Asalaam Aleiykum,
Leo nimetamani kukupeni zawadi hii nikiwa na Imani na kuamini kama Mtu atayafahamu haya ninayo andika basi atapata faida ya kujua mambo kwa upeo mwengine kabisa, Atatumia mtu somo hili ndio iwe njia ya kumbadilisha au kubadilika kama atavotaka. Tukijaaliwa tutazipanda ngazi hizi moja baada ya nyengine kwa utaratibu ili tupate kujua katika kila ngazi kuna hazina gani na kama kuna faida na hazina hizo.
Pia napenda ufahamu inayopanda hizo ngazi ni (Roho)na wala sio Mtu ana madevu meupe, Na nikisema (Roho) wengine watataka kuitafuta waone inapanda vipi, hivyo ndio Binaadamu alivyo, lakini kama utasoma kwa makini utakujia ufunuo wa kufahamu kusudio la ngazi zenyewe na utapata kujua vipi hiyo (Roho)inavopanda. Ili kufahamu kwa undani zaidi itabidi tuanze na aya ya mwanzo iloteremka katika kitabu kitukufu Quraan, ili ituoneshe hizo ngazi zenyewe ziko wapi.Sura ya Alaq aya ya 3
ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ
Soma Mollah wako ni Karim(Mkarimu)
Umepatikana Ukarimu mkubwa kama utazingatia kwa makini, Amehadithia "Anas kasema Bwana Mtume s.a.w hakika ya Malaika wanasema"Mwenye enzi Mungu katuumba sisi, Ikisha kamuumba Mwanaadamu""Akamjaalia kula Chakula, akaweza kunywa vinywaji, akawa mwenye kuvaa nguo, Akawapa Wanawake, wakawa wanapanda wanyama,Wakawa wanalala na kuamka," Na wala hatukujaaliwa sisi chochote katika hayo, Akawajaalia Dunia ikisha baada yake kuna Akhera. Akajibu Mollah wako "Nimemjaalia yule niliyemuumba kwa mikono (Uwezo wangu)Ikisha nikampulizia (Roho)inayotokana na Mimi, kama alivosema Kuwa ikisha Ikawa".
Basi soma kwa ajili ya Mollah wako aliye Mkarimu, katika hadith hiyo Malaika wanaanza kukuonesha njia wanakumurikia (Torch)zione fadhila za Mollah wako kwenye ngazi hii ya kwanza, unaweza kuzingatia hayo, yanaingia akilini moja baada ya jengine, basi ikiwa ushaona njia soma aya ya 4 ya sura hiyo hiyo ili tuanze kupanda ngazi.
ٱلَّذِى عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ
Ambaye amemfundisha kwa Kalamu(Akili)
Nani Mfundishaji ? Mollah wako, Nani anae fundishwa Mwanaadamu, mafundisho hayo yanapita au kuingia kwenye hiyo Akili, kwa hiyo utagundua mafundisho yanatokea ndani, hapa itabidi tufahamu tafauti ya mafundisho(Understanding) na Elimu (Knowledge) utagundua (Understanding) inatokea ndani na Elimu (Knowledge) inatokea nje lakini pia ni matunda ya (Understanding)lakini naita ni (Dead Memory)(Understanding)ni (New Memory)mambo ya nje ni yenye kupandikizwa katika hiyo Akili, ndio utakuta unaambiwa kwa Mollah inapatikana (Hekima) na kwenye hizo (School, College, na Uni)zinapatikana hiyo Elimu ambayo ni Mamillion ya copy za Akili za watu ziloandikwa kwenye vitabu.
Lakini Ufahamu sahihi unatoka kwa Mollah ambaye kasema katika sura ya Taha aya ya 98.
إِنَّمَآ إِلَـٰهُكُمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِى لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَۚ وَسِعَ ڪُلَّ شَىۡءٍ عِلۡمً٨
Hakika Muabudiwa wenu ni Mwenye enzi Mungu tu, ambaye hakuna aabudiwaye kwa haki ila yeye, Amekienea kila kitu kwa Elimu.
Ukiweza kulijua hilo kuwa Mwenye enzi Mungu amekienea kila kitu kwa Elimu, ndio sasa utaingia na kuifahamu uzuri aya inofatia ya sura ya Alaq aya ya 5 ili tupate kujitaarisha kuipanda hiyo ngazi ya kwanza. Endelea part 2
Sunday, February 23, 2014
NGAZI SABA ZA ROHO PART 2(NGAZI 1)
Asalaam Aleiykum,
عَلَّمَ ٱلۡإِنسَـٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ
Amemfundisha Mwanaadamu (Chungu)ya Mambo aliyokua hayajui.
Mtizame Mtoto na vimacho vyake anavokuja katika Ulimwengu huu, akizaliwa tu maskini hajui chochote anaangaza huku na kule, kama kusema Akili yangu tupu sasa anzeni kujaza mambo yenu, lakini Mtoto (Hodari)anasikia pande zote mbili, anasikia mafundisho yanotoka kwa Mollah wake, na kusikiliza pia yanotoka kwenu, Na hivi ndio sote tunavofundishwa tokea kuzaliwa mpaka tunaingia kaburini, lakini tunafika pahala, tunasahau kusikiliza upande wa pili(Nyimbo, Ngoma,siasa zinatushughulisha)unakua husikii tena hayo mafundisho japo yanaendelea kuja(stage by stage)hiyo haki yako lazima uletewe lakini hutaki, wewe unashughulika na Elimu ya nje, umeambiwa (Elimu bila ya malipo) na kila mtu anapenda kitu cha bure, hapo tena unaanza kujazwa Mbinu za wizi, vipi utadhulumu, kuna njia ngapi za uongo, hata ukitimia miaka 21 wewe ushakua (Expert)unakabiziwa cheti unakua mtaalamu wa mipango yote, tizama sasa uharibifu unofatia unadumu na elimu hiyo mpaka ukipata kizazi chako unawarithisha ikisha huyo unajifia bila ya faida yoyote ya Uhai huu na ukarimu ulofanyiwa na Mollah wako.
Sasa unapata fundisho hili la kupanda ngazi kama utapenda utaondoka hapo ulipo ili upande hiyo ngazi kwa hiyari yako mwenyewe kumbuka hakuna anokulazimisha, Kwa ukweli wa dhati sote tuna fahamu vipi mahusiano yetu yalivyo na Namba 7 , sina haja ya kuyataja yote, ila nitalieleza hili moja ambalo pengine linaweza kuamsha kitu ndani ya Akili yako, inaweza Taa ikawaka ukapata maarifa kumbe ngazi yenyewe ilokusudiwa ndio hii, Na vile vile kumbuka somo hili hali hitaji Mabuku wala hadith (japo nimeitia moja)ili kukutosheleza fahamu yako iungane na kusudio langu, elewa haina haja ya Sheikh wala Maalim, wewe Mwenyewe ndio unakwenda katika Ngazi hizi na wewe Mwenyewe ndio utagundua sasa upo Ghorofa ya ngapi.
(1)Ngazi ya kwanza: Sote tunafahamu mahusiano yetu na hiyo Namba saba, Ukitizama kwa uangalifu katika upande wa Dini utajua kila baada ya miaka saba kunatokea mabadiliko katika maisha yako lichunguze hilo utalijua,( Wanasayansi wao wamesema kumi 7x10=70)hakuna alokosea)hiyo ndio (Life Span)ya Binaadamu wengi, wapo wanopitiliza na wapo wasofikia lakini dhumuni letu ni kuzungumzia ngazi hii ya Mwanzo na hazina zake.
endelea part 3
عَلَّمَ ٱلۡإِنسَـٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ
Amemfundisha Mwanaadamu (Chungu)ya Mambo aliyokua hayajui.
Mtizame Mtoto na vimacho vyake anavokuja katika Ulimwengu huu, akizaliwa tu maskini hajui chochote anaangaza huku na kule, kama kusema Akili yangu tupu sasa anzeni kujaza mambo yenu, lakini Mtoto (Hodari)anasikia pande zote mbili, anasikia mafundisho yanotoka kwa Mollah wake, na kusikiliza pia yanotoka kwenu, Na hivi ndio sote tunavofundishwa tokea kuzaliwa mpaka tunaingia kaburini, lakini tunafika pahala, tunasahau kusikiliza upande wa pili(Nyimbo, Ngoma,siasa zinatushughulisha)unakua husikii tena hayo mafundisho japo yanaendelea kuja(stage by stage)hiyo haki yako lazima uletewe lakini hutaki, wewe unashughulika na Elimu ya nje, umeambiwa (Elimu bila ya malipo) na kila mtu anapenda kitu cha bure, hapo tena unaanza kujazwa Mbinu za wizi, vipi utadhulumu, kuna njia ngapi za uongo, hata ukitimia miaka 21 wewe ushakua (Expert)unakabiziwa cheti unakua mtaalamu wa mipango yote, tizama sasa uharibifu unofatia unadumu na elimu hiyo mpaka ukipata kizazi chako unawarithisha ikisha huyo unajifia bila ya faida yoyote ya Uhai huu na ukarimu ulofanyiwa na Mollah wako.
Sasa unapata fundisho hili la kupanda ngazi kama utapenda utaondoka hapo ulipo ili upande hiyo ngazi kwa hiyari yako mwenyewe kumbuka hakuna anokulazimisha, Kwa ukweli wa dhati sote tuna fahamu vipi mahusiano yetu yalivyo na Namba 7 , sina haja ya kuyataja yote, ila nitalieleza hili moja ambalo pengine linaweza kuamsha kitu ndani ya Akili yako, inaweza Taa ikawaka ukapata maarifa kumbe ngazi yenyewe ilokusudiwa ndio hii, Na vile vile kumbuka somo hili hali hitaji Mabuku wala hadith (japo nimeitia moja)ili kukutosheleza fahamu yako iungane na kusudio langu, elewa haina haja ya Sheikh wala Maalim, wewe Mwenyewe ndio unakwenda katika Ngazi hizi na wewe Mwenyewe ndio utagundua sasa upo Ghorofa ya ngapi.
(1)Ngazi ya kwanza: Sote tunafahamu mahusiano yetu na hiyo Namba saba, Ukitizama kwa uangalifu katika upande wa Dini utajua kila baada ya miaka saba kunatokea mabadiliko katika maisha yako lichunguze hilo utalijua,( Wanasayansi wao wamesema kumi 7x10=70)hakuna alokosea)hiyo ndio (Life Span)ya Binaadamu wengi, wapo wanopitiliza na wapo wasofikia lakini dhumuni letu ni kuzungumzia ngazi hii ya Mwanzo na hazina zake.
endelea part 3
NGAZI SABA ZA ROHO PART 3(NGAZI 1)
Asalaam Aleiykum,
Ajiangalie Mwanaadamu nani alokufundisha kutambaa, akakufundisha kutembea, akakufundisha kuzungumza,akakufundisha hichi na kile, akakuonesha maajabu haya na yale, ukawa kila leo utotoni unagundua hichi na kile ukakifahamu bila ya kuwepo Mwalim mbele yako, na mengi mengineyo na ukisha ulipotimia miaka 14 akakufungulia ukurasa mpya wa (Sex Energy)au kumi na mitatu kwa Wanawake, Ukawa tayari sasa umeingia katika Ulimwengu wa Fahamu, Unaendelea kuishi katika ngazi hii ukiwa unapata mazoea ya kila kitu na mafundisho na baadhi ya elimu zinaendelea kumiminika samba samba katika Akili yako, hapo tena unafanya maamuzi nini unataka, nani unataka kuwa(Japo kwa wengi maamuzi hayo yanafanywa na wazazi)unachagua njia zako za kila aina, elewa katika kipindi hicho chote kuna (Group)tatu , mbili zinapigana kukusomesha na moja imetulia inakufundisha taratibu.
Ama (Group) ya mwanzo ya Kilimwengu inapigana kukusomesha mambo ya Kidunia, kukupa (Gossip)kukupa habari za maendeleo, zengine mpya zengine za zamani, wanakuhimiza nunua gari mpya, jenga nyumba mpya, oa mke huyu, olewa na mume yule, mambo yako yote ya Ulimwengu, na ile (Group)ya Pili ambayo ni ya watu wa dini nayo inajitahidi wewe funga, usiwache kusali, huko kuna pepo, huko kuna moto, kuna mateso makubwa, na hivi na vile.
Halafu linasalia hili lenye ukweli, lenye kukujulisha taratibu tena kwa uyakinifu, lenye kukufundisha kuijua haki kwa dalili na kukuonesha kwa uwazi uso shaka kuwa upande wa pili kuna hivi na vile, unaambiwa kwa utaratibu hivyo usifanye ni (Kosa)utadhurika,na unajua kweli hili ni kosa (Lakini wapi)unaambiwa unaona Moyo wako sasa hauchukui usije ukenda mbio huziwezi tena, sasa acha (Disco) na kwenda vilabu vya pombe ushakua mtu mzima, lakini husikilizi kabisa taarifa za ndani huna haja nazo kabisa, ukiona kero unafungua nyimbo, ukiona kina zidi sana unafungua senema(TV)ukiona maelezo yanazidi huyo unatoka kwenda Barazani kwenye mazungumzo, lakini kwa kuwa ni haki yako upande huo wa pili unaendelea kukufundisha na kukupa taaluma. Hii wewe hujachoka huoni marafiki wamepungua, huoni kama unapitwa na wakati, mbona hivi umeshughulika na mambo yaso maana katika umri wako ulo Adhimu, hebu kumbuka umefanyiwa Ukarimu, jee umelipa nini katika Ukarimu huo?
Nini kitu hicho?
Hiyo ni Roho yako ambayo iko ngazi ya kwanza inakufundisha kuwa zipo zengine sita, lakini hutaki kabisa kuisikiliza.(Mara moja moja ndio unaisikiliza ikisha unasema kweli Roho yangu ilikua nzito sikwenda pahala pal au sikusafiri ndio ajali imetokea unaona). Na kwanini tusifundishwe wakati (Baba yetu Adam a.s)alifundishwa, na wewe mpaka leo mafunzo hayo yanaendelea, lakini umekua mtoro, unayakimbia huyataki, hutaki kusikia habari hii, inakutia dhiki.
Ndio maana utakuta watu wengi habari za upande wa pili zinawafika lakini wameshughulika na Ulimwengu.
Sasa nakupa kidogo mfano wa mafundisho yenyewe ili usije ukaona labda mazinga ombwe, (Unapokua na Njaa unajuaje, hakuna chengine ila fahamu zinakujia kuwa sasa tumbo lina njaa, na sio tumbo mwili unapeleka taarifa tumboni ili uambiwe utafute chakula)
Unaposhikwa na usingizi mwili pia unakwambia tushachoka kalale, mwenyewe unasema usingizi umenishika, sasa hayo ni machache tu katika ngazi hii,sasa upo kwenye(Ghorofa ya fahamu hizo) lakini (Massage)zinakuja kutoka upande wa Pili lakini huzisikilizi, hutaki kufahamu, unazidi kushughulika na dunia, unagombea hichi na kile, Unamkuta mtu mzima bado anagombea vyeo, kama hapati cha siasa basi mpaka cha msikitini lazima awe Imam, kama haupati Uimam awe japo mkuu wa karata, awe msimamizi wa sadaka, awe chifu, au mjumbe wa nyumba kumi, kila kitu (Ambitions)za Ulimwengu huu, na utawakuta wengi wamebaki katika Umri uleule wa (Baleghe)bado wako kwenye maisha ya utotoni (Teens)bado wanatafuta (Boyfriend na Girlfriend)(Vimada)bado wametawaliwa na Ulimwengu wa anasa, bado anataka gari mpya, bado anataka nyumba nyengine, anashughulika Mja katika ngazi hii kutaka kujulikana, kutafuta cheo, na mambo mengi ya kipuuzi katika maisha haya huku akisahau kabisa sauti ya ukimya inayomfundisha "Ewe Mwanaadamu"kipo kitu chengine kwenye ngazi zengine"usibakie kwenye ngazi hiyo utakua hasarani, zipo sita hebu zitafute ukamilishe maisha yako, mbona umecharuka kulimbikiza mali, kuonea wenzio, kudhulumu haki za watu, hebu wacha uje kwenye ngazi ya pili uone kuna nini, njoo uchungulie ghorofa hii labda utazinduka usingizini ujue kumbe kuna zaidi ya haya.Na ukipanda Ngazi ya pili unapata (Shock)unakutana na kitu cha kustaajabisha kitu gani hicho?
Inshaallah tutaendelea wiki ijayo hiyo ngazi ya Pili
Ajiangalie Mwanaadamu nani alokufundisha kutambaa, akakufundisha kutembea, akakufundisha kuzungumza,akakufundisha hichi na kile, akakuonesha maajabu haya na yale, ukawa kila leo utotoni unagundua hichi na kile ukakifahamu bila ya kuwepo Mwalim mbele yako, na mengi mengineyo na ukisha ulipotimia miaka 14 akakufungulia ukurasa mpya wa (Sex Energy)au kumi na mitatu kwa Wanawake, Ukawa tayari sasa umeingia katika Ulimwengu wa Fahamu, Unaendelea kuishi katika ngazi hii ukiwa unapata mazoea ya kila kitu na mafundisho na baadhi ya elimu zinaendelea kumiminika samba samba katika Akili yako, hapo tena unafanya maamuzi nini unataka, nani unataka kuwa(Japo kwa wengi maamuzi hayo yanafanywa na wazazi)unachagua njia zako za kila aina, elewa katika kipindi hicho chote kuna (Group)tatu , mbili zinapigana kukusomesha na moja imetulia inakufundisha taratibu.
Ama (Group) ya mwanzo ya Kilimwengu inapigana kukusomesha mambo ya Kidunia, kukupa (Gossip)kukupa habari za maendeleo, zengine mpya zengine za zamani, wanakuhimiza nunua gari mpya, jenga nyumba mpya, oa mke huyu, olewa na mume yule, mambo yako yote ya Ulimwengu, na ile (Group)ya Pili ambayo ni ya watu wa dini nayo inajitahidi wewe funga, usiwache kusali, huko kuna pepo, huko kuna moto, kuna mateso makubwa, na hivi na vile.
Halafu linasalia hili lenye ukweli, lenye kukujulisha taratibu tena kwa uyakinifu, lenye kukufundisha kuijua haki kwa dalili na kukuonesha kwa uwazi uso shaka kuwa upande wa pili kuna hivi na vile, unaambiwa kwa utaratibu hivyo usifanye ni (Kosa)utadhurika,na unajua kweli hili ni kosa (Lakini wapi)unaambiwa unaona Moyo wako sasa hauchukui usije ukenda mbio huziwezi tena, sasa acha (Disco) na kwenda vilabu vya pombe ushakua mtu mzima, lakini husikilizi kabisa taarifa za ndani huna haja nazo kabisa, ukiona kero unafungua nyimbo, ukiona kina zidi sana unafungua senema(TV)ukiona maelezo yanazidi huyo unatoka kwenda Barazani kwenye mazungumzo, lakini kwa kuwa ni haki yako upande huo wa pili unaendelea kukufundisha na kukupa taaluma. Hii wewe hujachoka huoni marafiki wamepungua, huoni kama unapitwa na wakati, mbona hivi umeshughulika na mambo yaso maana katika umri wako ulo Adhimu, hebu kumbuka umefanyiwa Ukarimu, jee umelipa nini katika Ukarimu huo?
Nini kitu hicho?
Hiyo ni Roho yako ambayo iko ngazi ya kwanza inakufundisha kuwa zipo zengine sita, lakini hutaki kabisa kuisikiliza.(Mara moja moja ndio unaisikiliza ikisha unasema kweli Roho yangu ilikua nzito sikwenda pahala pal au sikusafiri ndio ajali imetokea unaona). Na kwanini tusifundishwe wakati (Baba yetu Adam a.s)alifundishwa, na wewe mpaka leo mafunzo hayo yanaendelea, lakini umekua mtoro, unayakimbia huyataki, hutaki kusikia habari hii, inakutia dhiki.
Ndio maana utakuta watu wengi habari za upande wa pili zinawafika lakini wameshughulika na Ulimwengu.
Sasa nakupa kidogo mfano wa mafundisho yenyewe ili usije ukaona labda mazinga ombwe, (Unapokua na Njaa unajuaje, hakuna chengine ila fahamu zinakujia kuwa sasa tumbo lina njaa, na sio tumbo mwili unapeleka taarifa tumboni ili uambiwe utafute chakula)
Unaposhikwa na usingizi mwili pia unakwambia tushachoka kalale, mwenyewe unasema usingizi umenishika, sasa hayo ni machache tu katika ngazi hii,sasa upo kwenye(Ghorofa ya fahamu hizo) lakini (Massage)zinakuja kutoka upande wa Pili lakini huzisikilizi, hutaki kufahamu, unazidi kushughulika na dunia, unagombea hichi na kile, Unamkuta mtu mzima bado anagombea vyeo, kama hapati cha siasa basi mpaka cha msikitini lazima awe Imam, kama haupati Uimam awe japo mkuu wa karata, awe msimamizi wa sadaka, awe chifu, au mjumbe wa nyumba kumi, kila kitu (Ambitions)za Ulimwengu huu, na utawakuta wengi wamebaki katika Umri uleule wa (Baleghe)bado wako kwenye maisha ya utotoni (Teens)bado wanatafuta (Boyfriend na Girlfriend)(Vimada)bado wametawaliwa na Ulimwengu wa anasa, bado anataka gari mpya, bado anataka nyumba nyengine, anashughulika Mja katika ngazi hii kutaka kujulikana, kutafuta cheo, na mambo mengi ya kipuuzi katika maisha haya huku akisahau kabisa sauti ya ukimya inayomfundisha "Ewe Mwanaadamu"kipo kitu chengine kwenye ngazi zengine"usibakie kwenye ngazi hiyo utakua hasarani, zipo sita hebu zitafute ukamilishe maisha yako, mbona umecharuka kulimbikiza mali, kuonea wenzio, kudhulumu haki za watu, hebu wacha uje kwenye ngazi ya pili uone kuna nini, njoo uchungulie ghorofa hii labda utazinduka usingizini ujue kumbe kuna zaidi ya haya.Na ukipanda Ngazi ya pili unapata (Shock)unakutana na kitu cha kustaajabisha kitu gani hicho?
Inshaallah tutaendelea wiki ijayo hiyo ngazi ya Pili
Sunday, February 16, 2014
NJIA KUMI ZA KUIPATA PEPO PART 1
Asalaam Aleiykum,
Elewa utakapo kutana na Ukweli shaka itakuondoka, Hapo utagundua Ukweli hautaki Wakili wala Utetezi, Utajua pia Ukweli hauna ubaguzi na unamkaribisha kila Mja kuufikia, Ndio Maana utakuta ukisema uongo mmoja unatakiwa uulinde kwa uongo mengine 99. Na Ukweli huo una njia nyingi kuufikia japo mimi leo nimechagua hizi kumi(10)ili tupate faida zake kwa pamoja, nazingumza hizi ili asije kutokea Mtu na (Fantasy)zake akawa anakwambia shika ukweli wangu ndio utapata mafanikio, kumbuka ukweli utaupata kwa juhudi zako mwenyewe na hakuna juhudi za kumfata yoyote yule ambaye anaweza kuwa hajui njia kama ulivo wewe.
Kumbuka mambo yote ya Dini yanafanyika ndani ya kifua cha Siri, chochote kile ufanyacho kuonesha watu au kujionesha mwenyewe kinakua hakina thamani katika Ulimwengu wa Dini, Ni njia tunazo ziita (Attention seeking) na hilo neno la mwisho ni zuri sana ukilisoma moja moja(See King)(Muone Mfalme) ni mambo ya kujionesha(Showing-Off). Unatakiwa Mja wewe Mawasiliano yako na upande wa Pili uyafanye kwa siri kubwa ndio unaweza kufanikiwa, Hakutakiwi maonesho huko wala watu wakuone, hutakiwi uwajulishe watu uko hivi ama vile, Ni wewe na Mollah wako siri hiyo.
Sasa kwanini nikazichagua njia hizi kumi ambazo kidogo zitakushangaza, Ni kutokana na tafauti tulonazo Binaadamu ndio maana njia zikawekwa tafauti huyu anaweza kupita ile wewe ukapita hii, Yule anaweza kwenda kwa haraka wewe ukenda taratibu lakini la muhimu nyote mtafika kwenye hiyo (Haki)ama huo Ukweli. Kumbuka tatizo sio kuchelewa bali kama jee utafika?,
Hapa natilia mkazo ukiona Mtu yoyote anatilia mkazo lazima ushike au uifate njia yake ndio ufike kwenye (Haki)Basi elewa huyo muongozaji mwenyewe hajui njia na huna haja ya kumfata atakupoteza na unatakiwa umkimbie haraka.
Tunaingia Darsa hii na tunakutana na aya ya 35 sura ya Ahzab ambayo tutaishi katika maneno hayo ili tuzijue hizo njia kumi zilokusudiwa ni zipi ili tupate faida zake. Na uzuri wa njia hizi unaweza kuchagua mwenyewe yoyote ukaifata njia hiyo ili ikupe manufaa yake. Hapa nakutaka uishi ndani neno sio kupita ukakamata neno na ukaacha maana yake. zingatia sana kisemwacho na kitakua na faida kubwa na wewe.
Endelea Part 2
Elewa utakapo kutana na Ukweli shaka itakuondoka, Hapo utagundua Ukweli hautaki Wakili wala Utetezi, Utajua pia Ukweli hauna ubaguzi na unamkaribisha kila Mja kuufikia, Ndio Maana utakuta ukisema uongo mmoja unatakiwa uulinde kwa uongo mengine 99. Na Ukweli huo una njia nyingi kuufikia japo mimi leo nimechagua hizi kumi(10)ili tupate faida zake kwa pamoja, nazingumza hizi ili asije kutokea Mtu na (Fantasy)zake akawa anakwambia shika ukweli wangu ndio utapata mafanikio, kumbuka ukweli utaupata kwa juhudi zako mwenyewe na hakuna juhudi za kumfata yoyote yule ambaye anaweza kuwa hajui njia kama ulivo wewe.
Kumbuka mambo yote ya Dini yanafanyika ndani ya kifua cha Siri, chochote kile ufanyacho kuonesha watu au kujionesha mwenyewe kinakua hakina thamani katika Ulimwengu wa Dini, Ni njia tunazo ziita (Attention seeking) na hilo neno la mwisho ni zuri sana ukilisoma moja moja(See King)(Muone Mfalme) ni mambo ya kujionesha(Showing-Off). Unatakiwa Mja wewe Mawasiliano yako na upande wa Pili uyafanye kwa siri kubwa ndio unaweza kufanikiwa, Hakutakiwi maonesho huko wala watu wakuone, hutakiwi uwajulishe watu uko hivi ama vile, Ni wewe na Mollah wako siri hiyo.
Sasa kwanini nikazichagua njia hizi kumi ambazo kidogo zitakushangaza, Ni kutokana na tafauti tulonazo Binaadamu ndio maana njia zikawekwa tafauti huyu anaweza kupita ile wewe ukapita hii, Yule anaweza kwenda kwa haraka wewe ukenda taratibu lakini la muhimu nyote mtafika kwenye hiyo (Haki)ama huo Ukweli. Kumbuka tatizo sio kuchelewa bali kama jee utafika?,
Hapa natilia mkazo ukiona Mtu yoyote anatilia mkazo lazima ushike au uifate njia yake ndio ufike kwenye (Haki)Basi elewa huyo muongozaji mwenyewe hajui njia na huna haja ya kumfata atakupoteza na unatakiwa umkimbie haraka.
Tunaingia Darsa hii na tunakutana na aya ya 35 sura ya Ahzab ambayo tutaishi katika maneno hayo ili tuzijue hizo njia kumi zilokusudiwa ni zipi ili tupate faida zake. Na uzuri wa njia hizi unaweza kuchagua mwenyewe yoyote ukaifata njia hiyo ili ikupe manufaa yake. Hapa nakutaka uishi ndani neno sio kupita ukakamata neno na ukaacha maana yake. zingatia sana kisemwacho na kitakua na faida kubwa na wewe.
Endelea Part 2
NJIA KUMI ZA KUIPATA PEPO PART 2
Asalaam Aleiykum,
إِنَّ ٱلۡمُسۡلِمِينَ وَٱلۡمُسۡلِمَـٰتِ
Hakika ya Waislam Wanaume na Wanawake.
(1)Hiyo njia ya kwanza ilotajwa hapo ambayo wengi tunazaliwa mpaka kufikia kuondoka Ulimwengu huu tunabaki hapo hapo, si wengi wenye kupiga hatua ya kuendelea mbele kwenye njia hii.
Nini Uislam? ni (Surrender)kujisalimisha, na hakuna taabu kubwa kama kujisalimisha kwa jambo usoweza kuliona, rahisi kujisalimisha kwa kitu unachoweza kukiona lakini vigumu sana kujisalimisha kwa kitu ambacho hukioni, inataka moyo wenye salama kukipata kitendo kama hicho, ndio maana utaona kujisalimisha kwetu kumekua kidogo kidogo, unaacha hiki, halafu unaacha kengine taratibu kwa kuwa (Surrender)yako sio kamilifu, bado mbishi, bado una afya, unakwenda ukirudi, mambo yakiwa magumu unataraji labda mzimu haujafurahi, pengine shetani kakasirika, labda nina nukusi imeniganda, kujisalamisha kwako jichunguze kukoje, nakupa (Mifano hai)jitizame jee umeingia kikamilifu katika sheria zote za Kiislam, Na kama hujaingia basi wewe ni Muislam kwa sababu moja tu umejikubalisha kujisalimisha, Na kutokana na hilo huenda ukajisalimisha upo njiani,kwa hiyo Waislam wanaume na waislam wanawake(Sote Tumo) ila kwa yule atakae amua kujitenga mwenyewe na vitendo viovu akadumu navyo.
وَٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَـٰتِ
Na Waumin Wanaume na Waumin Wanawake
(2)Njia ya pili, Ukipata kujisalimisha kwa ukamilifu nini kinatokezea? Kuna kitu kinatokezea katika Moyo wako (From Beyond)si cha Ulimwengu huu,(Something New)kitu kipya kinatawala Moyo wako unaondoka katika Njia ya Uislam na kuendelea katika Kundi la Waumin, kundi hili matendo yake, maneno yake, na kila kitu chao kimejaa uaminifu, hata ukitaka kumdhuru habadiliki tena, kuna kitu kipya kinaishi ndani ya Moyo wake, Ulimwengu huu anauona kwa njia nyengine kabisa tafauti na yule wa njia ya mwanzo, anaamini yote yanotokezea yupo mpangaji wake na yeye ni mwenye kufata, Kwenye Furaha anafurahi kwenye dhiki anakubali, kwenye huzuni anahuzunika, huku anaamini Mollah wake ni mwenye kusimamia kila jambo, anaamini yeye ni Mwenye kulitoa Jua na kuuleta Usiku, Yeye ni Mwenye kuvilaza viumbe ikisha akavihuuisha, Yeye ni Mwenye Kuleta Nuru na pia kuongoza vyote vilivyomo kwenye Ulimwengu huu, Mwenye Imani hutokwa na Machozi akijua yeye kala jirani yake hajala, hushikwa na huzuni iwapo kama Rafiki yake kafikwa na Maradhi au Misiba humshukuru Mollah wake kila anapoanza jambo au kulimaliza na hudumu na Imani hiyo kwa kipindi chote cha Uhai wake bila ya kutetereka.
وَٱلۡقَـٰنِتِينَ وَٱلۡقَـٰنِتَـٰتِ
Watiifu Wanaume na Watiifu wanawake
(3)Njia ya tatu, Ukishapita katika Njia ya pili moja kwa moja unaingia katika njia ya tatu ambayo ya Utiifu, unakua simwenye kumuasi Mollah wako katika sheria zake zote unazifata, katika njia hii unakuwa safi katika kila jambo lako, unaogopa kuigusa haramu hata iwe chembe ndogo, unazungukwa na Utiifu huo kuenea kila sehemu ya maisha yako, Unawatii wazee wako, unamtii Mumeo au Mkeo, katika mambo yote ya Uhalali.
وَٱلصَّـٰدِقِينَ وَٱلصَّـٰدِقَـٰتِ
Na Wasemao ukweli Wanaume na Wanawake.
Ukweli wenyewe upi? Ukishapita katika Njia hizo tatu za Juu moja kwa moja unageuka kuwa Ukweli, unathibitisha Ukweli wa Mambo ya Kilimwengu na ya Huko ya Upande wa Pili usionekana, kwa sababu unafunguliwa ukweli na Mwenyewe Mwenye Enzi Mungu, huwezi tena kukamata Kitabu chake halafu ukawa unakwenda Kinyume cha Ukweli, Na ukifika kwenye Njia hii basi (Shindano unaita Shindano)Huwezi kuita Msumari tena, Unasimama na msimamo wako bila ya Kuyumba, kwa sababu ushaujua ukweli, Unakuwa Mkweli, Unasema Ukweli, Huna haja ya kwenda kinyume cha huo Ukweli, (Mfano sasa hivi unaona Taa lakini hujui inakuaje hata ikawa Taa)Hujui taa imetokea wapi kwanini ikawaka sababu zake nini kuwaka taa hii, hayo ni katika Ulimwengu huu, ikisha Ghafla Mollah wako anakuonesha Nuru ambayo ni zaidi ya Taa na wewe hujapata kuiona, hapo unakua umeshauona Ukweli, sasa hivi hujaona ukweli wala hujaona hiyo taa, ila unaona vilomurikwa na Taa lakini taa yenyewe huijui, Itafute taa au Nuru ndio utaujua Ukweli.
Endelea part 3
إِنَّ ٱلۡمُسۡلِمِينَ وَٱلۡمُسۡلِمَـٰتِ
Hakika ya Waislam Wanaume na Wanawake.
(1)Hiyo njia ya kwanza ilotajwa hapo ambayo wengi tunazaliwa mpaka kufikia kuondoka Ulimwengu huu tunabaki hapo hapo, si wengi wenye kupiga hatua ya kuendelea mbele kwenye njia hii.
Nini Uislam? ni (Surrender)kujisalimisha, na hakuna taabu kubwa kama kujisalimisha kwa jambo usoweza kuliona, rahisi kujisalimisha kwa kitu unachoweza kukiona lakini vigumu sana kujisalimisha kwa kitu ambacho hukioni, inataka moyo wenye salama kukipata kitendo kama hicho, ndio maana utaona kujisalimisha kwetu kumekua kidogo kidogo, unaacha hiki, halafu unaacha kengine taratibu kwa kuwa (Surrender)yako sio kamilifu, bado mbishi, bado una afya, unakwenda ukirudi, mambo yakiwa magumu unataraji labda mzimu haujafurahi, pengine shetani kakasirika, labda nina nukusi imeniganda, kujisalamisha kwako jichunguze kukoje, nakupa (Mifano hai)jitizame jee umeingia kikamilifu katika sheria zote za Kiislam, Na kama hujaingia basi wewe ni Muislam kwa sababu moja tu umejikubalisha kujisalimisha, Na kutokana na hilo huenda ukajisalimisha upo njiani,kwa hiyo Waislam wanaume na waislam wanawake(Sote Tumo) ila kwa yule atakae amua kujitenga mwenyewe na vitendo viovu akadumu navyo.
وَٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَـٰتِ
Na Waumin Wanaume na Waumin Wanawake
(2)Njia ya pili, Ukipata kujisalimisha kwa ukamilifu nini kinatokezea? Kuna kitu kinatokezea katika Moyo wako (From Beyond)si cha Ulimwengu huu,(Something New)kitu kipya kinatawala Moyo wako unaondoka katika Njia ya Uislam na kuendelea katika Kundi la Waumin, kundi hili matendo yake, maneno yake, na kila kitu chao kimejaa uaminifu, hata ukitaka kumdhuru habadiliki tena, kuna kitu kipya kinaishi ndani ya Moyo wake, Ulimwengu huu anauona kwa njia nyengine kabisa tafauti na yule wa njia ya mwanzo, anaamini yote yanotokezea yupo mpangaji wake na yeye ni mwenye kufata, Kwenye Furaha anafurahi kwenye dhiki anakubali, kwenye huzuni anahuzunika, huku anaamini Mollah wake ni mwenye kusimamia kila jambo, anaamini yeye ni Mwenye kulitoa Jua na kuuleta Usiku, Yeye ni Mwenye kuvilaza viumbe ikisha akavihuuisha, Yeye ni Mwenye Kuleta Nuru na pia kuongoza vyote vilivyomo kwenye Ulimwengu huu, Mwenye Imani hutokwa na Machozi akijua yeye kala jirani yake hajala, hushikwa na huzuni iwapo kama Rafiki yake kafikwa na Maradhi au Misiba humshukuru Mollah wake kila anapoanza jambo au kulimaliza na hudumu na Imani hiyo kwa kipindi chote cha Uhai wake bila ya kutetereka.
وَٱلۡقَـٰنِتِينَ وَٱلۡقَـٰنِتَـٰتِ
Watiifu Wanaume na Watiifu wanawake
(3)Njia ya tatu, Ukishapita katika Njia ya pili moja kwa moja unaingia katika njia ya tatu ambayo ya Utiifu, unakua simwenye kumuasi Mollah wako katika sheria zake zote unazifata, katika njia hii unakuwa safi katika kila jambo lako, unaogopa kuigusa haramu hata iwe chembe ndogo, unazungukwa na Utiifu huo kuenea kila sehemu ya maisha yako, Unawatii wazee wako, unamtii Mumeo au Mkeo, katika mambo yote ya Uhalali.
وَٱلصَّـٰدِقِينَ وَٱلصَّـٰدِقَـٰتِ
Na Wasemao ukweli Wanaume na Wanawake.
Ukweli wenyewe upi? Ukishapita katika Njia hizo tatu za Juu moja kwa moja unageuka kuwa Ukweli, unathibitisha Ukweli wa Mambo ya Kilimwengu na ya Huko ya Upande wa Pili usionekana, kwa sababu unafunguliwa ukweli na Mwenyewe Mwenye Enzi Mungu, huwezi tena kukamata Kitabu chake halafu ukawa unakwenda Kinyume cha Ukweli, Na ukifika kwenye Njia hii basi (Shindano unaita Shindano)Huwezi kuita Msumari tena, Unasimama na msimamo wako bila ya Kuyumba, kwa sababu ushaujua ukweli, Unakuwa Mkweli, Unasema Ukweli, Huna haja ya kwenda kinyume cha huo Ukweli, (Mfano sasa hivi unaona Taa lakini hujui inakuaje hata ikawa Taa)Hujui taa imetokea wapi kwanini ikawaka sababu zake nini kuwaka taa hii, hayo ni katika Ulimwengu huu, ikisha Ghafla Mollah wako anakuonesha Nuru ambayo ni zaidi ya Taa na wewe hujapata kuiona, hapo unakua umeshauona Ukweli, sasa hivi hujaona ukweli wala hujaona hiyo taa, ila unaona vilomurikwa na Taa lakini taa yenyewe huijui, Itafute taa au Nuru ndio utaujua Ukweli.
Endelea part 3
NJIA KUMI ZA KUIPATA PEPO PART 3
Asalaam Aleiykum,
وَٱلصَّـٰبِرِينَ وَٱلصَّـٰبِرَٲتِ
Na Wanaosubiri Wanaume na Wanawake.
(5)Njia ya tano ni hii ya Subira, Katika Njia hii unatakiwa ujifunge kustahamili yote yatakayo kukuta, Inatakiwa uyabebe mazuri na mabaya,Inatakiwa uwe msubirifu wa hali ya juu kuipita njia hii hususan ukiwa unaishi na viumbe wenzio wenye tabia tafauti, unaishi na Familia wenye mwenendo tafauti, unaishi katika Ulimwengu wenye mabadiliko kila leo, Unaishi kwenye (Body)Mwili wako unabadilika kila siku, Unaishi na Akili yako yenye mabadiliko ya kila wakati, kuna mambo yenye kutokea katika Ulimwengu huu kila saa na dakika, Basi ikiwa yatakugusa wewe unatakiwa uwe mwenye subira katika njia hii nzito.
Nini Subira? Subira ni njia ya (Awareness)ya kufahamu kila linalojiri lina chanzo chake na mimi ninachotakiwa ni kusubiri chanzo hicho kichukue muda wake, na hilo jambo likipita bila ya wewe kuteleza hapo unakua umeshapata subira, Shida zikija unasubiri, mateso yakija unasubiri, Raha zikija unasubiri, Ukikerwa unasubiri, msiba ukikukuta unasubiri hapo tena unakua Mja wa subira.
وَٱلۡخَـٰشِعِينَ وَٱلۡخَـٰشِعَـٰتِ
Na Wanyenyekevu Wanaume na Wanawake.
(6)Njia hii ya sita ni ya Unyenyekevu, Wapi unatokea unyenyekevu, Unyenyekevu unatokea Moyoni.
Nini Unyenyekevu?
Unyenyekevu ni hali ya kufanywa Mtumwa kwa hiari yako, Kumbuka Utumwa ni jambo la kulazimishwa, iwe kwa nguvu au kwa pesa, lakini Utumwa huo ukigeuka ukawa hiyari basi unageuka kuwa unyenyekevu, (Mfano) anatakiwa kiongozi muadilifu kuwanyenyekea walomchagua ili awatumikie, na uongozi ni kokote iwe nyumbani kazini au kwengine kokote na ukiupata huo Unyenyekevu basi jua wewe unavyo vitu viwili muhimu huwezi kuwa na Unyenyekevu ila lazima una subira, na hakuna yoyote mwenye subira ila anakua mwenye kuipata Sala, Na hakuna Mwenye kuipata Sala ila anapata matunda ya Unyenyekevu nayo ni kusamehewa na kukubaliwa dua zake, kuupata unyenyekevu lazima ukubali kuwa(Nothing)ndani ya hiyo(nothing)ndipo inatokea (Something)siwezi kuhadithia haina mfano hali ya unyenyekevu ambayo ikikuingia kwa ukamilifu inakupata (Khofu)na ikikupata khofu unakua ushakwenda (Beyond).
وَٱلۡمُتَصَدِّقِينَ وَٱلۡمُتَصَدِّقَـٰتِ
Na watoao Sadaka Wanaume na Wanawake
Nani Mtoa Sadaka?
(7)Njia ya Saba, Mtoa Sadaka ni yule alosadikisha Ukweli wa kuamini kwamba yeye kapewa zawadi ya Uhai na vyote alivochuma ni zawadi kutoka kwa Mollah wake, Na yeye hana Ujira wala cha kufanya ila atumie zawadi hizo na viumbe wenzie, huyo ndio mtoa Sadaka, Anatoa akijijua yeye sie mwenye kutoa ila Mwenye Enzi Mungu ndie Mwenye kutoa kupitia kwenye chanzo chake yeye, Ametangulia kwenye kheri nyingi yule Mwenye kutoa Sadaka kwa
Wingi.
وَٱلصَّـٰٓٮِٕمِينَ وَٱلصَّـٰٓٮِٕمَـٰتِ
Na Wanaofunga Wanaume na Wanawake
Nini Kufunga?
(8)Njia ya Nane.Wanaofunga ni wale ambao wameamua Kuishi Kiroho, Funga zipo za kila aina, lakini zote ni zenye kuushirikisha Mwili (Body)Kwa sababu Roho Daima inafunga, kwa hiyo Funga yoyote ni (Brain Discipline) ukenda (Deep)utagundua ni (Control) Ya Akili yako, Ndio maana mwanzo unapoanza (Kufunga)unakua unahangaika na njaa, ukiweza ku (Control) Akili inaelekea kwengine unaanza kutamani hiki na kile mpaka wakati wa kufungua kwako, kwa hiyo mwenye kufunga kweli ambao walotajwa hapo ni wale wenye kufunga Mwili(Body) na (Mind)Akili.
وَٱلۡحَـٰفِظِينَ فُرُوجَهُمۡ وَٱلۡحَـٰفِظَـٰتِ
Na Wanao hifadhi Tupu zao Wanaume na Wanawake.
(9)Njia ya Tisa, Tunaizungumza (Most Powerful Energy)(Sex)hapa ndipo anapofeli kila mmoja wetu, Hatari zote zinatokezea hapo, ndio maana mkaambiwa msikurubie, Kuhifadhi tupu ndio mtihani mgumu kupita yote, ukiichezea (Chemical)hii kwa njia ya haramu itakuharibia maisha yako, na ukiweza kuimudu(Control)basi wewe umefaulu, vipi wewe unaweza kushindana na kitu ambacho kutokana na hiyo(Energy)wewe umezaliwa, (Everything)Kimezungukwa na (Sex)jitizame kutwa nzima wewe unaona nini, au mara ngapi yanapita mawazo ya kitu hicho katika Akili yako, kwa hiyo atakaeweza kuhifadhi tupu yake ikawa hachezi na (Energy)hii isipokua kwa njia ya halali, basi njia hii itampa ushindi ulio mkubwa kabisa katika kuisogelea hiyo haki.
وَٱلذَّٲڪِرِينَ ٱللَّهَ كَثِيرً۬ا وَٱلذَّٲڪِرَٲتِ
Na Wanaomtaja Mwenye Enzi Mungu kwa wingi Wanaume na Wanawake.
(10)Njia ya Kumi, Nini Kutaja?
Kutaja ni kukumbuka, Huwezi kutaja ila Umekumbuka, Na huwezi kukumbuka ila ulicho kikumbuka kiko karibu yako, Ima kwenye Akili au Mbele yako, Na hiyo ndio maana ya kumtaja Mollah wako kwa wingi, Na kwanini ikawa kwa wingi sababu Mollah wako yuko (Both)kwenye Akili na (Present), Kila kitu katika Ulimwengu huu kinaonesha uweza wa kuwepo kwake, Kuanzia Miti,Vidudu,Maua,Mbingu,Nyota,Jua,Mwezi na Milima na Vingi vilivyomo katika Ardhi hii, havikutoshi hivyo vyote kukumbusha Mollah kwa Wingi. Basi ukiifata kikamilifu Njia hizo nini Kinatokea.
أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُم مَّغۡفِرَةً۬ وَأَجۡرًا عَظِيمً۬ا
MWENYE ENZI MUNGU AMEWAANDALIA MSAMAHA NA UJIRA MKUBWA
Ametoa Ahadi Mwenye Enzi Mungu ya Kwanza kusamehe wale wote wenye kuzifata hizo njia 10, Japo moja ukiishika basi haikupotezi, isipokua ikiwa hutaki mwenyewe huo msamaha, Na hizo njia kumi nilizozitaja ni kama mtego ukiikamata yoyote inakuongoza kwenye haki, inakupeleka kwenye Ahadi ya Pili nayo ni ya kulipwa Ujira, Na hakuna ujira anostahiki Mja isipokua hiyo Pepo, amabayo imeandaliwa na Mwenye Enzi Mungu kwa ajili yetu, ikiwa Raha na Furaha za Uhai hali hii, Ina hali gani hiyo Pepo kwa Viumbe sisi wenye tamaa ya kuipata hiyo pepo.
Basi hakuna cha kufanya isipokua Fata njia hizo kumi ambazo zina kuhakikishia kupata huo msamaha na hiyo Pepo. Mollah wetu tujaalie tuwe Miongoni wa wenye kupata Msamaha wako na ujira ulo tuwekea kutupa.Amin
وَٱلصَّـٰبِرِينَ وَٱلصَّـٰبِرَٲتِ
Na Wanaosubiri Wanaume na Wanawake.
(5)Njia ya tano ni hii ya Subira, Katika Njia hii unatakiwa ujifunge kustahamili yote yatakayo kukuta, Inatakiwa uyabebe mazuri na mabaya,Inatakiwa uwe msubirifu wa hali ya juu kuipita njia hii hususan ukiwa unaishi na viumbe wenzio wenye tabia tafauti, unaishi na Familia wenye mwenendo tafauti, unaishi katika Ulimwengu wenye mabadiliko kila leo, Unaishi kwenye (Body)Mwili wako unabadilika kila siku, Unaishi na Akili yako yenye mabadiliko ya kila wakati, kuna mambo yenye kutokea katika Ulimwengu huu kila saa na dakika, Basi ikiwa yatakugusa wewe unatakiwa uwe mwenye subira katika njia hii nzito.
Nini Subira? Subira ni njia ya (Awareness)ya kufahamu kila linalojiri lina chanzo chake na mimi ninachotakiwa ni kusubiri chanzo hicho kichukue muda wake, na hilo jambo likipita bila ya wewe kuteleza hapo unakua umeshapata subira, Shida zikija unasubiri, mateso yakija unasubiri, Raha zikija unasubiri, Ukikerwa unasubiri, msiba ukikukuta unasubiri hapo tena unakua Mja wa subira.
وَٱلۡخَـٰشِعِينَ وَٱلۡخَـٰشِعَـٰتِ
Na Wanyenyekevu Wanaume na Wanawake.
(6)Njia hii ya sita ni ya Unyenyekevu, Wapi unatokea unyenyekevu, Unyenyekevu unatokea Moyoni.
Nini Unyenyekevu?
Unyenyekevu ni hali ya kufanywa Mtumwa kwa hiari yako, Kumbuka Utumwa ni jambo la kulazimishwa, iwe kwa nguvu au kwa pesa, lakini Utumwa huo ukigeuka ukawa hiyari basi unageuka kuwa unyenyekevu, (Mfano) anatakiwa kiongozi muadilifu kuwanyenyekea walomchagua ili awatumikie, na uongozi ni kokote iwe nyumbani kazini au kwengine kokote na ukiupata huo Unyenyekevu basi jua wewe unavyo vitu viwili muhimu huwezi kuwa na Unyenyekevu ila lazima una subira, na hakuna yoyote mwenye subira ila anakua mwenye kuipata Sala, Na hakuna Mwenye kuipata Sala ila anapata matunda ya Unyenyekevu nayo ni kusamehewa na kukubaliwa dua zake, kuupata unyenyekevu lazima ukubali kuwa(Nothing)ndani ya hiyo(nothing)ndipo inatokea (Something)siwezi kuhadithia haina mfano hali ya unyenyekevu ambayo ikikuingia kwa ukamilifu inakupata (Khofu)na ikikupata khofu unakua ushakwenda (Beyond).
وَٱلۡمُتَصَدِّقِينَ وَٱلۡمُتَصَدِّقَـٰتِ
Na watoao Sadaka Wanaume na Wanawake
Nani Mtoa Sadaka?
(7)Njia ya Saba, Mtoa Sadaka ni yule alosadikisha Ukweli wa kuamini kwamba yeye kapewa zawadi ya Uhai na vyote alivochuma ni zawadi kutoka kwa Mollah wake, Na yeye hana Ujira wala cha kufanya ila atumie zawadi hizo na viumbe wenzie, huyo ndio mtoa Sadaka, Anatoa akijijua yeye sie mwenye kutoa ila Mwenye Enzi Mungu ndie Mwenye kutoa kupitia kwenye chanzo chake yeye, Ametangulia kwenye kheri nyingi yule Mwenye kutoa Sadaka kwa
Wingi.
وَٱلصَّـٰٓٮِٕمِينَ وَٱلصَّـٰٓٮِٕمَـٰتِ
Na Wanaofunga Wanaume na Wanawake
Nini Kufunga?
(8)Njia ya Nane.Wanaofunga ni wale ambao wameamua Kuishi Kiroho, Funga zipo za kila aina, lakini zote ni zenye kuushirikisha Mwili (Body)Kwa sababu Roho Daima inafunga, kwa hiyo Funga yoyote ni (Brain Discipline) ukenda (Deep)utagundua ni (Control) Ya Akili yako, Ndio maana mwanzo unapoanza (Kufunga)unakua unahangaika na njaa, ukiweza ku (Control) Akili inaelekea kwengine unaanza kutamani hiki na kile mpaka wakati wa kufungua kwako, kwa hiyo mwenye kufunga kweli ambao walotajwa hapo ni wale wenye kufunga Mwili(Body) na (Mind)Akili.
وَٱلۡحَـٰفِظِينَ فُرُوجَهُمۡ وَٱلۡحَـٰفِظَـٰتِ
Na Wanao hifadhi Tupu zao Wanaume na Wanawake.
(9)Njia ya Tisa, Tunaizungumza (Most Powerful Energy)(Sex)hapa ndipo anapofeli kila mmoja wetu, Hatari zote zinatokezea hapo, ndio maana mkaambiwa msikurubie, Kuhifadhi tupu ndio mtihani mgumu kupita yote, ukiichezea (Chemical)hii kwa njia ya haramu itakuharibia maisha yako, na ukiweza kuimudu(Control)basi wewe umefaulu, vipi wewe unaweza kushindana na kitu ambacho kutokana na hiyo(Energy)wewe umezaliwa, (Everything)Kimezungukwa na (Sex)jitizame kutwa nzima wewe unaona nini, au mara ngapi yanapita mawazo ya kitu hicho katika Akili yako, kwa hiyo atakaeweza kuhifadhi tupu yake ikawa hachezi na (Energy)hii isipokua kwa njia ya halali, basi njia hii itampa ushindi ulio mkubwa kabisa katika kuisogelea hiyo haki.
وَٱلذَّٲڪِرِينَ ٱللَّهَ كَثِيرً۬ا وَٱلذَّٲڪِرَٲتِ
Na Wanaomtaja Mwenye Enzi Mungu kwa wingi Wanaume na Wanawake.
(10)Njia ya Kumi, Nini Kutaja?
Kutaja ni kukumbuka, Huwezi kutaja ila Umekumbuka, Na huwezi kukumbuka ila ulicho kikumbuka kiko karibu yako, Ima kwenye Akili au Mbele yako, Na hiyo ndio maana ya kumtaja Mollah wako kwa wingi, Na kwanini ikawa kwa wingi sababu Mollah wako yuko (Both)kwenye Akili na (Present), Kila kitu katika Ulimwengu huu kinaonesha uweza wa kuwepo kwake, Kuanzia Miti,Vidudu,Maua,Mbingu,Nyota,Jua,Mwezi na Milima na Vingi vilivyomo katika Ardhi hii, havikutoshi hivyo vyote kukumbusha Mollah kwa Wingi. Basi ukiifata kikamilifu Njia hizo nini Kinatokea.
أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُم مَّغۡفِرَةً۬ وَأَجۡرًا عَظِيمً۬ا
MWENYE ENZI MUNGU AMEWAANDALIA MSAMAHA NA UJIRA MKUBWA
Ametoa Ahadi Mwenye Enzi Mungu ya Kwanza kusamehe wale wote wenye kuzifata hizo njia 10, Japo moja ukiishika basi haikupotezi, isipokua ikiwa hutaki mwenyewe huo msamaha, Na hizo njia kumi nilizozitaja ni kama mtego ukiikamata yoyote inakuongoza kwenye haki, inakupeleka kwenye Ahadi ya Pili nayo ni ya kulipwa Ujira, Na hakuna ujira anostahiki Mja isipokua hiyo Pepo, amabayo imeandaliwa na Mwenye Enzi Mungu kwa ajili yetu, ikiwa Raha na Furaha za Uhai hali hii, Ina hali gani hiyo Pepo kwa Viumbe sisi wenye tamaa ya kuipata hiyo pepo.
Basi hakuna cha kufanya isipokua Fata njia hizo kumi ambazo zina kuhakikishia kupata huo msamaha na hiyo Pepo. Mollah wetu tujaalie tuwe Miongoni wa wenye kupata Msamaha wako na ujira ulo tuwekea kutupa.Amin
Sunday, February 9, 2014
KUFA HUKU UMEFURAHI PART 1
Asalaam Aleiykum,
Tunaingia katika ile Darsa ambayo sote tunaiogopa, Maudhui ambayo yakitajwa Mtu anasema huyoo keshanza kututia dhiki, lakini ni wajibu wangu kukumbusha na kufundisha vipi utaikabili siku hii Adhimu, yenye vishindo na machungu makubwa ambayo mwanaadamu anakumbana nayo, Imekua siku hii kila Mtu anaiogopa na yuko tayari anywe madonge kama Mlima kuepukana nayo, au kama kuna vidonge vya kuweza kuisahau basi atakunywa ili asikumbuke, lakini vidonge hakuna ila kuna Milima ya Dhanmbi ambayo Mwanaadamu ndio kaamua kujificha ili Kifo kikija kimjie ghafla, hataki kukijua hataki kukikumbuka na akikumbushwa anakua mkali. Sasa kwanini wakati wa Mauti unakua na hofu kubwa?.
Khofu inakuja sababu kubwa ni ile ya kumsahau Mollah wako Muumba, Ni kwa ajili ya kujua sasa unakwenda kukutana naye, Na hujui nini kitakukuta, Na kwa wakati huo wa Mauti unakua wewe mweupe, safi, huna cha kukukera akili imeshasimama haitumiki tena, Inakua Baina ya Roho na wale walokuzunguka viumbe wasiri(Malaika)Unazinduka wakati huo ukitokea usingizini wa Uhai na kuingia kwenye mzinduko wa Mauti, Hapo tena unayaona yote ulokua unaambiwa ukawa unayatilia mashaka yanatokea (Live)na wewe ukiwa Shahidi wake, unaanza kuonja Uchungu wa kutolewa (Roho)Unaanza kujua vipi Maumivu ya kukosa (Oxygen) na balaa yake, jasho linakumiminika huku ukiwaza lau wangejua wangenipa (Pipa)zima la (Oxygen). Hivo ndio inavotokea wakati wa kufa, pale (Body)Ishaanza Ku(Shut Down)taratibu, na huku unashangaa Nani hawa walonizunguka mbona hawacheki, na hii Operesheni wanonifanyia ya nini? hapo ndipo unaposomewa aya ya 92mpaka93. "Kwani situlikwambia kama utakua hivo ulivo sasa na sisi tutakutana na wewe tukujulishe".
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّين
"Na kama akiwa ni miongoni mwa waliokadhibisha, wapotofu" Hiyo ndio hali unayokutana nayo, Mauti yanakua shida tupu,
فَنُزُلٌ۬ مِّنۡ حَمِيمٍ۬
Basi karamu (yako)ni maji ya moto yachemkayo, Vuke lenye kukata (Oxygen), basi ikiwa wewe Mwenye kujiwa na hofu na siku hii ya miadi, au ikiwa unaghafilika nayo siku hii basi inapasa ujiulize Mwenyewe kwa Mwenyewe "Ewe Moyo Wangu" Nihadithie kwani kuna Jambo gani kubwa umefanya hata nikawa nina hofu mimi ya siku hii? Mbona naogopa sana, lazima iko sababu pengine kwa haya ninayoyatenda, na kama unaendelea kuyatenda (Ushauri utokao kwangu nakushauri ili uweze kuacha basi fanya uone Maiti japo tatu, itakusaidia sana kuchenji mwenendo wako, utabadilika uwe Mtu mwengine kabisa) Naam, utapata mateso makubwa siku yako ya kutoka Roho ikiwa una maradhi ya Mali au cheo, Au umebakisha chuki moyoni, Tahadhari sana kuweka hamaki na ghadhabu utakua hasarani siku hiyo ya siku, ondosha sasa hivi kama una husda au wivu na choyo kwa Binaadamu wenzio usije ukateseka siku ya kutolewa Roho yako, kwani ukiyaweka Rohoni ni lazima (Malaika)waanze kuyakumta hayo kwanza halafu ndio waanze kuifanyia kazi Roho, huku watu wanaulizana vipi hali yake, wanajibiwa siku ya tatu leo yumo kwenye msukosuko mkubwa, huku wewe umelala kwenye tandiko la Mauti, na visasi vyako, unaondoka na magonvi umeyashikilia Rohoni, weka mbali na zile Dhanmbi ulizokua hujatubu kumbuka vitakupa uzito mkubwa siku yako ya kutolewa Roho.
Sasa Ufanye nini uondokane na hali hiyo?
Endelea Part 2
Tunaingia katika ile Darsa ambayo sote tunaiogopa, Maudhui ambayo yakitajwa Mtu anasema huyoo keshanza kututia dhiki, lakini ni wajibu wangu kukumbusha na kufundisha vipi utaikabili siku hii Adhimu, yenye vishindo na machungu makubwa ambayo mwanaadamu anakumbana nayo, Imekua siku hii kila Mtu anaiogopa na yuko tayari anywe madonge kama Mlima kuepukana nayo, au kama kuna vidonge vya kuweza kuisahau basi atakunywa ili asikumbuke, lakini vidonge hakuna ila kuna Milima ya Dhanmbi ambayo Mwanaadamu ndio kaamua kujificha ili Kifo kikija kimjie ghafla, hataki kukijua hataki kukikumbuka na akikumbushwa anakua mkali. Sasa kwanini wakati wa Mauti unakua na hofu kubwa?.
Khofu inakuja sababu kubwa ni ile ya kumsahau Mollah wako Muumba, Ni kwa ajili ya kujua sasa unakwenda kukutana naye, Na hujui nini kitakukuta, Na kwa wakati huo wa Mauti unakua wewe mweupe, safi, huna cha kukukera akili imeshasimama haitumiki tena, Inakua Baina ya Roho na wale walokuzunguka viumbe wasiri(Malaika)Unazinduka wakati huo ukitokea usingizini wa Uhai na kuingia kwenye mzinduko wa Mauti, Hapo tena unayaona yote ulokua unaambiwa ukawa unayatilia mashaka yanatokea (Live)na wewe ukiwa Shahidi wake, unaanza kuonja Uchungu wa kutolewa (Roho)Unaanza kujua vipi Maumivu ya kukosa (Oxygen) na balaa yake, jasho linakumiminika huku ukiwaza lau wangejua wangenipa (Pipa)zima la (Oxygen). Hivo ndio inavotokea wakati wa kufa, pale (Body)Ishaanza Ku(Shut Down)taratibu, na huku unashangaa Nani hawa walonizunguka mbona hawacheki, na hii Operesheni wanonifanyia ya nini? hapo ndipo unaposomewa aya ya 92mpaka93. "Kwani situlikwambia kama utakua hivo ulivo sasa na sisi tutakutana na wewe tukujulishe".
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّين
"Na kama akiwa ni miongoni mwa waliokadhibisha, wapotofu" Hiyo ndio hali unayokutana nayo, Mauti yanakua shida tupu,
فَنُزُلٌ۬ مِّنۡ حَمِيمٍ۬
Basi karamu (yako)ni maji ya moto yachemkayo, Vuke lenye kukata (Oxygen), basi ikiwa wewe Mwenye kujiwa na hofu na siku hii ya miadi, au ikiwa unaghafilika nayo siku hii basi inapasa ujiulize Mwenyewe kwa Mwenyewe "Ewe Moyo Wangu" Nihadithie kwani kuna Jambo gani kubwa umefanya hata nikawa nina hofu mimi ya siku hii? Mbona naogopa sana, lazima iko sababu pengine kwa haya ninayoyatenda, na kama unaendelea kuyatenda (Ushauri utokao kwangu nakushauri ili uweze kuacha basi fanya uone Maiti japo tatu, itakusaidia sana kuchenji mwenendo wako, utabadilika uwe Mtu mwengine kabisa) Naam, utapata mateso makubwa siku yako ya kutoka Roho ikiwa una maradhi ya Mali au cheo, Au umebakisha chuki moyoni, Tahadhari sana kuweka hamaki na ghadhabu utakua hasarani siku hiyo ya siku, ondosha sasa hivi kama una husda au wivu na choyo kwa Binaadamu wenzio usije ukateseka siku ya kutolewa Roho yako, kwani ukiyaweka Rohoni ni lazima (Malaika)waanze kuyakumta hayo kwanza halafu ndio waanze kuifanyia kazi Roho, huku watu wanaulizana vipi hali yake, wanajibiwa siku ya tatu leo yumo kwenye msukosuko mkubwa, huku wewe umelala kwenye tandiko la Mauti, na visasi vyako, unaondoka na magonvi umeyashikilia Rohoni, weka mbali na zile Dhanmbi ulizokua hujatubu kumbuka vitakupa uzito mkubwa siku yako ya kutolewa Roho.
Sasa Ufanye nini uondokane na hali hiyo?
Endelea Part 2
KUFA HUKU UMEFURAHI PART 2
Asalaam Aleiykum,
Inatakiwa uanze kuchukua tahadhari sasa ungali mzima bado una hema, inabidi tukukumbushe zile operesheni mbili moja wanakufanyia wanaadamu wenzio kukuponesha maradhi yako, na ya Pili wanakufanyia Malaika kuitoa Roho yako katika hiyo (Body). Sasa Utakua na hali gani kama nikikujulisha kuwa kuna uwezekano wa kukutana na siku hii ukiwa umefurahi, jee uwezekano huo Upo?.
Naam Uwezekano upo, safari hiyo wewe unakwenda kila siku huku umefurahi kwanini siku hiyo iwe hujafurahi, Mwenye Enzi Mungu anasema katika Sura ya Al-Anaam aya ya 60.
"وَهُوَ ٱلَّذِى يَتَوَفَّٮٰڪُم بِٱلَّيۡلِ وَيَعۡلَمُ مَا جَرَحۡتُم بِٱلنَّہَارِ ثُمَّ يَبۡعَثُڪُمۡ فِيهِ لِيُقۡضَىٰٓ أَجَلٌ۬ مُّسَمًّ۬ىۖ "
Naye (Mollah wenu)Ndiye anayekufisheni(Kufa)wakati wa usiku, Na anakijua mlichofanya mchana, ikisha Yeye hukufufueni humo mchana ili muda ulowekwa utimizwe.(Mpaka mwisho wa aya)
Sasa ikiwa pahala hapo hapo kila usiku unakwenda mwenyewe kitandani ili upate kwenda huko ulikotokea leo vipi uwe na mashaka, kwanini usifurahi kama unavofurahi siku zote, na ukiamka tu unatuhadithia jana nimelala vizuri, kwani ile (Final)uwe na woga mkubwa kupita kiasi, (Hufikiri kama lazima kuna kitu hapo)umekichunguza kitu gani. Tunaendelea.
Uwezekano upo na wengi wa Waja wema wameondoka kwenye Ulimwengu huu wanafuraha ya kukutana na Mollah wao, sasa kwanini na wewe usiwe miongoni mwao?
Kuna visa vimetokea itabidi munipe Radhi zenu ili niwahadithie, vipo vingi lakini nakupeni viwili ambavyo mimi nimekua Shahidi wake. Kuna waja wema wanaondoka katika Dunia hii wanapanga mpaka maziko yao yawe vipi, huku kashanunua Sanda yake kwa Pesa za halali, Na ikisha anaagiza fulani na fulani ndio waingie kwenye kaburi langu, na kweli unashuhudia siku ya maziko yake hayo yote yanafanyika, Sasa wao walikua wanajua nini ambacho kimewafikisha katika daraja hiyo, Na kwanini sisi leo ambao wengi wetu tunasema watu wa zamani hawakusoma dini, sisi ndio tulosoma, mbona tunaogopa kununua Sanda, wangapi leo wenye Sanda zao majumbani,(Utakuta Mtu anaandika "Will"(Karatasi ya Urithi)lakini anaogopa kununua Sanda)sasa ndio unafanya nini? vipi leo ukiumwa na Kichwa tu unaanza kutetemeka, Nini kimekukuta?.
Masiku ya karibuni hivi nilikutana na Mzee Mmoja ambaye masiku yake yakuondoka Ulimwenguni yashakaribia, kwa kuwa anafahamu mimi natambua baadhi ya ishara akataka anifahamishe au anifundishe kitu kama nitakua nimesahau, Akanambia Mwanangu sasa mimi niko tayari kwenda, mimi nishajiandaa, kila kitu kiko tayari, (Na huko ndio njia ya kufahamiana kwa lugha ya Mystcism)nikamjibu naelewa, huku machozi yanatoka katika moyo wangu, kwa sababu watu kama hao akikwambia maneno kama hayo basi inakua hamalizi miezi sita, na kweli kabla ya miezi sita kutimia hiyo Roho yake ikarudi kwa Mollah wake, na mimi nikapata bahati ya kuwepo kwenye mazishi yake basi nilmbusu kipaji cha sura yake kwa (Elimu)aliyoniachia kwa njia ya (Communion).
Kwanini usiondoke umefurahi wakati kila usiku unakwenda huko huko ulipotokea, tafauti yake siku ya mwisho unaamshwa ndani ya usingizi, kuna wengine wanapata kwa bahati, (Hunipa habari nikawa nacheka sababu siwezi kuwafahamisha wakafahamu hicho walichokutana nacho ni kitendawili gani)anahadithia mtu ndani ya ndoto yake kaamka na anaiona ile ndoto, umepata kujiuliza nani Mwenye kuiona hiyo Ndoto, unaijua ladha ya kuamka ndani ya usingizi ukawa unaona ndoto yako, basi wako wenye kupata bahati hiyo mtu akakwambia na mimi nimejiona nimo kwenye ndoto, siku zote kumbuka ukiota hujioni kwenye ndoto, au huchunguzi kwanini huoti hapo ulipolala?, kwa hiyo siku ya Mauti, inakua hali kama hiyo ya kuamka kwenye Ndoto yako, unauona usingizi wako, kwanini sasa una woga, kwanini hufurahi kama alivokwambia Mollah wako
Fajr aya ya 27 mpaka 30 "يَـٰٓأَيَّتُہَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَٮِٕنَّةُ "
Ewe Nafs iliyo tua,
Ipi nafs iliyotua? Unaijua Nafs ilotua, Ushawahi kuyaona maji yalivotulia kwenye (Mtungi) hakuna hata kitone chenye kutingishika, Kutulia huku kunakuwa kuondokewa na yale yote niloyataja hapo mwanzoni yakawa hayamo kwenye Roho yako, kutulia kwenyewe kunakuwa umeshapita daraja zote za matamanio, anaweza kuja Mwanaume au Mwanamke ikawa ndani ya Maumbile yako hakuna chochote chenye kutokea(Jitizame sasa hivi unakuaje wakitokezea), Unaweza kuona mapesa ikawa hushtuki kabisa, unaweza kutaka kupewa cheo ukawa huna hata haja nacho, ndani ya nafs yako hakuna cha kukushtua umetulia makini huna magonvi wala chuki, huna mashaka kabisa ya kilimwengu, umepoa baridi, kinachokujia katika utulivu huo ni kumkumbuka Mollah wako, ukiingia mchana unasubiri usiku ufike ili uwe karibu na Mollah wako, na ukimalizika usiku una hamu uingie mchana ili upate utulivu wa kushuhudia zawadi ya uhai inavotenda kazi zake, haupatikani usemi katika ulimi wako au fikra isipokua maneno ya kumsabahi Mollah wako, hayaaingii tena mawazo ya kipuuzi katika kichwa chako. Hapo tena unakithiri katika Ibada na kuomba mapenzi ya Mollah wako yakushukie, ukidumu katika hali hiyo Mollah wako anakwambia Nini?
Endelea Part 3
Inatakiwa uanze kuchukua tahadhari sasa ungali mzima bado una hema, inabidi tukukumbushe zile operesheni mbili moja wanakufanyia wanaadamu wenzio kukuponesha maradhi yako, na ya Pili wanakufanyia Malaika kuitoa Roho yako katika hiyo (Body). Sasa Utakua na hali gani kama nikikujulisha kuwa kuna uwezekano wa kukutana na siku hii ukiwa umefurahi, jee uwezekano huo Upo?.
Naam Uwezekano upo, safari hiyo wewe unakwenda kila siku huku umefurahi kwanini siku hiyo iwe hujafurahi, Mwenye Enzi Mungu anasema katika Sura ya Al-Anaam aya ya 60.
"وَهُوَ ٱلَّذِى يَتَوَفَّٮٰڪُم بِٱلَّيۡلِ وَيَعۡلَمُ مَا جَرَحۡتُم بِٱلنَّہَارِ ثُمَّ يَبۡعَثُڪُمۡ فِيهِ لِيُقۡضَىٰٓ أَجَلٌ۬ مُّسَمًّ۬ىۖ "
Naye (Mollah wenu)Ndiye anayekufisheni(Kufa)wakati wa usiku, Na anakijua mlichofanya mchana, ikisha Yeye hukufufueni humo mchana ili muda ulowekwa utimizwe.(Mpaka mwisho wa aya)
Sasa ikiwa pahala hapo hapo kila usiku unakwenda mwenyewe kitandani ili upate kwenda huko ulikotokea leo vipi uwe na mashaka, kwanini usifurahi kama unavofurahi siku zote, na ukiamka tu unatuhadithia jana nimelala vizuri, kwani ile (Final)uwe na woga mkubwa kupita kiasi, (Hufikiri kama lazima kuna kitu hapo)umekichunguza kitu gani. Tunaendelea.
Uwezekano upo na wengi wa Waja wema wameondoka kwenye Ulimwengu huu wanafuraha ya kukutana na Mollah wao, sasa kwanini na wewe usiwe miongoni mwao?
Kuna visa vimetokea itabidi munipe Radhi zenu ili niwahadithie, vipo vingi lakini nakupeni viwili ambavyo mimi nimekua Shahidi wake. Kuna waja wema wanaondoka katika Dunia hii wanapanga mpaka maziko yao yawe vipi, huku kashanunua Sanda yake kwa Pesa za halali, Na ikisha anaagiza fulani na fulani ndio waingie kwenye kaburi langu, na kweli unashuhudia siku ya maziko yake hayo yote yanafanyika, Sasa wao walikua wanajua nini ambacho kimewafikisha katika daraja hiyo, Na kwanini sisi leo ambao wengi wetu tunasema watu wa zamani hawakusoma dini, sisi ndio tulosoma, mbona tunaogopa kununua Sanda, wangapi leo wenye Sanda zao majumbani,(Utakuta Mtu anaandika "Will"(Karatasi ya Urithi)lakini anaogopa kununua Sanda)sasa ndio unafanya nini? vipi leo ukiumwa na Kichwa tu unaanza kutetemeka, Nini kimekukuta?.
Masiku ya karibuni hivi nilikutana na Mzee Mmoja ambaye masiku yake yakuondoka Ulimwenguni yashakaribia, kwa kuwa anafahamu mimi natambua baadhi ya ishara akataka anifahamishe au anifundishe kitu kama nitakua nimesahau, Akanambia Mwanangu sasa mimi niko tayari kwenda, mimi nishajiandaa, kila kitu kiko tayari, (Na huko ndio njia ya kufahamiana kwa lugha ya Mystcism)nikamjibu naelewa, huku machozi yanatoka katika moyo wangu, kwa sababu watu kama hao akikwambia maneno kama hayo basi inakua hamalizi miezi sita, na kweli kabla ya miezi sita kutimia hiyo Roho yake ikarudi kwa Mollah wake, na mimi nikapata bahati ya kuwepo kwenye mazishi yake basi nilmbusu kipaji cha sura yake kwa (Elimu)aliyoniachia kwa njia ya (Communion).
Kwanini usiondoke umefurahi wakati kila usiku unakwenda huko huko ulipotokea, tafauti yake siku ya mwisho unaamshwa ndani ya usingizi, kuna wengine wanapata kwa bahati, (Hunipa habari nikawa nacheka sababu siwezi kuwafahamisha wakafahamu hicho walichokutana nacho ni kitendawili gani)anahadithia mtu ndani ya ndoto yake kaamka na anaiona ile ndoto, umepata kujiuliza nani Mwenye kuiona hiyo Ndoto, unaijua ladha ya kuamka ndani ya usingizi ukawa unaona ndoto yako, basi wako wenye kupata bahati hiyo mtu akakwambia na mimi nimejiona nimo kwenye ndoto, siku zote kumbuka ukiota hujioni kwenye ndoto, au huchunguzi kwanini huoti hapo ulipolala?, kwa hiyo siku ya Mauti, inakua hali kama hiyo ya kuamka kwenye Ndoto yako, unauona usingizi wako, kwanini sasa una woga, kwanini hufurahi kama alivokwambia Mollah wako
Fajr aya ya 27 mpaka 30 "يَـٰٓأَيَّتُہَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَٮِٕنَّةُ "
Ewe Nafs iliyo tua,
Ipi nafs iliyotua? Unaijua Nafs ilotua, Ushawahi kuyaona maji yalivotulia kwenye (Mtungi) hakuna hata kitone chenye kutingishika, Kutulia huku kunakuwa kuondokewa na yale yote niloyataja hapo mwanzoni yakawa hayamo kwenye Roho yako, kutulia kwenyewe kunakuwa umeshapita daraja zote za matamanio, anaweza kuja Mwanaume au Mwanamke ikawa ndani ya Maumbile yako hakuna chochote chenye kutokea(Jitizame sasa hivi unakuaje wakitokezea), Unaweza kuona mapesa ikawa hushtuki kabisa, unaweza kutaka kupewa cheo ukawa huna hata haja nacho, ndani ya nafs yako hakuna cha kukushtua umetulia makini huna magonvi wala chuki, huna mashaka kabisa ya kilimwengu, umepoa baridi, kinachokujia katika utulivu huo ni kumkumbuka Mollah wako, ukiingia mchana unasubiri usiku ufike ili uwe karibu na Mollah wako, na ukimalizika usiku una hamu uingie mchana ili upate utulivu wa kushuhudia zawadi ya uhai inavotenda kazi zake, haupatikani usemi katika ulimi wako au fikra isipokua maneno ya kumsabahi Mollah wako, hayaaingii tena mawazo ya kipuuzi katika kichwa chako. Hapo tena unakithiri katika Ibada na kuomba mapenzi ya Mollah wako yakushukie, ukidumu katika hali hiyo Mollah wako anakwambia Nini?
Endelea Part 3
KUFA HUKU UMEFURAHI PART 3
Asalaam Aleiykum,
ٱرۡجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً۬ مَّرۡضِيَّةً۬
Rejea kwa Mollah wako Mlezi umeridhika, Na Umemridhisha,
Vipi utaridhika, utaridhika pale utakapokua umeshajisafisha kikamilifu, vipi utajisafisha kikamilifu, inabidi uende ndani kwanza kujutia moja baada ya jengine yale uloyafanya, na utake Maghfira(Msamaha)kwa kila kosa ulolitenda, yale unoweza kuyasawazisha, basi yasawazishe, na yale usoweza basi egemea kwa Mollah wako kwa maombi ya msamaha na Ibada za kila wakati na huko ndiko kumridhisha, na ukifanya hivyo sasa utakua tayari wewe kurejea kwa Mollah wako kwa Usalama na bila ya shaka yoyote.
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Basi ikiwa huyo (Anofariki)ni miongoni walokaribishwa(Na Mollah wao). Basi hapo furaha tupu, Roho inatoka huku unahadithia kama kisa cha mzee wetu huyu wapili ambaye yeye wakati wa kifo chake alikua yumacho, na hakuna kifo kizuri kama hicho, inaonesha umeridhika kwenda kukutana na Mollah wako, Huyu yeye alikua anakufa huku anaona Roho yake inavotolewa, akawa anahadithia bila ya machungu wala woga, na wala hakuchagua kufa huku kalala, au kufa huku kazimia, yeye aliamua kufa huku anahadithia Roho inavotolewa, akisema nini? "Hao wameanza kunitoa kwenye kidole, wananitoa taratibu sasa washafika miguuni sina hisia tena, akasema sasa wanapanda kidogo kidogo sehemu ya kiunoni sina nguvu tena, akaendelea kusema wamefikia kwenye mbavu wanaivuta Roho taratibu, akasema sasa wacheni nikuageni wanakaribia kwenye moyo, nahisi watakapofika kwenye ulimi nitashindwa kuhadithia, akamwambia mwanawe nipe mkono nikuage kabla nguvu hazijaniishia kabisa, Mwisho akasema hao wanaipandisha mabegani, akatizama juu kimya, ikisha hayo macho yake yakabiruka na kuondoka katika Ulimwengu huu.
فَرَوۡحٌ۬ وَرَيۡحَانٌ۬ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ۬
Basi ni Raha(ilioje)na Manukato na mabustani yenye neema.
Hicho ndio kifo cha Shahada unakufa hakuna machungu wala woga, hakuna kuteseka wala vitisho na cha zaidi unahadithia mambo yanavotokea, Wanayapataje haya hao wanofurahi katika vifo vyao(Usije ukaona furaha wanapiga makofi)kusudio lake wameridhika, ni bora waihame Dunia waende kwa Mollah wao, na ukitamani kurudi kwa Mollah wako ni furaha kubwa Mwanaadamu huwezi kuilinganisha na jambo lolote.
Sasa nini ufanye ukipate kifo hiki?
Unatakiwa uwe Mtu mwema sana, Uwe Mcha Mungu mwenye kuyatafuta mapenzi ya Mollah wako kikweli kweli,unatakiwa uanze kubadilika sasa hivi, Na kubadilika kwenyewe ni huko kujiuliza hili Swali?
Wapi nimetokea? Na nini nilifanya ili kuibebesha Roho yangu mizigo hii nilonayo. Wapi ninapokwenda na nini itakua khatima yangu? siku yangu ya kutolewa Roho, zikikujia hisia hizo anguka kwa Mollah wako na umuombe "Ewe Mollah yabadilishe mabaya yangu kuwa mema"na hayawezi kubadilika mpaka uonekane kweli sasa huna haja ya Ulimwengu huu, nikimaanisha chochote kile unamwachia Mollah wako ndie awe muamuzi na ukifikia daraja hiyo unakua (Non-Attachment) hapo unaishi katika maisha ya kutulia, kila kitu umekiridhia, Mauti yakija sawa, maradhi yakija sawa, mvua ikinyesha kwako sawa, jua likitoka kwako sawa, unakua ni mwenye kumtegemea Mollah wako nakuridhia kila alokupangia, ndio hata wakati wa kufa kwako unakua na furaha unajua sasa wakati umefika wa mimi kwenda kwa Kipenzi Mollah wangu, na kama nani mwenye kuhamaki kukutana na kipenzi chake, Usiwe na Woga na hamaki za kukataa kwenda kukutana na mpenzi mollah wako.
Na Fahamu kumbe Maisha yameumbwa na kifo kimeumbwa, vyote ni njia lazima nipite, lazima niridhie ni mambo katika jambo la uhai.
Mollah wetu tujaalie mwisho mwema. Amin.
ٱرۡجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً۬ مَّرۡضِيَّةً۬
Rejea kwa Mollah wako Mlezi umeridhika, Na Umemridhisha,
Vipi utaridhika, utaridhika pale utakapokua umeshajisafisha kikamilifu, vipi utajisafisha kikamilifu, inabidi uende ndani kwanza kujutia moja baada ya jengine yale uloyafanya, na utake Maghfira(Msamaha)kwa kila kosa ulolitenda, yale unoweza kuyasawazisha, basi yasawazishe, na yale usoweza basi egemea kwa Mollah wako kwa maombi ya msamaha na Ibada za kila wakati na huko ndiko kumridhisha, na ukifanya hivyo sasa utakua tayari wewe kurejea kwa Mollah wako kwa Usalama na bila ya shaka yoyote.
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Basi ikiwa huyo (Anofariki)ni miongoni walokaribishwa(Na Mollah wao). Basi hapo furaha tupu, Roho inatoka huku unahadithia kama kisa cha mzee wetu huyu wapili ambaye yeye wakati wa kifo chake alikua yumacho, na hakuna kifo kizuri kama hicho, inaonesha umeridhika kwenda kukutana na Mollah wako, Huyu yeye alikua anakufa huku anaona Roho yake inavotolewa, akawa anahadithia bila ya machungu wala woga, na wala hakuchagua kufa huku kalala, au kufa huku kazimia, yeye aliamua kufa huku anahadithia Roho inavotolewa, akisema nini? "Hao wameanza kunitoa kwenye kidole, wananitoa taratibu sasa washafika miguuni sina hisia tena, akasema sasa wanapanda kidogo kidogo sehemu ya kiunoni sina nguvu tena, akaendelea kusema wamefikia kwenye mbavu wanaivuta Roho taratibu, akasema sasa wacheni nikuageni wanakaribia kwenye moyo, nahisi watakapofika kwenye ulimi nitashindwa kuhadithia, akamwambia mwanawe nipe mkono nikuage kabla nguvu hazijaniishia kabisa, Mwisho akasema hao wanaipandisha mabegani, akatizama juu kimya, ikisha hayo macho yake yakabiruka na kuondoka katika Ulimwengu huu.
فَرَوۡحٌ۬ وَرَيۡحَانٌ۬ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ۬
Basi ni Raha(ilioje)na Manukato na mabustani yenye neema.
Hicho ndio kifo cha Shahada unakufa hakuna machungu wala woga, hakuna kuteseka wala vitisho na cha zaidi unahadithia mambo yanavotokea, Wanayapataje haya hao wanofurahi katika vifo vyao(Usije ukaona furaha wanapiga makofi)kusudio lake wameridhika, ni bora waihame Dunia waende kwa Mollah wao, na ukitamani kurudi kwa Mollah wako ni furaha kubwa Mwanaadamu huwezi kuilinganisha na jambo lolote.
Sasa nini ufanye ukipate kifo hiki?
Unatakiwa uwe Mtu mwema sana, Uwe Mcha Mungu mwenye kuyatafuta mapenzi ya Mollah wako kikweli kweli,unatakiwa uanze kubadilika sasa hivi, Na kubadilika kwenyewe ni huko kujiuliza hili Swali?
Wapi nimetokea? Na nini nilifanya ili kuibebesha Roho yangu mizigo hii nilonayo. Wapi ninapokwenda na nini itakua khatima yangu? siku yangu ya kutolewa Roho, zikikujia hisia hizo anguka kwa Mollah wako na umuombe "Ewe Mollah yabadilishe mabaya yangu kuwa mema"na hayawezi kubadilika mpaka uonekane kweli sasa huna haja ya Ulimwengu huu, nikimaanisha chochote kile unamwachia Mollah wako ndie awe muamuzi na ukifikia daraja hiyo unakua (Non-Attachment) hapo unaishi katika maisha ya kutulia, kila kitu umekiridhia, Mauti yakija sawa, maradhi yakija sawa, mvua ikinyesha kwako sawa, jua likitoka kwako sawa, unakua ni mwenye kumtegemea Mollah wako nakuridhia kila alokupangia, ndio hata wakati wa kufa kwako unakua na furaha unajua sasa wakati umefika wa mimi kwenda kwa Kipenzi Mollah wangu, na kama nani mwenye kuhamaki kukutana na kipenzi chake, Usiwe na Woga na hamaki za kukataa kwenda kukutana na mpenzi mollah wako.
Na Fahamu kumbe Maisha yameumbwa na kifo kimeumbwa, vyote ni njia lazima nipite, lazima niridhie ni mambo katika jambo la uhai.
Mollah wetu tujaalie mwisho mwema. Amin.
Sunday, February 2, 2014
UCHA MUNGU WA GHAFLA PART 1
Asalaam Aleiykum,
Kuna Baadhi ya watu wanapenda njia za rahisi, namie nimewatafutia hii moja labda kama wataiweza wanaweza kuupata Ucha Mungu kwa wepesi kabisa, Na kuna baadhi ya wengine wanapata shida na kuona mambo mazito katika kuupata Ucha Mungu, na kila wakiwaendea Wanazuoni masharti wanayopewa magumu, inabidi wakimbie wakakae njia panda, Sasa mimi katika wachache ambaye natoa (Cheap Ticket)Nakwambia usipate tabu zipo njia za Rahisi kuupata Ucha Mungu, sina vizuizi wala kuambatanisha shuruti lolote lile, sikwambii Shk fulani kasema hivi wala fulani kasema vile, mie nakupeleka kisimani, nakwambia maji haya unaweza chota unywe, huwezi tena mimi hapo sina msaada, Kwangu mie Waumini wote sawa, wote wako katika njia moja ila kwenye njia kuna mabonde na mashimo na yatakiwa umshike mkono kumuonesha mwenzio njia, na hiyo ndio kazi ninayo fanya mimi, Neno langu ninalo kwambia ni moja (Kama kweli mpenzi wa Mungu chupa ujiunge nami).
Bwana Mtume s.a.w Kabla ya kuondoka katika Ulimwengu huu alitupa ishara moja kubwa sana na inafaa kuzingatiwa, Lau kama sisi wenye kuutaka Uislam na kuitafuta hiyo (Taqwa) na kweli tunampenda Mwenye Enzi Mungu basi ishara hii tuloachiwa ni kigezo cha kutosha kuipata hiyo (Taqwa),na sote mwisho wetu ungekua mzuri wa kupigiwa mfano. Alifanya nini kabla ya kufa kwake kipenzi chetu?.
"Alimwita mkewe Bibi Aisha"Akamuuliza ""Ewe Aisha" Ndani ya Nyumba kuna kiasi gani"Wakati huo Bwana Mtume s.a.w yupo katika (Sakaratul Mauti), Na kapata nafuu kidogo, anakuja juu anamuuliza mkewe ndani ziko kiasi gani""Anajibu Bibi Aisha zimebaki (Dirham 7)""Akasema Bwana Mtume s.a.w basi zitowe sadaka" ikisha huyo akazama tena kwenye (Sakaratul Mauti) alipokuja juu tena akamuuliza tena Bibi Aisha umeshazitoa zile (Dirham)Bibi Aisha akajibu hapana maradhi yako yamenishughulisha Ewe Mjumbe wa Mwenye Enzi Mungu, Bwana Mtume s.a.w Akatoa sauti ya Ukali, "Akamwambia Ewe Aisha zitoe upesi hizo pesa" zilipotolewa hiyo Roho ya kipenzi cha Umma huu ikarejea kwa Mollah wake.
"Ewe Muumin, Ewe Muislam kuna mafundisho gani katika tukio hili? Na kwanini zikawa Pesa? tunaingia katika maudhui hii ikiwa yatagonga kwenye Moyo wako, basi moja kwa moja, au hapo hapo linaweza kutokea tukio la wewe Kurehemewa na kupata mabadiliko katika mwenendo wako na mtizamo wako wa mambo ya Kidini, Unaweza kububujikwa na machozi ukaona kumbe hivi, siku zote mimi nimeganda kwenye mapesa wakati hayana faida yoyote, kumbe haya mapesa ndio kizuizi kikubwa cha mimi kuupata huo Ucha Mungu.
Sasa Kwanini Bwana Mtume s.a.w akatumia wakati wa kufa kwake ndio atufundishe Darsa hii ya mwisho.?
Endelea Part 2
Kuna Baadhi ya watu wanapenda njia za rahisi, namie nimewatafutia hii moja labda kama wataiweza wanaweza kuupata Ucha Mungu kwa wepesi kabisa, Na kuna baadhi ya wengine wanapata shida na kuona mambo mazito katika kuupata Ucha Mungu, na kila wakiwaendea Wanazuoni masharti wanayopewa magumu, inabidi wakimbie wakakae njia panda, Sasa mimi katika wachache ambaye natoa (Cheap Ticket)Nakwambia usipate tabu zipo njia za Rahisi kuupata Ucha Mungu, sina vizuizi wala kuambatanisha shuruti lolote lile, sikwambii Shk fulani kasema hivi wala fulani kasema vile, mie nakupeleka kisimani, nakwambia maji haya unaweza chota unywe, huwezi tena mimi hapo sina msaada, Kwangu mie Waumini wote sawa, wote wako katika njia moja ila kwenye njia kuna mabonde na mashimo na yatakiwa umshike mkono kumuonesha mwenzio njia, na hiyo ndio kazi ninayo fanya mimi, Neno langu ninalo kwambia ni moja (Kama kweli mpenzi wa Mungu chupa ujiunge nami).
Bwana Mtume s.a.w Kabla ya kuondoka katika Ulimwengu huu alitupa ishara moja kubwa sana na inafaa kuzingatiwa, Lau kama sisi wenye kuutaka Uislam na kuitafuta hiyo (Taqwa) na kweli tunampenda Mwenye Enzi Mungu basi ishara hii tuloachiwa ni kigezo cha kutosha kuipata hiyo (Taqwa),na sote mwisho wetu ungekua mzuri wa kupigiwa mfano. Alifanya nini kabla ya kufa kwake kipenzi chetu?.
"Alimwita mkewe Bibi Aisha"Akamuuliza ""Ewe Aisha" Ndani ya Nyumba kuna kiasi gani"Wakati huo Bwana Mtume s.a.w yupo katika (Sakaratul Mauti), Na kapata nafuu kidogo, anakuja juu anamuuliza mkewe ndani ziko kiasi gani""Anajibu Bibi Aisha zimebaki (Dirham 7)""Akasema Bwana Mtume s.a.w basi zitowe sadaka" ikisha huyo akazama tena kwenye (Sakaratul Mauti) alipokuja juu tena akamuuliza tena Bibi Aisha umeshazitoa zile (Dirham)Bibi Aisha akajibu hapana maradhi yako yamenishughulisha Ewe Mjumbe wa Mwenye Enzi Mungu, Bwana Mtume s.a.w Akatoa sauti ya Ukali, "Akamwambia Ewe Aisha zitoe upesi hizo pesa" zilipotolewa hiyo Roho ya kipenzi cha Umma huu ikarejea kwa Mollah wake.
"Ewe Muumin, Ewe Muislam kuna mafundisho gani katika tukio hili? Na kwanini zikawa Pesa? tunaingia katika maudhui hii ikiwa yatagonga kwenye Moyo wako, basi moja kwa moja, au hapo hapo linaweza kutokea tukio la wewe Kurehemewa na kupata mabadiliko katika mwenendo wako na mtizamo wako wa mambo ya Kidini, Unaweza kububujikwa na machozi ukaona kumbe hivi, siku zote mimi nimeganda kwenye mapesa wakati hayana faida yoyote, kumbe haya mapesa ndio kizuizi kikubwa cha mimi kuupata huo Ucha Mungu.
Sasa Kwanini Bwana Mtume s.a.w akatumia wakati wa kufa kwake ndio atufundishe Darsa hii ya mwisho.?
Endelea Part 2
UCHA MUNGU WA GHAFLA PART 2
Asalaam Aleiykum,
Ilikuaje Bwana Mtume s.a.w akaamua na kusisitiza aondoke msafi katika Ulimwengu huu, Hapa kwa Mwenye Akili na yule anayetaka Ucha Mungu kuna mazingatio makubwa na faida isiyo na mwisho,"Ewe Aisha zitoe haraka" Vipi Kipenzi cha Mwenye Enzi Mungu atarejea kwa Mollah wake akiwa na (Dirham 7), Yeye anaelewa kaja katika Ulimwengu huu hana chochote, Na hivi ndio sote tunavokuja katika Ulimwengu huu tukiwa Weupe hata nguo inabidi tusaidiwe, Na tukiondoka pia tunaondoka katika hali kama hiyo, Na huo ni mfano wa hakika wa kila Mmoja wetu.
Sasa tizama leo wangapi wameondoka katika Ulimwengu huu, huku nyuma watu wanapiga hesabu ya pesa zake zilizopo kwenye (Account),wamekusanyana ndugu na watoto wanapanga mipango vipi watazikaanga, Vipi watazidi kukuchoma moto kwa Million zako mwenyewe, huyu anawaza atafungua (Guest house)yule anawaza (Hotel) ya aina gani itamfaa, na hivi ndio wengi tunavoondoka katika Ulimwengu huu (Account)limefurika, na huko uendako unaulizwa vile tulokua tunakuruzuku ulikua unavitoa?
Utajibu nini wakati huo, ndio Maana Mtume s.a.w akatuonesha (Symbol)ya (Dinar)kuzitoa, Toweni msije mkaacha mapesa mnarudi kwa Mollah wenu huku nyuma watu wanayatafuna wanavotaka, na kukutia kero zaidi hata dua hawakuombei, washaitupa maiti hao wanakwenda zao.
Sasa kwa ajili gani ikawa pesa? Sababu nikuwa pesa ni kitu kigumu sana mtu kukiacha, Mtu anaweza kuacha yote lakini pesa ikamshinda, watizame wenye pesa, hata akiwa Hospital mahatuti anauliza Ngapi zimetumika,ngapi zimebakia, hesabu ikoje, na nyinyi mlomzunguka mnamuona tajiri mkubwa, lakini kwa wenye kufahamu, wale wacha Mungu wanamuona maskini mkubwa kalala kwenye kitanda, wanamuona hakuna fukara kama yeye, Lau angejikaza kidogo, akafanya bidii angejua kuwa ndani ya (Body)yake ana (Gas) hajachimba, kuna (Petrol)hajavumbua kuna madini ya kila aina lakini bado hajapata ujuzi wa kuitumia mali (Ghafi)hiyo.
Muulize Tajiri baada ya pesa ana nini chengine cha kutoa , utamkuta hana chochote kile cha kutoa, kama kula kiasi kile kile unachokula wewe na yeye ndio anachokula,umaskini umemshika wa Ucha Mungu, lakini muulize Mcha Mungu aliyegundua Utajiri wa Mollah wake atakwambia, Mie nina mambo mengi yaso na idadi, naweza kutoa kila kitu tuka (Share)nina furaha chukua na wewe kidogo, nina Dua sogea nikuombee, Nina Afya (Alhamdullilah) Nina mapenzi kaa karibu na mimi utayapata, nina Usalama ukiwa na mimi utasalimika, nina Imani ukiwa na karibu na mimi utaihisi, nina hichi na kile lakini huwezi kuvipata mpaka uwe karibu na mimi(Uwe karibu na Mollah wako), au ufate mwenendo wangu hayo na mengi mengine kutoka kwa Mollah wangu simalizi kuyahadithia.
Nakuona hivi na wewe una shauku ya kuyataka hayo, unashangaa vipi yanapatikana, Pengine wewe ni Tajiri au unapata Mshahara wa kutosha,, au Maskini hohe hahe nyote mnataraji kuupata huo utajiri wa kutoka kwa Mollah waenu, Mnatamani (Ghafla Uwe Mcha Mungu) lakini hujui ufanye nini, cha kufanya kipo, lakini jee uko tayari kukifanya?.
Endelea part 3
Ilikuaje Bwana Mtume s.a.w akaamua na kusisitiza aondoke msafi katika Ulimwengu huu, Hapa kwa Mwenye Akili na yule anayetaka Ucha Mungu kuna mazingatio makubwa na faida isiyo na mwisho,"Ewe Aisha zitoe haraka" Vipi Kipenzi cha Mwenye Enzi Mungu atarejea kwa Mollah wake akiwa na (Dirham 7), Yeye anaelewa kaja katika Ulimwengu huu hana chochote, Na hivi ndio sote tunavokuja katika Ulimwengu huu tukiwa Weupe hata nguo inabidi tusaidiwe, Na tukiondoka pia tunaondoka katika hali kama hiyo, Na huo ni mfano wa hakika wa kila Mmoja wetu.
Sasa tizama leo wangapi wameondoka katika Ulimwengu huu, huku nyuma watu wanapiga hesabu ya pesa zake zilizopo kwenye (Account),wamekusanyana ndugu na watoto wanapanga mipango vipi watazikaanga, Vipi watazidi kukuchoma moto kwa Million zako mwenyewe, huyu anawaza atafungua (Guest house)yule anawaza (Hotel) ya aina gani itamfaa, na hivi ndio wengi tunavoondoka katika Ulimwengu huu (Account)limefurika, na huko uendako unaulizwa vile tulokua tunakuruzuku ulikua unavitoa?
Utajibu nini wakati huo, ndio Maana Mtume s.a.w akatuonesha (Symbol)ya (Dinar)kuzitoa, Toweni msije mkaacha mapesa mnarudi kwa Mollah wenu huku nyuma watu wanayatafuna wanavotaka, na kukutia kero zaidi hata dua hawakuombei, washaitupa maiti hao wanakwenda zao.
Sasa kwa ajili gani ikawa pesa? Sababu nikuwa pesa ni kitu kigumu sana mtu kukiacha, Mtu anaweza kuacha yote lakini pesa ikamshinda, watizame wenye pesa, hata akiwa Hospital mahatuti anauliza Ngapi zimetumika,ngapi zimebakia, hesabu ikoje, na nyinyi mlomzunguka mnamuona tajiri mkubwa, lakini kwa wenye kufahamu, wale wacha Mungu wanamuona maskini mkubwa kalala kwenye kitanda, wanamuona hakuna fukara kama yeye, Lau angejikaza kidogo, akafanya bidii angejua kuwa ndani ya (Body)yake ana (Gas) hajachimba, kuna (Petrol)hajavumbua kuna madini ya kila aina lakini bado hajapata ujuzi wa kuitumia mali (Ghafi)hiyo.
Muulize Tajiri baada ya pesa ana nini chengine cha kutoa , utamkuta hana chochote kile cha kutoa, kama kula kiasi kile kile unachokula wewe na yeye ndio anachokula,umaskini umemshika wa Ucha Mungu, lakini muulize Mcha Mungu aliyegundua Utajiri wa Mollah wake atakwambia, Mie nina mambo mengi yaso na idadi, naweza kutoa kila kitu tuka (Share)nina furaha chukua na wewe kidogo, nina Dua sogea nikuombee, Nina Afya (Alhamdullilah) Nina mapenzi kaa karibu na mimi utayapata, nina Usalama ukiwa na mimi utasalimika, nina Imani ukiwa na karibu na mimi utaihisi, nina hichi na kile lakini huwezi kuvipata mpaka uwe karibu na mimi(Uwe karibu na Mollah wako), au ufate mwenendo wangu hayo na mengi mengine kutoka kwa Mollah wangu simalizi kuyahadithia.
Nakuona hivi na wewe una shauku ya kuyataka hayo, unashangaa vipi yanapatikana, Pengine wewe ni Tajiri au unapata Mshahara wa kutosha,, au Maskini hohe hahe nyote mnataraji kuupata huo utajiri wa kutoka kwa Mollah waenu, Mnatamani (Ghafla Uwe Mcha Mungu) lakini hujui ufanye nini, cha kufanya kipo, lakini jee uko tayari kukifanya?.
Endelea part 3
UCHA MUNGU WA GHAFLA PART 3
Asalaam Aleiykum,
Mwanzo kabisa Bwana Mtume s.a.w katoa Dirham 7 ili ende kwa Mollah wake Msafi,, Sasa na wewe kama unataka kuyapata mapenzi na huo Ucha Mungu wa Ghafla, Unaambiwa Toa kama unaweza. Utoe Nini?(Al-Imran 92) لَن تَنَالُواْ ٱلۡبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُواْ مِمَّا تُحِبُّونَۚ
"Hamtoweza kuufikia(Kuupata)Wema mpaka mtoe katika vile mnavovipenda".
Nini Wema? Wema ni Mapenzi, Nini Mapenzi, Mapenzi ndio hiyo Taqwa, hamtoweza kuifikia hiyo Taqwa au Mapenzi mpaka mtoe vile mnavovipenda, (Wengine wanauliza Wema unauzwa wapi na mimi nikanunue) Leo ninakujulisha panapo uzwa Wema, wacha nikuoneshe duka linalouzwa huo Wema unalo Mwenyewe, (Shop keeper)Ni wewe bado hujagundua vipi Wema utaweza kuupata, Wewe na Mcha Mungu hamna tafauti, vile vote alokua navyo Mcha Mungu na wewe unavyo, Tafauti yake wewe hujui kuvifikia hivyo alonavyo Mcha Mungu, Ndio Maana unaambiwa ukitaka uvipate basi (Shuruti)lake toa katika kile unachokipenda, Sababu katika hicho unachokipenda nyuma yake kumejificha hiyo Taqwa, hicho unachokipenda ndio kizuizi baina yako na huo Wema, sasa unaambiwa Toa hicho unachokipenda uone (Result) yake, na (Result)yake ni hayo hayo Mapenzi, unatoa unachokipenda unapewa kinachokupenda, (Give n Take) Na kinachokupenda kina utajiri Mkubwa, kinachokupenda ndio chenye utajiri usokatika, kinachokupenda ndio kilokupa hayo unayoyapenda na mengi mengine ambayo yamo kwenye Ulimwengu huu, Kinachokupenda kinaendelea kutoa kila leo, kinachokupenda kwa mapenzi yake kimekupa mpaka huu Uhai na uwezo wa kuyapata hayo unayoyapenda, Yule ambaye anakupenda anakwambia kunifikia mimi, kuwa karibu na mimi, basi toa utengane na hicho unachokipenda, Na utakapo kitoa tu, basi mimi na wewe tunakutana na unakuwa Kipenzi changu, madhila na dhiki yanakuondoka, shida na matatizo zinatoweka, lakini lazima utoe unachokipenda, hiyo ndio (Thamani unayotakiwa ulipie Penzi la Taqwa).
Katika kutoa kuna Raha fulani inapatikana kwa anaepewa na mwenye kutoa, lakini ukiona umehisi raha fulani katika kutoa huko basi hiyo inakua bado hujatoa, kutoa ili uupate Ucha Mungu inatakiwa Mtowaji hayupo na nafasi yake kabaki Mwenye Enzi Mungu, "Ewe"Mwenye Mali au Mapesa unajiuliza kutoa huku kuna kuwaje ili nipate Ucha Mungu(Mfano)Una Million 20(Au Kidani chako chako cha Almasi), watafute Maskini kumi waambie nimeamrishwa na Mollah wangu hizi Million 10 kumi nikupeni nyinyi ili muanze biashara na hizi sikupeni mimi ila Amri ya Mollah wangu na mimi nimo katika kuitekeleza, Au una nyumba tatu unatoa moja kuwapa wasiokuwa na uwezo iwe yao mali yao, tena iwe ili nzuri unayoipenda, unawapa hii kakupeni Mollah wangu kaeni familia nzima.
Na "Ewe" Mwenye Mshahara mkubwa zikimbilie kheri za kuwalisha viumbe wenzio unaowajua wana shida. nyumba ina watoto 7 mzee wao ana hangaika kutafuta Riziki, sema kuanzia leo mimi nitakua naleta chakula mpaka mtakapopata uwezo, nusu mshahara wangu utakua haki yenu, nachukua dhamana hiyo kwa kutafuta Radhi za Mollah wangu.
Na "Ewe" Maskini msokitu wewe unakikubwa zaidi cha kujitolea, sema Mollah wangu najikabidhi kwako kwa haki ya uhai wangu niwe Mtumwa wako katika kukuabudu wewe, katika kuwatumikia viumbe vyako kama utavyoniamrisha, "Ewe"Mollah wangu unaujua udhaifu wangu mimi sina cha kutoa na wala sina ninachokipenda isipokua dhati yako yenye Uweza, basi nipe mimi Ridhaa yako ya kuupata huo Wema ulojaa Neema zako, wewe Mollah wangu ni mwenye kujaalia Mapenzi, basi naomba nichague katika wale viumbe vyako uloviongoza katika hayo Mapenzi yako ya Taqwa.
وَمَا تُنفِقُواْ مِن شَىۡءٍ۬ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٌ۬
"Na chochote mnachokitoa, Basi Mwenye Enzi Mungu anakijua"
usije ukajifanya mjanja unatoa nyumba yako mbovu, inayotakiwa ni ile mpya yenye (swimming Pool), au ukawapa pesa huku unawanongoneza ukipata utanirudishia, au unaomba dua Mollah nipe utajiri nishachoka kusubiri, toka nimenyanyukia nahangaika na maisha basi nipe na mimi ikisha ntafanya Ibada kwa wingi, Mollah ni mwenye kujua kila mipango yako ilofichika kwenye kifua chako.
Usiwe mwenye kutoa kama mwana siasa au mfanya biashara mpaka Wapiga picha wawepo, au watu wajue katoa, huko sikutoa kwa (Ikhlas) ni shirk ya kujionesha, kutoa kwa kweli ni kule unajua wewe tu na mpokeaji kama umetoa, huna haja ya matangazo au picha au usikike redioni, na ukitoa kama alivoamrisha Mollah wako basi kwa hakika yanaanza kukushukia mapenzi hiyo ni (Gurantee) wewe toa, utakuja nikumbuka ukitoa kile unachokipenda kweli katika moyo wako basi na huku (Something happen)katika moyo ikisha inaanza ku (Grow slowly) na kikisha ota kwa ukamilifu wewe Mcha Mungu, wewe ushaupata huo wema, na ni Bora kuishi na Wema kuliko kuwa Millionea. Sasa jitizame ukimpenda Mtu unakuwaje, sasa yapime mapenzi hayo hayo lakini yameongezeka mara million unapenda kitu usichokiona, na kila siku zikizidi unashauku ya kukisogelea karibu kutaka kukijua, na kila ukisogea mapenzi yanazidi, na maajabu yanaongezeka na huo ndio Ucha Mungu ambao tunamuomba Mollah atujaalie kwa sote. Amin.
Mwanzo kabisa Bwana Mtume s.a.w katoa Dirham 7 ili ende kwa Mollah wake Msafi,, Sasa na wewe kama unataka kuyapata mapenzi na huo Ucha Mungu wa Ghafla, Unaambiwa Toa kama unaweza. Utoe Nini?(Al-Imran 92) لَن تَنَالُواْ ٱلۡبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُواْ مِمَّا تُحِبُّونَۚ
"Hamtoweza kuufikia(Kuupata)Wema mpaka mtoe katika vile mnavovipenda".
Nini Wema? Wema ni Mapenzi, Nini Mapenzi, Mapenzi ndio hiyo Taqwa, hamtoweza kuifikia hiyo Taqwa au Mapenzi mpaka mtoe vile mnavovipenda, (Wengine wanauliza Wema unauzwa wapi na mimi nikanunue) Leo ninakujulisha panapo uzwa Wema, wacha nikuoneshe duka linalouzwa huo Wema unalo Mwenyewe, (Shop keeper)Ni wewe bado hujagundua vipi Wema utaweza kuupata, Wewe na Mcha Mungu hamna tafauti, vile vote alokua navyo Mcha Mungu na wewe unavyo, Tafauti yake wewe hujui kuvifikia hivyo alonavyo Mcha Mungu, Ndio Maana unaambiwa ukitaka uvipate basi (Shuruti)lake toa katika kile unachokipenda, Sababu katika hicho unachokipenda nyuma yake kumejificha hiyo Taqwa, hicho unachokipenda ndio kizuizi baina yako na huo Wema, sasa unaambiwa Toa hicho unachokipenda uone (Result) yake, na (Result)yake ni hayo hayo Mapenzi, unatoa unachokipenda unapewa kinachokupenda, (Give n Take) Na kinachokupenda kina utajiri Mkubwa, kinachokupenda ndio chenye utajiri usokatika, kinachokupenda ndio kilokupa hayo unayoyapenda na mengi mengine ambayo yamo kwenye Ulimwengu huu, Kinachokupenda kinaendelea kutoa kila leo, kinachokupenda kwa mapenzi yake kimekupa mpaka huu Uhai na uwezo wa kuyapata hayo unayoyapenda, Yule ambaye anakupenda anakwambia kunifikia mimi, kuwa karibu na mimi, basi toa utengane na hicho unachokipenda, Na utakapo kitoa tu, basi mimi na wewe tunakutana na unakuwa Kipenzi changu, madhila na dhiki yanakuondoka, shida na matatizo zinatoweka, lakini lazima utoe unachokipenda, hiyo ndio (Thamani unayotakiwa ulipie Penzi la Taqwa).
Katika kutoa kuna Raha fulani inapatikana kwa anaepewa na mwenye kutoa, lakini ukiona umehisi raha fulani katika kutoa huko basi hiyo inakua bado hujatoa, kutoa ili uupate Ucha Mungu inatakiwa Mtowaji hayupo na nafasi yake kabaki Mwenye Enzi Mungu, "Ewe"Mwenye Mali au Mapesa unajiuliza kutoa huku kuna kuwaje ili nipate Ucha Mungu(Mfano)Una Million 20(Au Kidani chako chako cha Almasi), watafute Maskini kumi waambie nimeamrishwa na Mollah wangu hizi Million 10 kumi nikupeni nyinyi ili muanze biashara na hizi sikupeni mimi ila Amri ya Mollah wangu na mimi nimo katika kuitekeleza, Au una nyumba tatu unatoa moja kuwapa wasiokuwa na uwezo iwe yao mali yao, tena iwe ili nzuri unayoipenda, unawapa hii kakupeni Mollah wangu kaeni familia nzima.
Na "Ewe" Mwenye Mshahara mkubwa zikimbilie kheri za kuwalisha viumbe wenzio unaowajua wana shida. nyumba ina watoto 7 mzee wao ana hangaika kutafuta Riziki, sema kuanzia leo mimi nitakua naleta chakula mpaka mtakapopata uwezo, nusu mshahara wangu utakua haki yenu, nachukua dhamana hiyo kwa kutafuta Radhi za Mollah wangu.
Na "Ewe" Maskini msokitu wewe unakikubwa zaidi cha kujitolea, sema Mollah wangu najikabidhi kwako kwa haki ya uhai wangu niwe Mtumwa wako katika kukuabudu wewe, katika kuwatumikia viumbe vyako kama utavyoniamrisha, "Ewe"Mollah wangu unaujua udhaifu wangu mimi sina cha kutoa na wala sina ninachokipenda isipokua dhati yako yenye Uweza, basi nipe mimi Ridhaa yako ya kuupata huo Wema ulojaa Neema zako, wewe Mollah wangu ni mwenye kujaalia Mapenzi, basi naomba nichague katika wale viumbe vyako uloviongoza katika hayo Mapenzi yako ya Taqwa.
وَمَا تُنفِقُواْ مِن شَىۡءٍ۬ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٌ۬
"Na chochote mnachokitoa, Basi Mwenye Enzi Mungu anakijua"
usije ukajifanya mjanja unatoa nyumba yako mbovu, inayotakiwa ni ile mpya yenye (swimming Pool), au ukawapa pesa huku unawanongoneza ukipata utanirudishia, au unaomba dua Mollah nipe utajiri nishachoka kusubiri, toka nimenyanyukia nahangaika na maisha basi nipe na mimi ikisha ntafanya Ibada kwa wingi, Mollah ni mwenye kujua kila mipango yako ilofichika kwenye kifua chako.
Usiwe mwenye kutoa kama mwana siasa au mfanya biashara mpaka Wapiga picha wawepo, au watu wajue katoa, huko sikutoa kwa (Ikhlas) ni shirk ya kujionesha, kutoa kwa kweli ni kule unajua wewe tu na mpokeaji kama umetoa, huna haja ya matangazo au picha au usikike redioni, na ukitoa kama alivoamrisha Mollah wako basi kwa hakika yanaanza kukushukia mapenzi hiyo ni (Gurantee) wewe toa, utakuja nikumbuka ukitoa kile unachokipenda kweli katika moyo wako basi na huku (Something happen)katika moyo ikisha inaanza ku (Grow slowly) na kikisha ota kwa ukamilifu wewe Mcha Mungu, wewe ushaupata huo wema, na ni Bora kuishi na Wema kuliko kuwa Millionea. Sasa jitizame ukimpenda Mtu unakuwaje, sasa yapime mapenzi hayo hayo lakini yameongezeka mara million unapenda kitu usichokiona, na kila siku zikizidi unashauku ya kukisogelea karibu kutaka kukijua, na kila ukisogea mapenzi yanazidi, na maajabu yanaongezeka na huo ndio Ucha Mungu ambao tunamuomba Mollah atujaalie kwa sote. Amin.
Subscribe to:
Posts (Atom)