Saturday, September 22, 2012

MADHARA YA MJA MWENYE CHUKI -PART -1

Asalaam Aleiykum.

Shukurani zisizo na upungufu anastahiki yule mwenye kutujaalia mapenzi baina yetu, Ikisha akatujulisha hili tukio la mapenzi linasababishwa na yeye na hilo ni katika Rehma zake anazo tuteremshia kila siku katika maisha yetu. Huku kuumbwa kwetu wanaadamu ni mapenzi yake Subhanna, hii afya alotupa na kuweza kuvuta pumzi, kulala kwetu na kuamka ni moja katika ishara za mapenzi yake kwetu sisi waja wake, unatakiwa Mwanaadamu kitu cha mwanzo unapoamka ushukuru kwa neema hizi.
Limezama neno hili la mapenzi kwenye nyoyo zetu mpaka imekua desturi yetu katika lugha kila kitu tunatumia hichi unakipenda au hukipendi, Na imekua bora kwetu sisi hatutumii neno(Umechukia)kwani ukitumia neno umechukia unakua umeshakwenda upande wa pili(Ambao)ni kusudio la Mada hii.
Unaposema jambo au kitu hukipendi jichunguze unabakia sehemu ya kati(Netural)unakua hukipendi lakini hukichukii, kwa hiyo inaonesha chuki ni sehemu ya pili ambayo sasa tunaingia ili tupate kuijua na kuifanyia kazi tuepuke na madhara yake.
Nini Chuki? Utashangaa nikikwambia chuki na mapenzi ni kitu kimoja lakini kinabadilika wakati inapoingia (Sumu)na hizi sumu zipo za aina nyingi ambapo leo tutachambua japo kwa uchache ili mtu apate kujijua jee yeye ana mapenzi au chuki ndani ya nafsi yake.
Mapenzi ni (Nature)yetu kama ilivyo afya, ndio maana viwili hivi huwezi kuvifafanua, unaona vipo tu na hujui kwanini. Lakini kutokana na kuandamwa kwetu na (Shetani)na vishawishi vilotangulizwa mbele ya macho yetu basi tunaikubali Sumu hii na hapo ndio tunapoanza kuibadilisha neema hii ya mapenzi na kugeuka Chuki. Hebu utizame (mfano) huu wa sumu inavoingia na kuharibu mapenzi, huenda ikawa Mke na Mume wanapendana akapita shetani ghafla akamshawishi mmoja wao kuteleza katika ile ndoa, Na akiteleza mmoja wao basi hapo sumu imeshaingia katika mapenzi na sasa utaona moja kwa moja inageuka kuwa chuki na ama iwe dhahiri au siri ya moyoni lakini chuki ni ile ile, Mapenzi hayabadiliki kuwa kitu chengine(Ukikera Chuki, Ukifurahisha mapenzi).
Tupia macho Marafiki wanavo gombana, Ndugu wanavo farakiana, yote haya yanatokana  hatutunzi Rehma hii ya Mapenzi alotushushia  Mollah wetu. Nguvu hii ya Mapenzi au (Rehma)ni chanzo kikubwa cha maradhi yetu wanaadamu, tizameni vipi watu wawili wakipendana halafu wakija kufarakiana nini kinatokea?
Endelea part 2

No comments:

Post a Comment