Asalaam Aleiykum
Ipokee uisome darsa yangu ya leo iwe kama Wasia kutoka kwangu kuja kwako, Endapo utahisi hukubaliani na wasia huu basi niachie mwenyewe, na pindipo utakubaliana na wasia huu basi fanya hima uwaeleze na wengine wasije wakakosa Fadhila hii ya Dua ya Maiti, nitaeleza nini dhumuni la dua, Nitakujulisha kwanini tuombe Dua, halafu nitakupa maana ya kuomba Dua ya pamoja na sababu zake.
Ikisha ntakupa nguvu ya hoja ili na wewe ufanye uamuzi vipi utataka uombewe Dua au kumuombea Maiti wako, au utakhiyari watu wakutupe ikisha wende zao kama yanavofanyika mafundisho ya sasa hivi, Kwanini nikasema hivyo kwa sababu siku hizi mambo yamezidi, mpaka imefikia Dua marufuku, unakwenda Nyumba ya msiba unakuta watu wamejificha nyuma ya makochi kimya, hata kulia haifai, ukiuliza unaambiwa Ustaadh kasema Dua haifai, au omba kimya kimya, au omba mwenyewe, na wao wanaendelea na porojo, cha ajabu zaidi huyo Ustaadh hajaifadhi hata hadith kumi, wala hajui nini Ibada, nini Dini, ukimtizama unamuona hana isipokua katawaliwa na Kiburi, na yeye anajijua hajui chochote lakini vipi atakubali hajui wakati anadanganya wasojua.
Wanasema Maiti atajiombea Mwenyewe kwa Amali zake, na nyie mnaendelea na mazungumzo mpaka Maiti huyo anazikwa hakuna jambo la Dua, hapa ndipo tulipofikishana, Na kama hilo halitoshi Maiti huyo pia marufuku Kusaliwa Msikitini(Naeleza haya yanatokea hapa Uk) huko kwengine sina ujuzi nayo. Lakini cha kushangaza Msikiti wa Makka wakati wote tunaona Maiti wanasaliwa, Na jambo jengine ambalo linafanyiwa kazi sasa ni hili la kuombewa Dua Maiti makaburini linaondoshwa kidogo kidogo.
Basi kabla halijaondoshwa kabisa nimeona nikupeni baadhi ya faida zake labda zitakufanyeni mzinduke usingizini mkatae mchezo huu wa kutupwa Makaburini na watu wakashika njia na kwenda zao.
Ntakupa hoja halafu wewe una khiyari ukibaki katika kundi la wanotupana au la wale wano ombeana dua, utakubali au kukataa Maiti yako aombewe Dua. Na utakapo pata msiba bora utangaze toka mwanzo mimi nataka dua, asotaka ende zake, na wala usiogope watu wa kustiri Maiti yako wako wengi na hilo si tatizo kabisa.
Basi kwanza tupate taaluma ya Roho ya Mwanaadamu inapotoka kwenye Kiwiliwili, kwanza inakua (Shock) kubwa kwako kutenganishwa na Kiwiliwili chako(Body), Huo Mwili umeishi nao takriban kwa Miaka 50 au 60 leo unauona umelala pale umetengana nao, kumbuka safari yako ya (Barzak) haianzi hapo hapo, unasubiri mpaka khitimisho la Mwili wako utakapo zikwa, kwa kuwa umekua (attach) na hiyo body kwa miaka yote uloishi, ndio maana wale wenye kupata (Near death Experience) wakirudi kwenye (Body) wanahadithia nilikua niko juu nakutizameni mlivokua mnajaribu kuni (Revive)shughulikia mwanzo mpaka mwisho.
Kwa hiyo napenda uelewe Roho ni yenye kubaki mpaka yafanyike mahojiano huko kwenye Kaburi, napenda ufahamu wako Malaika wenye kuitoa Roho, wako wenye kuhoji na wako wenye kukuchukua kwenda safari ya Barzak ulikopangiwa. Katika kipindi hichi ndio tumehimizwa kuwaombea kwa wingi Maiti zetu, Na wala hakuna hata sehemu moja hata ya hadith dhaifu ilokataza jambo la Dua, au kusema ombeni lakini kimya kimya, haya yote ni mambo mepya yenye kupandikizwa katika Dini hii na watu wa Karne hii tulonayo.
Cha kusikitisha zaidi watu ni wenye kukubali hawajui kitu maskini, na wala hawaulizi yametokea wapi na kwa ushahidi gani?, ila kila Mtu anapanda gari ya kukaa kimya anaambiwa usimsalie au kumuombea Maiti yako na yeye anakubali, ikisha anajuta kwenye maisha yake, kwanini alikubali, sasa tunataka kukufahamisha hakuna kosa katika kuomba Dua, na Dua ilianza lini?.
Endelea Part 2
No comments:
Post a Comment