Asalaam Aleiykum
Sasa unapata nafasi ya kujiuliza kwanini umeambiwa ukakae msikitini?.Na wapi umeambiwa maneno haya?.Quraan sura ya Baqarah aya ya 187 mwanzo mpaka mwisho wa aya na hapo unakutana na neno hili, وَلَا تُبَـٰشِرُوهُنَّ وَأَنتُمۡ عَـٰكِفُونَ فِى ٱلۡمَسَـٰجِدِۗ
"Na hali (yakua) mnakaa itikafu(Devotion)Msikitini".
Ikiwa umefahamu kilichosemwa mwanzoni sasa unatakiwa ukakae msikitini ukilinde, kalinde (Saum) yako japo kwa siku moja, chukua japo likizo(off work)ili upate mawasiliano na Mollah wako kwa kukaa Msikitini, kwanini ikawa hivyo, kwa kuwa huu ni mwezi maalum wa viumbe kuwa karibu na Mollah wao, pia kukumbuka ulipotoka, kujua dhumuni la kuumbwa kwako, kuzungumza na Mollah wako,Kuwapenda viumbe wenzio kwa misaada ya hali(Dua) na Mali, vipi utayapata mambo hayo kakae Msikitini.
Miezi kumi na moja zinaingia fujo tupu Kichwani mwako, Siasa zimo humo, Nyimbo zinaishi humo ndani, humo kuna magonvi, umerundika visasi, kila kitu kichafu unatupa ndani ya nafsi yako, Sasa ikiwa (Body) Mwili unapona kwa ajili ya Funga ya Ramadhani, Basi na Akili (Mind) inatakiwa kupumzishwa ndio unaambiwa (Kakae Msikitini), sio kuanzisha Baraza Msikitini na vikao vya siasa na masikhara katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Vipi Kukaa huku?
Watu wengi wamekua na fikra tafauti na kikao hichi cha Msikitini, Kwa sababu kelele nyingi na mambo mengi yameingia Akilini, unaogopa kukaa kimya, ndio utaona unataka labda uvute uradi au ufanye mambo mengine, kikao hichi hakijataja hayo, wewe umeambiwa ukakae tu Msikitini, nini kitatokea ukiwa na Subira?. (Mfano)unaona ukikaa kimya unatizama mchezo wako kwenye TV ama taarifa ya habari, hufikiri kitu chochote chengine, na hali kama hiyo ndio unatakiwa ukae nayo Msikitini, ukiweza kufanya hivyo moja kwa moja na wewe utapata, au kukujia ile hali au daraja ya wale (Wanomkumbuka Mollah wao wakiwa wamesimama, au wamekaa, au kulala) na ukiipata hali hiyo wewe ushafuzu na ushaipata funga ya Ramadhani.
Aya haijasema ukadhikiri, wala kuvuta uradi, aya imekwambia kakae Msikitini (Just sit) Wafuasi wa Dini ya (Kikiristo) waliambiwa katika maandiko yao maneno mfano wa haya"(Kuwa Mtulivu na ujue mimi ni Mungu wako)"Wafasiri wakatafsiri kuwa mkimya ujue mimi ni Mungu wako, hapo wakafanya makosa makubwa sana, kwani ukimya siku zote unafatiwa na Makelele, na Binaadamu siku zote anaongozwa na utamaduni wake, ukichanganyika na Dini ndio unaona vipi unapata mseto wa kelele na kutupwa kwa Ibada, kwa sababu Binaadamu anaogopa kukaa kimya, ndio maana kaamua kuimba, kupiga miluzi, na firimbi, ngoma, ili iwe sehemu ya Ibada na kuondosha ukimya, lakini wangefasiri (Be still and know I'm your God) basi wangepata utulivu, na utulivu mwenzie harakati, kwa hiyo ukiambiwa tulia ina maana acha harakati, na kuacha harakati maana yake kaa kitako utulie, na hiyo ndio maana ile ile na maneno ya kikao cha msikitini, kakae utulie(Do Nothing)kuwa mtulivu, maneno ni yale yale lakini walipoonekana wameyatia mkono wanaadamu ndio Waislam wakaambiwa kakaeni Msikitini, itakujieni fahamu ya kumjua Mollah wako kwa njia anazozijua yeye Mollah wako.
Kwani nyakati nyengine si unakujia mfano unakutana na mtu humjui jina lake, una hangaika kutwa nzima hulipati lakini ukikaa ukatulia kimya mara linakujia, basi na Msikitini kakae utulie kuna faida chungu nzima utazipata zikiwamo na zile za kuepukana na machafu na maasi.
No comments:
Post a Comment