Asalaam Aleiykum,
Ametukuka Mwenye-enzi-Mungu aliyeumba Mwanamme na Mwanamke ili wapate kupeana (ushirikiano)wa maisha ya utulivu, wapate kupeana Mapenzi, katika (taasisi)ya ndoa. Ikisha baada ya hayo akajaalia kutokea katika miili yao kupatikana kizazi ambacho ni (Zawadi)kutoka kwa Mollah wao ili wapate kuishi kwa salama na kufata maamrisho ya Mwenye-enzi-Mungu na Mtume wake ambayo ni Mwanaadamu kudumu katika Ibada.
Ikasemwa ndani ya (Quraan-sura-ya-Rum-aya-ya-21)
"وَمِنۡ ءَايَـٰتِهِۦۤ أَنۡ خَلَقَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٲجً۬ا لِّتَسۡكُنُوٓاْ إِلَيۡهَا وَجَعَلَ بَيۡنَڪُم مَّوَدَّةً۬ وَرَحۡمَةًۚ إِنَّ فِى ذَٲلِكَ لَأَيَـٰتٍ۬ لِّقَوۡمٍ۬ يَتَفَكَّرُونَ"
"Na katika alama zake, amekuumbieni wake zenu(Partner)katika jinsi yenu ili mupate utulivu kwao, Akajaalia mapenzi na huruma baina yenu, hakika katika haya kuna alama kwa wenye kufikiri".
Imeanza hii aya ya Quraan kutaja Alama(Ishara)dalili zetu, ikisha mwisho wake ikamalizikia aya kwa kuwataja wenye kufikiri, hapo kuna uzinduo, lakini wapi wanaadamu tumo kwenye hasara kubwa wengi katika sisi hakuna hata mwenye kuota wacha kufikiri, sababu kufikiri unatakiwa uwe macho, na sisi sote mtu anatembea kalala, akikaa barazani kalala, mtu hata anazungumza huku kalala ndio maana utaona hata mambo yaliyomo kwenye nafsi yako yanakupita hivi hivi ukiwa umelala. Na kama hujalala jee? ushawahi hata siku moja kumtizama mkeo au mumeo japo dakika mbili machoni mkawa mnatizamana, jee ushawahi kujiuliza kwanini hususan mie nikamuoa au kuolewa na huyu?Ushawahi kujiuliza mbona tumefanana kidogo, vipi macho yake kama yangu? ilikuaje mie nikapiga goti kufunga ndoa na huyu, hivi kweli mie namjua mke au mume wangu, jee mimi naishi nae kimapenzi au tunaishi tu penzi lishakufa zamani?.Hamuwezi kutazamana unajua kwanini? kwa sababu kila mmoja ana (Masanamu-Skeleton)zake moyoni na anaogopa katika kutizamana kule yasije ya kamdondoka akaadhirika, na mwisho ushajiuliza Jee hapa Rehma zipo? Yakikujia Mawazo kama hayo basi hapo umekuwemo katika lile kundi la wenye kufikiri, na wale wenye kufikiri huchukuliwa katika safari nyengine kabisa wakafunguliwa muono mpya kabisa na wakapata kujua kwa yakini yakuwa njia hii ya mimi kufunga ndoa na fulani Imepangwa na Mollah wangu.
Na ukipata hilo hapo unakua umeamka usingizini, unakua unaridhika, unakinai, huna pupa unajua haya amenitakia yule mwenye kunipangia kudra hii na mimi sina budi ila kuikubali. Sikua mimi mwenye kupanga haya, (Wala haitokei kama accident-ajali) yeye ndie aliyenishushia mapenzi na hamu na kuniongoza mimi kuja kumposa(Kumkubali)mwenzangu huyu, na lazima katika muongozo huu kanipangia kheri na amana atakazo nipa ambazo hakuna mwengine azijuae isipokua yeye Mollah wangu."
" وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٲجً۬ا وَجَعَلَ لَكُم مِّنۡ أَزۡوَٲجِڪُم بَنِينَ وَحَفَدَةً۬ وَرَزَقَكُم مِّنَ ٱلطَّيِّبَـٰتِۚ أَفَبِٱلۡبَـٰطِلِ يُؤۡمِنُونَ وَبِنِعۡمَتِ ٱللَّهِ هُمۡ يَكۡفُرُونَ"
"Mwenye-enzi-Mungu amekujaalieni (amekuumbieni)katika nafsi zenu wake, na akakujaalieni(kuumbieni)kutoka kwa wake zenu watoto na wajukuu, akakuruzukuni vitu (vilivyo)vizuri, Basi mmekua yale yaso haki mnayaamini(kuyafata)na Neema za Mwenye-enzi-Mungu(Mnazikimbia)Mnazikufuru(mnazikataa)"
"Ukiitupia macho hii aya utajua kwa uhakika kuwa huu mpango au njia kuwa mimi nimeshapangiwa(haitokei kama bahati)Nimepangiwa mimi nimuoe fulani na nikisha kumuoa atazaliwa fulani na fulani na hiyo ndio kazi alonipangia Mollah wangu, amenikabidhi amana ilotokana na damu yangu, viungo vyangu, sasa nini unafanya vitoto vikishazaliwa? vitoto pengine vitatu au vitano bado vidogo, viko katika hali ya kukuhitaji nini unafanya?-Endelea part 2
No comments:
Post a Comment