Asalaam Aleiykum
Taqwa ni Mti Mkubwa wenye jina la Mapenzi, Kwenye Mti huu kuna matawi mengi yenye kutoa matunda ya kila aina, leo hii mimi nimekuchumia Tunda la (Zaka) ili upate kuonja Ufahamu wake.
Nisiseme Mti watu wakataka kufunga safari ya kuutafuta Mti huu wakidhani labda uko Makka, kule utakutana na Mitende mitupu, Mti niloukusudia hapa ni ule unao ota ndani ya nafsi yako, mimi hapa nimetumia mfano ili uweze kunifahamu nini hiyo Taqwa ya (Zaka).
Basi kwanza wacha tujue tafauti usije ukavamia matawi ukawa hujui unachuma nini?, Watu wengi wanababaika kwenye mambo mawili haya baina ya Sadaka na Zaka. Unaingia kwenye Mwezi wa Ramadhani, Mwezi wenye kulea Roho na kufundisha mambo mazuri yenye faida na wewe hapa Ulimwenguni na kesho huko Akhera uendako kwenye safari ya ulazima.
Nini Sadaka?, Sadaka ni tendo la hiyari ambalo hulazimishwi, kiumbe ana uchaguzi kwa hilo, atoe au asitoe, lakini Zaka ni kitendo cha Amri ya maelekezo kutoka kwa Mollah wako, unatizamwa utaitekeleza au kuipinga, ukitekeleza Malipo yake hayana mfano, na ukiyapinga madhara yake pia makubwa ambayo wengi wetu hatuyatambui.
Zaka ziko za aina nyingi lakini kwa kuwa tunaingia katika Mwezi wa Ramadhani, Ni wajibu wangu kukumbusha zaka hii ambayo takribani wengi wetu tunaiweza, nayo ni zaka hii ya (Vitendo) wengi hatuna uwezo wa kutoa hiyo (Zaka) ya Mali, au ya Fedha, au ya Mazao, ili tusilalamike Mollah wetu katupa zaka ya nguvu za uwezo ili tuitekeleze.
ipi Zaka hiyo?
Endelea part.
No comments:
Post a Comment