Asalaam-Aleiykum.
Inaendelea kutokea sehemu ya pili,
Hakuna jengine litakalo kukujulisha hilo vazi la ndani la Ucha Mungu ila upitie sura ya (Tariq-aya-ya-5-7)
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَـٰنُ مِمَّ خُلِقَ (٥) خُلِقَ مِن مَّآءٍ۬ دَافِقٍ۬ (٦) يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآٮِٕبِ (٧)
"Na Ajitizame mwanaadmu, ameumbwa kwa kitu gani.Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa(Kasi).Yatokayo katikati ya mifupa ya mgongo na kifua(Mbavu)".
Wote tunaelewa maji haya yakishuka chini yanatengeneza (Uhai)kutokana na uwezo wa Mollah wetu, na yanatoka kwa wote wawili mke na mume,sasa leo nakwambieni pia yana njia nyengine maji haya yakipanda juu yanakuwa (Taqwa)Vazi la Mcha Mungu na hiyo ndio maana ya vazi hili,sasa usianze kunikamatia majambia pengine hujasoma mambo haya kwa Sheikh wako yafanyie uchunguzi huku ukiendelea kupata maalumati haya.
Katika Ulimwengu huu kuna kuna sheria mbili za (Nature)Yaani moja inaitwa(Gravitation)ambayo ina vuta kila kitu ardhini halafu kuna nyengine inaitwa (Levitation)hii inapandisha juu, katika sheria hii kila kitu kinapanda juu, lakini lazima kipate (Rehma)za Mollah wako, Maji ya Uzazi(Life Energy) yanatengenezwa pia na chakula yakija chini hii (life-Energy)inafanya kizazi,yakipanda juu yanakufanya uwe Mcha Mungu lakini kwa masharti yake;Ndio Maana Bwana Mtume s.a.w akasema "Ibada hazikubaliwi kabisa kwa muda wa siku arobaini ikiwa utakula chakula cha haramu(Taqwa)haiwezi kupatikana (system)haifanyi kazi na Mollah wetu katuhimiza katika aya nyingi(Mfano)(Baqarah-168)"Enyi wanaadamu kuleni vilivyomo katika ardhi, halali na vizuri,wala msifuate nyayo za shetani,bila shaka yeye ni adui kwenu".
Haiwezekani ufanye haramu, ule haramu halafu utarajie kuwa wewe Mcha Mungu huwezi kupata guo ukalivaa abadan, Amesema Bwana Mtume s.a.w Yoyote yule mwenye kupigana katika njia ya kutafuta kupata riziki ya halali basi atapata malipo kama yule alokufa kwa njia ya Mwenye-enzi-Mungu.Amesema Bwana Mtume s.a.w Yoyote yule atokula chakula cha halali kwa muda wa siku (40)basi Mollah wake ataungarisha moyo wake,na atamtia hikma katika moyo huo pamoja na ulimi wake, Bwana Mtume s.a.w katueleza kwa njia nyingi tu kama "alivosema:Ewe Umma wangu eleweni ya kwamba tumbo ni kama sehemu ya maji inotoa michirizi,na michirizi hii inapita katika njia za mwili ikiwa kitachopanda au kuteremka kikiwa halali basi mwili mzima utakua wenye kheri, na kikiwa kitokacho ni haramu basi hakuna kitofatia isipokua Maradhi matupu na shari, Masahaba baada ya kuijua siri hii walikua wakijitapisha na hadith ziko nyingi sana kuhusiana na kadhia hii,Alipewa Bwana mmoja Mcha Mungu chakula akakikataa, yule alompa akamuuliza imekuaje sahib yangu nimekupa chakula huja kitia mkono, akamjibu sili mimi isipokua chakula cha halali, Na kwa hilo moyo wangu unakua imara katika dini,nadumu katika ibada, na napata Ilham za Akhera, na kama nitakula haramu yoyote basi fadhila hizo zitapotea kwangu mimi,na hiyo ndio hali ya mawalii wacha mungu wanataka guo lao libakie safi halina dowa, Na siri hii ndio ilowafanya wakiristo wajipangie ule ukasisi kama inavosema Qur'aan-(Al-Hadyd-aya-ya 27).
ثُمَّ قَفَّيۡنَا عَلَىٰٓ ءَاثَـٰرِهِم بِرُسُلِنَا وَقَفَّيۡنَا بِعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَ وَءَاتَيۡنَـٰهُ ٱلۡإِنجِيلَ وَجَعَلۡنَا فِى قُلُوبِ ٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُ رَأۡفَةً۬ وَرَحۡمَةً۬ وَرَهۡبَانِيَّةً ٱبۡتَدَعُوهَا مَا كَتَبۡنَـٰهَا عَلَيۡهِمۡ إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ رِضۡوَٲنِ ٱللَّهِ فَمَا رَعَوۡهَا حَقَّ رِعَايَتِهَاۖ فَـَٔاتَيۡنَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنۡہُمۡ أَجۡرَهُمۡۖ وَكَثِيرٌ۬ مِّنۡہُمۡ فَـٰسِقُونَ (٢٧,
"Ikisha tukawafatishia nyuma yao Mitume wetu(wengine)tukamleta Isa Bin Mariam, Na tukampa Injili na Tukauweka upole na Rehema katika nyoyo za wale walomfata na huu Uruhubani(Utawa-Wanaume wasioe na wanawake wasiolewe)wameubuni (wenyewe)sisi hatukuyaandika hayo,(Waliamua wenyewe)ili kuitaka radhi ya Mollah wao, Lakini hawakuufata,kama INAVOTAKIWA kuufata, basi tukawapa wale walioamini miongoni mwao ujira wao,na wengi wao ni waasi".
Naam tupia macho neno katika aya hiyo neno hili(KAMA INAVOTAKIWA) hapo inakujulisha ipo (system)inayotakiwa kufatwa na hakuna njia nyengine isipokua (Saumu)funga ndio njia pekee inayobadilisha mwenendo huu baada ya kushuka chini maji haya yanapanda juu, ndio maana hapo mwanzoni ilipoteremka habari ya Ramadhani ikawa marufuku hata kufanya tendo la ndoa lakini watu ikawashinda japo kwa siku hizi chache za mwezi mmoja, ndipo ikashuka katika aya ya (187-sura-ya-Baqarah)أُحِلَّ لَڪُمۡ لَيۡلَةَ ٱلصِّيَامِ ٱلرَّفَثُ إِلَىٰ نِسَآٮِٕكُمۡۚ هُنَّ لِبَاسٌ۬ لَّكُمۡ وَأَنتُمۡ لِبَاسٌ۬ لَّهُنَّۗ عَلِمَ ٱللَّهُ أَنَّڪُمۡ كُنتُمۡ تَخۡتَانُونَ أَنفُسَڪُمۡ فَتَابَ عَلَيۡكُمۡ وَعَفَا عَنكُمۡۖ فَٱلۡـَٔـٰنَ بَـٰشِرُوهُنَّ وَٱبۡتَغُواْ مَا ڪَتَبَ ٱللَّهُ لَكُمۡۚ وَكُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ ٱلۡخَيۡطُ ٱلۡأَبۡيَضُ مِنَ ٱلۡخَيۡطِ ٱلۡأَسۡوَدِ مِنَ ٱلۡفَجۡرِۖ ثُمَّ أَتِمُّواْ ٱلصِّيَامَ إِلَى ٱلَّيۡلِۚ وَلَا تُبَـٰشِرُوهُنَّ وَأَنتُمۡ عَـٰكِفُونَ فِى ٱلۡمَسَـٰجِدِۗ تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ فَلَا تَقۡرَبُوهَاۗ كَذَٲلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ ءَايَـٰتِهِۦ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ (١٨٧).
"Mmehalalishiwa usiku wa Saumu kuingiliana na wake zenu, wao ni nguo kwenu na nyinyi nguo kwao,Mollah (wenu)anajua kwamba mlikuwa mkizihini(Mnapata taabu)nafsi zenu, kwa hiyo amekukubalieni toba yenu na amekusameheni, Sasa changanyikeni nao na takeni aliyokuandikieni Mollah(wenu)kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajiri katika weusi wa usiku, Ikisha itizimeni saumu mpaka usiku. Wala msichanganyike nao na hali (yakua)mnakaa itikafu misikitini,hiyo ni mipaka ya Mollah(wenu)basi msiikaribie, Namna hivi Mollah wenu anabainisha hoja zake kwa watu ili wapate kumcha(Kumtii).
Kama nilvoitaja wao wananguo(na huo ni mfano)kutokana na mwenendo wake wa kuenea mwili mzima na nyinyi mna nguo kwa ile kadara ya kushuka chini,kama ilivo kawaida ya kuvua na kuvaa, saumu ni njia moja ya kufanya (Energy)hii kupanda juu ndio maana ukaambiwa inakata matamanio, ndio maana ukaambiwa kakae msikitini usiipe nafasi (life Energy)hii kushuka chini katika mwezi huu, hebu ipe nafasi ipande juu, iwache ifanye kazi yake ili upate (Taqwa)ya Ramadhani, Jifunge usile haramu,na jiepushe na mambo ya kutizama mambo ya matamanio, Sasa nini kinatokea ikiwa utafanikiwa kutekeleza masharti yake likiwemo Riziki ya halali, Hapo utapata mambo haya,napenda pia uelewe hili ni vazi tu si vitendo itabidi ufanye vitendo kupata manufaa ya guo hili, dalili zake kama (life Energy)hii ishaanza kupanda juu utaona kwanza kabisa unakua mpole, unajaa huruma, imani inaongezeka, busara na hekima zinakushukia,unakua mtaratibu, mapenzi yanakuzidi kwa Mollah wako na Familia yako, utajiona unashiriki sana vitendo vya kheri, hata tabia zako kuelekea kwa mkeo zinabadilika, lakini yote hayo yanatokana na kula vya halali na saumu ilotimia ndio maana Bwana Mtume s.a.w "akawaambia wale vijana wasoweza kuoa juu yenu kuna Saumu na hiyo ni yenye kukata, ni (Method)ya kuzuia (Gravitation)kwani vijana wakiachiwa mtaani hapakaliki,na ikiwa watafunga vijana basi hapo itapatikana hiyo(Levitation)na panapatikana salama, vijana wanakua wacha Mungu, Kwani wewe hujui tafauti jee bado hujajichunguza(life Energy)hii ifanyavyo kazi zake, Inakuaje mmekaa kimya mnasoma darsa akiingia au akipita mtoto wa kike ndani ya chumba hali inabadilika mpaka akili hazifanyi kazi tena umepata kujiuliza kitu gani wakati ule kinatokea, basi kama bado anza uchunguzi wako,
Usije ukakubali maneno yangu bila ya kuyafanyia uchunguzi, usichukue maneno Sheikh kasema basi na wewe unayakubali laa fanya uchunguzi japo kwa wiki mbili jitahidi kuichunga (Energy)yako, jitahidi kula halali, halafu funga saumu yako, na kama chochote hakijatokea basi rejea kwangu uje kuniuliza mbona hakuna chochote, lakini shuruti zake ni hizo itabidi ujikaze katika kuzuia (life Energy)yako isishuke chini kila mara, na kama ni mwenye kuweza basi utaona hata Afya yako inaanza kubadilika, mapenzi yanakuzidi kuhusiana na mkeo, lakini ni lazima upate mapumziko, hapo maumivu yataondoka, matafurani yatapungua kwenye akili, usiwe mwenye kupoteza (life Energy)yako kipuuzi kila siku iache ifanye kazi zengine kwenye mwili na napenda ukumbuke haya yote hi khiyari na huu wangu ni ushauri, usije ukamkimbia mumeo au mkeo ukasema mimi nimesema laa tupo katika kuelimishana tunapeana elimu,wale wengine walokua hawajui wapate kufahamu.
Kazi yangu ni kukumbusha umuhimu wa maji ya uhai (life Energy)tulokua nayo katika miili yetu ikishuka chini(Creativeness)na ikipanda juu Vazi la Ucha Mungu(Holiness) na linalo subiri vazi hili ni vitendo vya kuelekea kwa Mollah wako. Nakumbusha tena Mzee wetu Nabii Adam a.s na Bi Hawa waliambiwa msiukaribie huu mti mkala tunda lake, na walipopinga ile amri wakafukuzwa peponi, na sisi Mollah wetu katupangia njia ya kurejea tena huko peponi, ndipo akatushushia (Vazi)la Ucha Mungu ndio iwe njia yetu, akatuwekea utaratibu wa kulivaa guo hili nao ni Saumu(Ramadhani)pia nguo hii ikipanda juu basi ina faida nyengine nayo inafanya(Repair)katika katika mwili inatibu maradhi mengi pasi nasi kujua,ndio maana tukaambiwa(Hakika ya hiyo Saumu ni kheri kwenu ikiwa mnajua), Kumbuka hapo mwanzoni (Shetani)Alituvua nguo hii na sasa tumepewa njia na Mollah wetu ili tuivae tena tupate kuwa kama hapo mwanzoni tuishi kwa salama na amani hapa ulimwenguni na huko akhera tuendapo.
Naomba Mollah wetu atujaalie tuifunge Ramadhani kwa salama, tulipate hilo guo(Nguo)ya (Taqwa)wakati wa itikafu yetu, ikisha atudumishe katika hiyo (Taqwa)wala guo lisituvuke milele inshaallah, Mwisho naomba ukumbuke ukiwa utakula haramu japo kidogo hupati (Rehma)hii ya Vazi la Ucha Mungu.
Mollah wangu anajua zaidi.
Abdulla Baja