Asalaam Aleiykum,
Jambo la kwanza (shetani) anokuonesha yakuwa mwenzako huyu uloishi naye miaka yote sasa keshakua mzee, Figure sikama ile ya zamani(Unasahau na wewe ushakua mzee)pengine sasa hapaki rangi ya kucha, Nini unafanya?.Wewe hutizami vile vitoto au mwenzio uloishi naye labda miaka mitano au kumi, wewe sasa unaanza kukimbilia nje, pengine sasa nyumbani hurejei mpaka watu wote washalala, Mkeo akiomba kutoka na wewe unamkimbia kwa kutangulia mbele, akitaka mshikane mkono ndio balaa inaanzia hapo unaweza hata kumpiga kibao, Hapo tena unaanza kutafuta kila sababu ya ugonvi ili upate kutoa talaka. Unatafuta sababu za kukimbia ulezi wa watoto wako mwenyewe, Unaanza kufikiria vipi uta-enjoy life na mwanamke mwengine, hutaki tena maisha ya ndoa, sasa dhamana zinakutia dhiki.
Mollah wako alipokataza zinaa alisema hivi:(Quraan-Isra-32)
"وَلَا تَقۡرَبُواْ ٱلزِّنَىٰٓۖ إِنَّهُ ۥ كَانَ فَـٰحِشَةً۬ وَسَآءَ سَبِيلاً۬"
"Na wala msikaribie zinaa, hakika huo ni uchafu, na njia mbaya"
kuhusu uchafu unajulikana kuanzia maradhi na mambo kadhaa mengine, Kusudio la neno njia (mbaya) ni ile ya kuzaliwa Mtoto maskini hana baba, hana malezi, mtoto yuko ovyo ovyo, hajui anakwenda au anarudi dhiki na balaa kubwa linamkuta yule kiumbe alozaliwa nje ya ndoa. Nini habari yako wewe ulozaa ndani ya ndoa ikisha ukageuka kutenda yale yale anotenda mzinifu kwa kutupa kizazi chake, wewe unafanya yale yale aloharamisha Mollah wako ndio maana ukaambiwa(katika hadith) talaka ni amri anoichukia Mollah wako(Hapa napenda kukumbusha)Mollah wako hapendi wala hachukii hiyo ni mifano mnopewa nyinyi wanaadamu kuonesha ubaya wa tendo hili la talaka.
Sasa nini unachofanya wewe Mzee unotupa kizazi chako ukakimbilia maisha mengine ya Raha na Mustarehe, Huku nyuma unaacha ile amana alokupa Mollah wako inateseka, unaipinga dini iloleta tendo hili la ndoa ili wawili nyie pamoja na familia yenu ipate utulivu, heshima na mapenzi, usalama pamoja na mahusiano ili mpate kufanya Ibada, mpate kuwa wacha Mungu. Hiyo ndio dhumuni la ndoa na uchambuzi wa neno Ibada ni mpana wenye upeo mkubwa, kama vile kila kitendo cha kheri ni Ibada, Tendo lolote la kuisaidia jamii ni Ibada, Maneno mema pia ni Ibada.
Mollah wako kakupa cheo baada ya kuoa na kuzaa vitoto sasa unaitwa (Mama au Baba)hiyo pekee inaonesha dhamana ulopewa ya kuvilea vitoto vyako mpaka viwe vikubwa, Lakini wapi umetumia maisha yako sasa unataka utumie na ya wenzako, Vijana wanashangaa mbona mzee fulani nyimbo zote anazijua, style yoyote ikitoka na yeye yumo, ndio maana utaona vizazi vyetu vingi vinaangamia, havina malezi mazuri ya msingi wa kidini, ukiuliza unaambiwa maskini baba yao kakimbia watoto wakiwa wadogo, kakimbia dhamana ya ulezi, kakimbia kuwatizama watoto wake, kakimbia kutoa hata kilo chake. Sasa anakuaje Mzee alotenda haya?enedelea part 3
No comments:
Post a Comment