Asalaam Aleiykum
Unapata Darsa kama hii ili uzinduke, isifike siku ya maulizo ukashangaa unapewa Daftari lako unalikuta jeupeee, wakati mwenyewe unajijua kipindi hakikupiti. Sasa kama unataka kuijua hiyo sala basi wacha nikwambie Sala ni lile tendo zima lenye kukutanisha wewe na Mollah wako, kwa ajili hiyo haiwezekani mkutano huo ukawa kama vile unavyokutana na rafiki yako(Saboso).
Lazima uwe katika katika hali nyengine yenye matumaini na ilojaa mapenzi, usifanye jambo la Sala kwa njia ya dharau, na vilevile tambua ukiipeleka Sala yako kama ilivosemwa kwenye aya ilotangulia, ikawa ina nidhamu kamili iliyokamilika, basi kuna mambo yanapatikana kama hilo la kuepushwa na Maasi na Machafu, kupata zawadi ya kusamehewa kutoka kwa Mollah wako, Kupata zawadi za Baraka na furaha, Na utaanza kupata ishara za kuipata Sala kwa kuanza kuacha baadhi ya mambo kama, kuimba Taraab, kuangalia TV, baraza za kipuuzi, utaacha mambo mengi, na huko kuacha usije uka (Force)utapata maradhi, kwa sababu huko kuacha kuna njia mbili wacha nizitaje.
Njia ya kwanza ni ile ya (Force)kuacha jambo bado unalitaka, ndio maana utaona watu wengi wanaadhirika, Mfano unatangaza sasa hulewi tena, watoto wakikutania tu kwa ghafla unataka (beer)unaruka ile Bardii, yaani iwe (cold) Unasahau kama umeacha, au umekua Kizee mambo huyawezi. Halafu kuna huku kuwacha kwa aina ya pili nako ni (Natural) umekwenda (Deep) na mara (Prayer's happen to you) ita utakavyo umeombewa dua, siku hizi (Khamsa Salawati)la Muhimu ukenda (Deep)kwenye Sala unakua umefika kwenye (Source).
Kwa hiyo ukirudi kwenye jukwaa la Ulimwengu unakua Mtu mpya, mambo ya zamani yanaondoka, Lakini ukiacha kwa njia ya force mambo bado yanabakia kwenye Akili(Mind), lakini ukiwacha kwa njia ya (Natural)hakuna kinachobakia. Sasa ufanye nini kuitunza Sala yako?, Kuna mambo mengi yenye kukuzuia kwenda (Deep) kwenye sala yako. Sina haja ya kuvitaja vitu vyote hivyo lakini nitakwambia kwa ufupi ili uanze kuchukua tahadhari na kuweza kuitunza Sala yako.
Itabidi uanze mataarisho angalau dakika kumi kabla ya kuanza sala yako, lakini siku hizi tunaweza kufundisha vipi kujiandaa huku nje lakini mambo yanatokea Msikitini sekunde chache kabla ya kuanza Sala yenyewe, "Anasimama" Imam wetu wa leo na kuamrisha wekeni safu sawa na kuhakikisha hamuachi nafasi "Ibilis" kupita, basi muda huo huo akimaliza maneno hayo vitizame visa vinavyotokezea kwa Maamuma huku nyuma.
endelea part 3
No comments:
Post a Comment