Saturday, September 1, 2012

ALAMA ZA WATU WA MOTONI(PART 4)

Asalaam Aleiykum
Wanasiasa:  Alama ya pili wanasiasa, hakuna ulevi mtu anodumu nao mpaka uzeeni kama siasa, tabu sana kuachia utamu huu wa vyeo na madaraka na utawala, Uteja huu unakupa uwezo fulani dhidi ya wenzio, unajenga joho la kiburi, mwanasiasa hawezi kuchanganya dini na siasa lazima azidi kumoja na wapi kazidi anajua mwenyewe, wachache sana wanakua wanasiasa na huku wanatenda mambo ya kheri, anajijua yeye mwenyewe vipi anawafanyia uadilifu Raia zake, tabu sana kumpata mwanasiasa kama huyu na akipatikana basi Dini inaamrisha alazimishwe kubakia kuendelea kuongoza, sasa inakuwaje mwanasiasa akawa hivyo, kwa sababu (system)yenyewe yote imeoza, imejengeka kwa dhuluma, uonevu,fitina na udhalilishaji kwa hiyo ufanyavo vyovyote Alama unayo, na mwenyewe ndio una hakika nayo hiyo Alama itakupeleka Peponi au Motoni.Bwana Mtume s.a.w aliwanasihi sana wanasiasa wa Kikureshi lakini kwa ajili ya kulinda maslahi yao walikataa kubadili mwenendo wao wakateremshiwa aya ambayo mpaka leo unaona inaendelea na (mfano)ni ule ule na pengine wewe mwanasiasa inakugusa ndio maana unakua mbishi na jeuri aya inasemaje:(Yaasin-aya-ya-10)"سَوَآءٌ عَلَيۡہِمۡ ءَأَنذَرۡتَهُمۡ أَمۡ لَمۡ تُنذِرۡهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ" "Na ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini"
Utakavo mwambia mwanasiasa amesahaulishwa kabisa mambo ya Mollah wake, dini anayoifata ni itikadi ya chama chake, hana habari kama anaangamiza nchi yake au dini yake, anapoteza kizazi chake, analeta uharibifu katika jamii yake na hata ukimfahamisha hataki kuamini chochote, kwa hiyo ukimuonya au usimuonye yeye alama yake ndio hiyo, keshaamua kwenda kukaa motoni milele na huwezi kumbadilisha ila atake mwenyewe.
"نَّمَا تُنذِرُ مَنِ ٱتَّبَعَ ٱلذِّڪۡرَ وَخَشِىَ ٱلرَّحۡمَـٰنَ بِٱلۡغَيۡبِۖ فَبَشِّرۡهُ بِمَغۡفِرَةٍ۬ وَأَجۡرٍ۬ ڪَرِيمٍ "
Unaweza kumuonya yule anaefata(kuyasikia)mawaidha na kumuogopa mwingi wa Rehma japo kuwa hamuoni, Basi mbashirie huyo(kuyapata)msamaha na ujira wenye heshima,
Basi mpe habari akigeuza Alama yake huyo mwanasiasa atakua sio tena mtu wa motoni na atapata kuridhiwa na Mollah wake, lakini tabu sana kwa mwanasiasa kubadilika na kuwa na iman hiyo, na wala usishtuke mbona anasali sana, mbona sijda kubwa, msikitini hatoki visikushughulishe vitendo hivyo wewe tazama  alama zake utajua mtu wa aina gani ni lazima alama itajitokeza tu haijifichi.
"إِنَّا نَحۡنُ نُحۡىِ ٱلۡمَوۡتَىٰ وَنَڪۡتُبُ مَا قَدَّمُواْ وَءَاثَـٰرَهُمۡۚ وَكُلَّ شَىۡءٍ
 أَحۡصَيۡنَـٰهُ فِىٓ إِمَامٍ۬ مُّبِينٍ۬"
"Hakika sisi tutawauhisha(Kuwafufua)wafu(watu)na tunaziandika (Amali zote wanazozifanya zisoacha athari) (nyuma yake) na (zile wanazozifanya zikaacha) taathira (nyuma yake)na kila kitu tumekihifadhi katika daftari,(Linalohifadhi kila kitu)linalobainisha kila jambo".
Atahadhari sana mtu kuingia katika Medani ya siasa na dhamira ya ufisadi, akawacha Alama yake hapa duniani, ikiwa ya kheri atapata faida yake hapa duniani na huko Akhera, lakini ikiwa Alama ya shari basi ole wake ajionee huruma yeye mwenyewe yatakayo mkuta kesho motoni, ambako hakuna muombezi, ni mfano kama vile usivoweza kumuomba Allah akuepushe na Mauti na huko motoni kwenye joshi kubwa itakua hivo hivo huwezi kuomba Mollah niepushe na Moto.

No comments:

Post a Comment