Saturday, September 22, 2012

MADHARA YA MJA MWENYE CHUKI-PART-3

Asalaam Aleiykum,

Chuki inakuumiza kwa (mfano)huu, Tizama akiingia mtu unayempenda inakuaje? na akiingia mtu unayemchukia inakuaje?, akiingia ambaye unayempenda (Nothing change)hakuna kinacho badilika, lakini jitizame ndani ya nafsi yako anapoingia yule unaye mchukia ghafla (inside)unabadilika, nini kinacho badilika ni (Chemical)katika mwili wako zinasumbuka, hazijui nini kimetokea, dakika iliyopita ulikua unacheka machozi yanakutoka kila kitu (Normal)mara kaingia mtu unamchukia (Brain)unaimrisha sasa peleka (Chemical)za hamaki hapo una (Confused)system yote unaanza kujiharibu mwenyewe ndani kwa ndani, maana huwezi kusema wala kupigana unabakia kujiumiza katika nafsi yako mpaka huyo uno muona adui akiondoka unakua umeshajichoma vya kutosha kwa (Chemical)mbili moja ya kucheka na nyengine ya hamaki mwilini mwako.
Na hapo ndio tena unaharibu mapafu na moyo, unaharibu tabia na hulka yako, ukitizamwa machoni kwa wenye kujua wanafahamu sasa wewe mgonjwa, chuki inakula kidogo kidogo sababu kubwa una ishi na sumu katika viungo vyako, utaanza kuchukia kila mtu mwisho mpaka wewe mwenyewe unaanza kujichukia, na maradhi yakizidi tena yanahamia kwenye viungo, mara hichi mara kile, ukifikia hali kama hiyo sasa unahamia katika darja nyengine unaanza kufitinisha watu, unaanza kuitapakaza sumu hivi na vile, unakua bingwa wa kuzulia watu uwongo, mambo yako yote yanakua ya kishetani, hapo ndipo viungo husema kuwambia (Ulimi)"Ewe ulimi, wewe ni kiongozi wetu basi tufanyie ihsani ya kutupunguzia adhabu, kwanza kwa kujichunga wewe nasie tufatie" na ishara za kuanza kwa kukusanyika kwa chuki ni kama vile "Ukiona mtu anakusalimia humjibu, basi chuki inaanza, ukimuona  mtu halafu unamgeuzia uso,chuki inaanza, unamsema mtu mambo ya uongo,chuki inaanza, unamnunia mtu bure, chuki inaanza,ukiona mafanikio ya mwenzio yanakuuzi, chuki inaanza, ukiona tabu kumsifia mwenzio japo anastahili, chuki inaanza na mengi mengine nyie mnayajua. Sasa ikiwa ishara hizi zote mtu kasha zigundua na bado hataki kujitakasa basi chuki inamchukua  na kumuweka katika kundi la (Shetani)na ukiweka katika kundi hili basi wanaadamu inabidi wapate kinga kutoka kwa Mollah wako kama inavosema sura ya(Naas)kwa sababu mambo haya yamo kwenye nafsi yako basi ni lazima ashtakiwe yule mwenye kumiliki hiyo nafsi.
"قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ"
Sema najikinga kwa mlezi wa wanaadamu(watu)
" مَلِكِ ٱلنَّاسِ"
Mfalme wa watu
"إِلَـٰهِ ٱلنَّاسِ"
Mwenye kuabudiwa na watu
"مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ"
Na shari ya mwenye kutia wasi wasi (ikisha)akarejea nyuma.
Na hivi ndivo inavokua mtu sumu ikimzidi anakwenda kuzua mambo kwa watu ikisha anakaa pembeni kuangalia mtafaruku utakao tokea, anakua anasingizia mambo au mtu jambo ambalo yule mtu hata hajasema, hivi na vile, fulani jinsi kadhaa wa kadhaa, maradhi yanakua yameshamvaa, hana muokozi.
"لَّذِى يُوَسۡوِسُ فِى صُدُورِ ٱلنَّاسِ"
Anatia wasi wasi nyoyoni mwa watu.
Na Mtu kama huyu anakuwa katawaliwa na shetani, kila kitu chake kina milikiwa na shetani, na inakua hivi kwa sumu zake anazotia watu wanakua hawajui waamini kweli au sikweli, hivo fulani ndio kweli kanisema hivi au hajanisema, mtu kama huyu anatapakaza sumu kila anapokwenda.
"مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ"
Ni miongoni mwa majini na wanaadamu(Watu)
Hapa lazima ifahamike kazi hii ya sumu inaanzwa na (Shetani)na anashirikishwa mwanaadamu mpaka na yeye anakua katika kundi la mashetani, anashiriki kutapakaza sumu mpaka shetani mwenyewe ana shangaa.
Mwisho kabisa namalizia kwa kukuombeni jaribuni kusamehe, kama jambo lipo au limepita basi kubali limetokea na haliwezi kurudi tena likajirekebisha, tuondoshe mafundo kwenye mioyo yetu,  ukifanya hivyo utaona maisha yako unaishi kwa utulivu kitu kama hukipendi unakuwa sehemu ya kati wala huendi upande wa chuki, na ukiwa (natural)ndio unaipata salama. 
Namuomba Mollah atujaalie kuwa katika kundi la waja wa kati na kati. Amin
Abdulla Baja

No comments:

Post a Comment