Sunday, June 14, 2015

KARIBU RAMADHANI PART 3

Asalaam Aleiykum

Kwa mara ya mwanzo unakwenda (Beyond) unaishi katika hicho kinachotakiwa kifanye nacho ni(Taqwa)(Hapo ndipo wanapofunga mawalii na wacha Mungu)Funga yako itakua nyengine kabisa, ukiweza ku(control) viwili vya mwanzo unabakia (Pure Being)Muumin, hapo sasa ndio unaupata uwezo wa kubadilisha Tabia kwenye haya masiku machache, Sasa kwanini ikawa Mchana ndio unatakiwa kufunga?.
Kwa sababu Mchana ndio wakati wa Shughuli za maisha na katika wakati huu ndio una kawaida ya kila tabia imo humo, ndio wakati wakumsahau Mollah wako na vyote ulivyoamrishwa, ni wakati wa pirikapirika za maisha, Mollah wetu katujua tuna makosa yasio idadi, Sasa ili tukumbuke turejee kwenye mapenzi aliyotuamrisha ya Kumuabudu yeye, kuwatizama maskin na mayatima na wasiojiweza, ndio katuletea Ramadhani, ili tupate kuifata hiyo nidhamu ya Ucha Mungu, asaa tunaweza kuendelea nayo tukaishi hivyo hata huu mwezi utakapomalizika, na hiyo ndio ile maana ya pili ya vitendo(Taqwa).
Sasa unatakiwa ufanye nini katika Ramadhani, ikiwa umepata hiyo daraja ya tatu unatakiwa ubadilishe Tabia zako zote za mwaka mzima, vipi utabadilisha, cha mwanzo ujizuie kula na kunywa(Body)ukishajizuia mambo hayo mawili, sasa chukua (Control) ya maisha yako ili upate kubadilika kivitendo, hilo ndio la pili, acha tabia ya uchoyo Futarisha wenzio wasokua na uwezo, Ulikua huendi Msikitini sana sasa fanya hima uwepo kila wakati, Acha mambo ya kuangalia TV japo kwa Mwezi huu tu, acha kusikiliza muziki, wasamehe walokukosea, ondosha maskhara, usiseme uongo, acha kutukana,Usichukue Rushwa,usifanye biashara ya haramu,jiepushe na mikusanyiko ya jinsia tafauti, jizuie na matamanio, ondosha chuki moyoni, jilinde na kila baya na lilo haramu.
Ukiweza kufanya hivyo mchana kutwa basi wewe utakua umefunga, Na zinapofika nyakati za usiku unatakiwa uilinde Funga yako kwa mambo ya kheri na Ibada. Ukiweza kuyafanya hayo katika kumi la mwanzo uka (Master)Nidhamu hiyo utayaona mabadiliko makubwa makubwa katika funga yako ya mwaka huu.
Sasa ikiwa umedumu katika hali hiyo ndio kwa mara ya mwanzo utaona unaanza kushukiwa na Rehma za Taqwa. Mollah wako atakupa zawadi unayostahiki ya Ucha Mungu, utapewa kitu ambacho utakigundua wewe mwenyewe kwa furaha ulonayo, Ndani ya Ramadhani utaanza kupenda Ibada, Mawazo yako yote yatakua kwa ajili ya Mollah wako, zitaanza kukushukia huruma na mapenzi ya kuwapenda viumbe wenzako.
Utakua Mwenye kusikia Raha na saum yako, utakua ukitamani saa ngapi kukuche ili upate kufunga, kama una uwezo utaanza kutoa ili ufurahi na wenzio,itakua kila saa na dakika umo furahani ndani ya mwezi huu, utakua huna wasiwasi na kukubaliwa funga yako, ukiwa katika hali hiyo ndio sasa utakua umemkaribisha mgeni, na Mgeni daima analeta zawadi, na safari hii unapata zawadi za Rehma na msamaha, na pia kuepushwa na Moto wa Jahannam.
Sasa ikiwa kila mwaka unampokea Mgeni huyu kwa desturi hiyo jee utakua na haja ya kuhuzunika wakati unaondoka kwenye Ulimwengu huu. Majibu unayo mwenyewe ikiwa utaitekeleza hiyo funga ya Ramadhani.

No comments:

Post a Comment