Sunday, January 27, 2013

MTAFUTA DINI,LAZIMA DUNIA IMPOTEE-PART-2

Asalaam Aleiykum,

Nini Dunia? ukimuuliza Mcha Mungu atakujibu Dunia ni (A state of  Unconsciousness)hali ya mvinyo, usahulivu, au ni ulevi wa kuilaza (Roho)Nikifafanua zaidi nina maana mambo yote ya kidunia ni yenye kukusahaulisha(Akhera)ambako ndiko kwenye maisha ya Dini na kusudio zima la kuumbwa kwako. Usije ukasema nini maana ya kuletwa hapa duniani basi, wala hujaambiwa usiishi, bali unachotakiwa ukumbuke uliko toka na ndiko unako rudi, sasa kama unajikaza kuwa wewe husahau uliko toka, tembelea mifano hii, halafu mwenyewe utajijua umesahau dini au unaikumbuka, jee unataka Akhera au hapa Duniani.
Yametuzonga maisha ikisha tumetawaliwa na Shetani(Ibilis)kakaa katika usingizi wetu hatuwezi kuamka hata yakipigwa (Matarumbeta)kila mmoja wetu ni kuhitaji mali, kila mtu anapigana ajenge nyumba, kila mtu anataka apate mwanamke huyu au mwanamme yule, wengine wanahitaji dhahabu, wengine wanaabudu biashara na pesa, wengine ibada zao mipira, wengine wanasujudu kwenye muziki, wengine ndio wamejitosa katika bahari ya siasa wako tayari kuzamisha wenzao lakini wao wakae juu, kuna baadhi wamekita katika dhuluma, na wengine ni wenye kuhitaji vyeo kwa hali yoyoyte ile lazima akipate, na wako wengine ni wenye kusuguliwa roho na watoto tu, halafu na wengine maisha yao yamekua baina ya kazini na kwenye TV lazima vipindi vyake visimpite, huyu hana jengine, na haya kwa uchache ndivyo yalivyo maisha yetu na kila mmoja kazongwa na(drugs)yake hawezi kuiacha hao wote nilowataja na wengine nisowataja ni wenye kuhitaji dunia, Na Mwenye-enzi-Mungu ana wakidhia mahitajio hayo (Alhamdullillah).
Anawapa magari, na anawapa majumba na kila wanacho hitaji hao wanaendesha maisha yao(Unconscious)huku wakiwa wamelala, na kuna wengine wasopata usingizi mzuri hapo tena wanatafuta mirungi, pombe, na aina zengine za (drugs)ili wapate kukoroma vizuri.
"Enhe sasa wepi wenye kutaka Akhera"" Aya ikaendelea wenye kutaka huko Akhera tutawapa huko, ikamalizikia kwa kusema na kwa yakini tutawalipa wenye kushukuru" Nani hawa wenye Kushukuru? Na kwanini wakatajwa hapa, hawa ni wale wenye kuishi maisha yao(With-Conscious)Hadhir, wako macho, hawako ndani ya usingizi, Nini tafauti na wale walolala, Huyu kagundua kwamba dini ni maisha ya kudumu, huyu Imemjia nuru ya fahamu na kuona kwamba mauti yakija yanachukua kila kitu, lakini kuna kitu mauti hakichukui nayo ni (Life)hichi nabaki nacho, sura ya Mulk aya ya 2 "ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلۡمَوۡتَ وَٱلۡحَيَوٰةَ لِيَبۡلُوَكُمۡ أَيُّكُمۡ أَحۡسَنُ عَمَلاً۬‌ۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡغَفُورُ"
"Ambaye ameumba Mauti na Uhai ili kukujaribuni(Mtihani)ni nani miungoni mwenu mwenye vitendo vizuri, na yeye ni Mwenye Nguvu na Mwenye Msamaha".
Yeye huyu kafahamu yakuwa Mauti na Uhai ni mpito katika njia ya maisha(Life)na anajua hakuna tena kifo huko anapo rejea kama ilivyotajwa katika sura ya Ad-dukhan aya ya 56,
"لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلۡمَوۡتَ إِلَّا ٱلۡمَوۡتَةَ ٱلۡأُولَىٰ‌ۖ وَوَقَٮٰهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ "
"Humo hawataonja mauti ila mauti ya mwanzo, Na atawalinda na adhabu ya Jahanamu"
Kwa hiyo baina ya Uhai na Mauti kuna (Life)Maisha, ukigundua hili ndio umegundua dini, kwa hiyo unaweza kuishi hayo maisha hapa Ulimenguni na huko Akhera uendako, tafauti yake uelewe kuwa kumbe maisha ni safari, na wewe umo safarini na katika safari hii unaruhusiwa kufanya biashara ukachagua malipo ulipwe hapa au huko unapokwenda, uchaguzi unao mwenyewe na huo uchaguzi huupati mpaka uwe (Conscious)Hadhir, ni lazima uwe macho masaa ishirini na nne, na umacho wenyewe ni hiyo (Dhikr)Kukumbuka.
Na huku kukumbuka kuna darja zake ambazo unaendelea kuzipanda kila ukizidi kukumbuka, na kila ukipanda darja unapata ufunguo wa kujua ya kwamba hili nilochagua mimi linanipeleka katika uhai wa daima, unapata kujua pale inapotokea furaha, unapata kujua pale inapotokea afya na hapo ndipo unapoipata dini na dini haina mwisho, unaanza kuwa Mcha Mungu wa kweli na kidogo kidogo Dunia inaanza kukupotea, unakuwepo duniani lakini unaishi kidini, Mali ipo lakini haikulevi wala kukusahaulisha, dhahabu zipo huna shauku nazo, zikiibiwa sawa zikiwepo sawa, maradhi yakija sawa, afya ikiwepo sawa, kila kitu unamwachia Mollah wako.Endelea-part-3

No comments:

Post a Comment