Asalaam Aleiykum
Ukiitwa Muislam unakua yule Mtu kakubali kusilimu, yuko tayari ku(Surrender) bado anafanya hayo mazoezi ya kua Muumin, Bado kabakia kwenye Kichwa anatawaliwa na (Mind)Akili. Lakini unapoitwa Muumin ina maana ushaingia daraja nyengine, au kwa maana nyengine ushateremka moyoni, (Kwa sababu moyo ndio wenye kuamini), Na Moyo unatawaliwa na nini?, Moyo unatawaliwa na Mapenzi tu, hakuna chengine, Na mapenzi yakikaa moyoni basi mabaya yanatoweka, na Mabaya yakitoweka unakua ni Mwenye kumpenda Mollah (automatic) na Hiyo ndio (Taqwa).
Sasa kama Muumin wa kweli umefika wakati Mwenye Kuumiliki huo Moyo anakwita.
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡڪُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِڪُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
Enyi Mloamini Mmeamrishwa kufunga(Saum)kama walivoamrishwa waliokua kabla yenu ili mpate kumcha Mungu.
Ukiangalia kwa undani Maneno kwenye hiyo aya yana sehemu mbili, sehemu ya kwanza ni ile ya kufunga, hapa ni lazima ifahamike maana ya kufunga kama nilivyo sema mwanzo ili upate kuipata hiyo Ramadhani, Na sehemu hiyo ya pili ni hiyo ya vitendo(Discipiline) maalum ya kuweza kuipata hiyo (Taqwa) Na ukipata hiyo funga ndio unaweza kumcha Mungu, kama hujachanganya viwili hivyo basi itakua unapata funga lakini hupati Ucha Mungu ambao ndio sababu yenyewe ya wewe kufunga.
Sasa hebu tuanze na maana ya Funga(Saum)Nimekwambia mwanzoni ntakujulisha vipi Marafiki wa Mwenye enzi Mungu (Mawalii) wanavo funga. Nini Funga(Saum)? Nimeyasema katika darsa za nyuma, na leo nafafanua zaidi ili upate kujua kitu kwa undani, twende (Deep) kwenye (Saum) tujue dhumuni la hii Funga.
Soma kwa Makini ukifunga mwaka huu uwe umepata mabadiliko ya ukamilifu katika funga yako. Ulipoitwa Muumin umeitwa (Personal) unatakiwa ufunge, sasa kufunga kuna daraja tatu, ntazitaja daraja hizi na kukuonesha wapi mfungaji anatakiwa aishi katika daraja hizo.
Daraja ya Mwanzo ya Funga ni ile ya Mwili(Body)(Wengi wanaishia hapa)unachukua uamuzi kuwa wewe mwili wangu kwa siku ya leo hutopata chakula, Mwili una kawaida ukifika wakati wake unadai chakula, mfungaji unasema najua huu wakati wako lakini leo siwezi kutekeleza ombi lako hili utabidi usubiri mpaka magharibi.
Daraja ya pili ya Funga ni ile ya (Akili), na hii ndio ngumu kwa sababu (Brain) ina nguvu, kwa hiyo unaiambia Akili najua unatamani senema, kutizama maasi, kucheza bao, mazungumzo ya siasa na mipira, kusema watu na uongo, lakini unaiambia Akili mwaka huu mimi nafunga siwezi kutekeleza amri zako kabisa, ukiweza kuvimiliki viwili hivyo, nini kinatokea?
Endelea part 3
No comments:
Post a Comment