Saturday, September 1, 2012

ALAMA ZA WATU WA MOTONI(PART 5)

Asalaam Aleiykum
Matajiri:
Naam kila mtu yumo, atahadhari sana mwenye uwezo, ajilinde sana awe anajuta na kutoka machozi, kwani ajue amepewa mtihani sawa na mwanasiasa au kumpita, yeye Alama yake kubwa huonesha waziwazi hajifichi, basi aogope sana mwenye mali asije akaitumia Alama hii kwa njia ya kumpeleka motoni, Isije ikawa anapata usingizi na huku jirani yake hajatia riziki kinywani na yeye anajua.
Asije akawa Alama yake inawaka moto hapa hapa duniani kama inavosema aya:"أَلۡهَٮٰكُمُ ٱلتَّكَاثُرُ""Meghafilika katika kuchuma kwa wingi wa (Mali na kujisifu)"
Hii ndio kawaida ya tajiri yoyote hatosheki lazima apate sifa, lazima watu wamjue, anasikia fakhari watu wakenda kumuomba, kiburi ndio uteja wake, ndio maana ukaambiwa tajiri tabu sana kuingia peponi isipokua wachache Mollah wao alowapa utajiri ikisha akawaruzuku siri ya kuishi kama maskini katika roho zao,(hao wamefaulu)wamepewa fadhila kubwa kabisa na Mollah wao kuliko huo utajiri  mnaouona nyinyi machoni mwenu.
"حَتَّىٰ زُرۡتُمُ ٱلۡمَقَابِرَ""Mpaka mmehudhuria makaburini",
Tajiri Amekufa ghafla,amevamiwa na kutolewa Roho kwa kishindo pengine(heart attack)ulikua umekaa kwenye kiti unatizama(Bank statement)ilivojaa, unacheka na mauti yanakuhudhuria, na watu wanavotaka kukurithi haraka haraka mara wamekuchukua wanakufukia kwenye shimo la futi(6 feet)makaburini, basi tahadhari sana pale umeshaingia kaburini mara jitu la ajabu linakufungu sanda ikisha mnatizamana, na aogope sana mwanaadamu kumkuta hali kama hiyo na yeye ana Alama ya Motoni."  لَتَرَوُنَّ ٱلۡجَحِيمَ ""Hakika mtauona moto".
Jambo la kwanza lepe lepe la mauti linakutoka unauona moto, ukijifanya huoni uzuri, hujui imekuaje mbona uko hapa,kwanini mie."ثُمَّ لَتَرَوُنَّہَا عَيۡنَ ٱلۡيَقِينِ""Ikisha Mtauona kwa yakini Moto".
Ukijifanya hamnazo hufahamu kitu, unasogezwa karibu ili upate yakini yakua humu ndio itakua makaazi yako, na yakini maana yake kuthibitishiwa haya ndio yatakua maskani yako ya kudumu, ukiuliza kwanini, nimefanya nini." ثُمَّ لَتُسۡـَٔلُنَّ يَوۡمَٮِٕذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ""Ikisha mtaulizwa siku hiyo juu ya neema".
Vipi ulitazamaje mayatima, ulitoa kuwapa maskini,wasojiweza walifaidika na misaada yako, jee ulifanya kheri yoyote,ulisaidia wagonjwa, uliwastiri vizee wasojiweza, ikiwa huna jawabu ya maswali haya na mengine basi matokeo utayajua mwenyewe, labda ikiwa kabla umri haujakatika ulipata nafasi kuibadilisha Alama yako ikawa sio ya motoni tena, lakini mpaka sasa hivi alama ipo vile vile na kivumbi cha mateso kipo pale pale, fanya haraka ubadilishe mwendo wako asaa utafutiwa Alama ya motoni na kupewa alama ya peponi na hiyo ndio yenye kheri kubwa.
Endelea part 6

No comments:

Post a Comment