Sunday, November 3, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(BASIRA)PART 2

Asalaam Aleiykum,

Kwanini kila ukitizama Mbinguni huoni tafauti na wala hizo Mbingu saba , Kwa sababu kuona kwetu viumbe kuna daraja au kikomo, ndio maana ndege ana kiasi chake, kuku ana kiasi chake, samaki ana upeo wake wa kuona, na yote hayo yamemilikiwa na mwenyewe mwenye huo Ufalme wa kuona, Lakini wewe Mwanaadamu kiumbe chake alokufanya Khalifa kwenye Ulimwengu huu kakupa zawadi ya kutizama isiyokua na kikomo.
Na ndio maana kwenye hiyo aya imetajwa tizama na wala sio angalia, Basi kafanye majaribio hayo ya kutizama ukimaliza kusoma, Nenda Nje angalia Mbingu au upande wowote usokua na kizuizi cha Miti au Majumba utajua siri hiyo ya upeo wako usokua na mwisho.
Picha au (Telescope)zinachukua (Still Image) kutokana na mafundisho yako, wewe unaona na kuweka kumbukumbu kutokana na uwezo na mafundisho ya Mollah wako, Yeye pekee ndio Mwenye huo uwezo na Ufalme wa Kuona, Na katika kuona huku kupo kwa aina mbili unaweza kuona Nje na ukipata mafundisho ya kuondoa pazia basi utaona na ndani(au mambo ya siri),  hivi sasa unaona lakini bado pazia limekufunika, labda mpaka siku ya kufa kwako ndio huondoshwa hilo pazia ukawa unaona pasi shaka na hicho unacho kiona, Kwa hiyo fanya hima katika kuona kwako ili utumie jina hili la Basira likuondoshee pazia na uyaone mambo makubwa makubwa yaliyo mazuri katika Ulimwengu huu.

No comments:

Post a Comment