Friday, June 12, 2015

HAKI YA KUMUOMBEA DUA MAITI PART 2

Asalaam Aleiykum

Sasa Dua tumefundishwa na nani? Dua tumefundishwa na Mwenyewe Mwenye Enzi Mungu alipompelekea Baba yetu Nabii Adam a.s maneno ya kusema katika Toba, sio kukaa kimya, maneno ambayo na wewe unayasema kumuombea Maiti wako vipi utakua unafanya makosa?, Halafu akatupa mfano mwengine wa dua ya Milele ambayo tunaisoma kila siku, Sura ya Ahzab aya ya 56.
"إِنَّ ٱللَّهَ وَمَلَـٰٓٮِٕڪَتَهُ ۥ يُصَلُّونَ عَلَى ٱلنَّبِىِّۚ يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ صَلُّواْ عَلَيۡهِ وَسَلِّمُواْ تَسۡلِيمًا"
Hakika Mwenye enzi Mungu na Malaika wake wanamsalia mtume, Basi enyi Mloamini Msalieni Mtume na Muombeeni amani.
Iliposhuka aya hii Masahaba walishtuka na kuuliza vipi Mwenye enzi Mungu anamsalia kiumbe chake, wakaambiwa hakika hiyo ilokusudiwa hapo ni Rehma, Na Sala ya Malaika ni Maghfira, na Sala yenu nyinyi Waumini kwake ni Dua ya Rehma na Amani, na hii tunaifanya kila siku na yenye kudumu milele.
Sasa la kutizamwa mwanzo katika Darsa hii jee na sisi tunapata hizo Rehma kutoka kwa Mollah wetu, jawabu ndio tunapata, Jee tunapata kuombewa Maghfira na Malaika jawabu ndio Quraan aya ya 5 sura ya Ash-Shura.
"تَكَادُ ٱلسَّمَـٰوَٲتُ يَتَفَطَّرۡنَ مِن فَوۡقِهِنَّ‌ۚ وَٱلۡمَلَـٰٓٮِٕكَةُ يُسَبِّحُونَ بِحَمۡدِ رَبِّہِمۡ وَيَسۡتَغۡفِرُونَ لِمَن فِى ٱلۡأَرۡضِ‌ۗ أَلَآ إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ "
Zinakaribia Mbingu kupasuka juu yao,(Kwa kumuogopa Mollah) Na Malaika wanamtukuza Mollah wao na kumshukuru, na kuwaombea Msamaha(Maghfira) walio katika Ardhi, Hakika Mwenye enzi Mungu ni Mwingi wa Msamaha na Mwenye Huruma.
Sasa kilichopunguzwa hapo ni Dua yako na yangu, unaambiwa usimuombee mwenzio, (Wangekua na uwezo wangewaambia mpaka hawa Malaika wasituombee). Unajua kwanini imeanza kukatazwa siku hizi za karibuni, sababu kubwa kuna Dhehebu Fulani wanaomba Makaburini, kwa hiyo ikaamuliwa kwenye hili Dhehebu mnaloingia nyinyi bila ya kujijua sasa wasiombe makaburini au waombe kimya kimya, lakini dhamira iondoshwe watu kuomba Makaburini, kwa dhana yakua mtakuja kuabudu hayo Makaburi, ndio sasa ikaanza kampeni muachishwe kuombea Maiti au kama mtakua wabishi basi kila mmoja wenu akae na kuomba kimya.
Sasa Bwana Mtume s.a.w Akiwaombea Masahaba zake walipokua wanakufa kwa sauti, jawabu ndio, sio kuwaombea tu alikua akenda na kusali sala ya Maiti hapo hapo Makaburini na kuomba dua na masahaba wakaitikia Aamin. 
Sasa nini faida ya kuombewa kwenye Makaburi (Open Space) wa kwanza kabisa tumuulize Nabii Nuhu a.s nini Faida yake, Quraan As-Saffat aya ya 75 na 76.
"وَلَقَدۡ نَادَٮٰنَا نُوحٌ۬ فَلَنِعۡمَ ٱلۡمُجِيبُونَ "
Na Kwa yakini Nuhu alitwita(Katuomba Tumnusuru)Basi ni waitikiaji wema sisi.
" وَنَجَّيۡنَـٰهُ وَأَهۡلَهُ ۥ مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ "
Na tulimuokoa yeye na watu wake katika msiba mkubwa(Mafuriko yalogharikisha kila kitu).
Nuhu aliita kwenye (Open space) Sasa nini habari yetu sisi tukisimama Makaburini, Wakapatikana Waumin wakafata maneno ya Bwana Mtume s.a.w Muombeeni Maiti yenu kwa Ikhlas. vipi mtafanya hiyo Ikhlas mkisoma kimya kimya, wakati ikiwa hiyo Sala huipati utapata Dua kweli, (Jamani msicheze na Maiti za watu mnachukua majukumu makubwa). Sasa tunawafanyia Ikhlas vipi, kama alivofanya Bwana Mtume s.a.w Yeye anasoma Masahaba wanaitikia, na sisi Mmoja wetu anasoma na wengine tunaitikia, nini kinapatikana katika wakati ule, itizame Ikhlas inavopatikana msomaji kafungika anasoma, wakati unasoma huwezi kuwa unafikiri kitu chengine(Brain) haiwezi kuchukua mambo mawili, na wale wanoitikia wanakua wameingia kwenye (Mode) ya usikilizaji kwa hiyo wote wamefungika wanapeleka Dua yao kwa Ikhlas huku wakiitikia Aamin.
"Ndio Sasa Msomaji anasema Mollah wetu Kiumbe chako Dhaifu sasa tumesha kikabidhi kwenye ardhi yako, kiko mbele yako, Weye ni Mwenye Kujua Kheri na Shari zake, na katika hilo sisi hatuna maamuzi isipokua kumuombea Maiti wetu huyu umsamehe Makosa yake, Mnusuru na Moto wa Jahannam, Mwepushie adhabu za Kaburi, Ewe Mollah wetu Mwenzetu huyu ni mchache wa Ibada, na Mwingi wa Madhanbi, alikua dhaifu wa Dua lakini Mwoga wa Ufalme wako, basi Mollah wetu kwa kuwa wewe ni Mwenye kuwapenda Viumbe vyako, Umempa Rehma hii ya sisi kumuombea Mwenzetu huyu basi msamehe makosa yake, mkusanye na waja wema, ikisha umpe yalo mazuri katika ufalme wako". Kwa utajo wa maneno hayo Watu, Miti, ndege wanaitikia Amin.
Sasa Muujiza gani unatokea katika Dua ya Makaburini? utizame muujiza unaopatikana katika hiyo Dua mnayoomba, na ukisha kuijua una khiyari utamuombea Maiti wako au utamtupa asipate fadhila hizi, kinachotokea hapo(Nature)Ulimwengu unarekodi Dua hiyo, Kwa hiyo maombi yako yanasikika Daima(Hiyo ndio Hekima waloigundua waombaji kwa sauti Makaburini na kusoma Quraan) Wanasema Wanasayansi katika Ulimwengu huu sauti inadumu milele, haipotei kabisa,(Jee wewe hutaki kila siku linasikika jina lako unaombewa usamehewe) kama hutaki basi bakia na kiburi chako utaona faida yake.
Haiwi (Hitler) kazungumza miaka 50 ilopita na kurekodiwa kwenye karatasi tunamsikia hadi leo, nini habari yetu sisi kwa Maiti mwenye kupata dua za kheri kwenye Ulimwengu huu, Quraan pia imethibitisha hilo kwa kusema katika sura ya Maryam aya ya 80.
"وَنَرِثُهُ ۥ مَا يَقُولُ وَيَأۡتِينَا فَرۡدً۬ا"
Na tutamrithi anayoyasema, Na atatujia peke yake.
Endelea part 3


No comments:

Post a Comment