Asalaam Aleiykum,
Sasa kamatana na mimi mkono kwa mkono twende kwa daktari wa Akili zetu halafu tukifika tujiulize nini kinatokea wakati tumesimama tuna Sali, ukitaka usitake kuna mambo matatu yanatokea, Jambo la kwanza unasoma sura ndani ya Quraan kwa njia ya (Automatic)(1)halafu Akili iko kwengine kabisa, pengine unafikiri nitakula nini, au kama unakwenda harusini ndio manyago matupu, au mpira umeanza unasikia watu wanashangiria itizame sala yako inakuaje(2)na la Tatu ambalo hilo ndio linalotakiwa litende hicho kitendo chenyewe cha Sala ni pale unaporejea kwa ghafla ukajisuta mwenyewe kuwa ulikua umesafiri, kuna kitu kinakukumbusha ewe mja we, wewe unasali, upo mbele ya Mollah wako wewe, hapo unarejea na inakutoka (Allahu-Akbar)kubwa ikisha huyo (Una-Rukuu)hapo unaporejea huyo ndio wewe na huyo ndio hili jambo la (3)ambalo unatakiwa uwepo kwenye Sala nzima katika hiyo namba(3)lakini hukai hata sekunde (10)mara huyo ushakimbilia kwengine.
Inapatika hali hii ya fungu la tatu(Mfano)pale Sheikh anaposoma ukalia, au ukicheka au ukirejea mwenyewe katika hizo sekunde chache, ninacho himiza hapa basi ikiwa wewe ndio mbovu wa mawazo hayo, basi tafuta mawazo yenye kheri na dua zilizo nzuri, ili kila ukenda kwa Mollah wako uwe umejitahidi mpaka pale utakapofika kutekeleza Sala kwa ukamilifu isiyo na mawazo wala mahitaji, pale ambapo Mtume s.a.w alipomrejesha yule kijana asali tena mara tatu, pahala pale ambapo Nabii Isa a.s. alipoulizwa na wanafunzi wake vipi unasali alianguka moja kwa moja na kusujudu.
Sala ni mapenzi makubwa juu ya Mollah wako, uwe tayari kuvikosa vyote iwe mali yako au watoto wako au mkeo, uvikusanye vyote kwenye gunia uwe tayari kuvitosa baharini kwa ajili ya Mollah wako, uwe unajua hivi vyote wewe ndie muumba wake namie niko tayari kuvikosa au vinikose kwa ajili yako Mollah wangu. Kumbuka kisa cha Nabii Ibrahim a.s sura ya As-Saffat-102-112"Alipoota kumchinja mwanawe hakusita kwa mapenzi ya Mollah wake mpaka ilipoletwa fidia ya mnyama ili atoe sadaka"Muumin ndio unatakiwa uwe katika hali kama hiyo kwa ajili ya Mollah wako, wewe hujaambiwa kuchinja ila unatakiwa uende kwenye hiyo sala japo kidogo umejawa na mapenzi, japo kidogo kila kipindi cha sala uwe na hamu ya kukutana na kuzungumza na Mollah wako, uwe na shauku ya kumhadithia yalo kukera na kukufurahisha na yupi alokukosea umemsamehe kwani na wewe kila kipindi cha hiyo sala unasamehewa kutokana na mapenzi ya Mollah juu yako, vipi unasamehewa? pata maana ya udhu kwa undani ili sasa ukenda kutia udhu uwe muangalifu, uache maneno ya kipuuzi, uwache habari zote za kidunia.
Nini Udhu?
Udhu una (Symbol)alama mbili kwako Binaadamu, kama ilivyo nguo, ukivaa ya kike na ya kiume unavo tafautisha tabia zako, au Nurse akivaa nguo za kawaida na akivaa (uniform) yake anavobadilika na shindano lake mkononi, au Mwanajeshi akiwa na nguo za kawaida au za kazini tabia inabadilika kabisa. Sasa ikiwa nguo zinakwenda (Deep) na kumbadilisha mtu tabia, nini habari yetu sisi kuhusiana na (Udhu)Alama hii ya udhu inaashiria mambo mawili, yepi endelea-part-3
No comments:
Post a Comment