Asalaam Aleiykum,
Hapo tena unajua kumbe maisha ni kitu kinachokaa ndani, si kitu chenye kutegemea matukio ya nje, vitu vya nje vyote vinakwenda na kubadilika, isipokua nafsi yangu, Na mtu ukigundua nafsi yako unakua tajiri wa maisha, Sasa vipi inatokezea kuitambua nafsi yako?. Imehimizwa katika dini suala la kukumbuka, kwanini ikahimizwa? kwa sababu kadhia ya kukumbuka ni ngumu sana, mfano ni kama huu (ukimtizama mtoto wako basi kumbuka na wewe unotizama)fanya japo kwa saa chache tu ikiwa utaweza basi wewe rahisi kukipata hicho ninacho zungumza, lakini ni vigumu sana, ndio maana ukaambiwa Tajiri vigumu kuingia peponi kwa sababu ni vigumu kukumbuka Mollah na faida kwa wakati mmoja.
Ukiweza Kuishi hivyo ina maana wewe unaishi Hadhir(Conscious)umacho, binaadamu tuko katika shughuli ya kukumbuka kitu kimoja aidha unakumbuka mali, au hukumbuki chochote, fikra zetu ziko sana katika dunia, huwezi kuwa na mali halafu ukamkumbuka Mollah wako tabu sana, huwezi kuwa na cheo ukamkumbuka Mollah wako vigumu mno, utakwenda kutisha mara moja moja misikitini lakini hupo kabisa, unafata kundi tu huku umelala, na huwezi kuwa maskini na huku ukamkumbuka Mollah wako, sababu fikra zote ukakope wapi, utakula nini, ufanye nini, itakuaje mpaka uamue au ukujie muongozo yakua sasa nataka kuitafuta dini, na uwe tayari dunia kukupotea, na kama nani anotaka dunia impotee?.
Tizama nini imekua hali zetu, mahusiano yetu yote ni matendo ya nje. hakuna hata mmoja mwenye kutaka mahusiano ya ndani na nafsi yake, tunazihusisha furaha lazima kipatikane kitu cha nje, iwepo kitchen party mtu ndio afurahi, na kuna wengine ndio wana maradhi kama hakupata kwenda barazani anaumwa, imekua baraza muhimu kuliko familia yake, anaweza mtu kupuuza kitoto chake kinaumwa lakini lazima akahudhurie barazani, furaha yake yote inategemea baraza, na wale wagonjwa wenzie kama hawajamuona na wao hawana raha, wanakuja kumuuliza vipi leo baraza haijachangamka hujaonekana, hivi ndivyo furaha zetu zilivyo, hasara ilioje, lau tungejua furaha inatokea ndani sio nje, kama vile afya inavo tokea ndani sio nje, mwenye furaha ya kweli ni yule anayefata dini, wala hana haja ya dunia, anacheka akiona watu wanavyo hangaika kujenga majumba ikisha hao wanakufa, kukimbilia vyeo ikisha vinawatokea puani, Mtafuta dini yupo anaishi Ulimwenguni lakini dunia ishampotea zamani hana haja nayo, yeye anaishi maisha tafauti kabisa sio ya wale wenye kubadilisha tabia kabla hawajapata dini, ndio utaona maonesho makubwa lakini maskini nafsi zao hazijabadilika, nje anafata maisha ya dini, lakini ndani kajaa dunia anakaribia kuanguka, kwanza badilisha nafsi yako ikisha tabia itafatia, usipite ukasema husikilizi muziki halafu kichwani kutwa unaimba, hutizami TV story zote za michezo unazijua, usibadilishe tabia kwanza badilisha nafsi, tabia zitafatia, na tabia zikifatia unakaa katika mizani unakua kati kati huyumbi tena, unajua mali zipo nje na watoto wapo nje, lakini Mollah wangu anakaa moyoni, hapo tena unakua unaishi ndani na nje na ukianza kuishi hivyo kidogo kidogo dunia itaanza kukupotea mpaka kuna siku inabaki dini pekee hapo unakua(Wake-up)umeamka umeshahama kwenye usingizi, ndio maana utaona mambo yakiwa mengi kichwani hupati usingizi na dini ikikujaa kichwani hulali tena usingizi wa kidunia. Naumomba Mollah wetu atuamshe katika giza hili totoro-Amin.
No comments:
Post a Comment