Asalaam Aleiykum
Hakuna tatizo gumu kama kukaa usifanye jambo, Jaribu uone kama unaweza kukaa usifanye chochote, yatakujia mambo hayapungui mia moja, hiyo ndio hulka ya mwanaadamu, utaanza kuwashwa, mara umejikuna, fujo tupu huwezi kukaa ukatulia.
Wewe umepewa nafasi hii kwa sababu za msingi ili upunguze mambo kwenye (Mind) ukifunga viungo vinafanyiwa ukarabati, na huku kukaa kimya Akili inapunguzwa mizigo usije ukapata matatizo baadae, ukikaa Msikitini mawazo yatakujia ya kila aina usiogope hiyo ndio (Process) ya kuondoshewa mazito yaliyomo kwenye (Mind) yako.
Ukitoka katika (Funga) unakuwa mweupe chuki, hasada, choyo,uadui vyote vinakuondoka na unabaki wewe kuwa Mcha Mungu. Umeambiwa ukakae Msikitini lakini hujaambiwa nini kitatokea, Kwa sababu ukiambiwa utaanza shughuli ya kungojea na kusubiri hicho kitakacho tokea, lakini umeambiwa kakae, kimetokea kitu shukuru, hakikutokea shukuru, lakini katika kikao hicho kuna faida kubwa utayoipata, Napenda ukumbuke chochote kile kitokacho kwa Mollah wako ni chenye Faida kubwa juu yako.
Sasa wacha nikupe dalili labda utazinduka na hii faida ya kukaa kimya Msikitini, Basi huoni wewe ukitulia kimya usingizi ndio unakuja?, Huoni wewe ukitulia ukasikiliza kwa utulivu ndio unafahamu vizuri?, Hivyo hujui kama ukitulia hata jambo ulilosahau linakujia na unalikumbuka, Basi kwa hayo machache nenda sasa na Saum yako kakae kimya peke yako Msikitini asaa kuna mambo au shufaa utaipata kutoka kwenye Dunia ya miujiza na kukufikia Mja wewe ukiwa umekaa kwenye Msikiti, Najua na wanawake watauliza na sisi jee, na nyie ndio mshaondoshewa Jinsia ya Kiume mbele yenu, basi kwa hiyo kaeni na nyinyi katika zile sehemu zenu mnazofanyia Ibada na nyinyi mtayapata yale yale wanayopata wenzenu wa Kiume, kwani Mwenye enzi Mungu, hambagui kiumbe wake katika kumpa Rehma zake, mbele ya Ufalme wake nyinyi nyote mko sawa. Na hicho ndio kikao cha Msikitini kama utakipata ipasavyo utaona Raha na furaha ya Funga yako ilo jaa tafauti mwaka huu.
No comments:
Post a Comment