Sunday, November 3, 2013

MAJINA YA MWENYE ENZI MUNGU(BASIRA) PART 1

Asalaam Aleiykum,

(Basiran) Mwenye kuona, Kabla ya kuendelea na jina hili wacha tujue tafauti ya kuona na kutizama, kutizama ni kitendo cha kuwepo mbali ukawa unaangalia, Kuona ni kitendo cha kuwepo karibu na ukawa unashuhudia, Na shahada ni jambo la yakini halina wasiwasi, kutizama inaweza kuwa yule ndie au siye huna uhakika, lakini kuona unasema moja kwa moja huyu ndie, hiyo ndio tafauti yake, Sasa hii sifa ya kuona imekusanya kila jambo linaonekana (in detail)kuona huku hakuna pazia wala kikomo, tunapo zungumza kuona huku si kule kuona kwa kawaida unavofahamu mimi na wewe, kuona huku kwenye kutajawa hapa kuna muhusu yule ambaye amejaalia huku kuona, kwa hiyo isije kukutuma akili yako ukadhani anaona kama unavoona wewe, hizo zako ni (tashbiha)umeletewa ili upate kutumia hilo jina la kuona kwa ajili ya maombi yako.
Usije ukazuka nakuanza kufikiri anaona kwa macho gani, usifananishe kabisa na kitu chochote, (Basira)Mwenye kuona, Kumekua kuona huko ni alama ya kuwepo na kukienea kila kitu, huna wakati au sehemu ikawa huonekani, ikiwa upo peke yako yeye wapili wako(Na kuna Method ya kulijua hilo ukifikia upeo fulani wa kufahamu utafahamishwa)Yeye ni Mwenye kukiona kila kila kitu kwa undani wake, hakuna chochote kiwezacho kuepuka kutoonekana na Mollah wako.
Yeye ndiye aliyekupa Roho na anakuona ndani ya hiyo Roho, Vipi linakua tukio lenyewe, Napenda ieleweke kuwa kitendo cha kuona ni (Temprory)katika matumizi ya macho, lakini ni cha kuendelea kwenye matumizi ya kiroho ndio maana ukilala unaendelea kuona ndoto zako, kwa hiyo inayoona ni hiyo Roho. Kwa hiyo hilo tendo limeitwa Jaala kwa sababu mara nyingi unaondoshewa hata katika hiyo Roho huoni kitu(Ndio unaamka na kusema leo nimelala fofofo, Kwa hiyo yeye ni mwenye kumiliki huko kuona, ndio maana akakwambia kwenye surat(Mulk 3-4)
مَّا تَرَىٰ فِى خَلۡقِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ مِن تَفَـٰوُتٍ۬‌ۖ فَٱرۡجِعِ ٱلۡبَصَرَ هَلۡ تَرَىٰ مِن فُطُورٍ۬ 
"Tizama katika Uumbaji wa Rahmani huoni tafauti (Yoyote)Rejesha macho (Yako utizame)jee unaona kosa"
ثُمَّ ٱرۡجِعِ ٱلۡبَصَرَ كَرَّتَيۡنِ يَنقَلِبۡ إِلَيۡكَ ٱلۡبَصَرُ خَاسِئً۬ا وَهُوَ حَسِيرٌ۬ 
"Tena rejesha macho(yako)mara nyingi zaidi, jicho lako litarudi hali ya kuwa limehasirika na umechoka"
Tizama, sababu Mbinguni  mbali, kwa hiyo nyanyua jicho utizame kama utaona tafauti yoyote, halafu ukaambiwa tazama tena na hali utarejesha jicho lako ukiwa hasarani, kwa sababu huko kuona kakupa yeye Mwenyewe uwezo huo , Na hizo mbingu saba kazitengeneza yeye, Basi kama unazitafuta.Endelea Part 2


No comments:

Post a Comment