Asalaam Aleiykum,
Anasema Mwenye enzi Mungu "Enyi viumbe mimi nimejiharamishia kudhulumu, Ikisha nikajaalia baina yenu haramu kudhulumiana", Msifanye kabisa vitendo vya kudhulumiana. Na huku kudhulumiana kuko kwa aina nyingi na mbolea yake kubwa ya Mti huu wa dhuluma ni Uongo na Mateso, Waweza kumdhulumu mtu kwa kumdanganya na kuchukua Mali yake, waweza bure ukamsingizia mambo ya uongo au ukampiga ukachukua kilicho chake, Na pia unaweza kuleta visingizio vya ajabu na sababu zisizohusu ukamtia Gerezani pengine kulinda maslahi yako na hilo ni dhanbi kubwa katika dini hii ya Kiislam.
Nini anasema Bwana Mtume s.a.w katika Hadith iliyosimuliwa na (Muslim na Tirmidhy)kutoka kwa Abu Huraira r.a"Kasema Bwana Mtume s.a.w Jee mnamjua Muflis(Yule alofilisika)?""Wakajibu Masahaba muflis ni yule ambaye hana (Dirham-Pesa)wala starehe yoyote ile, Akasema Bwana Mtume s.a.w "Alofilisika katika umati wangu ni yule atakae kuja siku ya Kiyama na Sala zake, na Zaka zake na Funga yake na pia Hijja yake, Ikisha na huku anakuja kachukua Mali ya huyu, Kamshtumu (Kumsingizia)huyu, Kampiga huyu, Kamwaga Damu ya huyu, Basi yatachukuliwa yale Mema yake wapewe wale alowadhulumu na ikisha kama hayajatosha basi atapewa maovu ya wale walotenda alowadhulumu halafu achukuliwe huyo kupelekwa Motoni".
Hizo ndio hali zetu Waislam wa leo hao ndio alowataja Bwana Mtume s.a.w, Leo tunakua Mbele kusheherekea Dhuluma na huku tukiendelea kudhulumu na Ibilis anatwambia hapana neno mko wengi kila mtu ana sheherekea kwanini na wewe upitwe jiunge na kundi, na kitu kikifanywa na wengi wasiwasi unaondoka kabisa imekua sasa dhuluma kitu cha kawaida. Na sasa tumefikia Waislamu wenyewe kwa wenyewe tunaadhibiana eti kwa kuwaridhisha watu fulani kwamba sisi tuna uwezo hata wakukamata Waislam wenzetu na kuwaweka Gerezani(Jela) Na hakuna jambo zito katika dini hii kama mwenzio uliyekua unasali naye ukamsingizia uongo au ukamdhulumu kwa kumuweka Gerezani(Mahabusu)Tambua haipatikani nusura kwako wala usamehevu ikiwa kwa mbinu au mipango umempeleka Muislamu mwenzio ndani hususan ukijua hana kosa.
Sasa kwanini Ikawa hivyo? Tunaingia katika maudhui ya Dhuluma safiri na mimi ili upate kujua dhuluma ilivo na athari zake halafu ufanye bidii kuiepuka, Kwanza kabisa katika Uislam hakuna (Jela au Mahabusu) Nitataja sababu zake na hukumu mbili ili na wewe upate kutumia Akili yako kama unakubaliana nazo au unapinga.
Hukumu ya Jela Mwenye-enzi-Mungu kawatengea wanaadamu huko Akhera kama ilivosema Quraan sura ya (Mulk aya ya 7-8)
"إِذَآ أُلۡقُواْ فِيہَا سَمِعُواْ لَهَا شَہِيقً۬ا وَهِىَ تَفُورُ"
"تَكَادُ تَمَيَّزُ مِنَ ٱلۡغَيۡظِۖ كُلَّمَآ أُلۡقِىَ فِيہَا فَوۡجٌ۬ سَأَلَهُمۡ خَزَنَتُہَآ أَلَمۡ يَأۡتِكُمۡ نَذِيرٌ۬ "
"Watakapotupwa humo watasikia(sauti)ya Ngurumo(Kishindo cha Moto)lake na hali yakuwa unafoka(Mfano wa Volcano)".
"Unakaribia kupasuka kwa hasira(Kwa ajili ya wafungwa wanotumbukizwa humo)kila mara linapotupwa kundi, walinzi wake watawauliza jee hajakufikieni Muonyaji".
Naam hiyo ndio Jela Mollah kaiweka siku ya malipo hapa Ulimwenguni katupa adhabu za kufanya lakini tusifungane(Jela)ambazo nitazitaja kwa uchambuzi huko mbele, sasa kwanini tusipelekane (Jela) hapa duniani? Hakuna Shari kubwa ya Roho kama ukiinyima Uhuru wake, na kama unataka kuyajua hayo-Endelea Part-2
No comments:
Post a Comment