Nini Kuomba?
Kuomba ni Ibada, Kwa sababu ndani ya kuomba kuna unyenyekevu(Humbleness)kuomba maana yake sasa sina uwezo tena, njia zote nishamaliza(Kiburi kishanitoka)nimeishiwa na ujuzi wote, sasa nategemea Rehma yako pekee ndio inivue kwenye matatizo yote.
Nini Kuombewa?
Kuombewa nikuwa mimi muombaji sasa sina uwezo tena wa hata kuomba, uwezo huo nimeondoshewa kwenye enzi yako, zilobaki ni Rehma zako ulizowapa viumbe kuniombea kwa niaba yangu, Na kwa Baraka zako ili uweze kunisamehe.
Hizo ndio baadhi ya ufafanuzi wa Dua mnazokatazwa msiombe, na hao wanokukatazeni walifikia hadi kutaka kuvunja Alkabba mwaka 1979 wakishirikiana na Mtu Mmoja aitwaye (Juhayman Al Otaibi) akishirikiana na Masheikh wake ambao hatimaye walifukuzwa Makka, basi ulizeni habari zao, tafuteni Akida zao na Tawhid wanayofata ikisha ndio muwafate , msisimame tu mkawa mnafata mambo hamyajui mwanzo wake wala mwisho wake.
Sasa jee kwani inaruhusiwa kuomba Dua na kusoma Quraan kwenye Makaburi.
Wacha tuwaulize Wanazuoni watupe (Fatwa)zao. Wanaanza kutufahamisha kwanza tusome sura ya Hashr aya ya 10,
"وَٱلَّذِينَ جَآءُو مِنۢ بَعۡدِهِمۡ يَقُولُونَ رَبَّنَا ٱغۡفِرۡ لَنَا وَلِإِخۡوَٲنِنَا ٱلَّذِينَ سَبَقُونَا بِٱلۡإِيمَـٰنِ وَلَا تَجۡعَلۡ فِى قُلُوبِنَا غِلاًّ۬ لِّلَّذِينَ ءَامَنُواْ رَبَّنَآ إِنَّكَ رَءُوفٌ۬ رَّحِيمٌ "
Na Wale waliokuja baada yao Wanasema Mollah wetu tusamehe sisi na ndugu zetu waliotangulia (Kufa) katika Uislam, Wala usijaalie katika nyoyo zetu undani kuwafanyia Waislam (Wenzetu)Mollah wetu hakika wewe ni mpole sana, na Mwenye Rehma.
Basi Wewe endelea na jeuri za kukataa kuombewa uone kama hizo Ibada zako zinatosha, lete kiburi mbele ya Mollah wako kuwa huna haja ya wenzio kukuombea.
Aya hiyo inaonesha kuruhusiwa kwa kuombea wenzetu na jambo hilo halina mushkeli, kwani lingekua linakatazwa isingetajwa kuwaombea walotangulia mbele ya haki.Na kutajwa Mollah kuwa mpole ni Mwenye kusamehe kwa Rehma zake.
Na Bwana Mtume s.a.w kasema wasomeeni Maiti zenu Yaseen imetajwa habari hii katika Sunan ibn Majah, kitabu Janaiz Hadith 1438.
Ibn Hibban kasema Hadith hii (sahih Hasan).
Imam Nawawi katika kitabu chake(Minhaj al Talibin) kasema yoyote yule atodhuru makaburi basi asome Quraan kidogo na amuombee dua Marehemu.
Ibn Taimiyya katika kitabu chake cha Mujmu al Fatawa pia kaandika Marehemu anapata ujira wa matendo yanayofanywa kwa niaba yake.
وذكر الخلال عن الشعبي قال كانت الأنصار إذا مات لهم الميت اختلفوا إلى قبره يقرءون عنده القرآن
Al Shubi kasema:Ansar, Walikua yoyote yule akifa miongoni mwao, wanakwenda kwenye Kaburi lake na kusoma Quraan.
Maneno haya yamo kwenye Kitabu cha Ibn Qayyim (Kitabu Ruh-Medani page 18.
Iko mifano na Hadith nyingi tu tena kwenye vitabu vingi yakua Waislam wanaruhusiwa kuomba Dua iwe Kwenye Nyumba, Msikitini au Makaburini halijakatazwa kabisa jambo hili.
Anahadithia Abd al-Haq"Ibn al-Kharrat al-Ishbili"Walii Mmoja"akamjia kwenye Ndoto na kusema kaka yangu alipokufa wakati kashafukiwa alikua anakuja Jitu Kubwa na Mwenge wa moto, lau isingekua kwa Dua mlokua mnaniombea basi ningeangamia.
Na Masheikh wengi wametaja katika vitabu vya kila aina basi vyote hivi viwe havifai, ila kifae kimoja tu, kweli hii ni sawa hebu jiulizeni kabla ya kufata jambo. Na Nukuu vitabu ili na nyinyi mkatafute myaone kwa macho yenu.
Nawawi kataja habari hii (Kitab al-adhkar.P229).
Shawkani katika (Tahfat al-adhakirin).
Abu Daud katika Sunan(Janaiz)
Al-Nasai katika (Amal yawm wa layla)
Ibn Hibban katika Sahih(Ihsan) na wengi wa Masheikh wasokua na Idadi.
Namalizia kwa Maneno ya Mwanasayansi Mmoja Maarufu aliulizwa nini Imani yako kuhusu kuwapo kwa Mwenye Enzi Mungu akajibu "Ni Bora niamini yupo kuliko kutoamini" Sababu nikija Kufa akiwepo nitakua nimeshinda, na hata kama hayupo basi pia nitakua nimeshinda, kwa kuwa haitonifika dhara yoyote. Sasa na wewe una uamuzi wako bora usomewe au usisomewe, nani atakula hasara, walobaki Duniani au wewe ulotangulia mbele ya haki.
Towa elimu tu sio jazba
ReplyDeleteTo