kwa (Doctor)atibiwe maradhi ya Roho, (Doctor)au Mganga wa kienyeji hatibu maradhi ya Roho, wao wanasaidia kukupa nafuu ya Mwili(body) na Akili(Mind)anafanya nini?anakupa matibabu ya aina tatu, anakupa Vidonge, anakupeleka kwa (Therapist) au (Counselling)sikatai vitu hivyo vinasaidia kuleta Nafuu kwenye (Body) na (Mind) lakini hakuna manufaa kwenye Ulimwengu wa Roho, Katika kuhangaika huko kidogo wamegundua kwa mbali kuwa kuna kitu nje ya viwili hivyo ambacho hakipo kwenye uwezo wao ambacho kama utakifanyia (therapy au counselling) unaweza kupata nafuu, ndio unaona watu wengi wanaishi kwenye nafuu tu, kwa wale wenye kupata angalau hayo matibabu ya kisayansi, Wengi wanataka kupona lakini masikini hawaijui dawa, hawajui wafanye nini.
Leo unapewa muelekeo wa hiyo Dawa ili maradhi yako yapone, ili na wewe uweze kuishi Furahani.
Endelea part 3
No comments:
Post a Comment