Sunday, November 10, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU (ALIIM) PART 2

Asalaam Aleiykum,

Naam nini  Elimu? Elimu ni (Gathering of Information) unakusanya huku na kule ikisha una hifadhi kichwani mwako, Na mwanzo wake imetokea kwenye hiyo (Source) na kutiwa katika Roho yako, Halafu tena wewe mwenyewe unafanya (Transfer)  kuipeleka kwenye akili, Na hapo ndio unaanza Ku(Shared) na watu wengine.
Lakini Ujuzi unaweza kubakia peke yako kama hutakai kuugeuza elimu, ikawa unajua mambo hayo ya siri pekee. Na anokupa Ukarim huo wa kujua hakuna Mwengine isipokua Yeye Mwenyewe (Yaa Aliim)Mjuzi wa kila kitu. Yeye ndie anaejua kila kitu kitokeacho Ardhini na Mbinguni, Kifanyike Baharini au Nchi kavu hakitokei bila ya Idhini yake au yeye kukijua.
Basi ikiwa hali yenyewe ndio iko hivyo ajijue kiumbe huko kufichaficha kwake na kufanya siri anajidanganya mwenyewe kwa mambo anayaofanya hali ya kuwa anajua fika Mollah wake anafahamu kila kitu.
Basi Niombeni kwa ajili ya Jina hili la (Aliim) ili mpate ujuzi zaidi wa kumfahamu Mollah wenu na Ulimwengu huu mnaoishi kwa Jumla, Ikiwa kwa Ukarimu wake kakufunzeni bila ya kumuomba, Nini Habari yenu nyinyi kama mtamuomba kwa dhati ya nafsi zenu, Basi kuanzia leo ikiwa mwenye kutaka kujua jambo la kheri utumie jina hili la Yaa Aliim kwa idadi nyingi kabisa huku unataja hilo kusudio lake uone faida zake. Na ulikumbuke jina hili kabla ya kulala, kuwa ukilala na jina hili, kuna mambo mawili yatatokezea ima utaamka ushapata jawabu au ufumbuzi, au utapewa habari kwa njia ya ndoto, Tunamuomba Mollah wetu atuzidishie ujuzi wa kumjua yeye na kumuabudu pasi na makosa, na huku tukitii amri zake.

No comments:

Post a Comment