Asalaam Aleiykum
Leo napenda kukuchukua kwenye Safari ya Elimu za Ajabu, Lakini Safari hii watakwenda wale wenye kupenda kuyajua mambo mepya, wale wasochoka na kupata habari zilofichika, na zaidi ni wale Dini yao haijaishia kwenye kutia (Udhu) peke yake, Roho daima ina uchu wa kutaka kujua mambo ndio maana wakati mwingi tunatumia katika viwanja vya kutafuta habari, Sasa ukija kwangu mimi daima utapata mambo mepya kwani naelewa Elimu za Mwenye Enzi Mungu hazina mwisho wala upeo, Bahari yake haina Kipimo kila ukizama unaendelea chini wala hufiki Mwisho kwa kuwa mwisho wake ndio mwanzo wake, Kwa hiyo sisi hatujui mwanzo wake, vipi leo tutajua mwisho wake.
Najua Wengine Darsa zangu zinawakera wanakimbia ikisha wanarudi tena kuchungulia safari hii kaleta nini, hiyo ni kazi yangu ninayoifanya kwa siri juu yako ili upate mabadiliko, na ukiona umerudi tena kuchungulia ina maana ushaanza kupata Muongozo fulani ambao unakufanya uchungulie tena, hiyo ni ishara nzuri endelea utapata mafanikio makubwa.
Sasa leo pata faida ya Safari wanayokwenda (Mystic). Nini (Mystic)?.
Nimekuja kufahamu kwamba (Mystic)ni Mwanasayansi wa Dini, Mnao wanasayansi wenu wa Dunia, Na sisi tuna hawa wetu wa Dini, Tafauti yao hawa wa Dunia wanachambua kwa njia ya nje mpaka mara inatokezea tu kwenye (Akili)zao wakapata hii ni (DNA)Nikisema inatokezea nina maana wanafunguliwa na Mwenye enzi Mungu hiyo elimu ya kujua.
Na Wanasayansi wa Dini wao Wanakwenda Ndani Wanataka kujua hiyo (DNA)imetokea wapi, Nani aloileta kwa hiyo kwa kutaka kuyajua hayo ndio lazima Mwanasayansi wa Dini achupe katika kiza kinene, kwani nje kuna muangaza lakini ndani kuna Giza zito lazima ulipite giza hilo ndio utokeze kwenye Muangaza wa Elimu za Ajabu, ndio maana kuwa Mwanasayansi wa Dunia ni rahisi lakini kuelekea Uwanasayansi wa Dini ni kazi nzito ambayo mashujaa peke wanoweza kuchupa, wengine wanafanikiwa na wengine wanadhurika wakawa waharibifu na hata kufikia kupoteza Akili kwa mambo makubwa wanayokutana nayo huko kwenye hii (Mystical Journey).
Ndani ya Safari hii ndio unakutana na hizo Elimu za Ajabu, Kama Elimu ya Kuruka(Ukapaa kama ndege)
Elimu ya Kupotea(Mara ukawa huonekani)
Elimu ya Kutibu ukiwa Mbali.
Elimu ya kuona Viumbe wengine.
Elimu ya Kutisha Viumbe wakakuogopa.
Elimu ya Kungara ukawa unapendwa na halaiki ya watu.
Na Elimu chungu nzima ambazo hazina idadi maalum ambazo katika safari hii kila ukigundua zinazidi kuongezeka na hapo ndio Kiumbe kwa papara za kutaka yote anarudi Safari hii pengine kaambulia kupata elimu moja tu katika maajabu hayo, Napenda uelewe Safari hiyo ni ndefu na inataka mataarisho makubwa, kuzidi kuyachambua haya mambo endelea part 2
Sunday, November 30, 2014
ELIMU ZA AJABU PART 2
Asalaam Aleiykum
Anahadithia Sayyidna Abu Huraira r.a "Akisema" Bwana Mtume s.a.w kanifundisha Elimu mbili ya kwanza nimekupeni, lakini ningekupeni hii ya pili mngenikata kichwa. Hayo ni maneno ya Sahaba wa Bwana Mtume s.a.w ambaye yeye kaenda hiyo safari kubwa ya (Mystical Journey)inayoitwa Miraji.Sura ya Israa aya 1.
سُبۡحَـٰنَ ٱلَّذِىٓ أَسۡرَىٰ بِعَبۡدِهِۦ لَيۡلاً۬ مِّنَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ إِلَى ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡأَقۡصَا ٱلَّذِى بَـٰرَكۡنَا حَوۡلَهُ ۥ لِنُرِيَهُ ۥ مِنۡ ءَايَـٰتِنَآۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ
Utukufu ni wake yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku kutoka msikiti Mtukufu wa(Makka)mpaka Msikiti wa mbali wa Aqsa(Bayyitul Muqadas)ambao tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake, ili tumuoneshe baadhi ya Alama zetu, Hakika (Mwenye enzi Mungu)ni Mwenye kusikia (na) kuona.
Kweli angekatwa kichwa kwa sababu ee hivi leo kuna baadhi ya watu wamo ndani ya Uislam wanaipinga safari hiyo kwa malumbano, seuze hayo mambo yalioko huko, kwa hiyo kuwa na hakika elimu hizo zipo na ziliwahi hata kuandikwa baadhi yake kwenye vitabu lakini maskini vikachomwa moto vyote mwanzoni mwa miaka ya 70 na (Library zote kufungwa), na hiyo ndio ikawa hasara ya (Generation)hii kunyimwa elimu hizi za Ajabu.
Imebakia sasa hivi elimu zinazofahamika ni zile za wazi, kwa hiyo umefika wakati sasa japo kuashiria, angalau kukumbusha kwamba hizi elimu zilikuwepo, zipo na zitaendelea kuwepo na pengine (Generation) ijayo itaweza kufatilia kwa undani. Kwani kutokana na aya hii ya sura ya (Fussilat 53)
"سَنُرِيهِمۡ ءَايَـٰتِنَا فِى ٱلۡأَفَاقِ وَفِىٓ أَنفُسِہِمۡ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَهُمۡ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّۗ "
Tutawaonesha(Ukweli wa)Maneno yetu haya katika nchi za mbali na katika nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli.
Kutokana na maneno hayo inaonesha wazi mambo makubwa ya ajabu yasokwisha yapo, yanaendelea kuvumbuliwa kwa njia ya nje na ndani katika fani zote za maisha haya ya Ulimwenguni, Lakini kwa (Mystic) inakua tabu kuyaandika au kuhadithia kwa kuwa ni ya ajabu na hayana mfano, kwa hiyo (Mystic) anakaa kimya na kuashiria tu kuna hichi na kile, ili uende ukaone mwenyewe.
Sasa Baada ya kuizungumza Dhumuni la darsa yetu hii sasa wacha tuanze safari yetu hii ili tupate angalau chembe ya muangaza wa Elimu hizi za Ajabu. Basi tuanze na ajabu ya mwanzo iliyomo ndani ya kitabu hichi cha Quraan, Kumbuka kitu kimoja vitabu vyote unasoma unavimaliza lakini hichi cha Quraan hukimalizi, unaambiwa kisome daima, Jee huoni Ajabu kwa Jambo hilo, kwanini ukisome ikisha ukirejee tena na tena mpaka mwisho wa umri wako?, mbona vyengine ukimaliza inakua basi, kwanini hichi tu ndio uendelee?.
Utajibiwa Swali lako hilo na baadhi ya aya za Quraan ili upate muongozo na mimi nita (Share) ajabu hiyo na wewe ili upate kuijua kwa vizuri.
Endelea part 3
Anahadithia Sayyidna Abu Huraira r.a "Akisema" Bwana Mtume s.a.w kanifundisha Elimu mbili ya kwanza nimekupeni, lakini ningekupeni hii ya pili mngenikata kichwa. Hayo ni maneno ya Sahaba wa Bwana Mtume s.a.w ambaye yeye kaenda hiyo safari kubwa ya (Mystical Journey)inayoitwa Miraji.Sura ya Israa aya 1.
سُبۡحَـٰنَ ٱلَّذِىٓ أَسۡرَىٰ بِعَبۡدِهِۦ لَيۡلاً۬ مِّنَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ إِلَى ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡأَقۡصَا ٱلَّذِى بَـٰرَكۡنَا حَوۡلَهُ ۥ لِنُرِيَهُ ۥ مِنۡ ءَايَـٰتِنَآۚ إِنَّهُ ۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ
Utukufu ni wake yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku kutoka msikiti Mtukufu wa(Makka)mpaka Msikiti wa mbali wa Aqsa(Bayyitul Muqadas)ambao tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake, ili tumuoneshe baadhi ya Alama zetu, Hakika (Mwenye enzi Mungu)ni Mwenye kusikia (na) kuona.
Kweli angekatwa kichwa kwa sababu ee hivi leo kuna baadhi ya watu wamo ndani ya Uislam wanaipinga safari hiyo kwa malumbano, seuze hayo mambo yalioko huko, kwa hiyo kuwa na hakika elimu hizo zipo na ziliwahi hata kuandikwa baadhi yake kwenye vitabu lakini maskini vikachomwa moto vyote mwanzoni mwa miaka ya 70 na (Library zote kufungwa), na hiyo ndio ikawa hasara ya (Generation)hii kunyimwa elimu hizi za Ajabu.
Imebakia sasa hivi elimu zinazofahamika ni zile za wazi, kwa hiyo umefika wakati sasa japo kuashiria, angalau kukumbusha kwamba hizi elimu zilikuwepo, zipo na zitaendelea kuwepo na pengine (Generation) ijayo itaweza kufatilia kwa undani. Kwani kutokana na aya hii ya sura ya (Fussilat 53)
"سَنُرِيهِمۡ ءَايَـٰتِنَا فِى ٱلۡأَفَاقِ وَفِىٓ أَنفُسِہِمۡ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَهُمۡ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّۗ "
Tutawaonesha(Ukweli wa)Maneno yetu haya katika nchi za mbali na katika nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli.
Kutokana na maneno hayo inaonesha wazi mambo makubwa ya ajabu yasokwisha yapo, yanaendelea kuvumbuliwa kwa njia ya nje na ndani katika fani zote za maisha haya ya Ulimwenguni, Lakini kwa (Mystic) inakua tabu kuyaandika au kuhadithia kwa kuwa ni ya ajabu na hayana mfano, kwa hiyo (Mystic) anakaa kimya na kuashiria tu kuna hichi na kile, ili uende ukaone mwenyewe.
Sasa Baada ya kuizungumza Dhumuni la darsa yetu hii sasa wacha tuanze safari yetu hii ili tupate angalau chembe ya muangaza wa Elimu hizi za Ajabu. Basi tuanze na ajabu ya mwanzo iliyomo ndani ya kitabu hichi cha Quraan, Kumbuka kitu kimoja vitabu vyote unasoma unavimaliza lakini hichi cha Quraan hukimalizi, unaambiwa kisome daima, Jee huoni Ajabu kwa Jambo hilo, kwanini ukisome ikisha ukirejee tena na tena mpaka mwisho wa umri wako?, mbona vyengine ukimaliza inakua basi, kwanini hichi tu ndio uendelee?.
Utajibiwa Swali lako hilo na baadhi ya aya za Quraan ili upate muongozo na mimi nita (Share) ajabu hiyo na wewe ili upate kuijua kwa vizuri.
Endelea part 3
ELIMU ZA AJABU PART 3
Asalaam Aleiykum
Ajabu yenyewe inaanzia katika maneno haya ya aya ya 5 na 6 sura ya (Muzzamil)"إِنَّا سَنُلۡقِى عَلَيۡكَ قَوۡلاً۬ ثَقِيلاً ""hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito""إِنَّ نَاشِئَةَ ٱلَّيۡلِ هِىَ أَشَدُّ وَطۡـًٔ۬ا وَأَقۡوَمُ قِيلاً ""Hakika kuamka usiku(Na kufanya Ibada)kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno (yake) yanatua zaidi.
Hapo pametajwa jambo la ajabu, umetajwa moyo ikatajwa kutua kwa maneno, Maneno yanatokea wapi?, kwenye Akili, Moyoni yanakwenda kupewa tafsiri au maana, ndio maana ukaambiwa nyanyuka usiku, kwanini ikawa usiku? Kwa sababu umelala na Akili isha (Process) mambo yanotokea mchana wote, Unaamka ukiwa Mweupe, unasoma kitabu cha Mwenye Enzi Mungu kwa utulivu wa hali ya juu pasipo kuwa na mawazo mengine, hapo tena neno linaanguka moyoni na likianguka tu wakati umepata utulivu ndio unapata hicho kitu kinaitwa (Awakening) na ukipata hali hiyo japo kwa aya moja basi ushaonja tone la (Mysticism) na unabadilika daima, aya moja inakufanya utembee kwenye Bahari, aya moja itakufanya uwatibie wenzio Maradhi yao, pamoja na wewe mwenyewe.
Na kwanini isiwe hivyo na wakati imetajwa ndani ya Quraan kuwa huu ni muongozo na ponesho la maradhi yaliyomo kwenye vifua vyenu, na kifua kina mambo mengi, husda imo humo, kutokuamini kumo humo, Ini limo humo, Figo limo humo, lakini kuupata huo muongozo na ponesho lenyewe linahitaji huyo msomaji yupo kwenye daraja gani.Maskini leo wako wapi wale (Mystic) walokua wakiyasomea maji kama unaumwa tumbo linapoa, kama Mwanamke hazai anapata uja uzito, Ndio maana ukatajwa Usiku ndio wakati bora wa kutokea tukio hilo, "Hakika tutakuteremshia maneno mazito".
Sasa nini habari ya wale wasojua kusoma au wanajua lakini hawana nafasi ya kusoma, wao wanaambiwa Al-Araf (204)
وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُ ۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na Itakaposomwa Quraan isikilizeni na nyamazeni ili mpate kurehemewa.
Kwanza isikilize halafu kaa kimya, yametajwa maneno mawili ya mfano mzuri sana, kwanini usikilize? kwa sababu wewe hufanyi yote mawili, pengine inasomwa wewe unasikiliza sauti ya msomaji badala ya Quraan, na huku Akili yako inatizama labda videvu vya Sheikh, au kakosea Nun au hajatia shada na huku maskini unakosa kitu adhimu kinakupita cha Rehma ya Mollah wako nilichokitaja hapo juu, kwa hiyo ndio unaambiwa sikiliza ikisha ukae kimya, yaani nje unasikiliza na ndani huna mawazo yanoendelea kwenye Akili yako hapo huenda likatokea hilo tukio la Ajabu.
Pengine aya huenda ikapita na kuupasua hilo jipo la fahamu ukabubujikwa na machozi bila ya kujielewa, Ndio maana mnaambiwa sikilizeni mawaidha asaa yanaweza kukubadilisha, Lakini inategemea msomaji na huyo msikilizaji. Ama kwa wale wanotaka kushuhudiwa wao waisome Alfajiri, (Angalia katika Darsa yangu ya kushuhudiwa na Quraan).
Basi Naam yasome maneno haya mazito yaloteremshwa na Mwenye Enzi Mungu ambayo Mwanaadamu hujui ndani yake kuna Ajabu gani, Soma upate kujua kwanini Jahazi ya Nabii Nuhu a.s ilikua ikenda na kusimama kutokana na maneno ya (Bismillahi Majriha wamursaha), hayo ndio baadhi ya maajabu machache niloyataja yaliyomo kwenye Quraan, yapo mengi lakini muda wetu hautoshi kuyazungumza yote kwa njia ya maandishi, na Mifano ya maajabu hayo ni kama vile kuzuia gari isiondoke, ukasoma mpaka ukafanya Treni ikusubiri, Ndege isiruke nk, najua mtashangaa ndio maana nikaita Elimu za Ajabu na hayo ndio mambo ya (Mysticsim).
Sasa tuingie katika Elimu ya (Kuruka au Kupaa) sisemi hivi mtu akaanza kuniuliza(Method) ya kufanya, mimi nazungumza kwa njia ya Elimu, wewe una hiyari yako kutafuta(Method) ukija kukwama kwenye Miti mimi sichukui dhamana, wapi imepatikana Elimu hii tutaendelea wiki ijayo kwenye Part 4.
Shukran.
Ajabu yenyewe inaanzia katika maneno haya ya aya ya 5 na 6 sura ya (Muzzamil)"إِنَّا سَنُلۡقِى عَلَيۡكَ قَوۡلاً۬ ثَقِيلاً ""hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito""إِنَّ نَاشِئَةَ ٱلَّيۡلِ هِىَ أَشَدُّ وَطۡـًٔ۬ا وَأَقۡوَمُ قِيلاً ""Hakika kuamka usiku(Na kufanya Ibada)kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno (yake) yanatua zaidi.
Hapo pametajwa jambo la ajabu, umetajwa moyo ikatajwa kutua kwa maneno, Maneno yanatokea wapi?, kwenye Akili, Moyoni yanakwenda kupewa tafsiri au maana, ndio maana ukaambiwa nyanyuka usiku, kwanini ikawa usiku? Kwa sababu umelala na Akili isha (Process) mambo yanotokea mchana wote, Unaamka ukiwa Mweupe, unasoma kitabu cha Mwenye Enzi Mungu kwa utulivu wa hali ya juu pasipo kuwa na mawazo mengine, hapo tena neno linaanguka moyoni na likianguka tu wakati umepata utulivu ndio unapata hicho kitu kinaitwa (Awakening) na ukipata hali hiyo japo kwa aya moja basi ushaonja tone la (Mysticism) na unabadilika daima, aya moja inakufanya utembee kwenye Bahari, aya moja itakufanya uwatibie wenzio Maradhi yao, pamoja na wewe mwenyewe.
Na kwanini isiwe hivyo na wakati imetajwa ndani ya Quraan kuwa huu ni muongozo na ponesho la maradhi yaliyomo kwenye vifua vyenu, na kifua kina mambo mengi, husda imo humo, kutokuamini kumo humo, Ini limo humo, Figo limo humo, lakini kuupata huo muongozo na ponesho lenyewe linahitaji huyo msomaji yupo kwenye daraja gani.Maskini leo wako wapi wale (Mystic) walokua wakiyasomea maji kama unaumwa tumbo linapoa, kama Mwanamke hazai anapata uja uzito, Ndio maana ukatajwa Usiku ndio wakati bora wa kutokea tukio hilo, "Hakika tutakuteremshia maneno mazito".
Sasa nini habari ya wale wasojua kusoma au wanajua lakini hawana nafasi ya kusoma, wao wanaambiwa Al-Araf (204)
وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُ ۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na Itakaposomwa Quraan isikilizeni na nyamazeni ili mpate kurehemewa.
Kwanza isikilize halafu kaa kimya, yametajwa maneno mawili ya mfano mzuri sana, kwanini usikilize? kwa sababu wewe hufanyi yote mawili, pengine inasomwa wewe unasikiliza sauti ya msomaji badala ya Quraan, na huku Akili yako inatizama labda videvu vya Sheikh, au kakosea Nun au hajatia shada na huku maskini unakosa kitu adhimu kinakupita cha Rehma ya Mollah wako nilichokitaja hapo juu, kwa hiyo ndio unaambiwa sikiliza ikisha ukae kimya, yaani nje unasikiliza na ndani huna mawazo yanoendelea kwenye Akili yako hapo huenda likatokea hilo tukio la Ajabu.
Pengine aya huenda ikapita na kuupasua hilo jipo la fahamu ukabubujikwa na machozi bila ya kujielewa, Ndio maana mnaambiwa sikilizeni mawaidha asaa yanaweza kukubadilisha, Lakini inategemea msomaji na huyo msikilizaji. Ama kwa wale wanotaka kushuhudiwa wao waisome Alfajiri, (Angalia katika Darsa yangu ya kushuhudiwa na Quraan).
Basi Naam yasome maneno haya mazito yaloteremshwa na Mwenye Enzi Mungu ambayo Mwanaadamu hujui ndani yake kuna Ajabu gani, Soma upate kujua kwanini Jahazi ya Nabii Nuhu a.s ilikua ikenda na kusimama kutokana na maneno ya (Bismillahi Majriha wamursaha), hayo ndio baadhi ya maajabu machache niloyataja yaliyomo kwenye Quraan, yapo mengi lakini muda wetu hautoshi kuyazungumza yote kwa njia ya maandishi, na Mifano ya maajabu hayo ni kama vile kuzuia gari isiondoke, ukasoma mpaka ukafanya Treni ikusubiri, Ndege isiruke nk, najua mtashangaa ndio maana nikaita Elimu za Ajabu na hayo ndio mambo ya (Mysticsim).
Sasa tuingie katika Elimu ya (Kuruka au Kupaa) sisemi hivi mtu akaanza kuniuliza(Method) ya kufanya, mimi nazungumza kwa njia ya Elimu, wewe una hiyari yako kutafuta(Method) ukija kukwama kwenye Miti mimi sichukui dhamana, wapi imepatikana Elimu hii tutaendelea wiki ijayo kwenye Part 4.
Shukran.
Sunday, November 23, 2014
MAMBO MATATU YANOKOSESHA PEPO PART 1
Asalaam Aleiykum
Siku moja Mcha Mungu Hadad alisisitiza katika maombi yake kwa Mungu aoneshwe kwenye usingizi wake nani Mcha Mungu zaidi katika Mji wake, "Akajibiwa kwenye usingizi ni Jirani yako" akafurahi sana kujua kumbe Jirani yake ndio kamshinda kwa Ibada na mapenzi ya Allah, Akaomba tena sasa naomba nijulishwe yule Mtenda Dhanmbi kubwa kuliko wote ili nipate kumjua, "Akajibiwa tena ndani ya Usingizi wake ni Jirani yako" Mambo haya yalimshangaza sana Hadad akawa hajui la kufanya, kwa sababu Ucha Mungu anauona kwa yule Jirani, ana Duka lake, anasali kama kawaida, anatoa Sadaka, Lakini anashindwa kuona nini maasi yake.
Sote tumejificha kama huyo Jirani, kwa sababu Jirani alikua na udhaifu mkubwa, vita vya kujizuia na hili jambo la mwanzo vilimshinda, akichukua watoto wa watu mitaani kwa siri na kuzini nao, akichukua wake za watu na kufanya nao mapenzi, Jambo hili la (1)(Sex)lilimuhujumu kabisa ikawa kwa Binaadamu wenzie wasomjua wanamuona Mcha Mungu kwa kuwa hatoki katika Nyumba za Ibada na kutenda mambo mema,na ana simamisha Sala sana, lakini usiku ukiingia anageuka (Dracula). Na hivi ndivo wengi tunavoishi upande (Sinner) na tukigeuzwa upande wa pili (Saints).
Sex ni adui wetu mkubwa wa kutuzuilia kuipata (Pepo) ya Mwenye enzi Mungu, Ni tendo lenye kuichafua Roho, na kukaribisha maradhi ya Mwili na Akili yake ikiwa itatumika sivyo na maamrisho kama yalivyoteremka kwenye sura ya Muuminun aya ya 5 na 6. وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَـٰفِظُونَ.
"Na wale ambao wanalinda Tupu zao"
Vinatakiwa kulindwa Vipande vya nyama hizi kwa ulinzi wa hali ya juu kabisa, kwani ikiwa kitatumika kwa njia nyengine isiyokua ya kisheria kipande cha nyama hichi kitaleta madhara makubwa kwa muhusika na jamii nzima kwa jumla, kitapita njia zisizo amrishwa na kufanya uharibifu mkubwa kama vile wa kuacha kizazi kisichokua na familia ya upande mmoja, Muhusika atakua akisambaza maradhi kutoka huku kwenda kule, atakua akiacha maumivu makubwa kwa wale anowatekeleza, Ikiwa jambo hili halikuwekewa ulinzi linakufukuza kabisa katika enzi ya kumkumbuka Mollah wako, ndio maana likaambiwa jambo hili limeruhusiwa lakini ila kwa.
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٲجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَـٰنُہُمۡ فَإِنَّہُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ
"Isipokua kwa wake zao au kwa(Wanawake)wale iliyowamiliki mikono yao ya Kiume(Kulia)Basi hao ndio wasiolaumiwa.
Endelea part 2
Siku moja Mcha Mungu Hadad alisisitiza katika maombi yake kwa Mungu aoneshwe kwenye usingizi wake nani Mcha Mungu zaidi katika Mji wake, "Akajibiwa kwenye usingizi ni Jirani yako" akafurahi sana kujua kumbe Jirani yake ndio kamshinda kwa Ibada na mapenzi ya Allah, Akaomba tena sasa naomba nijulishwe yule Mtenda Dhanmbi kubwa kuliko wote ili nipate kumjua, "Akajibiwa tena ndani ya Usingizi wake ni Jirani yako" Mambo haya yalimshangaza sana Hadad akawa hajui la kufanya, kwa sababu Ucha Mungu anauona kwa yule Jirani, ana Duka lake, anasali kama kawaida, anatoa Sadaka, Lakini anashindwa kuona nini maasi yake.
Sote tumejificha kama huyo Jirani, kwa sababu Jirani alikua na udhaifu mkubwa, vita vya kujizuia na hili jambo la mwanzo vilimshinda, akichukua watoto wa watu mitaani kwa siri na kuzini nao, akichukua wake za watu na kufanya nao mapenzi, Jambo hili la (1)(Sex)lilimuhujumu kabisa ikawa kwa Binaadamu wenzie wasomjua wanamuona Mcha Mungu kwa kuwa hatoki katika Nyumba za Ibada na kutenda mambo mema,na ana simamisha Sala sana, lakini usiku ukiingia anageuka (Dracula). Na hivi ndivo wengi tunavoishi upande (Sinner) na tukigeuzwa upande wa pili (Saints).
Sex ni adui wetu mkubwa wa kutuzuilia kuipata (Pepo) ya Mwenye enzi Mungu, Ni tendo lenye kuichafua Roho, na kukaribisha maradhi ya Mwili na Akili yake ikiwa itatumika sivyo na maamrisho kama yalivyoteremka kwenye sura ya Muuminun aya ya 5 na 6. وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَـٰفِظُونَ.
"Na wale ambao wanalinda Tupu zao"
Vinatakiwa kulindwa Vipande vya nyama hizi kwa ulinzi wa hali ya juu kabisa, kwani ikiwa kitatumika kwa njia nyengine isiyokua ya kisheria kipande cha nyama hichi kitaleta madhara makubwa kwa muhusika na jamii nzima kwa jumla, kitapita njia zisizo amrishwa na kufanya uharibifu mkubwa kama vile wa kuacha kizazi kisichokua na familia ya upande mmoja, Muhusika atakua akisambaza maradhi kutoka huku kwenda kule, atakua akiacha maumivu makubwa kwa wale anowatekeleza, Ikiwa jambo hili halikuwekewa ulinzi linakufukuza kabisa katika enzi ya kumkumbuka Mollah wako, ndio maana likaambiwa jambo hili limeruhusiwa lakini ila kwa.
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٲجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَـٰنُہُمۡ فَإِنَّہُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ
"Isipokua kwa wake zao au kwa(Wanawake)wale iliyowamiliki mikono yao ya Kiume(Kulia)Basi hao ndio wasiolaumiwa.
Endelea part 2
MAMBO MATATU YANOKOSESHA PEPO PART 2
Asalaam Aleiykum
Lakini utapojaribu njia nyengine yoyote ya kuiba zabibu za watu basi ujue utalaumiwa, Kwa sababu njia uliyoifata ni chafu na ina mambo ya kila aina, na ni Mwenendo mbaya kabisa ambao maradhi yake ni magumu kupona, Na pia yana tabia ya kujirejea kwa kuwa yanaishi Akilini na wewe huna uhodari wa kuishinda Akili pamoja na (Ibilis).
Ndio maana ukianza uzinifu ni vigumu kuepuka, inatakiwa ifanyike kazi kubwa sana mpaka utolewe katika mzunguko huu wa mapenzi ya zinaa, Sasa sababu gani ikakupelekea mpaka ukaikosa pepo, sababu zipo nyingi lakini mie nitazitaja hizi mbili ili tupate kuzizingatia, Sababu ya kwanza(Sex)inakushughulisha humkumbuki kabisa Mollah wako, kwa sababu mambo mawili hayo hayakai pamoja moja linalaza na moja linakuamsha, (na mfano unao mwenyewe ukiwa na huyo wa halali wako mke au mume mkitaka kufanya tendo la ndoa ukiambiwa tutie udhu tusali Rakaa mbili basi hamu yote hapo hapo inaondoka)Kwa sababu unakua ushaamshwa, ushatolewa katika hali yakua mnyama umerejeshwa kwenye ubinaadamu, sasa jitizame huko uendako usikoambiwa tia udhu unakuaje, Wewe na mnyama hamna tafauti.
Unalala ukikoroma ndio maana hutaki mambo ya dini, huwezi hata kusali, kutokana na tendo unalo jishughulisha nalo ni la kukatazwa, na chochote kile unachokatazwa kina kushughulisha sana, wewe chunguza pahala uambiwe usichungulie uone utakavo hangaika kutaka kujua kuna nini hata nisichungulie?.Kwa hivyo tulivyoambiwa Zinaa ni haramu tumeumia, inafikia ukisikia muazini una hamaki, yana kushughulisha mambo haya mpaka kufikia Utu uzima bado mambo yamekuganda Akilini, Tahadhari sana huku mwili ushachoka, maradhi yashawasili na wewe umeshakua Muflis huna tamaa tena ya pepo.
Na Jambo la pili ni ule uharibifu unopita kuufanya, unaumiza Roho za Binaadamu wenzio, Unawacha kizazi kisichokua na Familia, basi kama wanavoteseka hao binaadamu wenzio jua na wewe maandalizi ya Adhabu yanakusubiri bila ya shaka yoyote na hilo pekee linakutosha kukukosesha pepo.
Lakini utapojaribu njia nyengine yoyote ya kuiba zabibu za watu basi ujue utalaumiwa, Kwa sababu njia uliyoifata ni chafu na ina mambo ya kila aina, na ni Mwenendo mbaya kabisa ambao maradhi yake ni magumu kupona, Na pia yana tabia ya kujirejea kwa kuwa yanaishi Akilini na wewe huna uhodari wa kuishinda Akili pamoja na (Ibilis).
Ndio maana ukianza uzinifu ni vigumu kuepuka, inatakiwa ifanyike kazi kubwa sana mpaka utolewe katika mzunguko huu wa mapenzi ya zinaa, Sasa sababu gani ikakupelekea mpaka ukaikosa pepo, sababu zipo nyingi lakini mie nitazitaja hizi mbili ili tupate kuzizingatia, Sababu ya kwanza(Sex)inakushughulisha humkumbuki kabisa Mollah wako, kwa sababu mambo mawili hayo hayakai pamoja moja linalaza na moja linakuamsha, (na mfano unao mwenyewe ukiwa na huyo wa halali wako mke au mume mkitaka kufanya tendo la ndoa ukiambiwa tutie udhu tusali Rakaa mbili basi hamu yote hapo hapo inaondoka)Kwa sababu unakua ushaamshwa, ushatolewa katika hali yakua mnyama umerejeshwa kwenye ubinaadamu, sasa jitizame huko uendako usikoambiwa tia udhu unakuaje, Wewe na mnyama hamna tafauti.
Unalala ukikoroma ndio maana hutaki mambo ya dini, huwezi hata kusali, kutokana na tendo unalo jishughulisha nalo ni la kukatazwa, na chochote kile unachokatazwa kina kushughulisha sana, wewe chunguza pahala uambiwe usichungulie uone utakavo hangaika kutaka kujua kuna nini hata nisichungulie?.Kwa hivyo tulivyoambiwa Zinaa ni haramu tumeumia, inafikia ukisikia muazini una hamaki, yana kushughulisha mambo haya mpaka kufikia Utu uzima bado mambo yamekuganda Akilini, Tahadhari sana huku mwili ushachoka, maradhi yashawasili na wewe umeshakua Muflis huna tamaa tena ya pepo.
Na Jambo la pili ni ule uharibifu unopita kuufanya, unaumiza Roho za Binaadamu wenzio, Unawacha kizazi kisichokua na Familia, basi kama wanavoteseka hao binaadamu wenzio jua na wewe maandalizi ya Adhabu yanakusubiri bila ya shaka yoyote na hilo pekee linakutosha kukukosesha pepo.
MAMBO MATATU YANOKOSESHA PEPO PART 3
Asalaam Aleiykum
Jambo la pili nii hizi Hamaki tulonazo.
Sasa tunaingia kwenye Sumu ya maangamizi ambayo kama utakunywa sumu hii basi wewe kwa hiyari yako umejiharamishia Pepo. Hamaki ni madhara makubwa kama utaitizama kwa undani, magonvi yote yanaletwa na hamaki, chuki zote zinatokana na hamaki, Hebu tuliangalie tendo hili la hamaki mwanzo wake wapi.
Hamaki ni tendo linalotokea ndani ya mwili wako ambalo ni (Energy)maalum inayoripuka kutokana na kitendo cha nje kilichofanywa na Mtu mwengine, Nini kafanya? kajeruhi (Chemical) za (Kiburi) katika Akili yako, Na Ufalme wako wa (Kiburi)ukiguswa kidogo tu hata na mtoto mdogo jiangalie unakuaje, ukikataliwa na mwanamke jiangalie unakuaje, ukinyimwa cheo tizama unafanyaje, ukigombana kitu kidogo angalia huzungumzi milele pengine na ndugu zako.
Sasa nini kimetokezea umeikera ile (Energy) yenye kukupa huruma na upole na kuipeleka kwenye Akili kwa njia ya kasi ambapo ndio inazaa Hamaki, unafanya mambo ukiwa umelala usingizi, inakwenda kukaa (Energy) hiyo kwenye Akili yako na kila mara huwa inakukumbusha ulivyofanyiwa, hapo tena unaondoka na visasi, unaondoka na chuki za uharibifu hupumziki na wewe mpaka ulipize japo kwa siri kwa lile tendo alofanya fulani siku ile, utakwenda kutafuta ushirikina, utatuma watu ili wamdhuru, utapigana vita, utapoteza maisha ya watu kwa kitu kimoja, au utaanza kutapakaza habari zisizo za kweli ambazo zinaleta madhara kwa muhusika, hayo yote unayafanya kutokana na Hamaki zako,na ukienda safari hiyo unasahau kabisa kuwa kuna Mollah wako, unafanya hasira za kudumu hali yakua ungesubiri kidogo au uka kaa chini ile (Energy)irudi sehemu yake badala ya kukupeleka kwenye uharibifu ingekupeleka Peponi, kutokana na (Energy) hiyo hiyo zinazaliwa huruma za mapenzi na upole, lakini ukiifata wakati imekwenda kichwani hiyo ndio inakua sababu ya uharibifu na kukukosesha Pepo.
Jambo la Tatu Kupenda Mali.
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
"Na Mnapenda Mali Mapenzi mengi"(Makubwa)
Mnapenda majumba, Mnapenda magari, Mnapenda anasa za dunia, Mnapenda viumbe wenzenu Na Mali zenu hususan Pesa, zinakushughulisha kwa mapenzi makubwa, unasahau kabisa kama umeumbwa, unasahau kabisa kama unatakiwa ufanye Ibada, unatakiwa ufanye wema na Ihsan, unasahau kama mauti yanakunyanganya kila kitu na kukuacha mweupe, nini unafanya, unahesabu mali na kushughulika na watoto, unanyanganya huku na kule, uko tayari wende motoni ili wengine wastarehe na kufurahi kwa chumo lako, jiulize wewe unapata faida gani kwa shughuli hizo.
Angalia vipi mipango ya kazi na shopping ilivokuzonga, Fulani atavaa nini, leo tutakula nini, nani kenda nani karudi, harusi ya fulani iko lini, pesa ngapi zimetumika, kesho nani anacheza mechi ya mpira, kipindi changu cha Tv kinaanza saa ngapi, (Wassup)mbona sijapata (Msg) hivi ndivo tabia zetu za kila siku zenye kutusahaulisha mambo ambayo Mollah wetu katuamrisha ambayo ni ya kumkumbuka yeye na kufanya Ibada. Ukiangalia Mambo hayo yote Matatu ni yanokupelekea nje mja wewe, Maskini umekaa dirishani unashughulika na mambo ya Nje wakati huku ndani ya kifua chako, wamejificha (Hurulain)ndani kifuani kwako imejificha (Furaha ya Imani na Huruma na mapenzi) na humo ndani ya kifua chako kumejificha (Hazina) kubwa lakini wapi,, unashughulika na mambo ya nje kupita kiasi mpaka yanakua sababu ya adhabu yako, yanakutesa hapa duniani na unashindwa kujiuliza vipi itakua hali yako huko Akhera uendako. Basi Mja Unatakiwa Ujiulize hivyo uko tayari hapa Ulimwenguni uteseke na huko Uendako pia ukateseke, uamuzi unao mwenyewe, na kama umefahamu anza sasa ili usiikose Pepo ya Mollah wako,na kumbuka hayo yote unayafanya upate raha na furaha, Na Mollah wako kakwambia ukifanya Ibada, utayapata hayo yote na zaidi katika Ufalme wake wa Milele.
Jambo la pili nii hizi Hamaki tulonazo.
Sasa tunaingia kwenye Sumu ya maangamizi ambayo kama utakunywa sumu hii basi wewe kwa hiyari yako umejiharamishia Pepo. Hamaki ni madhara makubwa kama utaitizama kwa undani, magonvi yote yanaletwa na hamaki, chuki zote zinatokana na hamaki, Hebu tuliangalie tendo hili la hamaki mwanzo wake wapi.
Hamaki ni tendo linalotokea ndani ya mwili wako ambalo ni (Energy)maalum inayoripuka kutokana na kitendo cha nje kilichofanywa na Mtu mwengine, Nini kafanya? kajeruhi (Chemical) za (Kiburi) katika Akili yako, Na Ufalme wako wa (Kiburi)ukiguswa kidogo tu hata na mtoto mdogo jiangalie unakuaje, ukikataliwa na mwanamke jiangalie unakuaje, ukinyimwa cheo tizama unafanyaje, ukigombana kitu kidogo angalia huzungumzi milele pengine na ndugu zako.
Sasa nini kimetokezea umeikera ile (Energy) yenye kukupa huruma na upole na kuipeleka kwenye Akili kwa njia ya kasi ambapo ndio inazaa Hamaki, unafanya mambo ukiwa umelala usingizi, inakwenda kukaa (Energy) hiyo kwenye Akili yako na kila mara huwa inakukumbusha ulivyofanyiwa, hapo tena unaondoka na visasi, unaondoka na chuki za uharibifu hupumziki na wewe mpaka ulipize japo kwa siri kwa lile tendo alofanya fulani siku ile, utakwenda kutafuta ushirikina, utatuma watu ili wamdhuru, utapigana vita, utapoteza maisha ya watu kwa kitu kimoja, au utaanza kutapakaza habari zisizo za kweli ambazo zinaleta madhara kwa muhusika, hayo yote unayafanya kutokana na Hamaki zako,na ukienda safari hiyo unasahau kabisa kuwa kuna Mollah wako, unafanya hasira za kudumu hali yakua ungesubiri kidogo au uka kaa chini ile (Energy)irudi sehemu yake badala ya kukupeleka kwenye uharibifu ingekupeleka Peponi, kutokana na (Energy) hiyo hiyo zinazaliwa huruma za mapenzi na upole, lakini ukiifata wakati imekwenda kichwani hiyo ndio inakua sababu ya uharibifu na kukukosesha Pepo.
Jambo la Tatu Kupenda Mali.
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبًّ۬ا جَمًّ۬ا
"Na Mnapenda Mali Mapenzi mengi"(Makubwa)
Mnapenda majumba, Mnapenda magari, Mnapenda anasa za dunia, Mnapenda viumbe wenzenu Na Mali zenu hususan Pesa, zinakushughulisha kwa mapenzi makubwa, unasahau kabisa kama umeumbwa, unasahau kabisa kama unatakiwa ufanye Ibada, unatakiwa ufanye wema na Ihsan, unasahau kama mauti yanakunyanganya kila kitu na kukuacha mweupe, nini unafanya, unahesabu mali na kushughulika na watoto, unanyanganya huku na kule, uko tayari wende motoni ili wengine wastarehe na kufurahi kwa chumo lako, jiulize wewe unapata faida gani kwa shughuli hizo.
Angalia vipi mipango ya kazi na shopping ilivokuzonga, Fulani atavaa nini, leo tutakula nini, nani kenda nani karudi, harusi ya fulani iko lini, pesa ngapi zimetumika, kesho nani anacheza mechi ya mpira, kipindi changu cha Tv kinaanza saa ngapi, (Wassup)mbona sijapata (Msg) hivi ndivo tabia zetu za kila siku zenye kutusahaulisha mambo ambayo Mollah wetu katuamrisha ambayo ni ya kumkumbuka yeye na kufanya Ibada. Ukiangalia Mambo hayo yote Matatu ni yanokupelekea nje mja wewe, Maskini umekaa dirishani unashughulika na mambo ya Nje wakati huku ndani ya kifua chako, wamejificha (Hurulain)ndani kifuani kwako imejificha (Furaha ya Imani na Huruma na mapenzi) na humo ndani ya kifua chako kumejificha (Hazina) kubwa lakini wapi,, unashughulika na mambo ya nje kupita kiasi mpaka yanakua sababu ya adhabu yako, yanakutesa hapa duniani na unashindwa kujiuliza vipi itakua hali yako huko Akhera uendako. Basi Mja Unatakiwa Ujiulize hivyo uko tayari hapa Ulimwenguni uteseke na huko Uendako pia ukateseke, uamuzi unao mwenyewe, na kama umefahamu anza sasa ili usiikose Pepo ya Mollah wako,na kumbuka hayo yote unayafanya upate raha na furaha, Na Mollah wako kakwambia ukifanya Ibada, utayapata hayo yote na zaidi katika Ufalme wake wa Milele.
Sunday, November 16, 2014
URADI WA DHIKR YA (KUMTAJA MOLLAH) PART 1
Asalaam Aleiykum
Kukumbuka kuko kwa aina mbili, aina ya kwanza ya kukumbuka ni kwa njia ya kuona, na aina ya pili ni huko kusikia au kutaja ambacho ni kitendo kimoja kisichokua na tafauti na kuzungumza, kwani njia utaratibu ni uleule wa kusikia sauti ndio maana hata huyo mzungumzaji lazima atoe au apate (Gap) ya kuweza kulisikia analo zungumza au sivyo itakua tayari anasumbuliwa na matatizo kwenye Akili yake, (Ndio maana Mabingwa wa maradhi ya Akili wanatwambia tahadhari ukimuona mtu anazungumza sana bila ya kituo, jua huyo ana tatizo fulani na ukilichunguza utalijua).
Japokua kukumbuka ni jambo moja lakini hili la kutaja lina kazi maalum ambayo ndio msingi mzima wa darsa yetu ya leo ya (Kumtaja Allah).
Kabla ya kuanza na ufafanuzi huo napenda nikumbushe kitu kwa wale ambao kwa njia ya kusikia tu wanayapinga mambo bila ya kupata ithbati ya jambo hilo, bila ya kusoma au kufanya uchunguzi unasimama na kuharamisha kitu ambacho hufahamu undani wake, midamu umesikia Fulani kasema jambo hilo halifai na wewe unasimama kidete kulipinga, usifanye hivyo na wewe kwanza lipatie yakini ya kuto kufaa kwake, usisimame ukapinga na kukanusha kitu usichokua na uhakika nacho.
Kuna kisa kimoja itabidi mnipe nafasi nikieleze ili uwe mfano kwa watozingatia, Kuna kipindi katika Kisiwa cha (Zanzibar) walikuja (Wajapan) kwa ajili ya kujenga Barabara na wakatangaza wanataka wafanyakazi, wakenda vijana wenzangu na walipofika wakaambiwa kila mmoja aandike jina lake, walipokwisha andika yule (Mjapan) akaanza kuita yale majina akaita kama watu kumi yakabakia majina mawili "Na watu wawili tu ndio walobakia""Akaita (Sidilia Adalasi)kimya, akaita tena nani (Sidilia Adalasi)kimya akaendelea kuita lile jina lengine akabaki kijana mmoja kamuuliza wewe jina yako nani, yule kijana akajibu mimi naitwa (Said Bin Abdullah)akampa peni hebu andika jina lako, yule kijana akaandika (Sidilia Adalasi)"Maskini ikawa peke yake (Said Bin Abdullah) ndio alokosa kazi, Basi na wewe (Please)usianze kusimama ukawa unapinga mambo au kukataa Uradi, ukawa unawacheka wale wenye kudumisha utajo huu tukikupa kalamu uandike kumbe na wewe (Sidilia Adalasi) kasome nenda (Deep) jifunze ukisha kujua na kufahamu ndio njoo utuambie sasa nimegundua Uradi haufai.
Pia nataka uelewe kufahamu na kujua ni vitu viwili tafauti, kujua kunatokana na (Experience) na kufahamu kunatokana na hekima(Wisdom)ambayo anakupa Mollah wako, sasa kitizame kisa hichi kilichotokea kwenye kijiji fulani kwenye zama hizo za zamani, "Kwa Bahati katika kijiji kile alikuwepo Mtu mmoja tu ambaye kafundishwa kusoma, ikawa Barua za kijiji kizima anasoma yeye" yatizame mabega yake yakoje yalivyo beba kiburi ya kujiona kumbe peke yake ndie anayejua kusoma""Ikatokea siku moja Mama mmoja akamfata anataka aandikiwe Barua, Akamjibu Mguu unauma, yule Bibi akenda akarudi siku ya pili na kujibiwa tena mguu unauma, akasema yule Bibi leo siondoki mpaka unambie Mguu umehusiana nini na kuandika, akamjibu unajua kile kijiji iendako barua hii hakuna anoweza kusoma (Herufi)zangu mpaka nende mwenyewe" na siri kubwa kumbe alikua hajui kuandika, kwa hiyo kazi yake kuhifadhi yale maneno halafu ndio aende kijiji cha pili na kumwambia huyo alokusudiwa hiyo barua, na kijiji kikiwa mbali ndio lazima mguu utakuuma(umefahamu).
Endelea part 2
Kukumbuka kuko kwa aina mbili, aina ya kwanza ya kukumbuka ni kwa njia ya kuona, na aina ya pili ni huko kusikia au kutaja ambacho ni kitendo kimoja kisichokua na tafauti na kuzungumza, kwani njia utaratibu ni uleule wa kusikia sauti ndio maana hata huyo mzungumzaji lazima atoe au apate (Gap) ya kuweza kulisikia analo zungumza au sivyo itakua tayari anasumbuliwa na matatizo kwenye Akili yake, (Ndio maana Mabingwa wa maradhi ya Akili wanatwambia tahadhari ukimuona mtu anazungumza sana bila ya kituo, jua huyo ana tatizo fulani na ukilichunguza utalijua).
Japokua kukumbuka ni jambo moja lakini hili la kutaja lina kazi maalum ambayo ndio msingi mzima wa darsa yetu ya leo ya (Kumtaja Allah).
Kabla ya kuanza na ufafanuzi huo napenda nikumbushe kitu kwa wale ambao kwa njia ya kusikia tu wanayapinga mambo bila ya kupata ithbati ya jambo hilo, bila ya kusoma au kufanya uchunguzi unasimama na kuharamisha kitu ambacho hufahamu undani wake, midamu umesikia Fulani kasema jambo hilo halifai na wewe unasimama kidete kulipinga, usifanye hivyo na wewe kwanza lipatie yakini ya kuto kufaa kwake, usisimame ukapinga na kukanusha kitu usichokua na uhakika nacho.
Kuna kisa kimoja itabidi mnipe nafasi nikieleze ili uwe mfano kwa watozingatia, Kuna kipindi katika Kisiwa cha (Zanzibar) walikuja (Wajapan) kwa ajili ya kujenga Barabara na wakatangaza wanataka wafanyakazi, wakenda vijana wenzangu na walipofika wakaambiwa kila mmoja aandike jina lake, walipokwisha andika yule (Mjapan) akaanza kuita yale majina akaita kama watu kumi yakabakia majina mawili "Na watu wawili tu ndio walobakia""Akaita (Sidilia Adalasi)kimya, akaita tena nani (Sidilia Adalasi)kimya akaendelea kuita lile jina lengine akabaki kijana mmoja kamuuliza wewe jina yako nani, yule kijana akajibu mimi naitwa (Said Bin Abdullah)akampa peni hebu andika jina lako, yule kijana akaandika (Sidilia Adalasi)"Maskini ikawa peke yake (Said Bin Abdullah) ndio alokosa kazi, Basi na wewe (Please)usianze kusimama ukawa unapinga mambo au kukataa Uradi, ukawa unawacheka wale wenye kudumisha utajo huu tukikupa kalamu uandike kumbe na wewe (Sidilia Adalasi) kasome nenda (Deep) jifunze ukisha kujua na kufahamu ndio njoo utuambie sasa nimegundua Uradi haufai.
Pia nataka uelewe kufahamu na kujua ni vitu viwili tafauti, kujua kunatokana na (Experience) na kufahamu kunatokana na hekima(Wisdom)ambayo anakupa Mollah wako, sasa kitizame kisa hichi kilichotokea kwenye kijiji fulani kwenye zama hizo za zamani, "Kwa Bahati katika kijiji kile alikuwepo Mtu mmoja tu ambaye kafundishwa kusoma, ikawa Barua za kijiji kizima anasoma yeye" yatizame mabega yake yakoje yalivyo beba kiburi ya kujiona kumbe peke yake ndie anayejua kusoma""Ikatokea siku moja Mama mmoja akamfata anataka aandikiwe Barua, Akamjibu Mguu unauma, yule Bibi akenda akarudi siku ya pili na kujibiwa tena mguu unauma, akasema yule Bibi leo siondoki mpaka unambie Mguu umehusiana nini na kuandika, akamjibu unajua kile kijiji iendako barua hii hakuna anoweza kusoma (Herufi)zangu mpaka nende mwenyewe" na siri kubwa kumbe alikua hajui kuandika, kwa hiyo kazi yake kuhifadhi yale maneno halafu ndio aende kijiji cha pili na kumwambia huyo alokusudiwa hiyo barua, na kijiji kikiwa mbali ndio lazima mguu utakuuma(umefahamu).
Endelea part 2
URADI WA DHIKR YA (KUMTAJA MOLLAH) PART 2
Asalaam Aleiykum
Siri yenyewe yule Bwana alikua hajui kuandika ila yeye anajua kusoma, basi na wewe nenda kajifundishe elimu zote, elimu ni bahari ambazo kwenye Ulimwengu huu zipo tano,(Indian ocean, Pacific, Nk)kwa hiyo koga zote ili tukija kukuuliza usitwambie Mguu unakuuma, Na mwisho Usije kumlaumu(Doctor) wa Miwani kwa kuwa kakwambia ukipima miwani utaweza kusoma na kuandika, jilaumu mwenyewe kwanini hukujifunza kusoma na kuandika, ukimaliza hapo na wewe utakua na Mamlaka ya kusema (Dhikiri Haifai).
Sasa Tunaanza Darsa yetu kwa kujiuliza nini (Dhikiri)?ya kumtaja Mollah.
Wacha nikupe Dawa hii ambayo yaweza kukuponesha maradhi mengi na kukufanya Mja mwenye Afya nzuri kabisa, Kama nilivyosema mwanzoni Dhikiri zipo za aina mbili zenye kuashiria kitu kimoja, ile ya aina ya kwanza wewe imekushinda, ile ya kumkumbuka Mollah wako kwa kuona Nyota na Mwezi, kwa kuangalia Jua na Mbingu, kwa Kutizama Miti na Wanyama hayo yote haya kukumbushi Mollah wako, Na unaijua Sababu kubwa mpaka yakajiri hayo?. Sababu Kichwa kimejaa(Gossip)Kichwa kimejaa Siasa na Biashara, kichwa kina mambo mengi (Cinema)zimo humo, Utajiri umo humo, Umaskini umo humo, hasira na magonvi yote yamejaa kwenye kichwa hicho, wanawake na wanaume wote umewarekodi wewe, kila kitu Mja wewe unakihifadhi katika kichwa hicho, vipi leo unaweza kuwa na nafasi ya kumkumbuka Mollah wako.
Ukijiangalia Mja wewe kila baada ya sekunde chache Fikra za kila aina zinakujia kichwani humo, mara mipira mara madeni, mara nyimbo na mikasa ya kila aina, na kwa hali hiyo hakuna kabisa nafasi ya kumkumbuka Mollah wako.
Sasa nini Kifanyike?
Ndio Wale walotangulia wenye Hekima wakatafuta njia nyengine ya kumkumbuka Mollah wao kwa kuhama kutoka Juu kwenye Akili na kushuka chini kwenye Moyo. Na kwenye Moyo hakuna lugha nyengine inayofahamika isipokua utajo wa Mollah wako, huo ndio (Uradi), hiyo ndio dawa pekee ambayo ntakupa utumie kutwa mara zote. Sio ule Uradi wenu mnosoma wiki mara moja ile ni dua Uradi ni huu wa kudumisha kwa njia ya kurejea utajo wa Mollah wako, chukua dawa hii ya kumsabahi Mollah wako kwa majina yake yote 99.
Mimi nimekuchagulia hili la (Laa illah illah Allah)lidumishe ndani yake kuna siri kubwa, kuna mambo makubwa. Endelea part 3
Siri yenyewe yule Bwana alikua hajui kuandika ila yeye anajua kusoma, basi na wewe nenda kajifundishe elimu zote, elimu ni bahari ambazo kwenye Ulimwengu huu zipo tano,(Indian ocean, Pacific, Nk)kwa hiyo koga zote ili tukija kukuuliza usitwambie Mguu unakuuma, Na mwisho Usije kumlaumu(Doctor) wa Miwani kwa kuwa kakwambia ukipima miwani utaweza kusoma na kuandika, jilaumu mwenyewe kwanini hukujifunza kusoma na kuandika, ukimaliza hapo na wewe utakua na Mamlaka ya kusema (Dhikiri Haifai).
Sasa Tunaanza Darsa yetu kwa kujiuliza nini (Dhikiri)?ya kumtaja Mollah.
Wacha nikupe Dawa hii ambayo yaweza kukuponesha maradhi mengi na kukufanya Mja mwenye Afya nzuri kabisa, Kama nilivyosema mwanzoni Dhikiri zipo za aina mbili zenye kuashiria kitu kimoja, ile ya aina ya kwanza wewe imekushinda, ile ya kumkumbuka Mollah wako kwa kuona Nyota na Mwezi, kwa kuangalia Jua na Mbingu, kwa Kutizama Miti na Wanyama hayo yote haya kukumbushi Mollah wako, Na unaijua Sababu kubwa mpaka yakajiri hayo?. Sababu Kichwa kimejaa(Gossip)Kichwa kimejaa Siasa na Biashara, kichwa kina mambo mengi (Cinema)zimo humo, Utajiri umo humo, Umaskini umo humo, hasira na magonvi yote yamejaa kwenye kichwa hicho, wanawake na wanaume wote umewarekodi wewe, kila kitu Mja wewe unakihifadhi katika kichwa hicho, vipi leo unaweza kuwa na nafasi ya kumkumbuka Mollah wako.
Ukijiangalia Mja wewe kila baada ya sekunde chache Fikra za kila aina zinakujia kichwani humo, mara mipira mara madeni, mara nyimbo na mikasa ya kila aina, na kwa hali hiyo hakuna kabisa nafasi ya kumkumbuka Mollah wako.
Sasa nini Kifanyike?
Ndio Wale walotangulia wenye Hekima wakatafuta njia nyengine ya kumkumbuka Mollah wao kwa kuhama kutoka Juu kwenye Akili na kushuka chini kwenye Moyo. Na kwenye Moyo hakuna lugha nyengine inayofahamika isipokua utajo wa Mollah wako, huo ndio (Uradi), hiyo ndio dawa pekee ambayo ntakupa utumie kutwa mara zote. Sio ule Uradi wenu mnosoma wiki mara moja ile ni dua Uradi ni huu wa kudumisha kwa njia ya kurejea utajo wa Mollah wako, chukua dawa hii ya kumsabahi Mollah wako kwa majina yake yote 99.
Mimi nimekuchagulia hili la (Laa illah illah Allah)lidumishe ndani yake kuna siri kubwa, kuna mambo makubwa. Endelea part 3
URADI WA DHIKR YA (KUMTAJA MOLLAH) PART 3
Asalaam Aleiykum
Nini Uradi?
Uradi ni nyenzo au (Method) ya kuinyanganya (Mind)Akili uwezo wake wa kukutawala kama ifanyavyo hivi sasa, Ndio walo wema walotangulia wakafanya njia hii ya kuidunda(Kuipiga)Akili kwa Majina ya Mwenye enzi Mungu, wakafanya hivyo kwa kutumia mambo matatu (Body, Mind, and Soul)kwa hiyo msipite mkawakejeli(Kuwafanyia mzaha) wazee kwa kushika (Tasbih mikononi)Tasbih maana yake ni (Body) inakumbuka na (Mind)kazi yake inahesabu na (Soul)Roho inataja na hakuna maana nyengine isipokua ndio hiyo ya Uradi.
Na yakijumuika na kukusanyika pamoja mambo hayo matatu katika huo Uradi wa Kumtaja Mollah kwa njia ya marejeo (Repitition)utaanza kuona zile fikra za Maimuna au Muumin, au za mpira na nyimbo zinaanza kutoweka kidogo kidogo mpaka unafikia wakati hakuna tena mawazo au fikra za kipuuzi katika (Mind)Akili yako ila linabaki jina la Mollah wako.
Na ukifikia hatua hiyo inakua wewe sasa uko tayari kwenda (Beyond name to the Nameless)Utakuwa wewe tayari ushafika kwa wale wenye kutajwa katika sura ya (Al-Imran aya ya 191)
"ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَـٰمً۬ا وَقُعُودً۬ا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَڪَّرُونَ فِى خَلۡقِ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَـٰذَا بَـٰطِلاً۬ سُبۡحَـٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ"
Ambao humkumbuka Mwenye enzi Mungu wakiwa wima(Wamesimama)na wakikaa na wakilala, na hufikiri Umbo la Mbingu na Ardhi(wakasema)Mollah wetu hukuviumba hivi bure, Utukufu ni wako, Basi tuepushe na adhabu ya Moto.
Na wewe sasa utakua unamtaja Mollah wako mpaka ukiwa usingizini, akiwa kuna Mtu analala na wewe basi anaweza kusikia kukoroma kwako kunataja (Laa illah Ilah Allah).
Na hizo ndizo faida za Uradi umeshindwa kwenye akili sasa shuka moyoni uwe kama hao walotajwa katika hiyo aya, na utaanza kuona kwa mara ya mwanzo moyo unashukiwa na mapenzi, wakati wote utakua furahani ukiwa sokoni au barazani wewe utakua unamtaja Mollah wako, jaribu japo wiki uone faida yake, na ukijaa mapenzi ya Mollah wako ndio unapanda kwenye daraja nyengine ya Imani unaingia katika kundi la wale walotajwa katika sura ya (Israa aya ya 107)
"قُلۡ ءَامِنُواْ بِهِۦۤ أَوۡ لَا تُؤۡمِنُوٓاْۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ مِن قَبۡلِهِۦۤ إِذَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡہِمۡ يَخِرُّونَ لِلۡأَذۡقَانِ سُجَّدً۬ا "
Sema Iamini au Msiamini(Hiyo Quraan) Hakika wale walopewa Elimu (Zamani)kabla hii(ya Quraan)wanaposomewa(aya zetu)huanguka kifudi fudi wanasujdu.
Huo ndio Uradi , hivyo ndio ukishiba Jina la Mwenye enzi Mungu utakavyokua, japo kwa sasa utaona haya kwa kudhani watu watasemaje lakini utasujudu mayoni kama vile afanyavyo mgonjwa, Huo ndio Uradi udumishe ukupele (Beyond) hiyo ndio itakua dawa yako ya kuondokewa na Dhiki moyoni mwako na pia katika maisha yako. Ukitaka soma kwa sauti au kimya kimya kwenye moyo wako yote ni sawa. Sio Haramu wala hukosei.
Nini Uradi?
Uradi ni nyenzo au (Method) ya kuinyanganya (Mind)Akili uwezo wake wa kukutawala kama ifanyavyo hivi sasa, Ndio walo wema walotangulia wakafanya njia hii ya kuidunda(Kuipiga)Akili kwa Majina ya Mwenye enzi Mungu, wakafanya hivyo kwa kutumia mambo matatu (Body, Mind, and Soul)kwa hiyo msipite mkawakejeli(Kuwafanyia mzaha) wazee kwa kushika (Tasbih mikononi)Tasbih maana yake ni (Body) inakumbuka na (Mind)kazi yake inahesabu na (Soul)Roho inataja na hakuna maana nyengine isipokua ndio hiyo ya Uradi.
Na yakijumuika na kukusanyika pamoja mambo hayo matatu katika huo Uradi wa Kumtaja Mollah kwa njia ya marejeo (Repitition)utaanza kuona zile fikra za Maimuna au Muumin, au za mpira na nyimbo zinaanza kutoweka kidogo kidogo mpaka unafikia wakati hakuna tena mawazo au fikra za kipuuzi katika (Mind)Akili yako ila linabaki jina la Mollah wako.
Na ukifikia hatua hiyo inakua wewe sasa uko tayari kwenda (Beyond name to the Nameless)Utakuwa wewe tayari ushafika kwa wale wenye kutajwa katika sura ya (Al-Imran aya ya 191)
"ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَـٰمً۬ا وَقُعُودً۬ا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَڪَّرُونَ فِى خَلۡقِ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَـٰذَا بَـٰطِلاً۬ سُبۡحَـٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ"
Ambao humkumbuka Mwenye enzi Mungu wakiwa wima(Wamesimama)na wakikaa na wakilala, na hufikiri Umbo la Mbingu na Ardhi(wakasema)Mollah wetu hukuviumba hivi bure, Utukufu ni wako, Basi tuepushe na adhabu ya Moto.
Na wewe sasa utakua unamtaja Mollah wako mpaka ukiwa usingizini, akiwa kuna Mtu analala na wewe basi anaweza kusikia kukoroma kwako kunataja (Laa illah Ilah Allah).
Na hizo ndizo faida za Uradi umeshindwa kwenye akili sasa shuka moyoni uwe kama hao walotajwa katika hiyo aya, na utaanza kuona kwa mara ya mwanzo moyo unashukiwa na mapenzi, wakati wote utakua furahani ukiwa sokoni au barazani wewe utakua unamtaja Mollah wako, jaribu japo wiki uone faida yake, na ukijaa mapenzi ya Mollah wako ndio unapanda kwenye daraja nyengine ya Imani unaingia katika kundi la wale walotajwa katika sura ya (Israa aya ya 107)
"قُلۡ ءَامِنُواْ بِهِۦۤ أَوۡ لَا تُؤۡمِنُوٓاْۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ مِن قَبۡلِهِۦۤ إِذَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡہِمۡ يَخِرُّونَ لِلۡأَذۡقَانِ سُجَّدً۬ا "
Sema Iamini au Msiamini(Hiyo Quraan) Hakika wale walopewa Elimu (Zamani)kabla hii(ya Quraan)wanaposomewa(aya zetu)huanguka kifudi fudi wanasujdu.
Huo ndio Uradi , hivyo ndio ukishiba Jina la Mwenye enzi Mungu utakavyokua, japo kwa sasa utaona haya kwa kudhani watu watasemaje lakini utasujudu mayoni kama vile afanyavyo mgonjwa, Huo ndio Uradi udumishe ukupele (Beyond) hiyo ndio itakua dawa yako ya kuondokewa na Dhiki moyoni mwako na pia katika maisha yako. Ukitaka soma kwa sauti au kimya kimya kwenye moyo wako yote ni sawa. Sio Haramu wala hukosei.
Sunday, November 9, 2014
MUANGAZA WA ROHO PART 1
Asalaam Aleiykum
Leo nakuomba safiri na mimi ili tuishi katika aya ya 85 ya sura ya (Israa) tupate kuhisi Muangaza wa (Roho)tujue ikoje taa yake.
وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلرُّوحِۖ قُلِ ٱلرُّوحُ مِنۡ أَمۡرِ رَبِّى وَمَآ أُوتِيتُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِ إِلَّا قَلِيلاً۬
Na Wanakuuliza habari ya Roho, Sema Roho ni Jambo lilohusika na (Amri)ya Mollah wangu. Na nyinyi hamkupewa katika elimu isipokua kidogo (Hivi).
Kumbuka kila mmoja wetu anauliza swali hili, ikiwa haulizi kwa mtu anajiuliza yeye mwenyewe, nini hasa hii Roho? kwanini likaja swali hili, lazima (Deep) katika nafsi zetu kuna Kiu(Thirsty) ya kutaka kujua nini hii Roho? kweli inaishi maisha, na kila mtu anauliza swali hili kutaka kujitosheleza kwa kuamini hakuna mwisho ila kuna uwepo wa kudumu milele, hamu kubwa na shauku Mwanaadamu imemkamata kulijua hili, Na kila mara japo ukilisukuma swali hili lisirudi ndio kwanza linazidi kukuandama.
Sasa ufanye nini? ndio kila mara mtu inabidi aende kuchungulia katika kisima hichi cha fikra ili apate kuona kama kuna maji apate kukata kiu yake ya kuijua Roho. Lakini kawaida ya kisima inataka ufanye kazi kupata kuyaona hayo maji kama yapo, sababu kisima ni kikubwa sana, hata ukipata huo Muangaza ukayaona maji inabidi ufanye jitihada ya kuyachota maji hayo.
"Wanakuuliza nini Habari ya Roho"
Napenda utambue waulizaji wa habari hizi si watoto au vijana ni mara chache sana wenye umri wa rika hilo kuulizia habari kama hizi,Waulizaji wakubwa wa habari hizi ni wale walofikia Umuri wa makamo au rika ya uzee. Pia napenda kukufahamisha waulizaji wako wengi lakini wafatiliaji ni wachache sana, Na sababu kubwa safari hii ya uchunguzi wa kujua nini Roho inatisha, ni safari mja unatakiwa uende peke yako, huna mshirika, na hivi sasa wakati ndio umefika, pengine watoto wameshakua na kuondoka nyumbani, Majumba umeshajenga yamemalizika, Mapesa (Bank)yamefurika, huna tena la kufanya, hakuna la zaidi, sasa swali hili ndio linakuja kila mara nini Roho?.
Na ukiona swali hili linakujia mara kwa mara basi elewa bila shaka limegusana na Mauti(Sio kwamba unakufa lakini ni njia moja ya Ulimwengu huu kukupa habari za hiyo siku ya siku). kwa hiyo ukiwa katika wale walo wengi ambao wanaogopa swali hili hapo tena utaanza kutafuta vitu vya kukusahaulisha, utaanza kukimbilia senema(Cinema)mara kwenye ma(Disco)hukosekani, kwenye Taarab wewe unakua wa mwanzo kuingia na wa mwisho kutoka, na kila sehemu inayokufanya wewe usahau habari hii wewe ndio unakua (Kinara wake)ili upate nafasi ya kusahau kuijua kadhia hii ya Roho.
Endelea part 2
Leo nakuomba safiri na mimi ili tuishi katika aya ya 85 ya sura ya (Israa) tupate kuhisi Muangaza wa (Roho)tujue ikoje taa yake.
وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلرُّوحِۖ قُلِ ٱلرُّوحُ مِنۡ أَمۡرِ رَبِّى وَمَآ أُوتِيتُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِ إِلَّا قَلِيلاً۬
Na Wanakuuliza habari ya Roho, Sema Roho ni Jambo lilohusika na (Amri)ya Mollah wangu. Na nyinyi hamkupewa katika elimu isipokua kidogo (Hivi).
Kumbuka kila mmoja wetu anauliza swali hili, ikiwa haulizi kwa mtu anajiuliza yeye mwenyewe, nini hasa hii Roho? kwanini likaja swali hili, lazima (Deep) katika nafsi zetu kuna Kiu(Thirsty) ya kutaka kujua nini hii Roho? kweli inaishi maisha, na kila mtu anauliza swali hili kutaka kujitosheleza kwa kuamini hakuna mwisho ila kuna uwepo wa kudumu milele, hamu kubwa na shauku Mwanaadamu imemkamata kulijua hili, Na kila mara japo ukilisukuma swali hili lisirudi ndio kwanza linazidi kukuandama.
Sasa ufanye nini? ndio kila mara mtu inabidi aende kuchungulia katika kisima hichi cha fikra ili apate kuona kama kuna maji apate kukata kiu yake ya kuijua Roho. Lakini kawaida ya kisima inataka ufanye kazi kupata kuyaona hayo maji kama yapo, sababu kisima ni kikubwa sana, hata ukipata huo Muangaza ukayaona maji inabidi ufanye jitihada ya kuyachota maji hayo.
"Wanakuuliza nini Habari ya Roho"
Napenda utambue waulizaji wa habari hizi si watoto au vijana ni mara chache sana wenye umri wa rika hilo kuulizia habari kama hizi,Waulizaji wakubwa wa habari hizi ni wale walofikia Umuri wa makamo au rika ya uzee. Pia napenda kukufahamisha waulizaji wako wengi lakini wafatiliaji ni wachache sana, Na sababu kubwa safari hii ya uchunguzi wa kujua nini Roho inatisha, ni safari mja unatakiwa uende peke yako, huna mshirika, na hivi sasa wakati ndio umefika, pengine watoto wameshakua na kuondoka nyumbani, Majumba umeshajenga yamemalizika, Mapesa (Bank)yamefurika, huna tena la kufanya, hakuna la zaidi, sasa swali hili ndio linakuja kila mara nini Roho?.
Na ukiona swali hili linakujia mara kwa mara basi elewa bila shaka limegusana na Mauti(Sio kwamba unakufa lakini ni njia moja ya Ulimwengu huu kukupa habari za hiyo siku ya siku). kwa hiyo ukiwa katika wale walo wengi ambao wanaogopa swali hili hapo tena utaanza kutafuta vitu vya kukusahaulisha, utaanza kukimbilia senema(Cinema)mara kwenye ma(Disco)hukosekani, kwenye Taarab wewe unakua wa mwanzo kuingia na wa mwisho kutoka, na kila sehemu inayokufanya wewe usahau habari hii wewe ndio unakua (Kinara wake)ili upate nafasi ya kusahau kuijua kadhia hii ya Roho.
Endelea part 2
MUANGAZA WA ROHO PART 2
Asalaam Aleiykum
Lakini ukiwa katika wale wachache ambao kwa Ushujaa wanalikabili swali hili la nini Roho?, Basi wewe ndio katika wale wanoanza ile Safari ndefu yenye kutisha, yenye miujiza na mambo ya ajabu, Safari yenyewe ni ngumu lakini inaendeka. Kinachotakiwa katika safari yako hii ni yakini katika moyo wako kuwa sasa nachupa nimeamua kutumbukia kisimani kitachonikuta sawa lakini lazima nijijue mimi nani.
Na mwanzo kabisa ukiamua kuchupa kuanza safari hii na kuuliza nini Roho?ina maana ushafanya (Tafauti)baina yako na huo Mwili(Body)zishakujia fikra kuwa wewe sio huu Mwili, kuna kitu chengine ambacho unataka ukijue, hapo tena ndio unaanza hiyo(Sipiritual journey)ambayo imeitwa safari ndefu.
"Wanakuuliza habari ya Roho sema(Waambie)" wala hakuna makosa mtu kutaka kujua nini Roho, cha muhimu kwanza kabisa uelewe kuwa hata hiyo (Body) Mwili wako si mali yako, ni zawadi uliyopewa nusu kutoka kwa Baba yako na nusu nyengine kutoka kwa Mama yako, halafu tena ndio unaendelezwa Mwili wako huo kwa njia ya chakula, sasa ukiwa huu mwili ni hicho chakula mimi nilobakia nisokua chakula mimi ni nani?, Nimetokea wapi, na wapi ninapo kwenda. Nini habari yangu mimi siku ile nitakapozimika,nini kinatokezea?.
"Wanakuuliza nini habari ya Roho Sema" uwaambie hakika ya hiyo Roho ni (Amri)ya Mollah wangu, ndio maana utaona mambo yote yenye kuhusiana na Roho unayakabili peke yako, umeshapata kujiuliza nani huyu Mke wangu au Mume wangu, nani hawa watoto wangu, wote hawa wametokea wapi, mbona naona sote sisi kama wageni tulokutana katika Ulimwengu huu, Jee hii ndio ile maana ya watoto zenu na mali zenu ni adui kwenu? unainza safari hii kwa unyenyekevu mkubwa kabisa, huku ukijua kumbe katika mambo ya Kiroho niko peke yangu, na kila kitu nitakikabili peke yangu, hayatonifaa mali wala watoto ila lazima nirudi kwa Mollah wangu nikiwa safi, sasa Nani huyu anaye Rudi?
"Wanakuuliza nini habari ya Roho Sema" Waambie hiyo Roho ni kwa ajili ya (Amri) ya Mwenye enzi Mungu, Neno Amri inafaa tulizingatie sana tafsiri ya neno hili, Watu wengi wanadhani au wanashindwa kutafautisha baina ya Amri na maagizo, Amri ni tendo lisilopingika wala kubadilika isipokua mpaka atake huyo Mwenye kutoa Amri Mwenye Enzi Mungu mwenye Ufalme wa Milele.
Hizi zenu mnazotoa nyinyi si Amri sababu amri haipingiki, hayo yenu ni maagizo ndio maana kuna wakati mtu anakwenda kinyume na kiongozi au bosi wake, kwa kuwa hayo ni maagizo hawana hakika nayo ndio sababu pakawekwa washauri kuwasaidia kupitisha hayo maagizo. Ukilizingatia vizuri hili neno Amri litakusaidia pakubwa katika safari yako hii ya kutafuta Muangaza wa Roho.
Waambie habari hii wala usiwafiche kuwa imehusiana na Mwenye enzi Mungu na yoyote yule Mwenye kutaka kuijua habari hii anarudi kwa Mollah wake, Na kurudi huku ndiko kunakujulisha ukajua kila kitu katika Ulimwengu huu kinatii hiyo Amri ya Mwenye enzi Mungu, Mpaka huo Mwili wako (Body)unatii Amri hiyo, Moyo unapiga kwa kutii amri hiyo, Ini linasafisha damu kwa amri hiyo, damu inasambazwa kwenye Mwili kutokana na amri hiyo ikitimizwa na hewa itokayo nje unayovuta bila ya tabu wala kuitaka au kuikataa, ni katika mazingira ya kuitii Amri itokayo kwa Mollah wako, Mwili unahisi njaa unakula chakula, ikisha kinasagwa kwa kutii Amri hiyo, ikisha mwili ukichoka unalala hayo yote sio wewe, sasa wewe ni kitu gani?
Endelea part 3
Lakini ukiwa katika wale wachache ambao kwa Ushujaa wanalikabili swali hili la nini Roho?, Basi wewe ndio katika wale wanoanza ile Safari ndefu yenye kutisha, yenye miujiza na mambo ya ajabu, Safari yenyewe ni ngumu lakini inaendeka. Kinachotakiwa katika safari yako hii ni yakini katika moyo wako kuwa sasa nachupa nimeamua kutumbukia kisimani kitachonikuta sawa lakini lazima nijijue mimi nani.
Na mwanzo kabisa ukiamua kuchupa kuanza safari hii na kuuliza nini Roho?ina maana ushafanya (Tafauti)baina yako na huo Mwili(Body)zishakujia fikra kuwa wewe sio huu Mwili, kuna kitu chengine ambacho unataka ukijue, hapo tena ndio unaanza hiyo(Sipiritual journey)ambayo imeitwa safari ndefu.
"Wanakuuliza habari ya Roho sema(Waambie)" wala hakuna makosa mtu kutaka kujua nini Roho, cha muhimu kwanza kabisa uelewe kuwa hata hiyo (Body) Mwili wako si mali yako, ni zawadi uliyopewa nusu kutoka kwa Baba yako na nusu nyengine kutoka kwa Mama yako, halafu tena ndio unaendelezwa Mwili wako huo kwa njia ya chakula, sasa ukiwa huu mwili ni hicho chakula mimi nilobakia nisokua chakula mimi ni nani?, Nimetokea wapi, na wapi ninapo kwenda. Nini habari yangu mimi siku ile nitakapozimika,nini kinatokezea?.
"Wanakuuliza nini habari ya Roho Sema" uwaambie hakika ya hiyo Roho ni (Amri)ya Mollah wangu, ndio maana utaona mambo yote yenye kuhusiana na Roho unayakabili peke yako, umeshapata kujiuliza nani huyu Mke wangu au Mume wangu, nani hawa watoto wangu, wote hawa wametokea wapi, mbona naona sote sisi kama wageni tulokutana katika Ulimwengu huu, Jee hii ndio ile maana ya watoto zenu na mali zenu ni adui kwenu? unainza safari hii kwa unyenyekevu mkubwa kabisa, huku ukijua kumbe katika mambo ya Kiroho niko peke yangu, na kila kitu nitakikabili peke yangu, hayatonifaa mali wala watoto ila lazima nirudi kwa Mollah wangu nikiwa safi, sasa Nani huyu anaye Rudi?
"Wanakuuliza nini habari ya Roho Sema" Waambie hiyo Roho ni kwa ajili ya (Amri) ya Mwenye enzi Mungu, Neno Amri inafaa tulizingatie sana tafsiri ya neno hili, Watu wengi wanadhani au wanashindwa kutafautisha baina ya Amri na maagizo, Amri ni tendo lisilopingika wala kubadilika isipokua mpaka atake huyo Mwenye kutoa Amri Mwenye Enzi Mungu mwenye Ufalme wa Milele.
Hizi zenu mnazotoa nyinyi si Amri sababu amri haipingiki, hayo yenu ni maagizo ndio maana kuna wakati mtu anakwenda kinyume na kiongozi au bosi wake, kwa kuwa hayo ni maagizo hawana hakika nayo ndio sababu pakawekwa washauri kuwasaidia kupitisha hayo maagizo. Ukilizingatia vizuri hili neno Amri litakusaidia pakubwa katika safari yako hii ya kutafuta Muangaza wa Roho.
Waambie habari hii wala usiwafiche kuwa imehusiana na Mwenye enzi Mungu na yoyote yule Mwenye kutaka kuijua habari hii anarudi kwa Mollah wake, Na kurudi huku ndiko kunakujulisha ukajua kila kitu katika Ulimwengu huu kinatii hiyo Amri ya Mwenye enzi Mungu, Mpaka huo Mwili wako (Body)unatii Amri hiyo, Moyo unapiga kwa kutii amri hiyo, Ini linasafisha damu kwa amri hiyo, damu inasambazwa kwenye Mwili kutokana na amri hiyo ikitimizwa na hewa itokayo nje unayovuta bila ya tabu wala kuitaka au kuikataa, ni katika mazingira ya kuitii Amri itokayo kwa Mollah wako, Mwili unahisi njaa unakula chakula, ikisha kinasagwa kwa kutii Amri hiyo, ikisha mwili ukichoka unalala hayo yote sio wewe, sasa wewe ni kitu gani?
Endelea part 3
MUANGAZA WA ROHO PART 3
Asalaam Aleiykum
Kuna kitu ambacho ni muhimu sana kukijua ndio maana unahimizwa kukumbuka mauti, kwanini ikawa Mauti kwa sababu Mauti yanachukua kila kitu isipokua kitu hicho ambayo ndio hiyo Roho,ndio hiyo wewe ambaye sasa hivi unaisoma habari hii, Na siri ya kukumbuka Mauti nikuwa kila ukikumbuka Mauti unapunguza dhanmbi, na dhanmbi zikipungua inakua rahisi kuijua Roho yako(قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّٮٰهَا)"Bila shaka Amefuzu aliyeitakasa(Roho yake) .
"Wanakuuliza habari ya Roho Sema"
Tutizame sasa hili neno Amri linatokea wapi, Neno Amri ni tafsiri ile ile ya Majaala, na tutizame hili neno la kujaaliwa ni Amri hii inayopitishwa na Mwenyewe Mwenye enzi Mungu kama alivyosema kwenye aya nyingi mimi nitazitumia mbili ili zipate kutufungua macho tuweze kuona Muangaza wa Roho.
وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَىۡءٍ حَىٍّۖ
"Na tukajaalia(Kufanya)kwa maji kila kitu kilicho Hai"
Kitu chochote kilicho hai kimefanywa kwa Maji, hapo itakuonesha vipi vyengine ambavyo vikiwa havipo hai vinavyokua, mtizame Maiti wa Binaadamu au Mnyama akisha kufa anakuaje dalili ya mwanzo anaanza kuoza na (source)ya maji inakatika katika mwili huo ndio maana tunamwita Maiti na ukimfufua utaona keshakauka,maji yamemalizika, kwa hiyo katika Ulimwengu huu tumeoneshwa vilivyo hai na vilivyokufa, kimoja kinategemea maji na chengine maji yashatoweka, chochote kile kisichotegemea maji kinakua Maiti, ile amri ya maji kuwepo kwenye kitu hicho imeshakatika, kumbuka vyote vinaishi ila kimoja katika uhai na chengine katika umauti, Na hiyo Roho yako inaishi katika sehemu hizo zote mbili,kwa hiyo kama huamini kufufuliwa zingatia sana habari hii nilokupa halafu uifanyie kazi. Katika daraja hilo la maisha ndipo ilipo Roho yako kwa amri ya Mwenye enzi Mungu.
"Wanakuuliza nini habari ya Roho sema" Na waambie kwa Amri hiyo hiyo ya kujaaliwa na nyinyi mnapewa vitu muhimu sana navyo ni sura ya As-Sajda aya ya 9.
ثُمَّ سَوَّٮٰهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِۦۖ وَجَعَلَ لَكُمُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَـٰرَ وَٱلۡأَفۡـِٔدَةَۚ قَلِيلاً۬ مَّا تَشۡڪُرُونَ
Kisha akamtengeneza(Kumuumba) na Akampulizia Roho yake, na akakupeni masikio na macho na nyoyo, ni kidogo tu shukurani yenu.
Baada ya kwisha kuumbwa ukapuliziwa Roho itokayo na yeye Mwenyewe Mwenye enzi Mungu, ndio maana nikasema safari ya kutaka kuijua Roho ni kurejea kwa Mollah wako, ndio maana nikasema ni safari ya miujiza na yenye kutisha, ikapulizwa hiyo Roho katika hiyo (Body)yako, kwa hiyo Roho inaishi katika mwili wako lakini haikamatani na mwili wako, ndio maana ukaona mwili unafanya kazi zake pasi kuingiliwa na Roho,Lakini Roho ndio yenye ku (Control)huo mwili kwa kuwa wewe ni Khalifa wa huo mwili na hii Ardhi, halafu ukapewa hii amri au Jaala ya kuona na kusikia, Ifikiri sana habari hii ya kuona na kusikia, ina mazingatio makubwa katika muangaza wa Roho, huu ni uwezo wa kutoka kwa Mollah wako ndio maana utaona wakati wa usingizi wako amri hii unaondoshewa kwenye (Deep sleep)ukirejea kwa Mollah wako kikamilifu, na wakati Mwengine unakua nayo amri hii ndio unaona hizo ndoto na kusikia sauti, Ni lazima upewe viwili hivi adhimu ili upate uhai kwa ukamilifu na kama huna viwili hivi bado Roho yako iko hai lakini imenyimwa amri hii(Jaala)ya Muumba wako, ukapewa na huo Moyo ili uweze kujua, kumbuka macho ni kuona, masikio ni kusikia, halafu ukapewa na huu Moyo ili uwe na uwezo wa kujua, kupenda, kufahamu na hekima ya kuweza kuijua Roho yako. Kwa sasa hivi huwezi kujua moyo ulokusudiwa hapa mpaka ukifika mbali katika hiyo safari yako ya (Sipiritual Journey) ndio utajua alaa kumbe moyo una kazi mbili, na hii ya pili ndio ilokusudiwa katika Muangaza wa Roho.
Wanakuuliza nini habari ya Roho sema, ni jambo lilohusiana na (Amri) ya Mollah wangu, Na wala hamkupewa elimu isipokua kidogo.
Hakukataa Mwenye enzi Mungu wala hakuzuia mtu kutaka kujua nini hiyo Roho,ili kasema Elimu mliyopewa ni chache(Kidogo) basi mtu na aitafute asaa anaweza kupewa elimu ya Roho akaijua na ukiijua Roho yako, utapata ufahamu vipi ukawa wewe Khalifa katika Ardhi hii, usisubiri mpaka siku ya kufa ndio ukaijua Roho yako, anza sasa hivi kwa kujitakasa na kuusafisha moyo wako utaipata elimu hiyo, kumbukuka imetolewa kidogo lakini haikuzuiliwa kutolewa, Elimu zinazidi kutolewa, tunaendelea kuvumbua mambo,, na sote siku ya kufa tunakutana na roho zetu kwa hiyo hakuna jambo la kuogopa ima usubiri siku ya kufa au anza sasa hivi, na ukianza sasa hivi basi unakwenda (Beyond death),hiyo ndio maana "Ya Ewe Mja wangu mwema Rejea kwangu ukiwa umeridhi na kuridhiwa"(Operation ya Mauti inaendelea wewe unaangalia, unajijua sina cha kuhofia, mimi Roho narejea kwa yule alonileta, na wala sina khofu tena ya Operation hii), lakini kwanza lazima usafishe machafu yako, omba maghfira kwa wingi ili uitakase Roho yako,ikiwa safi hapo utaona Muangaza wake, utaona Muujiza wake, fanya safari hii muhimu ya Muangaza wa Roho na ukipata Muangaza huu wewe ushafanikiwa, hukai tena ukalinda mali ya Ulimwengu huu, hakuna chochote kitakacho kudhuru na utakua karibu sana na Mollah wako na hiyo ndio maana ya, nasi tukaribu naye zaidi kuliko huo mshipa wake wa shingo
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنۡ حَبۡلِ ٱلۡوَرِيدِ.
Kuna kitu ambacho ni muhimu sana kukijua ndio maana unahimizwa kukumbuka mauti, kwanini ikawa Mauti kwa sababu Mauti yanachukua kila kitu isipokua kitu hicho ambayo ndio hiyo Roho,ndio hiyo wewe ambaye sasa hivi unaisoma habari hii, Na siri ya kukumbuka Mauti nikuwa kila ukikumbuka Mauti unapunguza dhanmbi, na dhanmbi zikipungua inakua rahisi kuijua Roho yako(قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّٮٰهَا)"Bila shaka Amefuzu aliyeitakasa(Roho yake) .
"Wanakuuliza habari ya Roho Sema"
Tutizame sasa hili neno Amri linatokea wapi, Neno Amri ni tafsiri ile ile ya Majaala, na tutizame hili neno la kujaaliwa ni Amri hii inayopitishwa na Mwenyewe Mwenye enzi Mungu kama alivyosema kwenye aya nyingi mimi nitazitumia mbili ili zipate kutufungua macho tuweze kuona Muangaza wa Roho.
وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَىۡءٍ حَىٍّۖ
"Na tukajaalia(Kufanya)kwa maji kila kitu kilicho Hai"
Kitu chochote kilicho hai kimefanywa kwa Maji, hapo itakuonesha vipi vyengine ambavyo vikiwa havipo hai vinavyokua, mtizame Maiti wa Binaadamu au Mnyama akisha kufa anakuaje dalili ya mwanzo anaanza kuoza na (source)ya maji inakatika katika mwili huo ndio maana tunamwita Maiti na ukimfufua utaona keshakauka,maji yamemalizika, kwa hiyo katika Ulimwengu huu tumeoneshwa vilivyo hai na vilivyokufa, kimoja kinategemea maji na chengine maji yashatoweka, chochote kile kisichotegemea maji kinakua Maiti, ile amri ya maji kuwepo kwenye kitu hicho imeshakatika, kumbuka vyote vinaishi ila kimoja katika uhai na chengine katika umauti, Na hiyo Roho yako inaishi katika sehemu hizo zote mbili,kwa hiyo kama huamini kufufuliwa zingatia sana habari hii nilokupa halafu uifanyie kazi. Katika daraja hilo la maisha ndipo ilipo Roho yako kwa amri ya Mwenye enzi Mungu.
"Wanakuuliza nini habari ya Roho sema" Na waambie kwa Amri hiyo hiyo ya kujaaliwa na nyinyi mnapewa vitu muhimu sana navyo ni sura ya As-Sajda aya ya 9.
ثُمَّ سَوَّٮٰهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِۦۖ وَجَعَلَ لَكُمُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَـٰرَ وَٱلۡأَفۡـِٔدَةَۚ قَلِيلاً۬ مَّا تَشۡڪُرُونَ
Kisha akamtengeneza(Kumuumba) na Akampulizia Roho yake, na akakupeni masikio na macho na nyoyo, ni kidogo tu shukurani yenu.
Baada ya kwisha kuumbwa ukapuliziwa Roho itokayo na yeye Mwenyewe Mwenye enzi Mungu, ndio maana nikasema safari ya kutaka kuijua Roho ni kurejea kwa Mollah wako, ndio maana nikasema ni safari ya miujiza na yenye kutisha, ikapulizwa hiyo Roho katika hiyo (Body)yako, kwa hiyo Roho inaishi katika mwili wako lakini haikamatani na mwili wako, ndio maana ukaona mwili unafanya kazi zake pasi kuingiliwa na Roho,Lakini Roho ndio yenye ku (Control)huo mwili kwa kuwa wewe ni Khalifa wa huo mwili na hii Ardhi, halafu ukapewa hii amri au Jaala ya kuona na kusikia, Ifikiri sana habari hii ya kuona na kusikia, ina mazingatio makubwa katika muangaza wa Roho, huu ni uwezo wa kutoka kwa Mollah wako ndio maana utaona wakati wa usingizi wako amri hii unaondoshewa kwenye (Deep sleep)ukirejea kwa Mollah wako kikamilifu, na wakati Mwengine unakua nayo amri hii ndio unaona hizo ndoto na kusikia sauti, Ni lazima upewe viwili hivi adhimu ili upate uhai kwa ukamilifu na kama huna viwili hivi bado Roho yako iko hai lakini imenyimwa amri hii(Jaala)ya Muumba wako, ukapewa na huo Moyo ili uweze kujua, kumbuka macho ni kuona, masikio ni kusikia, halafu ukapewa na huu Moyo ili uwe na uwezo wa kujua, kupenda, kufahamu na hekima ya kuweza kuijua Roho yako. Kwa sasa hivi huwezi kujua moyo ulokusudiwa hapa mpaka ukifika mbali katika hiyo safari yako ya (Sipiritual Journey) ndio utajua alaa kumbe moyo una kazi mbili, na hii ya pili ndio ilokusudiwa katika Muangaza wa Roho.
Wanakuuliza nini habari ya Roho sema, ni jambo lilohusiana na (Amri) ya Mollah wangu, Na wala hamkupewa elimu isipokua kidogo.
Hakukataa Mwenye enzi Mungu wala hakuzuia mtu kutaka kujua nini hiyo Roho,ili kasema Elimu mliyopewa ni chache(Kidogo) basi mtu na aitafute asaa anaweza kupewa elimu ya Roho akaijua na ukiijua Roho yako, utapata ufahamu vipi ukawa wewe Khalifa katika Ardhi hii, usisubiri mpaka siku ya kufa ndio ukaijua Roho yako, anza sasa hivi kwa kujitakasa na kuusafisha moyo wako utaipata elimu hiyo, kumbukuka imetolewa kidogo lakini haikuzuiliwa kutolewa, Elimu zinazidi kutolewa, tunaendelea kuvumbua mambo,, na sote siku ya kufa tunakutana na roho zetu kwa hiyo hakuna jambo la kuogopa ima usubiri siku ya kufa au anza sasa hivi, na ukianza sasa hivi basi unakwenda (Beyond death),hiyo ndio maana "Ya Ewe Mja wangu mwema Rejea kwangu ukiwa umeridhi na kuridhiwa"(Operation ya Mauti inaendelea wewe unaangalia, unajijua sina cha kuhofia, mimi Roho narejea kwa yule alonileta, na wala sina khofu tena ya Operation hii), lakini kwanza lazima usafishe machafu yako, omba maghfira kwa wingi ili uitakase Roho yako,ikiwa safi hapo utaona Muangaza wake, utaona Muujiza wake, fanya safari hii muhimu ya Muangaza wa Roho na ukipata Muangaza huu wewe ushafanikiwa, hukai tena ukalinda mali ya Ulimwengu huu, hakuna chochote kitakacho kudhuru na utakua karibu sana na Mollah wako na hiyo ndio maana ya, nasi tukaribu naye zaidi kuliko huo mshipa wake wa shingo
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنۡ حَبۡلِ ٱلۡوَرِيدِ.
Subscribe to:
Posts (Atom)