Saturday, November 10, 2012

NANI KAMA MAMA?PART-3

Asalaam Aleiykum,

Mama ni wewe mpaka nikiwa mtu mzima mapenzi yako yanaendelea kama yalivo mwanzo, Leo hii nimekua mkubwa ukaja kuniozesha sasa niko na mke wangu au mume wangu eti nakukejeli mbele yake, Mimi nakupuuza na huku namuamini mume wangu au mke wangu na kukukadhibisha wewe, Mimi nina hali gani kama ghafla nitahudhuria kwa yule aloniumba. Leo imefikia eti nakutuma unikoshee vyombo, au uende dukani, na hivi ndivo jeuri ziliponifikisha.Nimefikia hali nayapuuza Maneno ya Bwana Mtume s.a.w alosema "Hakika ya hiyo pepo ipo chini ya nyayo za Mama zenu",Kwanini Bwana Mtume s.a.w akasema maneno haya na nini alikua anakusudia,"Kusudio hapo lilikua kukufahamisha ni lazima ujitupe, urejee katika hali ya chini kabisa mbele ya Mama yako, sio wewe umtume maji ya kunawa mkono Mama yako,ila unatakiwa wewe ukachukue hayo maji umnawishe Mama yako halafu usimame mpaka amalize kula hiyo ndio heshima na huko ndio kunyenyekea kwa mzee wako, wangapi katika sisi leo tunatenda hayo, leo akikuomba pesa ya kula  tu majibu yanayokutoka mpaka Malaika wanaogopa. Leo unasahau kama Mama yako alikua akienda msitu na nyika ili atie tonge kinywani mwako, yeye ndio kila akikaa anakuombea dua kwa siri na dhahir ili ufanikiwe.
Nani kama Mama?
Sasa kama unayatilia wasiwasi Maneno hayo ya Bwana Mtume s.a.w "Basi jikumbushe kisa cha kijana Alqamah"Yeye alikua  ni mwenye kujitahidi kufanya mambo mengi ya Ibadah, alikua akisimamisha Salah, (kipindi hakimpiti)akifunga sana(Saum ni kawaida yake)na katika mambo ya kutoa sadaka yeye alikua mbele sana katika kutoa, Yakaja kumpata maradhi na maradhi yale yakawa yanazidi, akamtuma mkewe akampe habari Bwana Mtume s.a.w"Akenda yule Mke kwa Bwana Mtume s.a.w "Akamwambia mume wangu Alqamah anaumwa Taabani Yaa Rasullallah"kanambia nije kukufahamisha. Bwana Mtume s.a.w akatuma Masahaba zake akiwemo Syd Bilal r.a wende nyumbani kwa Alqamah mkamtoleshe Shahada, wakenda Masahaba  wakamkuta Alqamah makhtuti, wakamwambia "Ewe Alqamah sema"(Laaillah-illa-Allah)Lakini ulimi wa Alqamah haukuweza kutamka, wakarejea kumpa habari Bwana Mtume s.a.w na akasema jee wazee wake Alqamah wa hai, akajibiwa Mama yake yupo hai lakini ni mtu mzima sana, akamtuma mtu akamwambie mama yake Alqamah kama ataweza kutembea na kuja kwa Bwana Mtume s.a.w laa kama hawezi basi Bwana  Mtume s.a.w atakwenda yeye.
Akainuka Mama yake Alqamah na fimbo yake akenda kwa Mtume s.a.w akamsalimia na Bwana Mtume s.a.w akarudisha salam ikisha akamwambia "Ewe Mama wa Alqamah niambie ukweli na kama ukidanganya basi utakuja wahyi kutoka kwa Mwenye-enzi-Mungu" ilikuaje hali ya Mwanao Alqamah(wakati yuko mzima)Akajibu Mama yake Alqamah alikua mwenye kusali sana, na akifunga sana, na akitoa sadaka sana, Akamuuliza tena Bwana Mtume s.a.w jee yalikua vipi mahusiano yako na mwanao Alqamah, yule mama akasema "Ewe Mjumbe wa Mwenye-enzi-Mungu, Hakika mimi nimefungika moyo wangu juu ya mwanangu"kwani alikua akimsikiliza Mkewe na akiniasi mimi(akinikadhibisha)Akasema Bwana Mtume s.a.w kufungika kwa Mama yake Alqamah ndio sababu mwanae hawezi kutoa Shahada, ikisha akamwambia Ewe Bilal r.a kanitafutie kuni(Mbao)ili apate kuchomwa moto Alqamah, Akasema Mama wa Alqamah hauwezi kuchukua moyo wangu kuona mwanangu anateseka, Akasema Bwana Mtume s.a.w adhabu ya Mwenye-enzi-Mungu ni kali kuliko hiyo na ni ya kuendelea, basi kama utataka asamehewe na Mollah wake itabidi Uridhie moyo wako na kama hukuridhia moyo wako hazitomfaa, sala zake wala funga zake wala utowaji wake wa sadaka midamu moyo wako umefungika juu yake.
Akasema Mama yake Alqamah Mwenye-enzi-Mungu ananishuhudia na Malaika wake na waislam wote walohudhuria hapa yakuwa mimi niko Radhi na mwanangu, Akasema Bwana Mtume s.a.w Ewe Bilal r.a nenda kamtizame Alqamah anaweza kusema (Laa-illah-illa-Allah)au hawezi, isije ikawa Mama yake Alqamah kasema kitu hakimo ndani ya moyo wake ila kanionea haya mimi, Akenda Bilal r.a akamsikia Alqamah anasema (Laa-illah-illa-Allah)akaingia ndani ya nyumba Bilal r.a na kuwaambia waliomo ndani kufungika kwa Mama yake Alqamah ndio kuliko fanya uzito wa kushindwa ulimi wa Alqamah kutamka shahada, mpaka aliporidhia mama yake ndio ulimi ukatamka na ukawa mwepesi, ikisha baada ya hapo Alqamah akafa siku ile ile.Sasa ikiwa Shahada imeshindikana nini habari ya kuipata hiyo pepo inakuaje? Endelea part-4

No comments:

Post a Comment