Saturday, September 15, 2012

HASARA YA BABA MWENYE KUTUPA KIZAZI CHAKE-PART 3

Asalaam Aleiykum,

Anakua moja kwa moja kamuasi Mollah wake, haingii huyu katika lile kundi lilotajwa katika sura ya (Muumin-aya-ya-8-)
"وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَـٰنَـٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٲعُونَ"
"Ambao Amana zao na (zile)Ahadi(Walochukua)wanaziangalia"
Wewe ulipo piga goti (kufunga ndoa)ukachukua ahadi ukaaminiwa na wazee pamoja na Mollah wako ikisha ukapewa dhamana ya vitoto sasa vimezaliwa wewe ndio unakimbia vipi utakua katika kundi la waliofaulu? vipi wewe utakua Muumin, ulikua Muumin pale ulipochukua ahadi ya kuzitunza amana, lakini sasa unakimbia vipi tena ubakie kuwa Muumin, wewe unakimbia tendo la Ibada, wewe una asi (Isipokua papatikane sababu za ukweli na uhakika sasa huwezi kuishi tena au huwezi kuiangalia amana hii)labda unatendewa vitimbi wazi wazi, hapo huna makosa una uhuru wa kuikimbia lakini sio kwa sababu za upuuzi na Mollah wako ni mwenye kujua japo utaficha moyoni mwako.
Vipi leo Unajiita Muumin na unasali Rakaa zisizo na idadi huku umetupa kizazi chako, unatoa sadaka huku kizazi chako kinateseka, hebu kumbuka wewe umetoa Ahadi mbele za watu na ukataka Mollah wako akushuhudie ikisha baada ya kupewa kizazi unachukua begi lako la mbao unaondoka tu bila ya fikira yoyote, ukiulizwa nini kimetokea mke kaunguza chakula, au kachelewa kurudi, au katoka bila ya ruhusa yangu, basi hee umeishi naye miaka kumi katoka siku moja ndio iwe talaka yake, ole wako wewe unayefanya kiini macho hichi cha kutupa kizazi chako kumbuka maneno ya (Luqman-aya-ya-16)"
يَـٰبُنَىَّ إِنَّہَآ إِن تَكُ مِثۡقَالَ حَبَّةٍ۬ مِّنۡ خَرۡدَلٍ۬ فَتَكُن فِى صَخۡرَةٍ أَوۡ فِى ٱلسَّمَـٰوَٲتِ أَوۡ فِى ٱلۡأَرۡضِ يَأۡتِ بِہَا ٱللَّهُ‌ۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَطِيفٌ خَبِيرٌ۬"
"Ewe mwanangu hakika jambo lolote mfano liwe japo chembe ya Hardali;liwe ndani ya jabali au mbinguni au katika ardhi, Mwenye-enzi-Mungu atalileta(Amlipe mtu)bila shaka Mwenye-enzi-Mungu ni mjuzi wa mambo yote(Yalo dhahiri na siri)".
Napenda uelewe mwenye kukimbia kizazi chako, kama inavosema aya chochote kile kina malipo yake, basi elewa hawateseki watoto wewe ukaachiwa, wakiteseka watoto na wewe Mungu anakuondoshea unakua huna furaha kabisa ya maisha yako, hawasumbuki watoto ila na wewe unasumbuka katika akili yako, hawapati maradhi watoto ikawa hakuna wa kuwaangalia ila na wewe unapewa maradhi huko ulipo, hawakosi mapenzi watoto ila na wewe huyapati mapenzi huko uliko isipokua kudanganywa, kwani elewa ukifanya jambo la kusudi ni lazima ulipwe kutokana na kusudi yako.
Basi wajitazame wale walokimbia vizazi vyao wana maisha gani ajiulize mwenyewe jee ana furaha majibu utayajua mwenyewe katika nafsi yako, Na hivo ndivo inavokua Mtu akipinga njia ya Mwenye-enzi-Mungu na kukimbia kuziangalia Dhamana zake na amana alopewa, Ajijue Mtu anachangia kwa ukamilifu uharibifu wa mwenendo mzima wa jamii ya kiislam. Anachangia kuharibika kwa wale watoto kwa kukosa kupata malezi ya Kiislam, kwa hiyo watahadhari mababa na waangalie kwa undani pale wanapotaka kutafuta viji sababu vidogo vidogo ili wapate kuzitekeleza amana walizopewa, na wale wasojua labda ni wape uelekezi huu kwa (Mume na Mke)kuna (Time)au (Age)umri fulani hususan kuanzia (miaka 35 mpaka 40) wazungu wanaita(Middle-age-crisis)pengine Mtu umekumbwa na hali kama hiyo unatamani utoto au ujana urejee tena kwa hiyo unaweza kufanya vituko visosemeka mtu inapaswa akumbuke kuwa (Mechanism)ya Mwili wake yanabadilika na mawimbi yanatokezea lazima mtu ajifundishe vipi atapigana au kuyakwepa mawimbi hayo ili bahari ikitulia aendelee kuishi na familia yake. Watahadhari pia Masheikh na hukumu zao za Talaka bila ya kuzingatia Mustakabal wa watoto, kwani ukifanya hivyo na wewe Sheikh unashiriki kuivunja Amana ya Mollah alompa Mja wake aingalie.
Enyi Mababa inatosha kukumbuka hawa mnaowakimbia ni watoto wenu, mkija kufa wanakurithini na nyie wakifa wao mnawarithi basi inatosha hilo kukujulisha na kukufariji ili usitupe kizazi chako, Na wale watofanya kwa kusudi basi wao wanajiandalia makaazi yao huko Akhera sehemu inayoitwa(Aaraf) hapo unakua Motoni hupo na peponi huendi utakaa hapo utaabike kama walivotaabika wanao, kama ulivotesa kizazi chako. Na Muomba Mollah atunusuru na kuzurura Akhera.
Abdulla Baja

No comments:

Post a Comment