Saturday, September 1, 2012

ALAMA ZA WATU WA MOTONI(PART 3)

Asalaam Aleiykum.
Mashekhe: Wakianza khutba Mashekhe husema Nausia nafsi yangu pamoja na kuhusia nafsi zenu, basi leo hapa naanza na Mashekhe au wale wanoingia katika taasisi za kidini, au kuvamia miskiti kwa ajili ya kula mali za yatima, au kuleta visingizio vyovyote katika jambo la kidini ili upate kudhulumu Waumini, basi Alama zenu mnazijua na sisi tunazijua na kama aya inavosema ambayo nyinyi mnakwenda kinyume chake mechoka kumkera Mollah wenu mitaani sasa mnamfata katika nyumba zake za Ibada aya inahimiza vipi (Sura ya Saff aya ya 10-11)"يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ هَلۡ أَدُلُّكُمۡ عَلَىٰ تِجَـٰرَةٍ۬ تُنجِيكُم مِّنۡ عَذَابٍ أَلِيمٍ۬ "
"Enyi Mloamini jee nikujulisheni biashara itakayo kuepusheni na adhabu iumizayo".
Nyinyi mnataka kufahamishwa biashara ya kufanya ili muepushwe na adhabu, lakini mmeamua kufanya kinyume chake mnakwenda kuiba huko huko kwenye kutoka hiyo adhabu, hasara ilioje juu yenu kwenda kufanya ufisadi kwa Waumini wa Mwenye-enzi-Mungu, mateso gani yatakukabili huko mbeleni Mollah ndio mwenye kuyajua, nyinyi mnazigeuza taasisi za Kidini ndio sehemu za kazi zenu za kuchota Sadaka za Jamii, watahadhari sana hata wale wanosaidia kufanyika ufisadi huu, ikiwa kina mama majumbani au mkubwa kazini, atahadhari mtu kuyanyamazia mambo haya kwani kunyamaza ni nusu ya kushiriki na wewe utapata fungu la malipo ya kunyamaza kwa hilo halina shaka.
Na kwanini unafanya hivo zitupie macho sababu katika aya inayaofatia utajua kwanini unatenda ufisadi kama huo.
"تُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَتُجَـٰهِدُونَ فِى سَبِيلِ ٱللَّهِ بِأَمۡوَٲلِكُمۡ وَأَنفُسِكُمۡ‌ۚ ذَٲلِكُمۡ خَيۡرٌ۬ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ "
"Mumuamini Mwenye-enzi-Mungu na Mtume wake, Na mpigane (kwa ajili)ya Dini ya Mwenye-enzi-Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu, hayo ni bora kwenu, Ikiwa mnajua."
Hiyo ndio Biashara yenyewe Mwenye-enzi-Mungu kashafanya yake, kakupa uhai, kakufanyia kheri zote,kakuruzuku afya, wewe una nguvu za kufanya kazi, katimiza upande wake wa biashara, sasa nini upande wako jee umekamilisha, na wala hakuhitaji mengi kutoka kwako kataka ufanye mema na ibada vitu viwili tu ili akupe faida nyingi zisizo malizika.lakini wapi Wewe ndio unamwendea huko huko kwa waumini wake kuanza kudhulumu, na ndio maana aya ikaanza kwa(nikujulisheni)sababu kitu hicho kipo na kigumu sana juu yenu wanaadamu(Adhabu iumizayo) basi mfanye nini jambo la kwanza(Iman)ukiona unakula mali za waumini,maskini,mayatima au hata wananchi basi jijue wewe huna iman ogopa sana kama Mollah wako atakuchukua uko katika hali hiyo,ukiweza kufanya hayo unayoyafanya basi humuamini Mwenye-enzi-Mungu wala Mtume wake, sasa vipi utaweza kupigana hiyo (Jihad)ya nafsi na Mali.Wewe unaambiwa uchume Mali ukatoe, leo wewe wale wale walokwambia ndio unakwenda kuwaibia, kuwadhulumu hivi na vile unakula haram, umejitia katika dini ya Mwenye-enzi-Mungu ndio unaifanya kitega uchumi, (Nimepokea habari wengine wanakwenda kwa waganga kulinda cheo au Uimam msikitini), Atahadhari sana mtu akiwa na Alama hii haifutiki abadan, na dhanmbi zake hazisemeki, asije akajidanganya mtu eti uwadhulumu watu ikisha umeumwa au umekua mzee tena hapo unaanza na (Istighfara)za Mdomo hukubaliwi abadan, wewe uchukue Mali au Pesa zinufaishe watoto wako, ikisha huku upeleke maneno,  hakuna toba hiyo, Kama ulivokopa ndivo utakavolipa.
Endelea part 4 

No comments:

Post a Comment