Sunday, June 7, 2015

TAWI LA TAQWA PART 3

Asalaam Aleiykum

Unatakiwa uteremke kutoka kwenye kiti chako cha Ufalme wa Kiburi uje chini kunyenyekea, Sababu kwenye Ku(Surrender) Kiburi lazima kipotee, Sasa ufanye nini ili kupata matendo na vitendo hivi vya zaka, ambavyo ni bora zaidi hata kuishinda hiyo Sadaka, Unatakiwa ujihusishe kwenye shida na matatizo ya watu kwa njia ya huruma,pia kuhusika kibinafsi katika matendo ya kuwasaidia watu, kama vipi?Nenda katoe huduma zako za nguvu Kwenye nyumba za wazee, kwenye nyumba za yatima, kwenye Mahospital.
Ramadhani inakuja pita Majumbani uulize watu wanashida gani uwasaidie, katafute watu wazima uwasaidie matatizo yao, pengine watoto hawana baba au mama na kwao hakuna uwezo, basi watafutie njia za kuwakwamua ili watoke kwenye matatizo yao, hayo yote ni matendo ya Zaka uyafanyao, hata ukiwapa ushauri yakamuondoka Mtu matatizo kwenye Akili yake, basi wewe umeshatenda tendo la zaka ya vitendo, Husika kwenye Misiba yao, pita ukihimiza watu kwenye uadilifu, fanya jitihada ili walogombana wapatane, wasaidie walemavu na wasojiweza, shiriki katika kuwajengea watu makaazi, huku kaa ukijua vitendo vyote uvifanyavo ni Zaka, na fadhila za malipo ajuae ni yule mlipaji wa matendo hayo ambaye ndie Mollah wako mlezi alokupa nguvu hizo na hekima za kuyatekeleza hayo, sifa zote na shukurani anastahiki yeye pekee Mwenye uweza wa kila jambo.

No comments:

Post a Comment