Saturday, January 12, 2013

MADHARA YA DHULUMA-PART-2

Asalaam Aleiykum,

Ukachukua Roho ya mwenzio na kuifunga pahala pamoja ikawa haina Uhuru, hilo ni Dhuluma kubwa kwa Binaadamu mwenzio ndio maana utaona Nabii Yunus a.s alipowekwa ndani ya tumbo la chewa kwa siku tatu tu akawa anaomba usiku na mchana anusuriwe
"وَذَا ٱلنُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَـٰضِبً۬ا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقۡدِرَ عَلَيۡهِ فَنَادَىٰ فِى ٱلظُّلُمَـٰتِ أَن لَّآ إِلَـٰهَ إِلَّآ أَنتَ سُبۡحَـٰنَكَ إِنِّى ڪُنتُ مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ "
"Na Dha-Nun(Yunus)(Mtaje)alipoondoka huku amechukia, na akadhani ya kwamba hatutamdhikisha, basi (uzito wa Roho ulipomzonga)aliita katika giza(ndani ya tumbo la chewa)(Akasema)Hakuna aabudiwaye isipokua wewe, (uliye) mtakatifu, hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu".
Sasa huyo ni nabii kakaa siku tatu tu na inatajwa hali hiyo ni ya (Kumdhikisha)akakiri mwenyewe kadhulumu kwa hiyo anaomba atolewe nini hali yetu sisi tunowekana ndani bila ya kuwa na uyakini kama kweli hao tunao waweka ndani wana hatia au wamesingiziwa tu, Mambo ya kuwekana ndani ni dhuluma kubwa watahadhari wale wenye kufurahikia wenziwao wanoteseka hapa Ulimwenguni basi wajiandae wao kuteseka huko Akhera, mambo ya ndani ni magumu ndio maana hata mtoto akifika miezi 9 hakai tena tumboni  anapiga mateke ili apate kutoka.
Sasa kwanini dini ya kiislam haikuweka (Jela)kisome kitabu cha haki na Umsikilize nini anasema Hakim wa siku ya Mwisho adhabu gani peaneni hapa Ulimwenguni ili matatizo yote yaondoke, kwani huko kuwekana (Jela)Takwimu zinasema wezi wanaendelea kuwa wezi wakitoka, majambazi wanaendelea na kazi zao zile zile hakuna mafunzo yoyote yanayo wageuza wakitoka humo ndani, sasa nini habari yetu sisi wale walotiwa ndani bure tunajenga au tunabomoa kabisa, isome kwa ufanisi Hukumu ya Mwenye-enzi-Mungu, ambazo baadhi ya watu wanazitilia mashaka na kuzishtumu katika dini hii:Anasema Mwenye enzi Mungu katika Quraan sura ya Maidah aya ya (38).
"وَٱلسَّارِقُ وَٱلسَّارِقَةُ فَٱقۡطَعُوٓاْ أَيۡدِيَهُمَا جَزَآءَۢ بِمَا كَسَبَا نَكَـٰلاً۬ مِّنَ ٱللَّهِ‌ۗ وَٱللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ۬"
"Mwizi mwanamme na Mwizi mwanamke, Ikateni mikono yao, malipo ya yale waliyoyachuma, ndio adhabu itokayo kwa Mwenye enzi Mungu na Mwenye enzi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye Hekima"
Sasa kwanini ikabidi akatwe kiganja chake? hapa pana hekima gani? pata maalumati haya ujuwe kwanini Mollah wako akatoa adhabu hiyo, Wallahi hakuna (Profession)kazi yenye kulaza na kuwa na Raha na iliyo rahisi na utamu kama wizi, Ndio maana utaona mwizi hawachi kazi yake, midamu kiko cha kuiba iwe serekalini au dukani au kwenye nyumba basi hawachi abadan.
Sababu ya wizi unaingia (Deep)kwenye Roho ya mwanaadamu na hakuna kiingiacho (Deep)ndani ya Roho ila kinakwenda kukulaza sasa kuamshwa kwa Roho lazima kipatikane ama machungu au mshituko au muamko(Awaken)ili apate kuzinduka, na vipi atazinduka basi akatwe kiganja chake na ili wengine wapate hiyo (Awaken)muamko, ukiona mwenzio hana kiganja hata ukitaka kuiba utafikiri mara mbili uchukue au uache, hiyo ndio hekima ya Mwenye-enzi-Mungu. Na pia tambua kulala kuko kwa aina mbili aina ya kwanza ni kulala kwa (Body)mwili na kulala kwa aina ya pili ni kulala kwa Roho ndio maana ukitaka kumumsha alo lala unamtingisha amka amka, sasa ukikatwa kiganja ndio unaamka moja kwa moja hulali tena kwa maana (utaogopa kuiba).
Na Wazinifu pia Roho haziamki mpaka apigwe mijeledi mia, na mpigaji lazima apatikane Baba kubwa la miraba sita litumie nguvu zote ili kuiamsha Roho, na watakao shuhudia hukumu hiyo kila mtu akili yake itakaa sawa, atajua nikikamatwa nimeumia, Hiyo ndio hukumu ya aliyetuumba. Sasa wanaadamu wakikataa hukumu hii nini kinafatia, Wanamchukua mzinifu wanampamba kwa mashada ya maua na cheo na sifa nyingi pamoja na mazawadi, halafu maskini wanamchukua mwizi wanamdhulumu Roho yake, Mwenye enzi Mungu kasema mkateni mkono nyie mnaua na kila anoshiriki kumpiga mwizi akasababisha kifo chake basi ajijue kadhulumu na yeye atahukumiwa kwa kosa hilo. 
Sasa kuna wengine watasema hee mbona adhabu yenyewe kali hakuna ya Tahfif, nyepesi kidogo ya kuweza kuwacha huu wizi, mbona hukumu kali mno, basi kulala huku hakuna njia nyengine ya kuamshwa ndio lazima upigwe mikwaju na ukatwe mkono?
Naam ukitaka kujua njia nyengine-Endelea-part-3

No comments:

Post a Comment