Saturday, January 12, 2013

MADHARA YA DHULUMA PART-5

Asalaam Aleiykum,

Nini kinawifika hapa Ulimwenguni wale walo zama katika dhuluma, wenyewe hawajioni lakini wakitizama kwa makini wanaweza kugundua mambo mengi yanayo wafika katika nafsi zao mpaka familia zao na kama aya ilivosema wanapururiwa, lakini mifano ni mingi madhara yanopatikana ni makubwa, kwa sababu sheria ya Ulimwengu huu chochote unachotenda kiwe kibaya au cha kheri basi kuwa na hakika utalipwa hapa duniani na huko akhera uendako, ukidhulumu wewe basi ujue chaweza kulipa kizazi chako midamu kama wameshiriki katika dhuluma hiyo Mollah lazima apitishe hukumu yake na mfano wa kwanza utaupata katika sura ya Kahf aya ya 79-82.
(79)"Ama ile jahazi, ilikua ya maskini wanofanya kazi zao baharini, na nilitaka kuharibu, kwani mbele kulikuwa na Mfalme(anayedhulumu)anakamata kila jahazi(nzuri)kwa jeuri."
(80)"Ama yule kijana, wazazi wake walikuwa Waislam kamili, tukahofia kwamba asije akawapeleka(Wazee wake)katika uasi na ukafiri.
(81)"Basi tulitaka Mollah wao awabadilishie mtoto aliye bora kuliko yeye kwa kutakasika, na aliye karibu zaidi kwa huruma".
(82)Na ama ukuta, ulikuwa wa watoto wawili mayatima katika mji ule, na chini yake kulikuwa na hazina yao, na baba yao alikuwa(Mja) mwema, kwa hivyo Mollah wako alitaka wafikie baleghe yao wajitolee khazina yao, Hiyo ni Rehma inayotoka kwa Mollah wako, nami sikuyafanya haya kwa amri yangu, hayo ndio katika yale ambayo hukuweza kuyavumilia.
Ukisoma kwa makini utaona vipi Madhara utakayoyapata kama wewe utakua mtu wa dhuluma, Ama kuhusu hii safari alokwenda yule msemezwa na Mwenye-enzi Mungu Nabii Musa a.s na yule alopewa ilmu Nabii Hidhr a.s, Ilikua lengo lake kuonesha vipi dhuluma ilivokua mbaya na vipi Mollah wako anavo ikinga kwa wanyonge na anavoangamiza wabaya, Na vipi ukiwa mtu mwema malipo yake yanavoendelea hata ukiondoka katika Ulimwengu huu Mollah anahifadhi mpaka familia yako. Ili kutoonesha sisi vipi dhuluma ilivyo mbaya na madhara yake, Mtawala anadhulumu Raia wake basi bora Jahazi izamishwe, Mtoto atawadhulumu wazee wake kwa kuwatia kwenye maasi basi bora afe, atakuja mtoto mwengine,Na wale watoto mayatima wawili kwa kuwa baba yao alikua mtu mwema tu, basi umejengwa ukuta ili wasije kudhulumiwa hazina yao, Kwa hiyo hata kulinda kipande chako cha ardhi usidhulumiwe ni haki yako, na umehalalishiwa simama katika haki hiyo kama walivyo simama walio wema kupigania haki. Sasa nawaombea dua wale walokuwemo katika dhiki Mollah awaondoshee na awape subira kama alivompa Nabii Yusuf a.s, Na wale walopata madhara ya maradhi au majeraha basi Mollah awape shifaa na subira ya Nabii Ayub a.s, Mollah tujaalie ulowapa Uweza juu yetu sisi basi watie huruma na Imani watutendee haki katika matakwa yetu ya kidunia, na wakishindwa basi sisi tunarejea kwako kwa muongozo wenye kheri.Amin.

1 comment:

  1. Mashaa Allah makala nzuri, na maneno yake mazito. Tunamuomba Allah atuepushe na kila aina ya dhulma, sisi na vizazi vyetu na jamii muslimina.

    ReplyDelete