Monday, June 1, 2015

KIKAO CHA MSIKITINI PART 1

Asalaam Aleiykum

Mwezi wa Ramadhani unakaribia, Mwezi ulo Mtukufu na kwa sababu hiyo na sisi inatubidi ndio uwe wakati muafaka wa kuanza mataarisho ya kuelekeza darsa zetu kwenye mwezi huu ambao ndio (Ustaadh wa kuzilea Roho zetu). Mwezi huu dhamiri yake kubwa ni kukumbusha kama yupo alokuumba na wewe unatakiwa uwe karibu nae.
Kutokana na sababu hiyo ndio ukaambiwa jizuie kula, kwani ukizuia kula kinatokea nini?, Unapo jizuia kula jambo la mwanzo lenye kutokezea unapata (Separation) tafauti baina yako na huo Mwili, siku zote ulikua hujui nini Mwili(Body), hebu Ramadhani hii jitizame, utaanza kujua nini njaa, miezi yote kumi na moja unakula hujui una njaa au umeshiba, unatia tumboni bajia, chauro, juice, keki, huangalii na wala hujui una njaa au umetamani, mara tangawizi, mara kahawa, (Ice cream) twende vyote vinaingia tumboni, lakini ukianza kufunga kwa mara ya mwanzo njaa inahudhuria, unaanza kupata mawasiliano na (Body)mwili wako, mwaka mzima hujawahi kushikwa na (Kiu) unaanza kujua nini kiu, kwa mara ya mwanzo unatamani (Juice) unatamani maji ya madafu, tumbo linaanza kunyonga, unajisikia uchovu. hayo ndio mawasiliano ya mwili yako ambayo unayapoteza mwaka mzima.
Na Dalili ya mwanzo utaona unaanza kuupenda mwili wako, kwenye njaa (hata tendo la ndoa) hutamani, hutaki mapenzi na mtu unajipenda mwenyewe, mpaka upate shibe ndio unajisahau na kuanza kupenda nje, (Maajabu makubwa yapo kwenye funga).
Lakini katika siku za kawaida mpaka ukucha ukuume ndio unashituka kumbe nina mwili(Body).Sasa ukiweza kujua hiyo (Separation)unapata kufahamu kumbe mimi na (Body) ni vitu viwili tafauti, ukiwa mtulivu ukaujua ukweli huo wa tafauti, ndio hapo inaanza hiyo funga ya Ramadhani.
Elewa kwamba hicho kilicho tafauti na mwili wako ndicho kinachotakiwa kufunga, ndicho kinachotakiwa kiwe karibu na Mollah wako, ndicho chenye kutarajiwa kufanya (taqwa), Usije kuona rahisi kwa kuwa nimehadithia, ukaona Ramadhani hii na mimi ntakipata, vizuri kujitahidi lakini weka mbele kukuponyoka kila mara kutokana na mazoea ya tabia yako, mara utakua umehamia kwenye njaa, mara kwenye fikira za mikungu ya ndizi, lakini usivunjike moyo jitahidi ukiweza kuishi nacho hata kwa nusu siku utaona raha ya funga yako.
Lakini kina masharti kitu hichi nacho usile sana, na hapo ndio matatizo yanapoanzia, kwani ukishiba tu unakipoteza ima kwa usingizi au usahaulivu, kwa hiyo unatakiwa ubakie kwenye hali ya katikati, ili uweze kuidhibiti hali hiyo, kwani ukiwa katika funga ya kweli ni vigumu kwako kutenda dhanmbi, uzito kwako kusengenya, huwezi kwenda kucheza bao na karata, hutaki hata kwenda barazani, sasa yote hayo ukisha yakataa nini kinafatia?, hapo ndipo unaambiwa nenda kwenye kikao cha Msikitini.
endelea part 2

No comments:

Post a Comment