Saturday, September 1, 2012

ALAMA ZA WATU WA MOTONI(PART 2)

Asalaam Aleiykum.

Tunaingia katika maudhui ya watu wa Motoni kila Mmoja ana kovu(Alama)zinatafautina katika ufafanuzi hapa leo nazizungumzia za watu wa Motoni kama ilivotajwa katika sura ya(yunus aya ya 27)وَٱلَّذِينَ كَسَبُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ جَزَآءُ سَيِّئَةِۭ بِمِثۡلِهَا وَتَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٌ۬‌ۖ مَّا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِنۡ عَاصِمٍ۬‌ۖ كَأَنَّمَآ أُغۡشِيَتۡ وُجُوهُهُمۡ قِطَعً۬ا مِّنَ ٱلَّيۡلِ مُظۡلِمًا‌ۚ أُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَصۡحَـٰبُ ٱلنَّارِ‌ۖ هُمۡ فِيہَا خَـٰلِدُونَ
"Wale waliochuma maovu, Malipo ya uovu wao ni mfano ule ule(kama walivo tenda)na watakua na udhalili(utawafika).Hawatakua na awezaye kuwalinda(zidi)ya Mwenye-enzi-Mungu,Zitakua Nyuso zao kama(Alama)zimefunikwa(zimezungukwa)na vipande vya usiku wenye kiza kikubwa, Hao ndio watu wa Motoni, na humo watakaa daima."
Inakuaje alama hizi, vipi unaweza kuitambua Alama hii na vipi wengine wanaijua alama yako jee tayari kipande cha giza kimekufunika?maswali hayo utajijibu mwenyewe ukiendelea kusoma na kupata kujua una Alama gani na kama huna basi wewe nenda kasome (Dalili za Mcha Mungu). Usishangae kuwa una Alama hata Mti (Tree)wanasayansi wanatwambia ukiupasua kati unakwambia tarehe fulani, mwaka fulani, saa fulani ilinyesha Mvua kikafatia na kimbunga, na vile vile mwaka huo huo kulikuwa na joto kali huo ni mti unatoa habari hizo waulize wanataaluma wa kilimo watakufahamisha.Sasa nini habari yako wewe kuhusiana na Alama yako.?Kazi yangu hapa kukujulisha hizo Alama za Motoni kwa ithbati kamili unajua wewe mwenyewe na Mollah wako kama unazo au huna Alama hizi, Anasema Mollah katika    Sura ya (Al-Qalam aya ya 7)"إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ "
"Hakika Mollah wako  anamjua aliyepotea katika njia yake, Na anawajua waloongoka". Yeye pekee ndie mwenye hakika fulani ni mtu mwema, na fulani ana ufisadi ndani ya nafsi yake, hakuna mwengine mwenye kujua siri hiyo, lakini visa vikizidi, vituko vikiongezeka, kusudi ikizidi na ikawa ndio dasturi yako hapo tena inabidi utiwe Alama na Binaadamu wapate kukujua usipite ukawa unazidi kuwafanyia hadaa, Mollah anawaonea huruma viumbe wake, ndio kama hadithi ya yule kijana alokua anamkera sana Bwana Mtume s.a.w na Waumini wengine ikabidi iteremshwe aya na kuambiwa(Al-Qalam aya ya 12)"مَّنَّاعٍ۬ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ"
"Azuiaye kheri, anayedhulumu viumbe wenzie, na ana Muasi Mwenye-enzi-Mungu". Huyu Bwana kero zake zilivozidi Waislam wakawa hawamfahamu basi sasa wakaambiwa katika aya ya (16)
"سَنَسِمُهُ ۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ " Tutamtia kovu juu ya pua yake" ili mpate kumjua, na hivi ndio mpaka leo watu wanaendelea kutiwa Alama makovu kila mtu anayo sijui lako wewe limejificha wapi, ndio maana utaona ukipenda pesa watu watakujua, ukiwa baghili watu watakujua, ukiwa mzinifu watu watakujua. ukiwa fisadi watu watakujua muradi kila mmoja ana Alama yake inajulikana na mwenyewe anaijua ilikojificha japo ataleta dharura, ikisha Mollah wako akakupa nafasi midamu Uhai upo, bado unavuta pumzi basi unayo nafasi ya kuifuta Alama hiyo lakini ukitaka. sasa wacha tuzitaje hizo Alama mimi nitazitaja(4)lakini zitakusanya(Majority)na nyengine zitajieleza zenyewe, Alama ya Mwanzo-Endelea part 3

No comments:

Post a Comment