Sunday, June 7, 2015

TAWI LA TAQWA PART 2

Asalaam Aleiykum

Zaka yenyewe ni hii ilotajwa katika sura ya Muuminun aya ya (4)
"وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِلزَّكَوٰةِ فَـٰعِلُونَ"
Na ambao (Nguzo ya)Zaka wanaitekeleza.
Hapo ni kufanya matendo ya Zaka, na hayo matendo yako mengi,na ikiwa Muislam ataishi katika matendo ya Zaka akawa hamshirikishi Mollah wake na kitu chochote basi hana sababu za kuadhibiwa kwa kuingia Motoni,lazima tukumbushane kwamba sadaka ni tendo la nje (Outer) na Zaka ni tendo la ndani (Inner) Wenzetu wengine wanafanya matendo kama haya lakini kwa kuwa hayana mashiko wanaita matendo hayo (Volunteer), Kwa hiyo Zaka ninayo izungumza leo ni ile Zaka ya matendo, Na huwezi kuifanya Zaka hii ya Matendo mpaka kwanza uwe karibu ya Mollah wako.
Itabidi ujitizame kwanza kama upo Karibu na Mwenye enzi Mungu, Na nini kipimo cha kuwapo karibu na Mollah wako ni (Humble) Unyenyekevu, na hilo kwa binaadamu wa kawaida sio jambo rahisi, Jitizame wewe kwanza nyumbani kwako unavotangaza ufalme, kila mtu mpaka mkeo lazima atetemeke juu yako, ndio maana utaona katika Ulimwengu wa sasa hivi utaona Mtu anawaibia Maskini Million mia, halafu anatangaza anawapa sadaka ya Million moja, Lakini kwenye Zaka ya vitendo unatakiwa uteremke kutoka wapi?. 

No comments:

Post a Comment