Asalaam Aleiykum
Kitendo cha kufunga lazima kiwe na mahusiano na uwepo wa tendo la Uwazi, ndio kunapatikana kufunga, hakuna shaka kabisa kuwa tunaishi katika huo uwazi, na katika maisha yetu uwazi huu ni mpana sana(Vast)tunayafanya tunayo yaweza na kuyapa jina matendo hayo la (Freedom) huo ndio uwazi wenyewe, katika miezi 11 yote Mtu anacheza sakata analo lijua, unatenda utendavyo katika uhuru huo hata bila ya kuwa na wasiwasi wowote, baada ya hiyo miezi 11 Mollah wako anajua kwenye Uhuru huo wewe umefanya mengi, una magunia kwa magunia ya Madhanmbi, Na sheria ya Ulimwengu huu na kwa masharti yalowekwa ikiwa mnataka Uhuru basi kila Dhanmbi, kila kosa ni Deni na lazima deni hilo lilipwe.
Mnajulikana wazi hamuwezi kuyalipa madeni yenu, Madeni ni mengi mno, Pengine umemcheka Mtu, labda umemsengenya huyu, Umemdhulumu yule, na mengine unayafanya bila kujua, umekikanyaga kinyama na kukiua, umemzulia fulani mambo ya uwongo, una Dhanmbi za macho hazina idadi, za masikio hazisemeki, takriban katika huo uhuru wako umefanya ya kufanya halafu ukaja tenda ile Dhanmbi kubwa ya kumsahau Mollah wako, basi ili usizidi kuangamia, usije kuharibikiwa kwenye uhuru huu, ndio Mollah wako kakuita kwenye mwezi huu, njoo kidogo tukufunge ili upate Rehma ya kupunguza hayo mambo, tupate kukumbusha kuwa upo upande wa pili na unaweza ukapiga jicho ukaona japo ishara kwa kufunga hii Ramadhan.
Na Waumini wanapewa nafasi ya kuangalia upande wa pili lakini sote tunaitupa nafasi hii na badala ya kumkumbuka Mollah jiangalie kwenye mwezi huu unakumbuka Nini?, Huna unacho kumbuka ila vyakula, Makaimati, masambusa, madizi mabivu, Njugu mawe, tena njaa ikikutafuna zaidi utaona unakimbilia jikoni kuagiza ziongezwe sukari, tunakosa nafasi adhimu ya funga yenyewe, Unaitupa kabisa raha ya Ramadhan ambayo ni ya kumkumbuka Mollah wako mwanzo wake mpaka mwisho wake.
Basi kama ulikua huijui hii Ramadhan ni nyenzo(Tools) ya (Awareness), sasa mwaka huu kuwa (Hadhir) (Alert)shindana na njaa yako, ili uipate Saum na Raha yake, ukikumbuka Katlesi, jilazimishe uone ndio unakumbushwa sala ya Sunna, Ukikumbuka mpira elewa ndio wakati wa darsa ushawasili, ukikumbuka TV kumbuka muda wa kusoma Quraan huo umefika kila ukikumbuka mambo yote yaliyomo ndani ya ile miezi 11 ilopita jitahidi ukumbuke ya huu mwezi mmoja nao ni huu wa Ramadhan.
Endelea part 2
Sunday, June 29, 2014
RAHA YA RAMADHAN PART 2
Asalaam Aleiykum
Na kila ukikumbuka mwezi huu wa Ramadhan kumbuka ni mwezi wa Ibada, basi na wewe ifanye ya aina yoyote ya Ibada ujira wake anaujua Mollah wako, Na utakapo kuzidisha Ibada ghafla utaona tabia yako imebadilika, utaanza kupenda Ibada kuliko mambo ya kipuuzi, Utakua unamfikiri Mollah wako kila saa na dakika, na ikikutokezea hali kama hiyo, hapo utakua umeipata Raha ya Ramadhan na faida zake, Na ikiwa utakua na dalili hizo basi Mollah wako anakupa ahadi ikiwa utakua na matatizo yoyote yale, kama una dhiki, au huna cha kukila, matatizo haya na yale kama kweli una mapenzi na Mollah wako basi jikumbushe mwisho wa aya ya pili na aya ya tatu sura ya (Talaq) inasemaje " وَمَن يَتَّقِ ٱللَّهَ يَجۡعَل لَّهُ ۥ مَخۡرَجً۬ا " Na anayemuogopa(Kwa kumpenda)Mwenye enzi Mungu humfanyia
Njia ya Kuokoka(Kutokea)
"وَيَرۡزُقۡهُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَحۡتَسِبُۚ وَمَن يَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِ فَهُوَ حَسۡبُهُ ۥۤۚ إِنَّ ٱللَّهَ بَـٰلِغُ أَمۡرِهِۦۚ قَدۡ جَعَلَ ٱللَّهُ لِكُلِّ شَىۡءٍ۬ قَدۡرً۬ا"
Na humpa Riziki kwa Namna asiyotarajia, Na anayemtegemea Mwenye enzi Mungu humtoshea, kwa hakika Mwenye enzi Mungu anatimiza kusudio lake, Hakika Mwenye enzi Mungu amekiwekea kila kitu kipimo chake.
Ukifunga kikweli na kufanya Taqwa Mwenye enzi Mungu atajaalia utoke kwenye hizo Dhiki, matatizo, shida, Dhanmbi, na zawadi yako itakua kuruzukiwa kwa njia usizotarajia wewe mwenyewe. Hapo tena ndio utaigundua Raha ya Ramadhan kumbe ndio inakua hivi, hizi ndio Raha zenyewe za kufunga, Basi hata itakapokwisha hiyo Ramadhan siku ya sikukuu wewe unakua husheherekei kama wafanyavo wengine, wewe unakua una Raha na ufanyalo nikuongeza Fu-Raha, Furaha ndio (Freedom) Maisha yote Mwenye enzi Mungu kaumba furaha, yote yalosalia viumbe tunayafanya kwa mikono yetu, Kwa hiyo funga kwa Imani, Ifanye Ramadhan yako ya aina nyengine mwaka huu, ifanye iwe tafauti na zote zilopita, badilisha tabia yako ya miezi 11 uzifunge kwa kutozifanya mwezi huu, basi ukimaliza mwezi wa Ramadhan utakua Mtu mwengine kabisa ambaye alo jaa Furaha, Mchache wa Dhiki za Roho, na zaidi ya yote sasa wewe ni Mcha Mungu, na hiyo ndio Raha ya Ramadhan ambayo tunamuomba Mollah atujaalie tuifunge kwa salama na afya njema,Mollah awasamehe na kuwapa ujira unaostahiki kwa wale wasoweza kutimiza Ibada hii ya kufunga, awaruzuku Ucha Mungu kwa njia nyengine zenye mfano wa mwezi huu wa Ramadhan. Amin
Na kila ukikumbuka mwezi huu wa Ramadhan kumbuka ni mwezi wa Ibada, basi na wewe ifanye ya aina yoyote ya Ibada ujira wake anaujua Mollah wako, Na utakapo kuzidisha Ibada ghafla utaona tabia yako imebadilika, utaanza kupenda Ibada kuliko mambo ya kipuuzi, Utakua unamfikiri Mollah wako kila saa na dakika, na ikikutokezea hali kama hiyo, hapo utakua umeipata Raha ya Ramadhan na faida zake, Na ikiwa utakua na dalili hizo basi Mollah wako anakupa ahadi ikiwa utakua na matatizo yoyote yale, kama una dhiki, au huna cha kukila, matatizo haya na yale kama kweli una mapenzi na Mollah wako basi jikumbushe mwisho wa aya ya pili na aya ya tatu sura ya (Talaq) inasemaje " وَمَن يَتَّقِ ٱللَّهَ يَجۡعَل لَّهُ ۥ مَخۡرَجً۬ا " Na anayemuogopa(Kwa kumpenda)Mwenye enzi Mungu humfanyia
Njia ya Kuokoka(Kutokea)
"وَيَرۡزُقۡهُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَحۡتَسِبُۚ وَمَن يَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِ فَهُوَ حَسۡبُهُ ۥۤۚ إِنَّ ٱللَّهَ بَـٰلِغُ أَمۡرِهِۦۚ قَدۡ جَعَلَ ٱللَّهُ لِكُلِّ شَىۡءٍ۬ قَدۡرً۬ا"
Na humpa Riziki kwa Namna asiyotarajia, Na anayemtegemea Mwenye enzi Mungu humtoshea, kwa hakika Mwenye enzi Mungu anatimiza kusudio lake, Hakika Mwenye enzi Mungu amekiwekea kila kitu kipimo chake.
Ukifunga kikweli na kufanya Taqwa Mwenye enzi Mungu atajaalia utoke kwenye hizo Dhiki, matatizo, shida, Dhanmbi, na zawadi yako itakua kuruzukiwa kwa njia usizotarajia wewe mwenyewe. Hapo tena ndio utaigundua Raha ya Ramadhan kumbe ndio inakua hivi, hizi ndio Raha zenyewe za kufunga, Basi hata itakapokwisha hiyo Ramadhan siku ya sikukuu wewe unakua husheherekei kama wafanyavo wengine, wewe unakua una Raha na ufanyalo nikuongeza Fu-Raha, Furaha ndio (Freedom) Maisha yote Mwenye enzi Mungu kaumba furaha, yote yalosalia viumbe tunayafanya kwa mikono yetu, Kwa hiyo funga kwa Imani, Ifanye Ramadhan yako ya aina nyengine mwaka huu, ifanye iwe tafauti na zote zilopita, badilisha tabia yako ya miezi 11 uzifunge kwa kutozifanya mwezi huu, basi ukimaliza mwezi wa Ramadhan utakua Mtu mwengine kabisa ambaye alo jaa Furaha, Mchache wa Dhiki za Roho, na zaidi ya yote sasa wewe ni Mcha Mungu, na hiyo ndio Raha ya Ramadhan ambayo tunamuomba Mollah atujaalie tuifunge kwa salama na afya njema,Mollah awasamehe na kuwapa ujira unaostahiki kwa wale wasoweza kutimiza Ibada hii ya kufunga, awaruzuku Ucha Mungu kwa njia nyengine zenye mfano wa mwezi huu wa Ramadhan. Amin
Sunday, June 22, 2014
MTUKUFU RAMADHAN PART 1
Asalaam Aleiykum
Watu wanakua na Furaha pale wanapoandaa harusi ya Mtoto, Kuandaa mikutano na Sherehe nyengine, lakini akipewa habari ya kujiandaa na Mwezi Mtukufu wa Ramadhan hapo hapo anabadilika uso, utaona rangi inabadilika hata kama anajificha, moyoni anasema "Mama wee"Kiama hicho.
Sisi wa Ulaya ukitajiwa tu unaanza kukiona kimbunga cha masaa 18 hayoo, Bali kila mmoja wetu ana sababu za kuuwekea alama ya kuuliza mwezi huu wa Ramadhan, hapo tena utaona wenye Maradhi yanakuja juu ghafla, na kwa kuwa hayajatajwa Maradhi gani basi hata ukucha unatosha kumpa mtu sababu ya kutokufunga, Lakini wale Wenye kumpenda Mollah na Maamrisho yake huwa wanausubiri kwa hamu zawadi hii ili wapate kujikurubisha zaidi kwa Mollah wao, wapate kuonesha mapenzi kwa ajili ya Ibada.
Na ikiwa wewe humo katika kundi hilo anza kupata wasiwasi, Wenye penzi la (Taqwa)wanajua yaliyomo kwenye mwezi huu, ndio maana wakafurahi kuwasili kwake.
Na wewe kama hujui kilichomo ndani ya Mwezi huu basi tega sikio, dondosha jicho upate kufaidika na maudhui hii ambayo kwa leo tunaanza kuchuma tunda la aya ya 185 iliyomo kwenye sura ya (Baqarah)"شَہۡرُ رَمَضَانَ ٱلَّذِىٓ أُنزِلَ فِيهِ ٱلۡقُرۡءَانُ هُدً۬ى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَـٰتٍ۬ مِّنَ ٱلۡهُدَىٰ وَٱلۡفُرۡقَانِۚ "(Mpaka mwisho wa aya)
"Mwezi huu wa Ramadhan (Ndio)ambao imetermshwa hii Quraan, Uwe Uongozi (Kwa) Watu, Na hoja zilizo wazi na upambanuzi".
فَمَن شَہِدَ مِنكُمُ ٱلشَّہۡرَ فَلۡيَصُمۡهُۖ وَمَن ڪَانَ مَرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٍ۬ فَعِدَّةٌ۬ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَۗ يُرِيدُ ٱللَّهُ بِڪُمُ ٱلۡيُسۡرَ وَلَا يُرِيدُ بِڪُمُ ٱلۡعُسۡرَ وَلِتُڪۡمِلُواْ ٱلۡعِدَّةَ وَلِتُڪَبِّرُواْ ٱللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَٮٰكُمۡ وَلَعَلَّڪُمۡ تَشۡكُرُونَ
"Basi atakae kuwa katika Mji katika Mwezi huu (Na) afunge, Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi (atimize) hisabu (ya siku alizowacha) katika siku nyengine, Mwenye enzi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, Na pia mtimize hisabu hiyo, Na kumtukuza Mwenye enzi Mungu kwa kuwa kakuongozeni, ili mpate kushukuru"
Basi leo tutazunguka kwenye Bustani ya aya hii ili tupate kuchuma matunda yake asaa unaweza kupata Vitamin ya Muongozo
Endelea part 2
Watu wanakua na Furaha pale wanapoandaa harusi ya Mtoto, Kuandaa mikutano na Sherehe nyengine, lakini akipewa habari ya kujiandaa na Mwezi Mtukufu wa Ramadhan hapo hapo anabadilika uso, utaona rangi inabadilika hata kama anajificha, moyoni anasema "Mama wee"Kiama hicho.
Sisi wa Ulaya ukitajiwa tu unaanza kukiona kimbunga cha masaa 18 hayoo, Bali kila mmoja wetu ana sababu za kuuwekea alama ya kuuliza mwezi huu wa Ramadhan, hapo tena utaona wenye Maradhi yanakuja juu ghafla, na kwa kuwa hayajatajwa Maradhi gani basi hata ukucha unatosha kumpa mtu sababu ya kutokufunga, Lakini wale Wenye kumpenda Mollah na Maamrisho yake huwa wanausubiri kwa hamu zawadi hii ili wapate kujikurubisha zaidi kwa Mollah wao, wapate kuonesha mapenzi kwa ajili ya Ibada.
Na ikiwa wewe humo katika kundi hilo anza kupata wasiwasi, Wenye penzi la (Taqwa)wanajua yaliyomo kwenye mwezi huu, ndio maana wakafurahi kuwasili kwake.
Na wewe kama hujui kilichomo ndani ya Mwezi huu basi tega sikio, dondosha jicho upate kufaidika na maudhui hii ambayo kwa leo tunaanza kuchuma tunda la aya ya 185 iliyomo kwenye sura ya (Baqarah)"شَہۡرُ رَمَضَانَ ٱلَّذِىٓ أُنزِلَ فِيهِ ٱلۡقُرۡءَانُ هُدً۬ى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَـٰتٍ۬ مِّنَ ٱلۡهُدَىٰ وَٱلۡفُرۡقَانِۚ "(Mpaka mwisho wa aya)
"Mwezi huu wa Ramadhan (Ndio)ambao imetermshwa hii Quraan, Uwe Uongozi (Kwa) Watu, Na hoja zilizo wazi na upambanuzi".
فَمَن شَہِدَ مِنكُمُ ٱلشَّہۡرَ فَلۡيَصُمۡهُۖ وَمَن ڪَانَ مَرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٍ۬ فَعِدَّةٌ۬ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَۗ يُرِيدُ ٱللَّهُ بِڪُمُ ٱلۡيُسۡرَ وَلَا يُرِيدُ بِڪُمُ ٱلۡعُسۡرَ وَلِتُڪۡمِلُواْ ٱلۡعِدَّةَ وَلِتُڪَبِّرُواْ ٱللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَٮٰكُمۡ وَلَعَلَّڪُمۡ تَشۡكُرُونَ
"Basi atakae kuwa katika Mji katika Mwezi huu (Na) afunge, Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi (atimize) hisabu (ya siku alizowacha) katika siku nyengine, Mwenye enzi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, Na pia mtimize hisabu hiyo, Na kumtukuza Mwenye enzi Mungu kwa kuwa kakuongozeni, ili mpate kushukuru"
Basi leo tutazunguka kwenye Bustani ya aya hii ili tupate kuchuma matunda yake asaa unaweza kupata Vitamin ya Muongozo
Endelea part 2
MTUKUFU RAMADHAN PART 2
Asalaam Aleiykum
Aya imeanza vizuri sana kwa kukueleza kuwa mwezi huu wa Ramadhan imeteremshwa hii Quraan, Unakumbushwa kwamba na wewe pia umeteremshwa na hii Ramadhan umetermshiwa iwe zawadi yako kutoka kwa Mollah wako, ili iwe nini? iwe huu Mualiko wako kila mwaka kumkumbuka Mollah wako alokuumba, Umeteremshiwa muongozo na hoja zilizo wazi kabisa zenye upambanuzi usiokua na shaka.
Hapa leo kazi yangu mimi kutoa huo ufafanuzi, ila nataka ukumbuke ufafanuzi ni wangu huna haja ya kuukubali, unaweza kubakia na kitambaa chako cha machoni na kuukataa ufafanuzi huu, Ufafanuzi wenyewe ni kuhusiana Baina ya Roho yako na hicho (Kiwiliwili)(Body) ilobeba hiyo Roho.
Wanazuoni wameugawa huu Mwezi wa Ramadhan kwenye mafungu matatu, (Kumi la mwanzo)Rehma na (Kumi la Pili)Maghfira na (kumi la tatu) kuepushwa na Moto, Na upambanuzi huo ni sahihi kabisa, kwani kinacho tokea katika mwezi huu ndio hicho hicho walichokieleza, Nini kinatokea?,
Katika kumi la mwanzo kama kweli utaifunga Ramadhan ipasavyo na kwa Imani ya ukweli kinatokezea kile kile kinacho tokezea kwenye (Ndoa) (Al Ruum 21).( مَّوَدَّةً۬ وَرَحۡمَةًۚ )
Najua utashangaa, wengine watasema hee kwani nafunga ndoa na Ramadhan, (Hayo ni mawazo finyu), sio kosa lako ukidhani hivyo, taratibu utakuja kufahamu, na mimi nilikua hivyo hivyo mpaka (Something of Beyond happen) kufungua fahamu yako, Tunakaribia Mwezi wa Ramadhan pata faida hii ili ujue nini kinatokea, tuko kwenye ufafanuzi na upambanuzi basi tuliza jicho na sikio, Kwenye (Ndoa) una ruzukiwa Mapenzi na watoto, na kwenye Ramadhan linatokea hili la Mapenzi kwa Mollah wako, Vipi?.
Unapoanza kufunga lazima ujue mambo mawili haya, unaunyima chakula mwili wako, kwa sababu hii (Body) inahitaji chakula, na ukiinyima chakula tu (Body) inaanza kushituka, unaipa (Shock) vipi mbona mambo yako hivi?, hapo moja kwa moja zinafunguka Rehma za kuhudumia Mwili ambapo (cells) zilo lala zinaanza kuamka, zinafanya marekebisho, zinatibu magonjwa Nk, Na kitu cha pili kinachotokezea (Mwili) ukinyimwa chakula(Automatic) unaipa Roho chakula chake nacho ni hayo mapenzi (Taqwa) vipi yanakua Mapenzi hayo? Ukimpenda Binaadamu mwenzako una (Share) unatoa huna kizuizi, hujali chochote, sasa mapenzi yenyewe katika mwezi huu yaangalie vizuri japo yamejificha, chakula unacho kwenye Friji, viporo vipo, maji baridi yapo na wewe una kiu kubwa, Mke au Mume yupo, vyote hivyo unaweza kuvifanya hakuna anokuzuia, lakini wewe kwa ajili ya mapenzi ya Mollah wako, jinsi ya Penzi lilivo kuzidi hata kusukutua unaogopa, wewe unaogopa kutizama mambo machafu, wewe unaogopa kufanya vitendo vya Haramu, wewe unaogopa kugombana au kugombanisha na sio kama kuna mlinzi au umelazimishwa, unafanya kwa hiyari yako na hayo ndio mapenzi na hiyo ndio Taqwa, ukiweza kufanya hivyo ukafikia (Stage) ya funga yako kukamilika, utaona wewe upo tafauti na mwili wako, tafauti na vitendo vyako, (Unaishi Kiroho) ukigundua hilo mapenzi yataanza ku (Shower)kuteremka, hutokubali tena kufutari peke yako, hutowacha maskini wateseke, utakua unampenda kila ajae kwako kwa mahitaji au kuwa karibu na wewe, na hapo utakua ushaupata utukufu wa Ramadhan na Taqwa yake. Mollah wetu tujaalie tuifunge kwa salama na tupate mapenzi yako yasokatika ndani ya mwezi huu.
Aya imeanza vizuri sana kwa kukueleza kuwa mwezi huu wa Ramadhan imeteremshwa hii Quraan, Unakumbushwa kwamba na wewe pia umeteremshwa na hii Ramadhan umetermshiwa iwe zawadi yako kutoka kwa Mollah wako, ili iwe nini? iwe huu Mualiko wako kila mwaka kumkumbuka Mollah wako alokuumba, Umeteremshiwa muongozo na hoja zilizo wazi kabisa zenye upambanuzi usiokua na shaka.
Hapa leo kazi yangu mimi kutoa huo ufafanuzi, ila nataka ukumbuke ufafanuzi ni wangu huna haja ya kuukubali, unaweza kubakia na kitambaa chako cha machoni na kuukataa ufafanuzi huu, Ufafanuzi wenyewe ni kuhusiana Baina ya Roho yako na hicho (Kiwiliwili)(Body) ilobeba hiyo Roho.
Wanazuoni wameugawa huu Mwezi wa Ramadhan kwenye mafungu matatu, (Kumi la mwanzo)Rehma na (Kumi la Pili)Maghfira na (kumi la tatu) kuepushwa na Moto, Na upambanuzi huo ni sahihi kabisa, kwani kinacho tokea katika mwezi huu ndio hicho hicho walichokieleza, Nini kinatokea?,
Katika kumi la mwanzo kama kweli utaifunga Ramadhan ipasavyo na kwa Imani ya ukweli kinatokezea kile kile kinacho tokezea kwenye (Ndoa) (Al Ruum 21).( مَّوَدَّةً۬ وَرَحۡمَةًۚ )
Najua utashangaa, wengine watasema hee kwani nafunga ndoa na Ramadhan, (Hayo ni mawazo finyu), sio kosa lako ukidhani hivyo, taratibu utakuja kufahamu, na mimi nilikua hivyo hivyo mpaka (Something of Beyond happen) kufungua fahamu yako, Tunakaribia Mwezi wa Ramadhan pata faida hii ili ujue nini kinatokea, tuko kwenye ufafanuzi na upambanuzi basi tuliza jicho na sikio, Kwenye (Ndoa) una ruzukiwa Mapenzi na watoto, na kwenye Ramadhan linatokea hili la Mapenzi kwa Mollah wako, Vipi?.
Unapoanza kufunga lazima ujue mambo mawili haya, unaunyima chakula mwili wako, kwa sababu hii (Body) inahitaji chakula, na ukiinyima chakula tu (Body) inaanza kushituka, unaipa (Shock) vipi mbona mambo yako hivi?, hapo moja kwa moja zinafunguka Rehma za kuhudumia Mwili ambapo (cells) zilo lala zinaanza kuamka, zinafanya marekebisho, zinatibu magonjwa Nk, Na kitu cha pili kinachotokezea (Mwili) ukinyimwa chakula(Automatic) unaipa Roho chakula chake nacho ni hayo mapenzi (Taqwa) vipi yanakua Mapenzi hayo? Ukimpenda Binaadamu mwenzako una (Share) unatoa huna kizuizi, hujali chochote, sasa mapenzi yenyewe katika mwezi huu yaangalie vizuri japo yamejificha, chakula unacho kwenye Friji, viporo vipo, maji baridi yapo na wewe una kiu kubwa, Mke au Mume yupo, vyote hivyo unaweza kuvifanya hakuna anokuzuia, lakini wewe kwa ajili ya mapenzi ya Mollah wako, jinsi ya Penzi lilivo kuzidi hata kusukutua unaogopa, wewe unaogopa kutizama mambo machafu, wewe unaogopa kufanya vitendo vya Haramu, wewe unaogopa kugombana au kugombanisha na sio kama kuna mlinzi au umelazimishwa, unafanya kwa hiyari yako na hayo ndio mapenzi na hiyo ndio Taqwa, ukiweza kufanya hivyo ukafikia (Stage) ya funga yako kukamilika, utaona wewe upo tafauti na mwili wako, tafauti na vitendo vyako, (Unaishi Kiroho) ukigundua hilo mapenzi yataanza ku (Shower)kuteremka, hutokubali tena kufutari peke yako, hutowacha maskini wateseke, utakua unampenda kila ajae kwako kwa mahitaji au kuwa karibu na wewe, na hapo utakua ushaupata utukufu wa Ramadhan na Taqwa yake. Mollah wetu tujaalie tuifunge kwa salama na tupate mapenzi yako yasokatika ndani ya mwezi huu.
Sunday, June 15, 2014
ANOSIKIA AMWAMBIE MWENZIE PART 1
Asalaam Aleiykum
Anosikia amwambie mwenzie yakwamba mwezi wa Ramadhan umeshawasili na upo pembezoni mwa Shaban. Katika makundi ya watu utawakuta wana tabia tafauti jinsi ya kumkaribisha mgeni, kuna wengine wanajiandaa kwa kukoga wakajisafisha, wakapamba nyumba zao kwa kila aina ya mapambo sababu mgeni anakuja, Na kuna wengine wao mpaka wasikie mgeni yupo mlangoni ndio wanaanza kukurupuka na maandalizi, Na wengine wao hawajali ikiwa mgeni atawakuta wachafu au vyovyote vile hawana habari au hawataki kumfanyia mgeni (Takrima) yoyote ile.
Na Mgeni anapowasili jambo la mwanzo analotizama ni nyumba ya mwenyeji ikoje, jee anaweza kukaa? akiangalia ndani kwenye hiyo nyumba ambayo ni huo mwili wako anakuta uchafu mtupu, imejaa majani ya mirungi, kuna vikopo vya Bia, kuna mali za wizi na haramu, damu imechafuka kwa michirizi ya rushwa, mifupa yote mizito kwa vitendo vya dhuluma na balaa chungu nzima zimesaki kwenye Jumba la Roho yako, Ramadhan inahuzunika hivi mimi nimeletwa kwenye nyumba hii ili nilete zawadi ya mapenzi ya Ibada na Rehma za Mwili, halafu niwachukulie dhamana hawa ya kuepushwa na moto, lakini sina nilichokikuta ila hawa Viumbe kila nikikaribia wao ndio wanafanya mazoezi ya kuingia motoni.
Hakuna idadi yoyote ile isipokua wachache sana wao ndio wamenusurika, lakini wengi wao nimewakuta wana matatizo makubwa na wamo wanajificha kwenye karata, mabarazani, kwenye ngoma na kila aina ya fujo, mpaka wamesahau kwamba wewe Mollah wao upo na unapaswa kupendwa kama ulivo wapenda na kuwapa zawadi ya Uhai.
Kiumbe kwenye miezi 11 umeshughulika na mambo yako, huna nafasi ya kumpenda na kumuabudu Mollah wako kwa ajili ya mambo ulo nayo, huna kituo kabisa uko (Busy) sasa basi kakutengea hizi siku chache mpeni yeye kwa shukran na kumkumbuka kila saa na dakika, vipi utamkumbuka ndio umepewa hii Ramadhan(Condition) Ufunge, vipi kufunga kwenyewe, shuruti lake hassa nini? (Bakara aya ya 183)
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡڪُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِڪُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
Enyi mloamini melazimishwa kufunga kama walivyo lazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu.
Haijambo inatia moyo watu wote wanao ukaribisha mwezi wa Ramadhan wanakutana katika jambo moja nalo la kukaa na njaa, lakini Ramadhan kusudio lake sio mkae na njaa, kusudio lake mpate mapenzi ya kumpenda Mollah wenu kwa (Devotion) na shukuran.
Endelea part 2
Anosikia amwambie mwenzie yakwamba mwezi wa Ramadhan umeshawasili na upo pembezoni mwa Shaban. Katika makundi ya watu utawakuta wana tabia tafauti jinsi ya kumkaribisha mgeni, kuna wengine wanajiandaa kwa kukoga wakajisafisha, wakapamba nyumba zao kwa kila aina ya mapambo sababu mgeni anakuja, Na kuna wengine wao mpaka wasikie mgeni yupo mlangoni ndio wanaanza kukurupuka na maandalizi, Na wengine wao hawajali ikiwa mgeni atawakuta wachafu au vyovyote vile hawana habari au hawataki kumfanyia mgeni (Takrima) yoyote ile.
Na Mgeni anapowasili jambo la mwanzo analotizama ni nyumba ya mwenyeji ikoje, jee anaweza kukaa? akiangalia ndani kwenye hiyo nyumba ambayo ni huo mwili wako anakuta uchafu mtupu, imejaa majani ya mirungi, kuna vikopo vya Bia, kuna mali za wizi na haramu, damu imechafuka kwa michirizi ya rushwa, mifupa yote mizito kwa vitendo vya dhuluma na balaa chungu nzima zimesaki kwenye Jumba la Roho yako, Ramadhan inahuzunika hivi mimi nimeletwa kwenye nyumba hii ili nilete zawadi ya mapenzi ya Ibada na Rehma za Mwili, halafu niwachukulie dhamana hawa ya kuepushwa na moto, lakini sina nilichokikuta ila hawa Viumbe kila nikikaribia wao ndio wanafanya mazoezi ya kuingia motoni.
Hakuna idadi yoyote ile isipokua wachache sana wao ndio wamenusurika, lakini wengi wao nimewakuta wana matatizo makubwa na wamo wanajificha kwenye karata, mabarazani, kwenye ngoma na kila aina ya fujo, mpaka wamesahau kwamba wewe Mollah wao upo na unapaswa kupendwa kama ulivo wapenda na kuwapa zawadi ya Uhai.
Kiumbe kwenye miezi 11 umeshughulika na mambo yako, huna nafasi ya kumpenda na kumuabudu Mollah wako kwa ajili ya mambo ulo nayo, huna kituo kabisa uko (Busy) sasa basi kakutengea hizi siku chache mpeni yeye kwa shukran na kumkumbuka kila saa na dakika, vipi utamkumbuka ndio umepewa hii Ramadhan(Condition) Ufunge, vipi kufunga kwenyewe, shuruti lake hassa nini? (Bakara aya ya 183)
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡڪُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِڪُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
Enyi mloamini melazimishwa kufunga kama walivyo lazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu.
Haijambo inatia moyo watu wote wanao ukaribisha mwezi wa Ramadhan wanakutana katika jambo moja nalo la kukaa na njaa, lakini Ramadhan kusudio lake sio mkae na njaa, kusudio lake mpate mapenzi ya kumpenda Mollah wenu kwa (Devotion) na shukuran.
Endelea part 2
ANOSIKIA AMWAMBIE MWENZIE PART 2
Asalaam Aleiykum
Ili kuyapata hayo mapenzi itakubidi ujitoe (muhanga) ufunge kila kitu, una mambo mengi wewe unafanya katika mwaka mzima, sasa ukitaka uipate (Saum) itakubidi uyafunge kama unavo ifunga milango ili mwizi asiingie, mambo yepi? una vikao vya Mpira, vikundi vya mazoezi, una biashara zisizo za muhimu, mikutano ya harusi, mkesha wa jumapili, Baraza ya usiku, jioni ya kutizama mandhar, vipindi vya TV, Kibaraza mawazo, kusoma vitabu vya hadith, takriban acha acha mambo ya kilimwengu katika mwezi huu kwa jumla, (hata ukiweza kujiepusha na kitanda kama utaweza kwa hiyari yako basi fanya, usione nimekwambia lala chini, laa kama utaweza kujiepusha na Mume au Mke fanya, Ramadhan mwanzo mpaka hayo yalipigwa marufuku mpaka watu yalipowashinda ndio wakapewa unafuu)sasa ukiacha hayo yote halafu ufanye nini? unaambiwa usifanye chochote nenda kakae Msikitini (Itikaf) وَلَا تُبَـٰشِرُوهُنَّ وَأَنتُمۡ عَـٰكِفُونَ فِى ٱلۡمَسَـٰجِدِۗ
Wala msichanganyike nao na hali mnakaa Itikaf msikitini.
Sasa kwanini ukae msikitini? kwa sababu ndani ya Msikiti kuna salio la (Energy) za Ibada za Waumin wanazofanya siku zote, miaka yote wanamsabahi Mollah wao wanaitikia Amin, Na Msikitini hakipotei kitu, hata zile Nguvu za walokufa miaka ya nyuma bado zimo na zitaendelea kuwamo, sasa wewe ukenda ukafanya hilo tendo la kukaa Itikaf, ukakaa Kimya na Saum yako unakua kivutio cha nguvu hizo kuja kwako, na zikiungana na wewe nguvu hizo unapata (Separation) na mambo yote ya kidunia kwanza yanakujia moja baada ya moja yakimalizika (Mpito wa Separation) ghafla utaona mapenzi yana miminika, utaanza kupenda Ibada, utapenda Binaadamu wenzio, kama una pesa unaanza kuzitoa, hufutari tena peke yako, unasaidia maskini na wagonjwa, Na unatamani kila wakati kufanya Ibada, na ukijiona katika hali hiyo basi ushayapata mapenzi ushaupata Ucha Mungu, ushaipata Saum na huko ndiko kufuzu katika dini, na hili anosikia amwambie mwenzie.
Ili kuyapata hayo mapenzi itakubidi ujitoe (muhanga) ufunge kila kitu, una mambo mengi wewe unafanya katika mwaka mzima, sasa ukitaka uipate (Saum) itakubidi uyafunge kama unavo ifunga milango ili mwizi asiingie, mambo yepi? una vikao vya Mpira, vikundi vya mazoezi, una biashara zisizo za muhimu, mikutano ya harusi, mkesha wa jumapili, Baraza ya usiku, jioni ya kutizama mandhar, vipindi vya TV, Kibaraza mawazo, kusoma vitabu vya hadith, takriban acha acha mambo ya kilimwengu katika mwezi huu kwa jumla, (hata ukiweza kujiepusha na kitanda kama utaweza kwa hiyari yako basi fanya, usione nimekwambia lala chini, laa kama utaweza kujiepusha na Mume au Mke fanya, Ramadhan mwanzo mpaka hayo yalipigwa marufuku mpaka watu yalipowashinda ndio wakapewa unafuu)sasa ukiacha hayo yote halafu ufanye nini? unaambiwa usifanye chochote nenda kakae Msikitini (Itikaf) وَلَا تُبَـٰشِرُوهُنَّ وَأَنتُمۡ عَـٰكِفُونَ فِى ٱلۡمَسَـٰجِدِۗ
Wala msichanganyike nao na hali mnakaa Itikaf msikitini.
Sasa kwanini ukae msikitini? kwa sababu ndani ya Msikiti kuna salio la (Energy) za Ibada za Waumin wanazofanya siku zote, miaka yote wanamsabahi Mollah wao wanaitikia Amin, Na Msikitini hakipotei kitu, hata zile Nguvu za walokufa miaka ya nyuma bado zimo na zitaendelea kuwamo, sasa wewe ukenda ukafanya hilo tendo la kukaa Itikaf, ukakaa Kimya na Saum yako unakua kivutio cha nguvu hizo kuja kwako, na zikiungana na wewe nguvu hizo unapata (Separation) na mambo yote ya kidunia kwanza yanakujia moja baada ya moja yakimalizika (Mpito wa Separation) ghafla utaona mapenzi yana miminika, utaanza kupenda Ibada, utapenda Binaadamu wenzio, kama una pesa unaanza kuzitoa, hufutari tena peke yako, unasaidia maskini na wagonjwa, Na unatamani kila wakati kufanya Ibada, na ukijiona katika hali hiyo basi ushayapata mapenzi ushaupata Ucha Mungu, ushaipata Saum na huko ndiko kufuzu katika dini, na hili anosikia amwambie mwenzie.
Sunday, June 8, 2014
TOBA NA MAANA YAKE PART 1
Asalaam Aleiykum
Binaadamu rahisi sana kujificha kwenye kundi la Werevu, kila mtu mjuaji, ukileta somo lolote yeye kesha khitimu, kitu chochote yeye anakijua zaidi kuliko wewe mletaji, hakubali kabisa mwanaadamu huyu kukaa katika kundi la wajinga, japokua anajijua anateseka kwa kutokujua kitu, Na siku zote tizama (Mfano) huu baina ya Mjanja na Mwerevu, ikitokea Mjanja(Mwerevu) kuibiwa anakua na Hamaki sana, lakini Mjinga akiibiwa ima atakua hana habari au akijua anacheka baadae, unajua kwanini?.
Kwa sababu moja tu Mjinga hana Fikira za Mbeleni, Nikisema mjinga nina maanisha(Innocent one), Lakini Mjanja mambo yake yote ya mipango mipango, mbele itakuaje, wakati hakuna yoyote yule ajuae kesho kitatokea nini. Na hivi ndivo wengi wetu tunavoishi tukiendekeza tamaa mwanzo, mateso baadae, Sasa katika jambo la (Toba) Mjanja hujipa tamaa kuwa kesha samehewa yote ayafanyao, hali ya kuwa haijui hata maana ya Toba.
Haijambo ukiwa Mjinga unakuwa unaishi kwenye maisha ya Khofu na Tamaa, kwa ajili ya khofu kwanza unatekeleza shuruti la Toba na kuacha yote ukisha kuyatambua kuwa haya ni makosa, halafu tamaa unafanya mema kwa kutaraji kusamehewa na Mollah wako, huyu kwenu nyinyi anaonekana Mjinga kwa ajili ya kuacha Raha zote za Kidunia, Lakini (Kwenye Jicho la Dini) Mtu huyu anathaminiwa sana katika kundi la Toba kutokana kwa hiyari yake kaacha (Disco) kwa Hiyari yake kaacha Ulevi, Kwa Hiyari yake kaacha Uzinifu, kwa hiyari yake kaingia kwenye Jihadi ya kuacha Rushwa, Kaacha Dhuluma, na mambo mengi ya kupigiwa mfano, huku nyinyi Mashabiki wa Ulimwengu mnamwita Mjinga, Huyu ndie aliyejua maana ya Kutubu na masharti yake, Na hapa ndio tunaingia kwenye Darsa yetu ya leo tupate kuifahamu maana halisi ya Toba.
Toba au Kusamehewa kuna pande mbili , Upande wa kwanza ni kwa yale ulomkosea Mwenye enzi Mungu kwa kupinga amri zake, Na upande wa pili kwa ajili ya makosa ulowafanyia Binaadamu wenzako, Halafu katika hiyo Samahani pia ipo ya aina mbili, yenye kuonekana na isoonekana, Ili kusamehewa unatakiwa uiyone dalili ya hii yenye kuonekana, ndio tena utakua na tamaa pengine asaa Mollah wangu atanisamehe na hayo mengine siku ya siku.
Kwanini sasa Tunaomba Msamaha? Kwanini tuna Tubu? kuyapata majibu hayo inatupasa tukumbuke kitu cha mwanzo kwamba Makosa ni Mtihani, Na mpaka Ukatubu ina maana Umefeli, na Kutubu unapewa (Chance) Nyengine ili ufanye tena, unaomba utizamwe vipi utajirekebisha kwenye hayo Makosa.
Endelea part 2
Binaadamu rahisi sana kujificha kwenye kundi la Werevu, kila mtu mjuaji, ukileta somo lolote yeye kesha khitimu, kitu chochote yeye anakijua zaidi kuliko wewe mletaji, hakubali kabisa mwanaadamu huyu kukaa katika kundi la wajinga, japokua anajijua anateseka kwa kutokujua kitu, Na siku zote tizama (Mfano) huu baina ya Mjanja na Mwerevu, ikitokea Mjanja(Mwerevu) kuibiwa anakua na Hamaki sana, lakini Mjinga akiibiwa ima atakua hana habari au akijua anacheka baadae, unajua kwanini?.
Kwa sababu moja tu Mjinga hana Fikira za Mbeleni, Nikisema mjinga nina maanisha(Innocent one), Lakini Mjanja mambo yake yote ya mipango mipango, mbele itakuaje, wakati hakuna yoyote yule ajuae kesho kitatokea nini. Na hivi ndivo wengi wetu tunavoishi tukiendekeza tamaa mwanzo, mateso baadae, Sasa katika jambo la (Toba) Mjanja hujipa tamaa kuwa kesha samehewa yote ayafanyao, hali ya kuwa haijui hata maana ya Toba.
Haijambo ukiwa Mjinga unakuwa unaishi kwenye maisha ya Khofu na Tamaa, kwa ajili ya khofu kwanza unatekeleza shuruti la Toba na kuacha yote ukisha kuyatambua kuwa haya ni makosa, halafu tamaa unafanya mema kwa kutaraji kusamehewa na Mollah wako, huyu kwenu nyinyi anaonekana Mjinga kwa ajili ya kuacha Raha zote za Kidunia, Lakini (Kwenye Jicho la Dini) Mtu huyu anathaminiwa sana katika kundi la Toba kutokana kwa hiyari yake kaacha (Disco) kwa Hiyari yake kaacha Ulevi, Kwa Hiyari yake kaacha Uzinifu, kwa hiyari yake kaingia kwenye Jihadi ya kuacha Rushwa, Kaacha Dhuluma, na mambo mengi ya kupigiwa mfano, huku nyinyi Mashabiki wa Ulimwengu mnamwita Mjinga, Huyu ndie aliyejua maana ya Kutubu na masharti yake, Na hapa ndio tunaingia kwenye Darsa yetu ya leo tupate kuifahamu maana halisi ya Toba.
Toba au Kusamehewa kuna pande mbili , Upande wa kwanza ni kwa yale ulomkosea Mwenye enzi Mungu kwa kupinga amri zake, Na upande wa pili kwa ajili ya makosa ulowafanyia Binaadamu wenzako, Halafu katika hiyo Samahani pia ipo ya aina mbili, yenye kuonekana na isoonekana, Ili kusamehewa unatakiwa uiyone dalili ya hii yenye kuonekana, ndio tena utakua na tamaa pengine asaa Mollah wangu atanisamehe na hayo mengine siku ya siku.
Kwanini sasa Tunaomba Msamaha? Kwanini tuna Tubu? kuyapata majibu hayo inatupasa tukumbuke kitu cha mwanzo kwamba Makosa ni Mtihani, Na mpaka Ukatubu ina maana Umefeli, na Kutubu unapewa (Chance) Nyengine ili ufanye tena, unaomba utizamwe vipi utajirekebisha kwenye hayo Makosa.
Endelea part 2
TOBA NA MAANA YAKE PART 2
Asalaam Aleiykum
Imekuaje mpaka ukafeli mtihani wako, Sababu ya mwanzo maskini hujui thamani ya Zawadi hii ya Uhai alokupa Mollah wako, Mollah wako kakuumba ikisha akataka ufanye mambo mawili tu, Nayo kama alivokuumba kwa Mapenzi yake na wewe umpende urejee kwake kwa njia ya Ibada ama tuseme (Taqwa) kumkumbuka yeye na kumtaja kwa kadir ya uwezo wako.
Na la pili kufata muongozo wake kwa kutii amri zake zote, Sasa jitizame nini wewe unafanya, unakwenda kinyume na hayo yote mawili na pahala hapo ndipo yanapoanzia matatizo yako yote ulo nayo sasa hivi mpaka kufikia kuiomba hiyo Toba. Mkasa huu wa Toba ulianzaje, Kwa kuwa Mwenye enzi Mungu kaumba kiumbe chake akakipa mtihani na huku anaujua udhaifu wake ndio akamuekea hili chaguo la Toba kama atataka, na kama ataendelea na Jeuri yake basi hilo ni shauri lake, Na mtihani wenyewe ni huu.
وَقُلۡنَا يَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ وَكُلَا مِنۡهَا رَغَدًا حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَـٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ
"Ewe Adam (a.s) kaa wewe na mkeo katika bustani hii (Ya Peponi) Na kuleni humo popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu, mkawa miongoni waliodhulumu"
Hatari kubwa inatokana na kujua, kila anojua mwanzo mpaka mwisho anadhulumu mpaka mwisho wake, jiangalie wewe ukijua peke yako ikawa wengine hawajui unakuwaje, unaanza na dhuluma ya kiburi, dharau inakuingia ndani kwa ndani kuhisi kumbe hawa hawajui kitu, kwanini ikawa hivyo sababu kubwa nikuwa Kiza ni kutokuwepo na Taa, lakini taa ikiwepo kiza hakikai, na kabla ya kuipata hiyo Taa ya kujua wewe ulikuwa sawa sawa na sisi wenzio tuliopo kizani, lakini baada ya kuipata Taa unadhani utakubali kuishi tena kizani, hiyo ndio maana ya kuingia kwenye dhuluma, ukipata kulila tunda tu ushaingia kwenye ujuzi na wala hutoki tena, na kwa sababu Taa ina athari zake, ndizo zinazokupoteza wewe,(Kama vile)utamchukua mtu wa kijijini kwa ghafla umtupe (Japan) anavokua huyo ndivo anavokua mtoto, Mtoto anakuaje? (Innocent)kila mtoto anaona maisha yake kama pepo, Na sote ukiambiwa uhadithie utoto wako unasema sie ilikua hivi ikawa vile, raha hizi na zile, lakini ukianza kupata Fahamu kwa njia ya (Baleghe) mambo yanabadilika kuanzia hapo, fujo yote inaanzia kutokea wakati huo.
Unatoka kwenye ujinga unaingia kwenye werevu, Na ukiingia tu unaanza kudhulumu nafsi yako na hapo unafukuzwa na wewe kwenye Neema ya Mwenye enzi Mungu, Nabii Adam a.s alipewa maneno ya kutubu baada ya kuonekana anasumbuka kwa majuto na kuhangaika, ikisha kwa kuwa kenda kinyume na amri ya Mwenye enzi Mungu akatolewa (Peponi) huo ni mfano chochote utakacho fanya lazima ukilipe, ndipo akatolewa peponi, kwa hiyo na wewe kumbuka kwanza (Kama ulivo kopesha ndivo utakavo lipwa).
Maneno alopewa Nabii Adam a.s yalikua yana kazi mbili ndani ya nafsi yake, moja ilikua ni kwa ajili ya kunyenyekea na kurudi kwa Mollah wake, na ya pili ni kutibu hiyo fahamu ilofanya kosa kwa kumkumbusha kama wewe mkosaji na umo kuomba Toba, na hivyo ndio mpaka leo tukawa ukifanya kosa unalijua hili kosa lakini unakuwa umezidiwa na nguvu ya hilo kosa.
Endelea part 3
Imekuaje mpaka ukafeli mtihani wako, Sababu ya mwanzo maskini hujui thamani ya Zawadi hii ya Uhai alokupa Mollah wako, Mollah wako kakuumba ikisha akataka ufanye mambo mawili tu, Nayo kama alivokuumba kwa Mapenzi yake na wewe umpende urejee kwake kwa njia ya Ibada ama tuseme (Taqwa) kumkumbuka yeye na kumtaja kwa kadir ya uwezo wako.
Na la pili kufata muongozo wake kwa kutii amri zake zote, Sasa jitizame nini wewe unafanya, unakwenda kinyume na hayo yote mawili na pahala hapo ndipo yanapoanzia matatizo yako yote ulo nayo sasa hivi mpaka kufikia kuiomba hiyo Toba. Mkasa huu wa Toba ulianzaje, Kwa kuwa Mwenye enzi Mungu kaumba kiumbe chake akakipa mtihani na huku anaujua udhaifu wake ndio akamuekea hili chaguo la Toba kama atataka, na kama ataendelea na Jeuri yake basi hilo ni shauri lake, Na mtihani wenyewe ni huu.
وَقُلۡنَا يَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ وَكُلَا مِنۡهَا رَغَدًا حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَـٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ
"Ewe Adam (a.s) kaa wewe na mkeo katika bustani hii (Ya Peponi) Na kuleni humo popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu, mkawa miongoni waliodhulumu"
Hatari kubwa inatokana na kujua, kila anojua mwanzo mpaka mwisho anadhulumu mpaka mwisho wake, jiangalie wewe ukijua peke yako ikawa wengine hawajui unakuwaje, unaanza na dhuluma ya kiburi, dharau inakuingia ndani kwa ndani kuhisi kumbe hawa hawajui kitu, kwanini ikawa hivyo sababu kubwa nikuwa Kiza ni kutokuwepo na Taa, lakini taa ikiwepo kiza hakikai, na kabla ya kuipata hiyo Taa ya kujua wewe ulikuwa sawa sawa na sisi wenzio tuliopo kizani, lakini baada ya kuipata Taa unadhani utakubali kuishi tena kizani, hiyo ndio maana ya kuingia kwenye dhuluma, ukipata kulila tunda tu ushaingia kwenye ujuzi na wala hutoki tena, na kwa sababu Taa ina athari zake, ndizo zinazokupoteza wewe,(Kama vile)utamchukua mtu wa kijijini kwa ghafla umtupe (Japan) anavokua huyo ndivo anavokua mtoto, Mtoto anakuaje? (Innocent)kila mtoto anaona maisha yake kama pepo, Na sote ukiambiwa uhadithie utoto wako unasema sie ilikua hivi ikawa vile, raha hizi na zile, lakini ukianza kupata Fahamu kwa njia ya (Baleghe) mambo yanabadilika kuanzia hapo, fujo yote inaanzia kutokea wakati huo.
Unatoka kwenye ujinga unaingia kwenye werevu, Na ukiingia tu unaanza kudhulumu nafsi yako na hapo unafukuzwa na wewe kwenye Neema ya Mwenye enzi Mungu, Nabii Adam a.s alipewa maneno ya kutubu baada ya kuonekana anasumbuka kwa majuto na kuhangaika, ikisha kwa kuwa kenda kinyume na amri ya Mwenye enzi Mungu akatolewa (Peponi) huo ni mfano chochote utakacho fanya lazima ukilipe, ndipo akatolewa peponi, kwa hiyo na wewe kumbuka kwanza (Kama ulivo kopesha ndivo utakavo lipwa).
Maneno alopewa Nabii Adam a.s yalikua yana kazi mbili ndani ya nafsi yake, moja ilikua ni kwa ajili ya kunyenyekea na kurudi kwa Mollah wake, na ya pili ni kutibu hiyo fahamu ilofanya kosa kwa kumkumbusha kama wewe mkosaji na umo kuomba Toba, na hivyo ndio mpaka leo tukawa ukifanya kosa unalijua hili kosa lakini unakuwa umezidiwa na nguvu ya hilo kosa.
Endelea part 3
TOBA NA MAANA YAKE PART 3
Asalaam Aleiykum
Nini Maana ya Toba.
Toba maana yake ni kurejea (Ujingani) lakini sasa ukiwa na fahamu, kumbuka kwanza ulikua ukijua, na sasa una fahamu (Vitu viwili tafauti) na nikisema ujinga nakusudia (Innocent) sasa imekuaje hata urejee, sote mfano wetu kama baba yetu Adam a.s , Haijambo yeye alitolewa Peponi sisi tukipata huko kujua tunakimbia wenyewe, tunakua werevu(Wajanja) tunaikimbia Bustani tunakimbilia Msituni.
Nini kinatokezea kwenye msitu huu wa Ulimwengu, wengine wanajeruhiwa na Simba, wengine wanatafunwa na Chui, Msitu mkubwa kuna wengine wanatafunwa na Nyoka, kuna na wengine wanachaniwa majuba na kanzu zao, kila mtu kabeba begi lake la mbao ndani kuna (Book) kubwa anapepesuka kutafuta njia ya kurudi lakini haijui, kashikwa na werevu wake hajui chochote anakua maskini wa kila kitu, na ukikimbia kutoka kwenye himaya ya Mwenye enzi Mungu na kupinga amri zake na Mollah wako na yeye anaondosha kidogo kidogo Neema yake ya mapenzi kwenye nafsi yako, ndio maana unajikuta huwezi kufanya (Taqwa) yanakutoka mapenzi yalojaa furaha, na kitu hicho kikiondoka ndio mnakua maadui nyinyi kwa nyinyi, Na mapenzi yakiondoka moyoni Roho inaingia mashakani kwa sababu Roho haiwezi kuishi bila ya Furaha, hapo ndio unaanza kuhangaika kutafuta chanzo, mpaka pale utakapo onewa huruma upewe(Maneno ya kutubu) muongozo wa Toba, hapo tena unaanza taratibu kurudi huko(Kwenye mlango wa peponi) ndio Toba yenyewe, na tafauti yako na Mcha Mungu mwenzio tayari keshafika Mlangoni na wewe unapiga hatua za (Mlevi) tatu mbele mbili nyuma, unatokea msituni na makovu chungu nzima huku umebeba (Skeleton)wako, na Toba unaambiwa huku hakutakiwi chochote, ukitaka kurudi uje mweupe, hatutaki hata hilo begi lako la mbao, hatutaki mali ya haramu, hatutaki hata vikosa vidogo vidogo, huko ndiko kutubu, na kama umetubu kweli basi huruhusiwi hata kugeuka nyuma.(Na hiyo ndio inaitwa Tawbat Nasuha),Mollah atujaalie tuipate kwa uweza wake.
Nini Maana ya Toba.
Toba maana yake ni kurejea (Ujingani) lakini sasa ukiwa na fahamu, kumbuka kwanza ulikua ukijua, na sasa una fahamu (Vitu viwili tafauti) na nikisema ujinga nakusudia (Innocent) sasa imekuaje hata urejee, sote mfano wetu kama baba yetu Adam a.s , Haijambo yeye alitolewa Peponi sisi tukipata huko kujua tunakimbia wenyewe, tunakua werevu(Wajanja) tunaikimbia Bustani tunakimbilia Msituni.
Nini kinatokezea kwenye msitu huu wa Ulimwengu, wengine wanajeruhiwa na Simba, wengine wanatafunwa na Chui, Msitu mkubwa kuna wengine wanatafunwa na Nyoka, kuna na wengine wanachaniwa majuba na kanzu zao, kila mtu kabeba begi lake la mbao ndani kuna (Book) kubwa anapepesuka kutafuta njia ya kurudi lakini haijui, kashikwa na werevu wake hajui chochote anakua maskini wa kila kitu, na ukikimbia kutoka kwenye himaya ya Mwenye enzi Mungu na kupinga amri zake na Mollah wako na yeye anaondosha kidogo kidogo Neema yake ya mapenzi kwenye nafsi yako, ndio maana unajikuta huwezi kufanya (Taqwa) yanakutoka mapenzi yalojaa furaha, na kitu hicho kikiondoka ndio mnakua maadui nyinyi kwa nyinyi, Na mapenzi yakiondoka moyoni Roho inaingia mashakani kwa sababu Roho haiwezi kuishi bila ya Furaha, hapo ndio unaanza kuhangaika kutafuta chanzo, mpaka pale utakapo onewa huruma upewe(Maneno ya kutubu) muongozo wa Toba, hapo tena unaanza taratibu kurudi huko(Kwenye mlango wa peponi) ndio Toba yenyewe, na tafauti yako na Mcha Mungu mwenzio tayari keshafika Mlangoni na wewe unapiga hatua za (Mlevi) tatu mbele mbili nyuma, unatokea msituni na makovu chungu nzima huku umebeba (Skeleton)wako, na Toba unaambiwa huku hakutakiwi chochote, ukitaka kurudi uje mweupe, hatutaki hata hilo begi lako la mbao, hatutaki mali ya haramu, hatutaki hata vikosa vidogo vidogo, huko ndiko kutubu, na kama umetubu kweli basi huruhusiwi hata kugeuka nyuma.(Na hiyo ndio inaitwa Tawbat Nasuha),Mollah atujaalie tuipate kwa uweza wake.
Sunday, June 1, 2014
UFUNGUO WA TOBA PART 1
Asalaam Aleiykum
Kila kiumbe anahitaji Toba ndio maana utaona Mtu anatafuta awe kwenye Dini ili apate kuwa karibu ya kutubu, kila mmoja wetu anajiuliza lini nitaacha? mbona nimezama? jee kweli haya nilo nayo yanaachika? nifanye nini nipate kuacha, hususan natia nia kila Ramadhan ikija nitaacha lakini nashindwa kuacha, na inapokwisha tu Ramadhan naanza tena nini kimenisibu?, mbona nateseka na mashaka haya.
Ama Mja kujiona na makosa peke yake ni maradhi, Halafu unaendelea kujiongezea maradhi kwa kutenda Dhanmbi zaidi, lini utapona na sasa uko hoi, Jee kweli wasemavo kuna hiyo Raba au Ufunguo nipate kuingia mimi kwenye hicho chumba cha Toba. Unajibiwa Naam Funguo ipo na leo ndio siku ya kukabidhiwa huo Ufunguo ukiwa unajitaarisha kuingia kwenye Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Sasa ukitaka kuipokea Funguo hii itabidi unyanyue mikono yako juu kama vile unapoitikia Aamin, kwa sababu kila wakati unapoitikia Aamin wewe huikamata Funguo hii au huwa inakuparaza vidoleni, lakini kwa kuwa Aamin yako sio (Deep)unaitikia kwa mazoea basi hukuponyoka Funguo hii. Kwanza kabisa wacha nikujulishe Funguo Yenyewe ili nipate kukufahamisha vipi utaitumia, kwa ajili hiyo inatubidi tuhudhurie sura ya (Qalam)aya ya mwanzo.
نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ
"Nuun.(Naapa kwa) kalamu na yale wayaandikayo(Kwa kalamu hizo)".
Anaapa Mwenye Enzi Mungu kwa Akili na kile kiandikacho Akili hiyo. Na akasema katika aya ya mbele yake, haikua neema hiyo ni wenda wazimu, Akili iko katika mizani nyepesi sana ukiifanyia mchezo kidogo tu unaupata huo Wazimu, Na kama unataka kuijua mizani yenyewe, au kama yangu iko sahihi jiangalie unapo hamaki unakuaje?, Dakika moja tulikuwa na wewe mzima, Mtu kamili nini sasa hivi kimekutokezea, umegeuka si Mtu mzuri tena, nini kimekusibu, mbona umegeuka na kua (Monster).
Hamaki sio wazimu, hamaki ni (Energy) katika mwili wako, ikipanda (Energy)hiyo kwenye Akili inageuza akili hiyo kuwa wazimu, na kama unaweza kui (Transform) inakua (Compassion) baina ya ncha hizo mbili wazimu unakaa kati kati, ukiirudisha moyoni ni (Huruma) ukiipandisha juu (Hamaki)"Ndio Maana Bwana Mtume saw" akatumia Hekima kukwambia ukihamaki (chutama) kufanya hivyo unarejesha (Energy) hii moyoni, unajiepusha na wazimu, na unaweza kusamehe.
Sasa unatakiwa Akili yako uitumie kwa njia za Neema kama alivohimiza Mwenye enzi Mungu, Lakini wewe unaanza kuharibikiwa wapi?, unaharibikiwa pale unapoanza kuitumia Akili hiyo ulonayo kwa njia ya Ufisadi, matatizo yanaanzia hapo, lakini kama utakumbuka Neema hiyo alokupa Mollah wako ndio ilo vumbua Madege, na Meli, ikavumbua Ujenzi na kila kitu uanacho leo hii haya ma(Computer)na mengineyo, ikisha ukagundua kwanini mimi namkera alonipa Neema hii mpaka nikapoteza Funguo hii ya Toba, basi utakua umeshaanza kuutafuta huo ufunguo kwa kukumbuka hilo tu.
Nini kimekufanya baada ya kufungua chumba cha (Thawabu) umekwenda kufungua chumba cha (Dhanmbi) Nani alokupa Funguo hiyo? Sasa tega Macho vizuri, Nyoosha mikono yako huenda labda ukadondoshewa hilo (Funguo) katika Darsa hii ya Ufunguo wa Toba ili na wewe upate kufuta machozi, nakuona unalia siku nyingi, sasa nyamaza tukupe Funguo asaa unaweza kufungua chumba cha hazina ambacho kipo mbele yako, lakini umo kizani unaendelea kupapasa vyumba vya Dhanmbi.
Endelea part 2 ukachukue funguo yako.
Kila kiumbe anahitaji Toba ndio maana utaona Mtu anatafuta awe kwenye Dini ili apate kuwa karibu ya kutubu, kila mmoja wetu anajiuliza lini nitaacha? mbona nimezama? jee kweli haya nilo nayo yanaachika? nifanye nini nipate kuacha, hususan natia nia kila Ramadhan ikija nitaacha lakini nashindwa kuacha, na inapokwisha tu Ramadhan naanza tena nini kimenisibu?, mbona nateseka na mashaka haya.
Ama Mja kujiona na makosa peke yake ni maradhi, Halafu unaendelea kujiongezea maradhi kwa kutenda Dhanmbi zaidi, lini utapona na sasa uko hoi, Jee kweli wasemavo kuna hiyo Raba au Ufunguo nipate kuingia mimi kwenye hicho chumba cha Toba. Unajibiwa Naam Funguo ipo na leo ndio siku ya kukabidhiwa huo Ufunguo ukiwa unajitaarisha kuingia kwenye Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Sasa ukitaka kuipokea Funguo hii itabidi unyanyue mikono yako juu kama vile unapoitikia Aamin, kwa sababu kila wakati unapoitikia Aamin wewe huikamata Funguo hii au huwa inakuparaza vidoleni, lakini kwa kuwa Aamin yako sio (Deep)unaitikia kwa mazoea basi hukuponyoka Funguo hii. Kwanza kabisa wacha nikujulishe Funguo Yenyewe ili nipate kukufahamisha vipi utaitumia, kwa ajili hiyo inatubidi tuhudhurie sura ya (Qalam)aya ya mwanzo.
نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ
"Nuun.(Naapa kwa) kalamu na yale wayaandikayo(Kwa kalamu hizo)".
Anaapa Mwenye Enzi Mungu kwa Akili na kile kiandikacho Akili hiyo. Na akasema katika aya ya mbele yake, haikua neema hiyo ni wenda wazimu, Akili iko katika mizani nyepesi sana ukiifanyia mchezo kidogo tu unaupata huo Wazimu, Na kama unataka kuijua mizani yenyewe, au kama yangu iko sahihi jiangalie unapo hamaki unakuaje?, Dakika moja tulikuwa na wewe mzima, Mtu kamili nini sasa hivi kimekutokezea, umegeuka si Mtu mzuri tena, nini kimekusibu, mbona umegeuka na kua (Monster).
Hamaki sio wazimu, hamaki ni (Energy) katika mwili wako, ikipanda (Energy)hiyo kwenye Akili inageuza akili hiyo kuwa wazimu, na kama unaweza kui (Transform) inakua (Compassion) baina ya ncha hizo mbili wazimu unakaa kati kati, ukiirudisha moyoni ni (Huruma) ukiipandisha juu (Hamaki)"Ndio Maana Bwana Mtume saw" akatumia Hekima kukwambia ukihamaki (chutama) kufanya hivyo unarejesha (Energy) hii moyoni, unajiepusha na wazimu, na unaweza kusamehe.
Sasa unatakiwa Akili yako uitumie kwa njia za Neema kama alivohimiza Mwenye enzi Mungu, Lakini wewe unaanza kuharibikiwa wapi?, unaharibikiwa pale unapoanza kuitumia Akili hiyo ulonayo kwa njia ya Ufisadi, matatizo yanaanzia hapo, lakini kama utakumbuka Neema hiyo alokupa Mollah wako ndio ilo vumbua Madege, na Meli, ikavumbua Ujenzi na kila kitu uanacho leo hii haya ma(Computer)na mengineyo, ikisha ukagundua kwanini mimi namkera alonipa Neema hii mpaka nikapoteza Funguo hii ya Toba, basi utakua umeshaanza kuutafuta huo ufunguo kwa kukumbuka hilo tu.
Nini kimekufanya baada ya kufungua chumba cha (Thawabu) umekwenda kufungua chumba cha (Dhanmbi) Nani alokupa Funguo hiyo? Sasa tega Macho vizuri, Nyoosha mikono yako huenda labda ukadondoshewa hilo (Funguo) katika Darsa hii ya Ufunguo wa Toba ili na wewe upate kufuta machozi, nakuona unalia siku nyingi, sasa nyamaza tukupe Funguo asaa unaweza kufungua chumba cha hazina ambacho kipo mbele yako, lakini umo kizani unaendelea kupapasa vyumba vya Dhanmbi.
Endelea part 2 ukachukue funguo yako.
UFUNGUO WA TOBA PART 2
Asalaam Aleiykum
Pokea Funguo kwenye Viganja vyako huku ukiitikia Aamin itokayo Moyoni tena kwa nguvu, kaa ukumbuke karibuni utaingia kwenye Madarsa ya Ramadhan yenye kulea Roho, Na wewe hutaki ubakie kwenye giza ukiendelea kupapasa, Na fanya Ihsan moja ukiipata Funguo yenyewe basi (Share) na wenzio, wape faida na wao waepukane na Madhnmbi wapate Toba, Na kila mmoja wao atoacha kwa ajili ya kumfundisha au kumuonesha Funguo hii ya Toba na wapi yalipoandikwa mafunzo haya, basi na wewe una ujira wako kwa tendo hilo.
Sasa tunaanza kuutafuta Ufunguo, Ukichunguza kwa makini utaona wingi wa Madhanmbi yako ni yale kwa yale, na yenye alama za kujirejea rejea, umepata kujiuliza kwanini, ushawahi kushangaa kwanini kwenye Quraan kuna kauli naambiwa nisikaribie, nijiepushe, niinamishe macho, kwani kuna kitu gani kinatokea, tukitaka kujua kitu gani kinatokezea itabidi turudi mwanzo wa aya tuliyoitaja hapo mwanzoni ya sura ya (Qalam).
Kaapa Mwenye enzi Mungu kwa kitu alichokiumba yeye Mwenyewe kwa ubora wa neema yake, na kiapo cha Mwenye enzi Mungu sisi Wanaadamu inatupasa kukirejesha kwake Mwenyewe na kusema "Ametukuka Mbora Mwenye kuumba", Kasema Mwenye enzi Mungu "Naapa kwa Akili na kile kiandikacho hiyo Akili"(Kusudio ni huo utendaji wake kazi) Sasa Funguo yenyewe ni hiyo Akili na matumizi yake uamuzi unao wewe, na hiyo ndio (Freedom)ukitaka kufungua mlango wa kushoto au wa kulia hiyari ni yako Mwenyewe.
Sasa nini kinatokea iwapo utafungua(Kutumia)mmoja katika Milango hiyo, kabla ya kuendelea naomba kwanza nikujulishe kitu, kuna vitu vingi vimetajwa kwenye Quraan, lakini nachagua viwili hivi kwa kuwa vimekamatana na kuona na kusikia, "Unaambiwa Angusha macho yako na Uhifadhi tupu yako (قُل لِّلۡمُؤۡمِنِينَ يَغُضُّواْ مِنۡ أَبۡصَـٰرِهِمۡ وَيَحۡفَظُواْ فُرُوجَهُمۡۚ) " la kwanza, na la pili "Unaambiwa jiepushe na mambo ya kipuuzi"(وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَنِ ٱللَّغۡوِ مُعۡرِضُونَ )
Sasa kwanini makatazo hayo muhimu matatu yakasisitizwa, lazima ipo sababu Quraan haiwezi kusisitiza kitu cha kukunyimeni Raha, Na sababu kubwa yenyewe ni hiyo Akili yako, ina tabia au (System)yakuandika mambo mengi yenye kuona na kusikia, Na Kiumbe ukisha andika siri yake lazima ukisome ulichoandika, ukiandika (sex) utaisoma mpaka utaitenda, na ukiandika tu inaandikwa kwenye (Book)lako walo shika (Malaika) na ikisha huku kwenye akili yako maandiko hayo yanakua yanajirejea mchana kutwa mpaka ulale, na hivyo ndivyo ifanyavyo Akili yako, haina kazi nyengine ila kukusomea yote uloandika, funga macho uitizame Akili yako inakusomea nini, (kama ntakutokea ghafla utanionea haya) Inachapa kazi Akili yako kwa kukusomea Biashara, Uongo ulosikia, Dhuluma ulopanga, na kusikiliza mambo ya kipuuzi, unaandika kila siku mambo Million, yale unayoyatenda ikiwa (Thawabu) wewe chunguza hayarejei tena ukakumbuka lakini ikiwa (Dhanmbi) inaongezeka utamu kama (Kiporo) yanarejea tena na tena, mpaka unakua Mteja (Addicted) kwa vile huna nguvu ya kuyazuia, mambo ya kawaida tu kichwani unayapanga ukiyarejea tena na kuyapangua nini habari yetu sisi kwenye utamu wa dhanmbi, vipi wewe utakwenda (Beyond) Dhanmbi ufikie Mlango wa Toba, ndio maana mkaletewa basi Alfajiri hebu anzeni na Quraan, pengine mtazingatia acha Quraan ikurejee itakua Shahid wako na kila ikirejea unaandikiwa (Thawabu)"إِنَّ قُرۡءَانَ ٱلۡفَجۡرِ كَانَ مَشۡہُودً۬ا ".
Endelea part 3
Pokea Funguo kwenye Viganja vyako huku ukiitikia Aamin itokayo Moyoni tena kwa nguvu, kaa ukumbuke karibuni utaingia kwenye Madarsa ya Ramadhan yenye kulea Roho, Na wewe hutaki ubakie kwenye giza ukiendelea kupapasa, Na fanya Ihsan moja ukiipata Funguo yenyewe basi (Share) na wenzio, wape faida na wao waepukane na Madhnmbi wapate Toba, Na kila mmoja wao atoacha kwa ajili ya kumfundisha au kumuonesha Funguo hii ya Toba na wapi yalipoandikwa mafunzo haya, basi na wewe una ujira wako kwa tendo hilo.
Sasa tunaanza kuutafuta Ufunguo, Ukichunguza kwa makini utaona wingi wa Madhanmbi yako ni yale kwa yale, na yenye alama za kujirejea rejea, umepata kujiuliza kwanini, ushawahi kushangaa kwanini kwenye Quraan kuna kauli naambiwa nisikaribie, nijiepushe, niinamishe macho, kwani kuna kitu gani kinatokea, tukitaka kujua kitu gani kinatokezea itabidi turudi mwanzo wa aya tuliyoitaja hapo mwanzoni ya sura ya (Qalam).
Kaapa Mwenye enzi Mungu kwa kitu alichokiumba yeye Mwenyewe kwa ubora wa neema yake, na kiapo cha Mwenye enzi Mungu sisi Wanaadamu inatupasa kukirejesha kwake Mwenyewe na kusema "Ametukuka Mbora Mwenye kuumba", Kasema Mwenye enzi Mungu "Naapa kwa Akili na kile kiandikacho hiyo Akili"(Kusudio ni huo utendaji wake kazi) Sasa Funguo yenyewe ni hiyo Akili na matumizi yake uamuzi unao wewe, na hiyo ndio (Freedom)ukitaka kufungua mlango wa kushoto au wa kulia hiyari ni yako Mwenyewe.
Sasa nini kinatokea iwapo utafungua(Kutumia)mmoja katika Milango hiyo, kabla ya kuendelea naomba kwanza nikujulishe kitu, kuna vitu vingi vimetajwa kwenye Quraan, lakini nachagua viwili hivi kwa kuwa vimekamatana na kuona na kusikia, "Unaambiwa Angusha macho yako na Uhifadhi tupu yako (قُل لِّلۡمُؤۡمِنِينَ يَغُضُّواْ مِنۡ أَبۡصَـٰرِهِمۡ وَيَحۡفَظُواْ فُرُوجَهُمۡۚ) " la kwanza, na la pili "Unaambiwa jiepushe na mambo ya kipuuzi"(وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَنِ ٱللَّغۡوِ مُعۡرِضُونَ )
Sasa kwanini makatazo hayo muhimu matatu yakasisitizwa, lazima ipo sababu Quraan haiwezi kusisitiza kitu cha kukunyimeni Raha, Na sababu kubwa yenyewe ni hiyo Akili yako, ina tabia au (System)yakuandika mambo mengi yenye kuona na kusikia, Na Kiumbe ukisha andika siri yake lazima ukisome ulichoandika, ukiandika (sex) utaisoma mpaka utaitenda, na ukiandika tu inaandikwa kwenye (Book)lako walo shika (Malaika) na ikisha huku kwenye akili yako maandiko hayo yanakua yanajirejea mchana kutwa mpaka ulale, na hivyo ndivyo ifanyavyo Akili yako, haina kazi nyengine ila kukusomea yote uloandika, funga macho uitizame Akili yako inakusomea nini, (kama ntakutokea ghafla utanionea haya) Inachapa kazi Akili yako kwa kukusomea Biashara, Uongo ulosikia, Dhuluma ulopanga, na kusikiliza mambo ya kipuuzi, unaandika kila siku mambo Million, yale unayoyatenda ikiwa (Thawabu) wewe chunguza hayarejei tena ukakumbuka lakini ikiwa (Dhanmbi) inaongezeka utamu kama (Kiporo) yanarejea tena na tena, mpaka unakua Mteja (Addicted) kwa vile huna nguvu ya kuyazuia, mambo ya kawaida tu kichwani unayapanga ukiyarejea tena na kuyapangua nini habari yetu sisi kwenye utamu wa dhanmbi, vipi wewe utakwenda (Beyond) Dhanmbi ufikie Mlango wa Toba, ndio maana mkaletewa basi Alfajiri hebu anzeni na Quraan, pengine mtazingatia acha Quraan ikurejee itakua Shahid wako na kila ikirejea unaandikiwa (Thawabu)"إِنَّ قُرۡءَانَ ٱلۡفَجۡرِ كَانَ مَشۡہُودً۬ا ".
Endelea part 3
UFUNGUO WA TOBA PART 3
Asalaam Aleiykum
Sasa nini ufanye ili upate huo Ufunguo, ili usiendelee kujidanganya, ukawa unapanda ile pembea ya (Merry go Round) ya kutubu na kufanya tena, kuepukana na hilo itabidi ukabidhiwe funguo ili upate Toba ya kweli (Tawbat Nasuha), Na Toba hii haipatikani mpaka pale utakapokata shauri la kumsikiliza huyo ano Kusamehe yeye kasema nini?
Kwanza kakwambia Jiepushe kwenye vikao vya kipuuzi, halafu na la pili kakwambia ukitembea angusha macho yako, (wacha hapa nikupe faida ndogo ya kuangusha macho yako)ukitembea ukawa unatizama macho chini jua una (Preserve) nguvu zako za mwili huchoki haraka, nguvu hazipotei, lakini ukiweka macho juu ukawa unataka uone kila kitu, elewa kila kitu ukitizama una (Realese)nguvu unazitoa kwenda nje, kwa hiyo ni faida ya kwanza ya kuangusha macho yako.Na faida ya pili Ukiweza kufanya hayo utakua ushaanza kutubu, ushakamata Funguo mkononi, halafu jambo la tatu kwa lugha nyepesi inaitwa kufuta, Sasa chukua na (Raba) kamata vitu hivi, vipi?(Furqan 70).
"إِلَّا مَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ عَمَلاً۬ صَـٰلِحً۬ا فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ يُبَدِّلُ ٱللَّهُ سَيِّـَٔاتِهِمۡ حَسَنَـٰتٍ۬ۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورً۬ا رَّحِيمً۬ا"
Ila yule atakaetubia na kuamini na kufanya vitendo vizuri, basi hao ndio Mwenye enzi Mungu atawabadilishia maovu yako kuwa mema, Na Mwenye enzi Mungu ni mwingi wa kusamehe (Na) Mwingi wa Kurehemu.
Kwanza Tubu, acha yote, geuza Akili yako kwenye mambo ya Neema, ikisha jitahidi kuamini, tafuta mambo yatokufanya uamini, basi hata (Mauti)hayakufanyi ukaamini?, halafu tenda vitendo vizuri(Tumia Raba) Mollah wako sio atavifuta vitendo vyako viovu bali atavibadilisha kuwa wema,(kwa kufanya yale mabaya yako yasahauliwe) na yeye Mollah wako ni Mwenye kusamehe na Kukurehemu mja wake kwa kukujulisha hiyo njia ya Ufunguo wa Toba.
Sasa vipi utatubu wakati ushasahau matendo yako maovu, Dhanmbi zako umesahau umefanya nini?. Kuhusu hayo mengine Mollah wako atakusaidia lakini hili la kwenye Akili yako itabidi ufanye Mwenyewe na hapo ndio inabidi ufanye kitu kiitwacho (Regress) uhudhurie tena yale makosa yako, na kila ukiyahudhuria na kuyakumbuka kama kweli unataka kutubia basi utajuta, na ukijuta tu ushalifuta hilo kwenye Akili yako. Lakini hivi sasa unakua umesahau unakumbushwa na Akili yako unarejea kufanya tena, lakini ukikumbuka mwenyewe unakua umekamilisha (Process) kumbuka kila kitu kina sehemu mbili, wewe umefanya sehemu moja tu ya kuandika lakini hujafuta, kamilisha (Full Circle)na hiyo ndio Raba.
Huo ndio Ufunguo wa (Mind) yako itakapokua (Empty) haijaandika mambo ya (Munkarat) machafu, hapo utakua ushafungua Mlango wa Toba, usharudi kwa Mollah wako, na kwa Mollah kama umetubu unaambiwa hivi (Hud 3)
وَأَنِ ٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ ثُمَّ تُوبُوٓاْ إِلَيۡهِ يُمَتِّعۡكُم مَّتَـٰعًا حَسَنًا إِلَىٰٓ أَجَلٍ۬ مُّسَمًّ۬ى وَيُؤۡتِ كُلَّ ذِى فَضۡلٍ۬ فَضۡلَهُ
Na ili Muombe msamaha kwa Mollah wenu, ikishi Mtubie kwake, atakustarehesheni kwa starehe nzuri mpaka muda maalumu,(Wa kuondoka Ulimwenguni)Na atampa (Akhera) kila mwenye fadhila, fadhila yake, (Mpaka mwisho wa aya).
hayo ndio uyapatayo ukianza kushika ufunguo wa Toba, Dhanmbi zina hama kwenye akili na Toba inatawala, mawazo yako yanakua ya vitendo vya Thawabu, Na Mollah wako anakufanyia kila zito kuwa wepesi, unaongezewa riziki, unakingwa na maradhi na kuepushwa na ajali, na hakuna wakati mzuri wa kuchukua funguo hii kama wakati huu wa kuukaribisha mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Inshaa Allah Mwenye Enzi Mungu atujaalie Tawbat Nasuha kwa sote. Aamin.
Sasa nini ufanye ili upate huo Ufunguo, ili usiendelee kujidanganya, ukawa unapanda ile pembea ya (Merry go Round) ya kutubu na kufanya tena, kuepukana na hilo itabidi ukabidhiwe funguo ili upate Toba ya kweli (Tawbat Nasuha), Na Toba hii haipatikani mpaka pale utakapokata shauri la kumsikiliza huyo ano Kusamehe yeye kasema nini?
Kwanza kakwambia Jiepushe kwenye vikao vya kipuuzi, halafu na la pili kakwambia ukitembea angusha macho yako, (wacha hapa nikupe faida ndogo ya kuangusha macho yako)ukitembea ukawa unatizama macho chini jua una (Preserve) nguvu zako za mwili huchoki haraka, nguvu hazipotei, lakini ukiweka macho juu ukawa unataka uone kila kitu, elewa kila kitu ukitizama una (Realese)nguvu unazitoa kwenda nje, kwa hiyo ni faida ya kwanza ya kuangusha macho yako.Na faida ya pili Ukiweza kufanya hayo utakua ushaanza kutubu, ushakamata Funguo mkononi, halafu jambo la tatu kwa lugha nyepesi inaitwa kufuta, Sasa chukua na (Raba) kamata vitu hivi, vipi?(Furqan 70).
"إِلَّا مَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ عَمَلاً۬ صَـٰلِحً۬ا فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ يُبَدِّلُ ٱللَّهُ سَيِّـَٔاتِهِمۡ حَسَنَـٰتٍ۬ۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورً۬ا رَّحِيمً۬ا"
Ila yule atakaetubia na kuamini na kufanya vitendo vizuri, basi hao ndio Mwenye enzi Mungu atawabadilishia maovu yako kuwa mema, Na Mwenye enzi Mungu ni mwingi wa kusamehe (Na) Mwingi wa Kurehemu.
Kwanza Tubu, acha yote, geuza Akili yako kwenye mambo ya Neema, ikisha jitahidi kuamini, tafuta mambo yatokufanya uamini, basi hata (Mauti)hayakufanyi ukaamini?, halafu tenda vitendo vizuri(Tumia Raba) Mollah wako sio atavifuta vitendo vyako viovu bali atavibadilisha kuwa wema,(kwa kufanya yale mabaya yako yasahauliwe) na yeye Mollah wako ni Mwenye kusamehe na Kukurehemu mja wake kwa kukujulisha hiyo njia ya Ufunguo wa Toba.
Sasa vipi utatubu wakati ushasahau matendo yako maovu, Dhanmbi zako umesahau umefanya nini?. Kuhusu hayo mengine Mollah wako atakusaidia lakini hili la kwenye Akili yako itabidi ufanye Mwenyewe na hapo ndio inabidi ufanye kitu kiitwacho (Regress) uhudhurie tena yale makosa yako, na kila ukiyahudhuria na kuyakumbuka kama kweli unataka kutubia basi utajuta, na ukijuta tu ushalifuta hilo kwenye Akili yako. Lakini hivi sasa unakua umesahau unakumbushwa na Akili yako unarejea kufanya tena, lakini ukikumbuka mwenyewe unakua umekamilisha (Process) kumbuka kila kitu kina sehemu mbili, wewe umefanya sehemu moja tu ya kuandika lakini hujafuta, kamilisha (Full Circle)na hiyo ndio Raba.
Huo ndio Ufunguo wa (Mind) yako itakapokua (Empty) haijaandika mambo ya (Munkarat) machafu, hapo utakua ushafungua Mlango wa Toba, usharudi kwa Mollah wako, na kwa Mollah kama umetubu unaambiwa hivi (Hud 3)
وَأَنِ ٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ ثُمَّ تُوبُوٓاْ إِلَيۡهِ يُمَتِّعۡكُم مَّتَـٰعًا حَسَنًا إِلَىٰٓ أَجَلٍ۬ مُّسَمًّ۬ى وَيُؤۡتِ كُلَّ ذِى فَضۡلٍ۬ فَضۡلَهُ
Na ili Muombe msamaha kwa Mollah wenu, ikishi Mtubie kwake, atakustarehesheni kwa starehe nzuri mpaka muda maalumu,(Wa kuondoka Ulimwenguni)Na atampa (Akhera) kila mwenye fadhila, fadhila yake, (Mpaka mwisho wa aya).
hayo ndio uyapatayo ukianza kushika ufunguo wa Toba, Dhanmbi zina hama kwenye akili na Toba inatawala, mawazo yako yanakua ya vitendo vya Thawabu, Na Mollah wako anakufanyia kila zito kuwa wepesi, unaongezewa riziki, unakingwa na maradhi na kuepushwa na ajali, na hakuna wakati mzuri wa kuchukua funguo hii kama wakati huu wa kuukaribisha mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Inshaa Allah Mwenye Enzi Mungu atujaalie Tawbat Nasuha kwa sote. Aamin.
Subscribe to:
Posts (Atom)