Sunday, October 18, 2015

NJIA YA KUHIFADHI SALA PART 1

Asalaam Aleiykum

Nimeona kuna sababu ya kuleta darsa hii baada ya kushuhudia hasara inayopatikana juu yetu katika kusali halafu ikawa huipati sala yenyewe, Na inachangia pia Mtu kutokujua maana nzima ya hiyo Sala.
Sasa wacha tuanze kwa kujua japo kwa ufupi  Nini Sala?, Sala ni(Maombi)ya Mapenzi ya Utiifu yanotokea Rohoni, Ni kwa ajili ya Shukurani ya kujua umeumbwa na mpaka wakati huo unasimamisha sala unathibitisha kwa yakini kuwa upo uwezo wa hali ya juu ambao hauna shaka ulokufanya  na kukupa wewe na vyengine nafasi ya kuufahamu na Kuabudu, Na sasa kwa unyenyekevu wewe binafsi umesimama kutokana na Uwezo huo usio ufahamu unasema "Allah Akbar", Wewe unakiri na kutaraji alokupa neema hizo zote azidi kukupa radhi zake za kuweza kukufunulia, kukufungulia zaidi milango ya fahamu na kwa mapenzi yake akupe uwezo wa kujua yalio zaidi katika ufalme wake.
Utaona nimetaja kufahamu na kutokufahamu kwa sababu kila ukenda (Deep)kwenye Sala yako mambo mepya yanafunguka, hisia tafauti zinaongezeke.
Hiyo ndio Sala ambayo unatanguliza shukurani kwa baraka na uwezo ulopewa wa kuweza kumfahamu yeye Mollah wako na kumtii, Sasa kwanini lazima uifanyie hifadhi sala yako, kabla ya kwenda mbele itabidi ujue tafauti ya (Kuhifadhi na Kulinda).
Kulinda ni tendo la nje lenye kuhakikisha hupati dhara, huibiwi, kwa ufupi ni tendo la nje, Lakini kuhifadhi maana yake ni kutunza,kua Muangalifu hicho kitu au jambo haliharibiki, kwenye kulinda unakua mtazamaji na kwenye kuhifadhi unakua muangaliji, kwa hiyo hifadhi ina mahusiano na tendo la ndani.
Ndio maana aya ikasema(Quraa-Baqarah-238)
"حَـٰفِظُواْ عَلَى ٱلصَّلَوَٲتِ وَٱلصَّلَوٰةِ ٱلۡوُسۡطَىٰ وَقُومُواْ لِلَّهِ قَـٰنِتِينَ "
Angalieni sana Sala(Zenu)na khasa ile sala ya kati na kati, Na simameni kwa unyenyekevu katika kumuabudu Mwenye enzi Mungu.
Kwanini ikawa Hifadhi na sio Linda? kwa sababu siku hizi umezuka mtindo unaambiwa linda, na mimi napiga kelele ili usiharibikiwe nakwambia hifadhi, unatakiwa Mja ukiipeleka sala yako kwa Mollah wako uwe mnyenyekevu na mapenzi ya hali ya juu, na hilo silioni kwa Waumin wengi, Sala zimeondoka nyoyoni mwetu na kilichobaki na kupatikana ni Sala ya njia ya nje kwenye taratibu za (Viungo), ndio maana unaona akimaliza Sala anatukana, akimaliza sala anafanya mzaha, akimaliza sala anakwenda kuiba, akimaliza sala anafanya zinaa, akimaliza sala anasema uongo, sasa hapo sala ipo wapi? vipi yanaweza kuwa maneno ya Mwenye enzi Mungu hayakamatani na matendo yako, inasema Quraan sura ya (Ankabut aya ya 45)
"ٱتۡلُ مَآ أُوحِىَ إِلَيۡكَ مِنَ ٱلۡكِتَـٰبِ وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ‌ۖ إِنَّ ٱلصَّلَوٰةَ تَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِ‌ۗ وَلَذِكۡرُ ٱللَّهِ أَڪۡبَرُ‌ۗ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ مَا تَصۡنَعُونَ "
Soma uliyoletewa Wahyi(Uliyofunuliwa)katika kitabu, na usimamishe sala, bila shaka Sala(Ikisaliwa itakiwavyo)humzuiliya (Mtu)mambo machafu na maovu, na kwa yakini Kumkumbuka Mwenye enzi Mungu(Ndani ya hiyo Sala ni jambo)kubwa kabisa, Na Mwenye enzi Mungu anayajua mnayoyatenda.
Aya imeweka wazi hapo mwanzo yasome yale yaloletwa kwenye kitabu, nenda (Deep) kwenye hiyo aya ulochagua kuisoma wakati unasimamisha Sala,(pengine ndani ya hiyo aya utapata maana itakayofungua jambo kwenye Akili yako)lakini wapi unasoma kama kasuku, hutulii ukachambua hicho ukisomacho, unasoma aya kama mazoea huku akili inapanga mambo mengine kabisa, ifanye Sala yako(Iwe mfano kama unavocheka, jiulize wakati unacheka kuna wazo lolote linaingia hakuna, na ukenda (Deep)kwenye kucheka utaona lazima yatoke machozi, kwa hiyo jua furaha na msiba viko pamoja na hivyo hivyo elewa kwenda (deep) kwenye Sala na kuepushwa na Maasi pia viko pamoja ila tafauti yako hujenda (Deep).
Endelea part 2


No comments:

Post a Comment